Tuesday, June 5, 2018

Chumi ashikilia shilingi kuitaka Serikali kutoa fedha za Miradi Viporo kama ilivyoahidi, Spika aokoa jahazi

Mbunge wa Mafinga Mjini Cosato Chumi ameitaka serikali kutoa fedha za miradi viporo kama ilivyoahidi kwa kuwa mwaka wa fedha unaelekea mwishoni.

Chumi alitoa hoja hiyo wakati Bunge limekaa kama Kamati kujadili bajeti ya Wizara ya Fedha na Mipango ambapo alisema kuwa, ni Serikali yenyewe ndio ilizitaka Halmashauri kuwasilisha miradi viporo ambayo mingi ilitokana na nguvu za wananchi.

Akijibu hoja hiyo, Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Ashantu Kijaji alisema kuwa Serikali inafanya uchambuzi wa miradi hiyo ndipo itoe fedha.

Hata hivyo, Chumi alihoji ni uchambuzi gani ikiwa miradi hiyo ilianishwa na kuchambuliwa kwa ushirikiano kati ya Halmashauri na Tamisemi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uchambuzi upi huo ambao serikali inaufanya ikiwa Halmashauri kwa kushirikiana na Tamisemi walishafanya? Naomba Waheshimiwa Wabunge mniunge mkono, tujadili jambo hili

Baada ya kauli hiyo, wabunge wengi walisimama kuunga mkono hoja. 

Hata hivyo, Spika ambaye kwa wakati huo alikuwa Mwenyekiti, aliitaka Serikali kuona uzito wa hoja hiyo na kwenda kulifanyia kazi.

Mheshimiwa Waziri Mkuu, jambo hili ni zito, mimi niwaombe Serikali, mlichukulie uzito unaostahili, Mheshimiwa Chumi unasemaje baada ya msisitizo huu

Akihitimisha hoja yake, Mbunge huyo wa Mafinga Mjini alisema kuwa, kwa msisitizo uliotoa Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaamini Serikali italifanyia kazi kwa uzito huo huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti umeshasema kwa msisitizo, na wewe Mwenyekiti ndiye uliyekikalia kiti, narejesha shilingi na kuisihi Serikali itoe fedha hizo ili kuongeza morali ya wananchi kujitolea katika shughuli za maendeleo

Akizungumza na mwandishi wetu baadae, Chumi alisema kuwa katika Jimbo la Mafinga Mjini waliainisha kukamilisha miradi ya ujenzi wa kituo cha Afya Bumilayinga, kukamilisha Zahanati za Kitelewasi, Kisada, Ulole na nyumba tatu za wauguzi, na ukarabati wa madarasa katika shule ya Msingi Kikombo.

Monday, June 4, 2018

MKURUGENZI WA NGOTI GREEN ACADEMY AWATAKA WAZAZI KUWALEA WATOTO KIMAADILI


 Mkuu wa shuleya Ngoti Green Academy  Jonson Mtewele kushoto akiwa na mkurugunzi wa Ngoti Green Academy Thomas Ngoti ambaye alikuwa anatoa neno kwa wazazi waliofika kwenye kikao cha pamoja baina ya wazazi walimu na wanafunzi wanaosoma katika shule hiyo
 Mmoja wa wazazi walifika katika shule ya Ngoti Green Academy akitoa neno mbele ya wageni waalikwa na mkurugunzi wa Ngoti Green Academy Thomas Ngoti 
Picha za pamoja baina ya wazazi,walimu na viongozi wa shule ya Ngoti Green Academy  
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya Ngoti Green Academy 

NA FREDY MGUNDA,IRINGA

Mkuu wa shule ya Ngoti Green Academy  amewataka wazazi na walezi mkoani Iringa kuwalea watoto katika maadili yanayostahili ili kuwa na kizazi chenye maadili na uwajibikaji kwa jamii na kuleta maendeleo ya nchi na familia zao.

Akizungumza na wazazi wa shule ya Ngoti Green Academy mkuu wa shule hiyo Jonson Mtewele alisema kuwa maadali ya mtanzania yanazidi kupotea kutoka na mmong’onyoko wa utandawazi

“Mimi nasema kuwa saizi tamaduni za kimagharibi zimeharibu sana utamaduni wenu maana wananchi wengi wanaiga bila kujua wanaiga maadili gani ndio maana saizi watoto wetu wengi wamekuwa hawana maadili” alisema Mtewele

Mtewele aliwataka wazazi kuacha kuwafundisha tamaduni za kimagharibi ambazo hazina maadili ya kimaendeleo kwa watoto wadogo ambao ndio wamekuwa waathirika wakubwa kwenye hizi tamaduni za kimagharibi.

“Mtoto kutoka mwaka mmoja hadi miaka nane ndio umri wa mtoto kupokea vitu vipya kichwani mwake ndio maana nasema ukikosea kumlea mtoto katika umri huo basi waweza kulea mtoto akiwa hana maadili yatayomuwezesha kufanikiwa katika maisha yake” alisema Mtewele

Aidha Mtewele alisema shule ya Ngoti Green Academy inawafundisha wanafunzi katika mfumo wa maadili ya dini kutoka na matendo ya bwana yesu aliyaonyesha duniani na kuwa mfano wa maadili bora.

“Tunataka mtoto akue katika maadili ya kikristo kwa maana kuwa tunamtaala wenye tabia njema siti ambazo bwana yesu alizionyesha akiwa duniani upole,unyenyekevu na wakati furani kukubali kuonewa na sio lazima abishe kila kitu na tunavyomuelekeza kwa namna hivyo tumegundua kuwa watoto watakuwa kati hali hiyo” alisema Mtewele  

Mtewele aliongeza kuwa shule hiyo inapokea watoto kuanzia mwaka mmoja hadi miaka nane kwa kuwa huo ndio wakati mzuri wa kuwalea watoto kimaadili na kuwajengea uelewa wa maisha ya baadae.

