Wednesday, November 25, 2015

Wahakumiwa Miaka 30 Jela Kwa Kumuibia Jaji wa Mahakama Kuu

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imewahukumu kwenda jela miaka 30 watu wanne baada ya kukutwa na hatia ya makosa kula njama, uporaji na unyang’anyi wa kutumia silaha vitu vyenye thamani ya Sh. milioni 15 mali ya Jaji John Mgeta, wa Mahakama Kuu Tanzania.
 
Waliopewa adhabu hiyo ni wafanyabiashara James Warioba (29) maarufu kama Sailensa, Abdulkarim Hussein ama Muddy, Seif Lusonzo ama Dege, Ally Mdege, Lusekelo Mundengese ama Tekero, Omary Hassan na mlinzi Benjamin Macklin, wote wakazi wa jijini Dar es Salaam.
 
Hukumu hiyo ilisomwa jana na Hakimu Mkazi Mwandamizi, Devotha Kisoka.
 
Alisema baada ya kupitia ushahidi uliotolewa na mashahidi 12 wa upande wa Jamhuri bila kuacha shaka, Mahakama imewatia washtakiwa hatiani.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More