Monday, November 23, 2015

CHADEMA KUMPATA MEYA WA MANISPAA YA IRINGA KESHO

 
 MWENYEKITI WA CHADEMA IRINGA MJINI FRANK NYALUSI

CHAMA  cha Demokrasia na maendeleo chadema Jimbo la Iringa mjini kimesema kesho/leo chama hicho kinaingia kwenye mchakato wa kura za maoni za nani  atakayekalia kiti cha Meya na Naibu Meya ambaye ataongoza halmashauri ya manispaa ya Iringa kwa kipindi cha mwaka 2015/2020.

 Mwenyekiti wa chadema wilaya ya Iringa ambaye pia ni diwani mteule wa chadema kata ya Mivinjeni Frank Nyalus alisema kuwa hadi sasa wameshajitokeza madiwani watatu sita ambao watatu wameingia kwenye kinyang’anyiro cha Meya na wengine watatu kwenye kinyang’anyiro cha Unaibu Meya.

Nyalusi aliwataja madiwani ambao wemejitokeza kuchukua fomu ya kugombea nafasi hizo huku wakisubiria maamuzi ya chama hicho.

Waliojitokeza kuwania nafasi ya Meya ni Diwani wa kata ya Mivinjeni Frank Nyalus,diwani wa kata ya Kitwiru Baraka Kimata na Diwani wa kata ya Isakalilo Alex Kimbe.

Waliojitokeza kuusaka unaibu Meya ni diwani wa kata ya Gangilonga Dadi Igogo,Diwani wa kata ya Kwakilosa Joseph Lyata na diwani wa kata ya mkimbizi Evaristo Mtitu.  

Mchakato wa uchukuaji wa fomu ulianza  Novemba 21 Mwaka huu na wanatarajia kurudisha fomu hizo leo Novemba 24 na kuingia kwenye kura za maoni huku gharama ya fomu zikiwa   Tsh.50,000 kwa kila moja.

Hata hivyo baadhi ya wananchi wa manispaa ya Iringa wakiwamo madiwani wenyewe wamekuwa na mchecheto wa kumjua nani atakaye kuwa mrithi wa Meya aliyemaliza muda wake na pia ni diwani mteule wa chama cha mapinduzi (CCM) kata ya Mlandege Aman Mwamwindi.

Akizungumza mmoja wa wafanyabiashara wa wadogo mjini Iringa Pendo Yugin alisema kuwa wao wanawataka madiwania hao kumchagua meya atakayetokana na wao ambaye atawatetea hata kwenye biashara zao badala ya kuwanyanyasa.

Aidha waliogombea nafasi ya Meya wameliambia Nipashe kwamba lengo lao la  kugombea ni kuifanya manispaa hiyo iwe ya mfano kwenye miradi ya maendeleo tofauti na kipindi cha meya aliyemaliza muda wake.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More