“Tumeruhusiwa kuwapokea watoto kuanzia umri wa mwaka mmoja hadi miaka nane baada ya hapo inakuwa vigumu kupokea watoto wa zaidi ya miaka hivyo kwa mjibu ya mtaala ambao tunao” alisema Mtewele

Naye mkurugunzi wa Ngoti Green Academy Thomas Ngoti alisema kuwa shule hiyo inatoa elimu iliyobora ambayo inatakiwa kitaifa na kimataifa kutokana na mtaala ambao wanautumia.

“Ngoti Green Academy inatoa elimu kwa upana wake ndio maana wazazi wengi wameanza kuwaleta watoto wao hapa kwa ajili ya watoto wao kupata elimu bora ambayo inapatika hapa nadio huo ubora wake” alisema Ngoti

Ngoti aliongeza kuwa wanampango wa kwenda kwenye ngazi ya sekondari na chuo kikuu kwa kuwa wamekuwa wakitoa elimu iliyobora hivyo hata serikali inawaamini kwa kuwa wanamtaala mzuri wa kutoa elimu bora kwa wanafunzi ambao watakuwa wanasoma kwenye sekondari na chuo kikuu.

“Ngoti Green Academy Thomas ni chombo kamili cha kuandaa watoto wadogo ambao bado hawajalishwa vitu vingi kichwani na ndio maana wanataka kuanziasha sekondari na chuo kikuu ili wanafunzi weweze kupata elimu bora kwa mtaala bora ambao wanautumia” alisema Ngoti

Ngoti alisema kuwa Ngoti Green Academy inapatikana maeneo ya Mtwivila sehemu inaitwa Mwambusi au unaweza kutembelea makao mkuu ya kampuni yalipo jingo la IMUCU gorofa namba moja chumba na kumi na nane lakini unaweza kupiga namba 0765800310 au 0718056561 hapo ndio itakuwa kazi rahisi kuwapata.

UMEME NI NISHATI MBADALA ILIYO NAFUU KWA MATUMIZI YA NYUMBANI: KAMOTE

 Bw. Ally M. Koyya, (kulia), kutoka idara ya Masoko TANESCO, akitoa maelezo kwa wananchi waliotembelea kwenye banda la Shirika hilo kwenye maonesho ya Nishati Mbadala yanayokwenda sambamba na Maadhimisho ya Wiki ya Mazingira Duniani kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam Juni 4, 2018.


NA K-VIS BLOG/Khalfan Said

SHIRIKA la Umeme Nchini (TANESCO) limesema hakuna sababu yoyote kwa wananchi kuogopa kutumia nishati ya umeme kwa matumizi mbalimbali ya nyumbani kwani ni nafuu mno ukilinganisha na nishati nyingine.
Afisa Mazingira wa Shirika hilo, Bw.Yusuf Kamote, amesema hayo kwenye maonesho ya Nishati mbadala ambayo ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Mazingira Duniani yanayoendelea kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo Juni 4, 2018, ambapo kauli mbiu ya mwaka huu ni “Mkaa ni ghali tutumie Nishati mbadala”.
“Siku zote tunasema umeme wa TANESCO ni umeme wa bei nafuu, jambo la msingi ambalo wananchi wanapaswa kuelewa ni matumizi sahihi ya vifaa vya umeme kulingana na mahitaji.” Alisema.
Alisema kwa mfano mtu anatumia kifaa kinachohitaji WATI 100 (100watts) kwa saa moja lakini anatumia kifaa cha WATI 200 (200Watts) kwa saa na kwa mahitaji yanayofanana, bila shaka hayo sio matumizi bora ya umeme.
Bw. Kamote pia alishauri, wananchi wanapotaka kununua vifaa vya umeme, wanapaswa kukague kiasi cha umeme kinachohitajika kwenye kifaa husika anachotaka kununua na vifaa hivyo hupimwa kwa kutumia WATI (Watt ).
“Ukitumia pasi ya umeme ya WATI 1000 (1000Watts), kwa saa moja ni sawa na kutumia Unit 1 ya umeme kwa hivyo hakuna sababu ya kununua pasi ya umeme ya WATI2000 (2000Watts), kwa matumizi ya kawaida kwani pasi ya aina hiyo kwa matumizi sawa na ile ya WATI1000, matumizi yake yataongezeka, kutoka unit 1 hadi uniti 2.” Alifafannua.
Akieleza zaidi Bw. Kamote hakuna sababu tena ya kutumia mkaa kama nishati ya kupikia kwani hivi sasa yapo majiko ya umeme ambayo yanasaidia kudhibiti matumizi yaumeme yasiyo sahihi kwani.
“Kinachohitajika mpishi unatakiwa kuandaa vyakula unavyotaka kupika kabla ya kuwasha jiko lako la umeme, vyakula vikiwa tayari hapo ndipo unatakiwa kuwasha jiko lako tayari kwa kupika.” Alisema na kuongeza
Maonesho hayoyakliyoandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Rais,  yalizinduliwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wiki iliyopita na yanatariwa kufungwa na Rais John Magufuli, Jumanne Juni 5, 2018.

 Wanafunzi wa shule ya sekondari Kanosa ya jijini Dar es Salaam, wakipatiwa maelezo ya kitaalamu na wataalamu wa TANESCO (Kushoto).
Afisa Mazingira wa Shirika la Umeme Nchini (TANESCO), Bw. Yusuf Kamote, (kulia), akimsikiliza Afisa Uhusiano wa Shirika hilo, Bi. Samia Chande.


 Wanafunzi wa shule ya sekondari Kanosa ya jijini Dar es Salaam, wakipatiwa maelezo ya kitaalamu kuhusu matumizi bora ya nishati ya umeme walipotembelea banda la Shirika hilo leo Juni 4, 2018.
 Bw. Ally M. Koyya, (kulia), kutoka idara ya Masoko TANESCO, akimsikiliza mwananchi huyu aliyefika kwenye banda la Shirika hilo kupata elimu ya umeme.

