Thursday, July 22, 2021





Na Fredy Mgunda,Irnga.

Mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo amesema kuwa wakandarasi watakao chelewesha au kujenga chini ya kiwango miradi ya kimaendeleo katika halmashauri ya Manispaa ya Iringa watarudia kwa gharama zao kwa ubora ule ule unatakiwa kutokana na thamani ya mradi husika.

Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua miradi ya kimaendeleo katika manispaa ya Iringa, mkuu wa wilaya Mohamed Hassan Moyo alisema kuwa amefanikiwa kukagua miradi mingi ambayo imejengwa kwa viwango vinavyotakiwa ila tatizo kubwa lipo kwa wakandarasi ambao wamekuwa wakipewa tenda za ujenzi wa miradi hiyo.

alisema kuwa wakati wa ziara aligundua kuwa wakandarasi wengi wameshalipwa fedha serikali kwa ajili ya kutekeleza miradi ya serikali ila wamekuwa wanaichelewesha kwa makusudi na kusababisha kuchelewa kuanza kufanya kazi kwa miradi hiyo.

Moyo alisema kuwa miradi mingi ilijengwa kwenye halmashauri ya Manispaa ya Iringa imejengwa kwa ubora unatakiwa kulingana na thamani ya fedha iliyotakiwa kutumika katika mradi husika.

Alisema kuwa watendaji wa Manispaa ya Iringa wanatakiwa kusimamia vilivyo fedha ambazo zinakuwa zinatolewa kwa ajili ya miradi ya kimaendeleo ili kusaidia kuwa na miradi iliyojengwa kwa viwango bora.

Moyo aliwataka wananchi wa manispaa ya Iringa kuhakikisha wanatunza miundombinu ya miradi ambayo imejengwa kwenye mitaa yao ili kuhakikisha miradi hiyo inatoa manufaa ambayo yamekusudiwa na serikali ya kuchangia kukuza maendeleo.

Mkuu huyo wa wilaya ya Iringa alifanikiwa kutembelea mbalimbali kama vile kukagua ujenzi wa choo cha zahanati ya Kitanzini,kukagua shule ya msingi Azimio,ujenzi wa choo cha shule ya msingi chemchem,ujenzi wa jengo la zahanati ya Itamba,ujenzi wa maabara shule ya sekondari ya Mivinjeni,ujenzi wa madarasa manne ya shule ya msingi mawelewele,ujenzi wa shule ya sekondari ya Kwakilosa na kutembelea ujenzi wa madarasa mawili shule ya msingi Njia Panda.

Kwa upande wake Meya wa Manispaa ya Iringa Ibrahim Ngwada alisema kuwa wameyapokea maagizo yote yaliyotolewa na mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo na watayafanyia kazi ili kuondoa kasoro ambazo zimejitokeza kwenye baadhi ya miradi ambayo kamati hiyo wameitembelea.

Aliwataka watendaji wote wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa kuhakikisha wanafanya kazi zao kwa weledi unaotakiwa ili kutumia fedha za wananchi vizuri kuendana na mradi ambao unakuwa unatekelezwa kwenye maeneo yao.





Monday, June 14, 2021

DC KASESELA : AWATAKA KAMPUNI YA MWENGA KUTENGENEZA MITA ZA WATEJA WAKE


Kaimu mkuu wa wilaya Mufindi ambaye ni mkuu wa wilaya ya Iringa Richad Kasesela akitoa neno kwenye mkutano wa maombi ya kurekebisha bei ya umeme wa Mwenga Power Limeted katika kijiji cha Igoda kilichopo wilaya ya Mufindi
Baadhi ya wananchi waliohudhuria mkutano huo wa wadau wanaotumia umeme wa kampuni ya Mwenga


Na Fredy Mgunda,Iringa.

MKUU wa wilaya ya Mufindi ameitaka kampuni ya Mwenga Power Services Limited kutengeneza mita za wateja zilizoharibika kwa wakati ili wananchi waendelee kufanya shughuli za kimaendeleo kwa kutumia nishati ya umeme ambayo inatolewa na kampuni hiyo.

Akizungumza kwenye mkutano wa maombi ya kurekebisha bei za umeme zinazotolewa na kampuni ya Mwenga,kaimu mkuu wa wilaya hiyo ambaye ni mkuu wa wilaya ya Iringa,Richad Kasesela alisema kuwa kampuni hiyo inatakiwa kutengeneza kwa wakati mita ambazo zimeharibika kwa wakati ili wananchi wasikose huduma hiyo.