VIONGOZI 11 WA UPINZANI WARUSHIWA KOMBORA LA UFISADI ZITTO KABWE ATAJWA KUWA NI NAMBA MOJA

 Mwanasheria Patrobas Katambi.
Mwenyekiti mstaafu wa Baraza la Umoja wa Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (BAVICHA), ambaye kwa sasa ni kada wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mwanasheria Patrobas Katambi, akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, kuhusu viongozi wa upinzani kujinufaisha kupitia elimu na vyeo vyao. Soma taarifa hiyo hapa chini.

TUHUMA NZITO ZISIZOKANUSHIKA ZINAZOWAKABILI VIONGOZI WA UPINZANI KUJINUFAISHA KUPITIA ELIMU NA VYEO VYAO.

Ndugu, Watanzania na Ndugu Waandishi wa habari, Asasi za Kiraia na Taasisi zote wadau wa Maendeleo Tanzania, nawasalimu kwa Jina la Amani. 

Nchi yetu tumepewa na Mungu, utajiri wa Rasilimali za kila aina, ila Watu wake ni Masikini na Nchi ni Masikini Kiuchumi. 
Sababu kubwa ni makosa ya Aina ya siasa, Mifumo na Uongozi katika Uamzi, Mipango, Utekelezaji, Rushwa na Mgongano kati ya Maslahi binafsi  na Uzalendo (Ufisadi).

Ugonjwa wa Kukosa Uzalendo na Uaminifu ndio chanzo ya cha Serikali ya CCM awamu ya Tano, Chini ya Uongozi wa Mhe. Rais JP Magufuli kuamua kufanya Uchunguzi na Mabadiliko katika Sheria, mifumo, miundo, na utendaji ili kuinusuru Nchi yetu na Taasisi washirika Kiuchumi.

Bila upendeleo wa utoaji taarifa(Double Standard), Vyombo vya Habari kwa niaba na faida ya Watanzania leo wajue wapo Mafisadi wakubwa kutoka Vyama vya Upinzani, Walipata wapi Uhalali na Uhodari wa kuchambua na kutuhumu wenzao kwa ufisadi huu? Sio vibaya nao Watanzania wakawajua na kutoa hukumu bila Upendeleo, ili kuisaidia Nchi kupata Viongozi Wazalendo wa kweli.

Ikumbukwe hakuna dhambi kubwa au ndogo, dhambi ni dhambi, Ulaji ni ulaji, Haramu ni haramu, Wizi ni wizi.

Haramu ya Kiongozi wa CCM au Serikali, haiwezi kuwa Halali kwa Kiongozi wa Upinzani (Haramu ni Haramu tu.)

Katika list hii ya Mafisadi-Mibuyu 11 wa Upinzani. 

Leo naanza na mmoja (kwa machache) ambae ni Mhe.
Zitto Kabwe (MB. ACT)Kigoma mjini.

Anajipambanua na kuhubiri yeye ni Mzalendo na Mjamaa...
Ikiwa yafuatayo yanamkabili anapata wapi uhalali wa kunyooshea watu vidole?

1. Mhe. Zitto alipokea hongo kutoka Barrick kuzibwa mdomo pamoja na vifaa vya kukarabati shule jimboni kwake  vyenye thamani ya Dola $20.000 kinyume na sheria (CSR), baada ya kuwa mwiba kwao katika kudai mabadiliko ya mikataba ya madini isiyo na faida kwa Taifa.Mchakato wote  ulimnufaisha kwa zaidi ya Tshs Bilioni 1. Baada ya hongo, ghafla alikuwa mkimya kwenye Bunge na katika Kamati ya Rais JK chini ya Jaji mstaafu Mark Bomani,  hakukomaa kuizungumzia kabisaa "The Boman Report" na hata katika utungaji sheria mpya ya madini-2009 hakua mpingaji kama ilivyotarajiwa, Ukweli huo ambao hajaukanusha mpaka leo,  umethibitishwa na uchunguzi uliofanywa na Adam Hooper kwenye report yake aliyoiwasilisha chuo kikuu cha Carlton mwezi July, 2011 kwa mujibu wa gazeti la Guardian la Uingereza la Sept4, 2011.Je! hii sio kutumia cheo kutishia ili apewe hongo kwa taasisi,makampuni au Serikalini.

2. Mhe. Zitto anatuhumiwa kumiliki Ghorofa kubwa Dodoma ambalo ujenzi wake hauendani na kipato chake halali. Na awali zilipopigwa kelele akamua kusitisha ujenzi. Ghorofa hilo hajalitaja kwenye mali zake lakini ukweli uliopo ni mali yake (Kwa mujibu wa nyaraka za...)na hata mke wake mara kadhaa ameonekana akisimamia kwa kificho finishing ya jengo hilo na wapo mashahidi katika idara zote zinazohusika viwanja na ujenzi wa kuthibitisha umiliki wake.

3.  Mhe.Zitto ametajwa kwenye Jarida la The Africa Confidential liloandika kuhusu ufisadi katika Mifuko ya hifadhi ya jamii tangu awamu ya tatu,  ufisadi ambao ulihusisha vigogo wengi kwa miaka mingi. Mhe. Zitto ni miongoni mwa wanasiasa waliotajwa kwa majina, kwa namna kamati aliyoiongoza kwa miaka minane (8) ilivyofumbia macho madudu katika mifuko ya hifadhi hususani NSSF kinyume na ilivyotarajiwa.

4. Mhe. Zitto kunaushahidi kuwa, kwa miaka yote aligeuza Kamati ya PAC kama duka binafsi kwa kutisha Wakurugenzi Wakuu wa Taasisi za UMMA,  baadhi ya waliokuwa wajumbe wako wanakili kupokea bahasha, ambapo wewe ulichukua kiasi kukubwa zaidi kama Mwenyekiti na kufumbia macho makosa ya wazi na ubadhirifu katika taasisi za umma kama NHC, NSSF, TANAPA,TANESCO TPA nk. mpaka baadae majipu haya yamekuja kutumbuliwa na Serikali ya awamu ya Tano. Waeleze Watanzania Uongozi wa Kamati hiyo uliupataje mara kwa mara, hata baadhi ya Wabunge wa CCM walishangazwa na ngekewa hiyo.

5. Mhe. Zitto Watanzania wanajiuiza majipu aliyoyatumbua Rais Magufuli baada ya kuingia madarakani katika Mashirika ya UMMA, kwanini Kamati yako iliyaacha na kuyafumbia macho kama hukuwa kwenye project ya kutumiwa na mafisadi?

6. Mhe. Zitto, kwanini mwanzo alionekana kuisifia sana Serikali awamu ya tano na hasa Rais Magufuli, na sasa unaipinga vikali? Je tuamini haya ni matokeo ya kukosa Uenyekiti wa PAC na badae kupoteza matumaini ya kuwa, ungeteuliwa  Uwaziri wa nishati na Madini bila kujali Chama chako kama ilivyokuwa kwa Prof. Kitila Mkumbo na Anna Mgwila? Kumbuka wapinzani wenzako walivotoka nje bungeni kupinga matokeo ya Zanzibar yeye alibaki kama mkakati wa kuishawishi CCM na Mwenyekiti wake wamuamini na upewe tena Uenyekiti wa PAC anawajua aliopanga nao huo mkakati. Baada ya hayo yote kugonga mwamba amegeuka Mbogo na nakuanza kuitafutia madoa kwa nguvu zote halali na haramu Serikali ya awamu ya tano.

7.  Mhe. Zitto, ulikaliliwa kupitia press conference akisema  na kuponda sana Muungano wa UKAWA na kusisitiza UKAWA ni "UKAWA ni Wasaka tonge"  pia siku za badae kupitia press, uliwahi kusisitiza (ushahidi upo) "Kama mtu anataka siasa za ulaghai basi aende UKAWA" akawa anaisifu Serikali ya awamu ya tano na baadae kwa kulinda maslahi yake kisiasa,  aligeuka nakuanza kuiponda Serikali ya awamu ya tano kuwa ni ya Kidikteta na inaminya demokrasia. Je! unatuambia nini Watanzania kuhusu siasa za ulaghai na usakatonge za kutumia cheo na elimu kupindisha mambo ili kulinda maslahi binafsi na si ya UMMA?

9. Mhe. Zitto, Alipofukuzwa Chadema alidai kaonewa kwa kifitna kuwa alitaka kumpindua Mhe. Mbowe katika kiti chake, na akawatuhumu CHADEMA kwa ubadhirifu mkubwa wa fedha na uongozi wa Kidikteta. Je ilikuwa kweli? na kama sio kweli kwanini alisema uongo? Je Watanzania tuendelee kukuamini kwa lipi? 

10. Mhe. Zitto, Ulipotoka CHADEMA, Mhe. T Lissu alisema yale waliyokutuhumu nayo pamoja na kupewa gari mbili na Mhe. Mkono, hukukanusha bali ulielekeza tuhuma kwa  Mhe.Mbowe kama ulivyokaliliwa hapo chini, ukimjibu Mhe.Lissu Je! kwa siasa za aina hii zisizo na chembe ya uzalendo, Watanzania tuendelee kukuamini kwa yapi ya ukweli na yapi ya uongo tusiyaamini?

*Mhe.  ZITTO KABWE* Ulisema haya ukimjibu Lissu ulipofukuzwa Chadema...

"Lissu anasema nimepewa magari 2 na Mzee Mkono. Anasema kaambiwa na Mkono. Naamini Mkono alimwambia pia mwaka 2005 alimpa Freeman Aikaeli Mbowe tshs 40m ili Mbowe asifanye kampeni Musoma vijijini. Nadhani alimwambia pia mwaka 2008 (baada ya orodha ya mafisadi kutangazwa 2007) Mkono alimpa Freeman tshs 20m za uchaguzi wa Tarime na Freeman akasema kwenye chama ametoa mkopo na akalipwa. Nadhani alimwambia pia kuwa Mwaka 2010 Mkono alimpa Mbowe tshs 200m za kampeni ya Slaa. Pia hakusahau kumwambia kuwa Rostam Aziz alimpa Mbowe tshs 100m za kampeni. Lissu anajua kuwa gazeti la Tanzania Daima limeanzishwa na fedha za chama kutoka Conservative party?

Nimefanya internship yangu kwa Mkono and Company Advocates kuhusu masuala ya mikataba. Mzee Mkono ni Mzee wangu na alisaini petition ya kumtoa Waziri Mkuu Pinda.

Lissu awaambie waliyemtuma wamwambie ukweli wote. Lissu ajue yeye ni kifaranga tu, Mimi namtaka mama wa kifaranga ajitokeze. Aeleze aliingia deal gani na Sumaye mwaka 2005 kufuatia deni lake NSSF. Aweke wazi mkataba kati yake na NHC kuhusu nyumba ya Umma ilipo Club Bilicanas.

They must know I am not a push over. Chacha died, I won't.

Mtu ambaye hawezi kuheshimu mke wake aliyemzalia watoto hawezi kunyooshea mtu kidole kuhusu maadili."

Mwisho wa kuku nukuu.


11. Mhe. Zitto, Je! Huoni kwamba usahaulifu wetu Watanzania, kutokusoma kwa udadisi pamoja na kutofatilia sana historia ya matukio ndio mtaji wa Wanasiasa maslahi na walaghai wanaohatarisha amani, umoja na mshikamano na maendeleo ya Taifa letu ?