Kasesela alisema kuwa jukumu la kuzitengeneza mita za umeme zilizoharibika ni jukumu la kampuni ya Mwenga Power Services limited ili kuondoa athari ambazo mteja anaweza kukutana nazo akiamua kuitengeneza yeye mwenyewe.

Alisema kuwa ni kosa kubwa kwa wananchi kutengeneza mwenyewe mita ambazo zimeharibika wakati mafundi wa kampuni ya Mwenga wapo kwa ajili ya hilo na wanajua namna ya kuzitengeneza na zisilete madhara  kwa wateja.

Kasesela aliongeza kuwa watumishi wa kampuni ya Mwenga Power Services limited wanatakiwa kutoa huduma bora kwa wateja ili kuondoa malalamiko ambayo wananchi wamekuwa wakiyatoa kwenye ofisini ya mkuu wa wilaya ya Mufindi.

Alisema kuwa nishati ya umeme inachangia kwa asilimia kubwa kukuza uchumi wa wananchi kwa kuwa wanategemea nishati hiyo katika kuzalisha bidhaa mbalimbali hata kutimiza majukumu ya kuleta maendelea kwa ujumla.

Kasesela aliwapongeza mamlaka ya udhibiti wa huduma za nishati na maji (EWURA) kwa namna wanavyofanya kazi zao kwa kushiikiana na wananchi ili kuhakikisha wanaondoa kero  ambazo hazina msingi kwenye kuleta maendeleo na kukuza uchumu kwa wananchi.

Aidha Kasesela alimalizia kwa kuwaomba wananchi wa vijiji 32 kuendelea kutumia umeme unaozalishwa na kampuni ya Mwenga Power Services limited ambao unagharama  nafuu na unasaidia kukuza uchumi wa wananchi wa vijiji hiyo na taifa kwa ujumla.

 

kwa upande wake kaimu mkurugenzi mkuu wa EWURA,Nzinyangwa Mchany alisema kuwa ili kampuni iruhusiwe kurekebisha bei ni lazima afuate kanuni za EWURA za umeme na gesi asilia za maombi ya kupanga bei za mwaka 2017 zilizofanyiwa marekebisho mwaka 2021 ambapo kuna hatua saba za kuzifuata.

Alisema kuwa wanatakiwa kupokea maombi,kupitia maombi na kuomba ufafanuzi mbalimbali kutoka kwenye mamlaka,kuweka mkutano wa hadhara(taftishi) ,kupokea maoni ya maandishi ,kufanya uchanbuzi wa kina na kuwasilisha mapendekezo kwenye bodi,kutoa maamuzi ya bodi na kutangaza maamuzi ya bodi kwenye gazeti la serikali na magazeti ya kawaida.

Mchany alisema kuwa sheria ya EWURA inasema kuwa kama kuna mtu hajaridhika na maamuzi hayo anahaki ya kukata rufaa kwenye baraza la ushindani wa haki katika biashara.

Alimalizia kwa kuwaambia wananchi kuwa maoni hayo ya marekebisho ya bei za umeme za kampuni ya Mwenga Power Services Limited kuna vikao ambavyo vitakaliwa ili kuhakikisha pande zote mbili zinaridhika kwa ajili ya kukuza uchumi wa nchi.

Naye  meneja wa fedha wa kampuni ya Mwenga Power Services Limited,Deograsias Massawe alisema kuwa Mwenga Power inazaidi ya kilomita 400 za laini za kusambaza umeme wenye nguvu ya gridi na umeme jadidifu katika vijiji37(vijiji 32 na 5 katika Wilaya za Mufindi na Njombe,mtawalia).

Massawe  alisema kuwa Mwenga Power inazaidi ya wateja 5,400 waliounganishiwa umeme katika Wilaya za Mufindi na Njombe na Hadi sasa Mwenga Power inatransifoma 80 za kupooza umeme huu unawafaidisha watu zaidi ya100,000 na kwa jinsi usambazaji unavyopanuka na kunatarajia kuwa faidisha watu wengi zaidi.

Alisema kuwa wanategemea kuhakikisha pande zote mbili zitanufaika kwa marekebisho hayo mapya ya bei za umeme wa kampuni ya mwenga. 

 


  

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More