12. Mhe. Zitto, Je Nini maoni yako kwa Siasa hizi  za kijasiliamali, kinafiki, chuki, fitna, uzandiki na uongo zenye ujamaa wa kibepari usio na chembe ya uzalendo kwa matendo katika maslahi na ustawi wa Taifa letu Tanzania? Je! tuendelee na siasa hizi ili tuangamie kama nchi nyingi tajiri kwa rasilimali za Kiafrika zinavyoangamizwa na Viongozi wake wenye tamaa za madaraka, mali na sifa?

13. Mhe. Zitto,  ni kwanini Mhe. Jussa aliwahi kukutuhumu na kukujibu akamaanisha wewe una ndimi mbili, Ukiwa kiongozi tunae kuamini ukweli wa kauli hiyo ni upi?

14. Mhe. Zitto, Je unaweza ukawaweka wazi watanzania Ukiwa mzalendo na mjamaa, muumini wa Azimio la Arusha na Tabora, mbali na pesa yako binafsi, ulipata wapi Milioni zaidi ya miasaba (700) za Kitanzania kuanzisha Chama ACT, na za Kampeni Uchaguzi Mkuu 2015. Ukisimamisha wagombea Ubunge na Udiwani katika majimbo 219 ukivizidi vyama kongwe vyote vya upinzani sambamba na ukwasi wa mali,hisa, na uwekezaji ulionao ndani na nje ya nchi wenye thamani ya Mabilioni kinyume na kipato chako halali,  mbali na mali ulizo orodhesha katika Tume ya Utumishi wa Umma?

15. Mhe. Zitto scandal ya Escrow na IPTL aliwahi kuchapisha kitabu/ kijarida na baadae hukukisambaza vikateketezwa. Alituhumiwa kupokea hongo kutoka kwa Sing Seth ya zaidi Tshs 50 Milioni na alikwepa kujibu tuhuma hizo.Watanzania wanakiu ya kujua ukweli juu ya tuhuma hizo?

MWISHO.

Mhe. Zitto ajue sina ugomvi wala maslahi binafsi na wewe, Kama watanzania wengine, sitilii shaka elimu yako ila natilia shaka aina ya Siasa yako, na uhalali wako wa kutuhumu wengine. Watanzania tuko tayari kukuamini endapo, utatuthibitishia tuhuma hizo za mda mrefu, sio za kweli kwa ushahidi usioacha shaka yoyote ili tuamini kuwa hautumii Elimu na cheo chako kisiasa kujinufaisha na sio kwa faida ya Taifa letu. Nipo tayari kwa lolote, hata ikibidi kwenda mahakamani.

Asanteni kwa kunisikiliza, list nitaendelea.

Na: 

Patrobas Katambi
Mwanasheria.
Mwana-CCM.
M/Kiti Mstaafu BAVICHA Taifa.
June 3, 2018.
Dar es Salaam.

MANENO YA MWISHO YA MAPACHA WALIOUNGANA KABLA HAWAJAKATA ROHO





“DAKTARI tunakufa” yalikuwa ni maneno pekee yaliyotolewa ndani ya dakika 15 na Consolata Mwakikuti baada ya kushuhudia pacha mwenzake Maria Mwakikuti akitangulia kukata roho katika tukio la kusikitisha lililotokea mjini Iringa juzi.

Pacha hao walioungana ambao habari zao zilikuwa gumzo katika vyombo mbalimbali vya habari toka udogo wao hadi sasa, walifariki majira ya saa 2.30 na saa 3.00 usiku wa Jumamosi wakiwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Iringa waliokokuwa wakiendelea na matibabu.

Akizungumza na wanahabari jana mganga mfawidhi wa hospitali hiyo, Dk Museleta Nyakirito alisema pacha hao walikuwa na tatizo kwenye njia ya hewa hatua iliyosababisha wafikwe na mauti.

Dk Nyakirito alisema Maria alikuwa wa kwanza kufa na wakati akikata roho, pacha mwenzake Consolata alitoa maneno hayo (Daktari tunakufa) kwa uchungu na baadaye akaa kimya na ndani ya Dakika 10 na 15 baada ya mwenzake kufa naye akafa.

“Juhudi za kunusuru maisha ya pacha hao zilikuwa zikiendelea katika hospitali hii tangu walipofikishwa hapa Mei 17, mwaka huu wakitokea hospitali ya Taifa ya Muhimbili walikokuwa wakipata matibabu,” alisema.

Alisema Januari, mwaka huu mapacha hao walilazwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Iringa wakisumbuliwa na magonjwa ya akina mama (hakuyataja) na ndipo walipopewa rufaa ya kwenda Muhimbili  walikokuwa wakitibiwa kwa zaidi ya miezi miwili kabla ya kurejea Iringa.

Alisema walirudishwa Iringa na kufikishwa katika hospitali hiyo majira ya saa 1.30 usiku wakiwa wamesindikizwa na daktari mmoja, muuguzi mmoja, mtaalamu wa wagonjwa mahututi (ICU) pamoja na teknishani wa mambo ya gesi (Oksijeni).

“Kwa taratibu zetu, baada ya kufariki walipelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti ambako miili yao imehifadhiwa hadi sasa wakati taratibu zingine za wanafamilia zikiendelea,” alisema.

Taratibu za mazishi
Akizungumza na wanahabari baadae Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Iringa ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesela alisema mazishi yanatarajiwa kufanyika Jumanne au Jumatano katika makaburi ya Kanisa Katoliki, katika kijiji cha Tosamaganga nje kidogo ya manispaa ya Iringa.

“Tunamsubiri Sista Mkuu wa Maria Consolata , Sista Jane ambaye yupo safarini akitokea Dar es Salaam kuja Iringa na atakapofika le oleo tutapanga taratibu za mwisho za mazishi yao” alisema.

Kasesela alisema kabla ya mazishi yao, mapacha hao wataagwa katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Ruaha (Rucu) walikokuwa wakisoma shahada ya ualimu.

Aliomba kama kuna ndugu wa mapacha hao popote pale nchini wajitokeze kushiriki mazishi hayo ili kuwapa faraja katika safari yao ya mwisho.

“Hatuna taarifa za ndugu wowote toka tumewafahamu mapacha hao, tunachojua wamekuwa wakilelewa kanisa Katoliki kwa msaada wa wadau mbalimbali kwa maisha yao yote,” alisema.

Wakati huo huo, Kasesela amemshukuru Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Pombe Magufuli kwa rambirambi yake ya Sh Milioni 5 aliyotoa kuomboleza kifo cha mapacha hao.

Nao wanafunzi wa chuo cha RUCu waliokuwa wakisoma na pacha hao wamesema wameupokea msiba huo kwa masikitiko makubwa.

“Baada ya kupokea taarifa hizi, chuo kilikuwa kama kimemwagiwa maji. Hakuna aliyeamini taarifa hizo japokuwa ukweli ndio huo. Mungu azilaze roho zao peponi,” alisema mmoja wao aliyejitambulisha kwa jina la Rose.

Maria na Consolata walizaliwa wilayani Makete mkoani Njombe mwaka 1996.

Walisoma shule ya Msingi Ikonda Makete na kuhitimu na kufaulu mtihani wa darasa la saba mwaka 2010, kisha wakajiunga na shule ya Maria Consolata iliyopo Kilolo mkoani Iringa ambapo walihitimu kidato cha nne mwaka 2014.

Baada ya hapo walijiunga na shule ya Sekondari ya Udzungwa wilani Kilolo walipohitimu kidato cha sita mapema mwaka 2017 na wote kufaulu kwa kupata daraja la pili na hatimaye Septemba 2017 wakajiunga na Chuo Kikuu cha Katoliki cha Ruaha (Rucu) walipokuwa wakisomea fani ya ualimu mpaka mauti inawafika.

Sunday, June 3, 2018

RAIS MAGUFULI KUZINDUA PROGRAMU YA KUENDELEZA SEKTA YA KILIMO AWAMU YA PILI (ASDP II)

Waziri wa Kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba (Katikati) akisisitiza jambo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uzinduzi wa programu ya kuendeleza sekta ya kilimo (ASDP II) katika jengo la Mikutano la kimataifa la Mwalimu Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es salaam, jana 1 June 2018. Wengine ni Katibu Mkuu wizara ya kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe na Naibu Katibu Mkuu wizara ya kilimo Dkt. Thomas kashililah. Picha zote Na Mathias Canal-WK
Wawakilishi wa vyombo mbalimbali vya habari wakifatilia mkutano wa Waziri wa Kilimo Mhe Dkt. Charles Tizeba katika jengo la Mikutano la kimataifa la Mwalimu Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es salaam, Jana 1 June 2018.
Katibu Mkuu wizara ya kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe (Kulia),  Mratibu wa ASDP II Mhandisi Januari Kayumbe (katikati) na Kaimu Mkurugenzi wa zana za kilimo Mhandisi Joseph Lubilo wakifatilia mkutano wa waziri wa kilimo na waandishi wa habari. Jana 1 June 2018.
Waziri wa Kilimo Mhe Dkt. Charles Tizeba akimsikiliza kwa makini Katibu Mkuu wa wizara ya kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe wakati wa maandalizi ya uzinduzi wa programu ya kuendeleza sekta ya kilimo ASDP II katika jengo la Mikutano la kimataifa la Mwalimu Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es salaam, Jana 1 June 2018.

Na Mathias Canal-WK, Dar es salaam

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. John Pombe Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika hafla ya uzinduzi wa programu ya kuendeleza sekta ya kilimo awamu ya pili (ASDP II) tarehe 4 June 2018.

Katika dhifa hiyo inayotarajiwa kuanzia Saa 2.00 asubuhi katika jengo la Mikutano la kimataifa la Mwalimu Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es salaam, Rais Magufuli ataambatana na wageni wengine wa kitaifa na kimataifa akiwemo makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa, Mkuu wa Mkoa wa Dara es salaam Mhe Paul Makonda, Mawaziri wa sekta za kilimo pamoja na wadau wote wa sekta ya hiyo.

Taarifa ya uzinduzi wa Programu hiyo ya kuendeleza sekta ya kilimo nchini imetolewa jana 1 June 2018 na waziri wa kilimo Mhe Dkt. Charles Tizeba wakati akizungumza na waandishi wa habari katika jengo la Mikutano la kimataifa la Mwalimu Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es salaam.

Dkt Tizeba alisema, Wizara za kisekta zikijumuisha Wizara ya Kilimo, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa-TAMISEMI, Wizara ya Viwanda Biashara na Uwekezaji, Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi na Wizara ya Maji na Umwagiliaji  ndizo zenye jukumu la kuhakikisha ASDP II inakuwa na mafanikio makubwa nchini na kuwa mkombozi wa wananchi katika kilimo.

Alisema kuwa ASDP II itatekelezwa katika mikoa na wilaya zote kwa kuzingatia mazao ya kipaumbele kufuatana na ikolojia ya kilimo ya kanda kwa miaka kumi (10) kwa vipindi viwili vya miaka mitano mitano ambapo kipindi cha kwanza kitaanza 2018/19 hadi 2023/24.

Katika hatua nyingine Dkt Tizeba ametaja lengo la Programu hiyo kuwa ni kuleta mageuzi katika sekta ya kilimo ili kuongeza uzalishaji na tija  katika kilimo, mifugo na uvuvi; kuongeza pato la wakulima, wafugaji na wavuvi; kuongeza pato la Taifa na kuwa na uhakika wa usalama wa chakula na lishe.

Aidha, Programu hii itatekeleza sera mbalimbali kama vile Sera ya Kilimo ya Taifa, Sera ya Mifugo ya Taifa, Sera ya Uvuvi, Sera ya Masoko ya Mazao ya Kilimo, Sera ya Umwagiliaji ya Taifa, Sera ya Usalama wa Chakula na Lishe, Sera ya Ugatuaji Madaraka, Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sera ya Mashirikiano kati ya Sekta za Umma na Sekta Binafsi.

Katika hatua nyingine Mhe Dkt Tizeba ameuarifu umma wa watanzania kuwa endapo mpango huo utatekelezwa kama ilivyopangwa hadi kufikia mwaka 2022 Tanzania itakuwa katika uchumi wa kati.

Katika utekelezaji wa ASDP II washiriki ni wadau wa sekta ya Kilimo, Mifugo, Uvuvi, Ushirika, Wizara, Taasisi za Serikali na zisizo za Serikali, Washirika wa Maendeleo, Sekta Binafsi na wananchi wote.

 MWISHO.

Saturday, June 2, 2018

NAIBU WAZIRI JULIANA SHONZA MGENI RASMI TAMASHA LA TAGOANE ARUSHA









Na Mwandishi wetu, Arusha

Mtandao wa Wasanii wa Injili na Maadili ya Utaifa Tanzania (Tagoane) umeandaa tamasha kubwa la ‘Tanzania Mama Niwathamani’ linaloitwa Tamani Festival "Asante Mama" lenye lengo la kumshukuru Mungu kwa ajili ya Mwanamke(Mama), kuonyesha thamani ya mama (Mwanamke) na kurejesha shukrani kwa mama kutokana na umuhimu wake kwenye jamii.

Akizungumza na waandishi wa habari, Rais wa Tagoane Dkt. Godwin Maimu alisema tamasha hilo litakalofanyika June 29-Julai mosi jijini Arusha litawashirikisha watu wengi wakiwamo wanamuziki wa Injili.

Alisema lengo hasa ni kurejesha shukrani kwa ‘mama’ Asante Mama ambapo pamoja na mambo mengine, watu watachangia damu salama kwa ajili ya kuokoa uhai wa mama na mtoto wakati wa kujifungua.

Dkt. Maimu alisema sio hivyo tu, tamasha hilo litatoa fursa kwa wanawake kupima afya bure yakiwemo magonjwa mbalimbali kama saratani, figo,shinikizo la damu na mengine yasiyo ya kuambukiza.Hivyo watakuwepo madaktari wabobezi kwa ajili ya kuangalia afya za mama zetu, ni sisi tunaopaswa kuangalia uhai wao na sio mwingine,” alisema.

“Ni tamasha kubwa la siku tatu, japo kutakuwa na uimbaji na mambo mbalimbali tutakuwa na Maonyesho ya kazi za ubunifu na ujasiriamali za kina mama kwa kuinua uchumi wao, mafunzo mbalimbali ya ujasiria mbali, maombezi na fursa za kunyanyuka kiuchumi.

Alitaja mengine yatakayofanyika kwenye tamasha hilo ni onyesha upendo la uzalendo kwa mama kutoa zawadi maalumu kwa mama (Asante Mama)ikiambatana na ziara maalumu ya kutembelea hifadhi za Taifa Manyara na Tarangire ikiwa ni kuenzi utalii wa ndani kwa vitendo aliongeza Dkt.Godwin Maimu Rais wa Tagoane.

Friday, June 1, 2018

WANAKIJIJI 772 WA KIJIJI CHA MLANDA WAPATA HATI MILIKI ZA KIMILA 1,777

 Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Robert Masunya na naibu mkurugenzi wa Mradi wa Urasimishaji Ardhi (LTA) unaofanywa chini ya mpango wa Feed The Future kwa ufadhili wa Shirika la Misaada la Marekani (USAID) Malaki Msigwa wakimkabidhi hati ya kimila mmoja ya wananchi wa kijiji cha Mlanda ambaye ni mlemavu 


 Naibu mkurugenzi wa Mradi wa Urasimishaji Ardhi (LTA) unaofanywa chini ya mpango wa Feed The Future kwa ufadhili wa Shirika la Misaada la Marekani (USAID) Malaki Msigwa akitoa neo kwa wananchi wa kijiji cha Mlanda wakati wa kutoa hati za kimila 
 Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Robert Masunya na naibu mkurugenzi wa Mradi wa Urasimishaji Ardhi (LTA) unaofanywa chini ya mpango wa Feed The Future kwa ufadhili wa Shirika la Misaada la Marekani (USAID) Malaki Msigwa wakimkabidhi hati ya kimila mmoja ya wananchi wa kijiji cha Mlanda ambaye alikuwa anawakilisha kundi la wazee
Baadhi ya wananchi waliojitokeza kushirikia zoezi la utoaji wa hati miliki za kimila zilizotolewa na Mradi wa Urasimishaji Ardhi (LTA) unaofanywa chini ya mpango wa Feed The Future kwa ufadhili wa Shirika la Misaada la Marekani (USAID)

Picha ya pamoja baina ya viongozi wa Mradi wa Urasimishaji Ardhi (LTA) unaofanywa chini ya mpango wa Feed The Future kwa ufadhili wa Shirika la Misaada la Marekani (USAID),viongozi wa halmashauri ya wilaya ya Iringa pamoja na baadhi ya wananchi walikuwa tayari wamepokea hati za kimila


NA FREDY MGUNDA.IRINGA.


JUMLA ya wanakijiji 772 kati ya 1890 wa kijiji cha Mlanda kata ya Magulilwa wilaya ya Iringa mkoani Iringa wamepimiwa maeneo na mashamba yao na kukukabidhiwa hati miliki za kimila zinazotolewa kupitia Mradi wa Urasimishaji Ardhi (LTA) unaofanywa chini ya mpango wa Feed The Future kwa ufadhili wa Shirika la Misaada la Marekani (USAID).


Hati hizo zilikabidhiwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Robert Masunya wakati wa sherehe fupi za kuwakabidhi hati hizo zilizofanyika kijijini hapo na kuhudhuriwa na umati mkubwa wa wananchi na wageni mbalimbali walikuwepo katika tukio hilo.

Akizungumza na wanakijiji hao baada ya kukabidhi hati hizo Masunya alisema kuwa hati hizo zitawasaidia kutenga maeneo kwa ajili ya matumizi mbalimbali kwa kuzingatia uwezo wa ardhi kuhimili idadi hiyo na kasi ya ongezeko la watu na mifugo kwa miaka mingi ijayo.

Masunya aliongezea kuwa,hatua hiyo itasaidia kupunguza migogoro ya ardhi kwa kuimarisha usalama wa miliki za ardhi na kuongeza thamani ambayo itawawezesha hata kukopesheka katika taasisi za kifedha zikiwemo benki.

“Usajili wa ardhi ni muhimu kwasababu unaongeza ulinzi wa umiliki wa ardhi, unawezesha uwekezaji, unaongeza thamani ya ardhi na unapunguza migogoro ya ardhi,” alisema Masunya

Masunya aliupongeza mpango huo akisema utasaidia kupunguza eneo kubwa la ardhi ya Halmashauri ya Wilaya ya Iringa ambayo haijapimwa.

Aidha Masunya aliwaomba Feed The Future wautanue mradi huo angalau ufike umalize kupima vijiji vyote vya Halmashauri ya Wilaya ya Iringa  huku akivikumbusha vijiji vyote vya wilaya hiyo kuendelea kutoa ushirikiano kwenye miradi ambayo inasaidia kukuza maendeleo ya nchi. 

“Tunataka katika kipindi ambacho Mradi wa Urasimishaji Ardhi (LTA) unaofanywa chini ya mpango wa Feed The Future kwa ufadhili wa Shirika la Misaada la Marekani (USAID) tuhakikishe tunapima ardhi na mipango ya matumizi bora na ipimwe ili kila mwenye kipande chake cha ardhi awe na hati yake,” alisema Masunya.

Alisema kwa kupitia sera hiyo, kutakuwa na usimamizi zaidi wa ulinzi wa ardhi ya watu masikini ili kupunguza uporaji wa rasilimali hiyo unaofanywa na matajiri.

“Marekebisho ya sera hiyo ya ardhi yatawezesha pia kufanyika kwa mrekebisho ya sheria mbalimbali za ardhi ili ziendane na sera na mazingira ya sasa,” alisema Masunya.


Masunya aliwataka wanakijiji wa kijiji hicho ambao hawajapimiwa maeneo yao kwa sababu mbalimbali ikiwemo ubishi na migogoro ya kifamilia kutumia vizuri muda ambao bado mradi huo upo katika wilaya hiyo na kuhakikisha nao wananufaika na zoezi hilo.

Wanakijiji ambao hawajapimiwa maeneo yao wanaweza kuendeleoa kuzalisha migogoro ambayo haina tija kwa maendeleo yao na kusababisha waendelee kuwa masikini kwa kuwa hawatakuwa na dhamana ya kwenda kukopa.

Awali naibu mkurugenzi wa Mradi wa LTA, Malaki Msigwa alisema kuwa kijiji cha Mlanda kinajumla ya wananchi 1890 na walio nufaika na Mradi wa Urasimishaji Ardhi (LTA) unaofanywa chini ya mpango wa Feed The Future kwa ufadhili wa Shirika la Misaada la Marekani (USAID) ni wananchi 772 na kufanikiwa kutoa jumla ya hati miliki za kimila 1777 ambapo wanaume walikuwa 409 na wanawake 363. 

Msigwa aliwapongeza wataalamu wa mradi huo kwa kuhakikisha wanawasaidia wananchi wa kijiji cha Mlanda kupima maeneo yao na kupata hati miliki za kimila ambazo zitakuwa msaada mkubwa kwenye maendeleo ya kiuchumi.

“Baadhi ya miradi imeibuliwa wakati wa upimaji wa ardhi hivyo ni fursa sasa kwa wananchi wenyewe kuitumia vizuri ardhi waliyopimiwa na kupewa hati miliki za kimila na kwa kuwa asilimia fulani kijiji hiki kimepimwa hivyo wanaweza kuwa kijiji cha mfano kwa kuwapa maendeleo hata wawekezaji wazuri kwa faida yao” alisema Msigwa

Msigwa alisema kati ya vijiji hivyo 41 vitakavyotayarishiwa mipango ya matumizi bora ya ardhi na kila mwenye ardhi kupimiwa na kupewa hati miliki za kimila, vijiji 36 vipo wilayani Iringa na vitano vipo wilayani Mbeya.

“Baada ya kukamilisha zoezi la upimaji mashamba na urasimishaji wa kijiji chote cha Mlanda, hivi sasa mradi unaendelea na upimaji mashamba katika vijiji vya mradi ambavyo vipo wilayani Iringa” alisema Msigwa

Naye diwani wa kata ya Magulilwa Jane Mhangala aliupongeza Mradi wa Urasimishaji Ardhi (LTA) unaofanywa chini ya mpango wa Feed The Future kwa ufadhili wa Shirika la Misaada la Marekani (USAID) kwa kuzingatia jinsia wakati walipokuwa wanaendesha zoezi la upimaji ardhi katika kijiji hicho.

“Hongera sana LTA kwa kuwapa elimu wanawake na wanaume na kuhakikisha kuwa wanapa haki zao sawa bila kuwa na mgogoro wowote tofauti na ilivyokuwa hapo awali,maana miaka ya nyuma mwanamke alikuwa anabaguliwa kwenye kila kitu wala alikuwa haruhusiwi hata kumili ardhi” alisema Mhangala

Mhangala aliongeza kwa kusema kuwa wanakijiji wa kijiji cha Mlanda baada ya kupata elimu ya kumiliki ardhi kumepunguza sana migogoro ambayo ilikuwa inaleta chuki kwenye familia.

“Kwa sasa ardhi ya kijiji hiki imepanda dhamani kwa kiasi kikubwa na tayari ishapimwa na mmepata hati miliki za kimila ambazo zitawasaidia katika maendeleo yenu ya kiuchumi” alisema Mhangala

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More