Thursday, October 5, 2023

DED MAKUFWE AWANOA WASIMAMIZI WA MIRADI YA ELIMU NA AFYA MAKETE.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Makete,  Ndg. William Makufwe (kushoto) akizungumza na Wasimamizi wa miradi ya Elimu na Afya, katika ukumbi wa Mikutano Bomani...akiwa pamoja Mganga mkuu wa Halmashauri Dkt. Ligobert Kalisa.

Na Fredy Mgunda, Makete.


MKURUGENZI mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Makete,William Makufwe, amewataka watumishi kuanzia ngazi ya kijiji hadi makao mkuu ya Halmashauri, ambao wanasimamia miradi kuhakikisha watimiza wajibu wao ili iweze kukamiliaka kwa wakati.

Makufwe amesema hayo wakati akizungumza na watendaji wa kata, vijiji, wakuu wa shule , waganga wafawidhi pamoja na wakuu wa idara na vitengo katika ukumbi wa mikutano Bomani,lazima viongozi washirikiane katika kukamilisha miradi ambayo imeletwa katika maeneo yao.

“hakikisheni mnashirikiana katika kukamilisha miradi sio kuachiana, kila mmoja ashiriki kikamilifu, hasa watendaji wa kata mnatakiwa kushirikiana moja moja katika kila mradi ambao unatekelezwa katika kata au kijiji husika, ili miradi ikamilike kwa wakati”

Amewataka watendaji kata pamaoja na wahusika wengine, kutoingiza maslahi binafsi katika utafutaji wa mafundi ambao watakuwa wakitekeleza ujenzi wa miradi ya serikali ili waweze kusimamiwa vizuri.

“hakikisheni mhandisi wa wilaya anashirikishwa katika utafutaji wa mafundi ambao wataenda kutekeleza miradi hiyo ya serikali ili kuwe na ufanisi katika ujenzi” alisema Makufwe

Sambamba na hayo DED Makufwe amewataka wasimamizi wa miradi, kufanya manunuzi kwa wakati kwasabu serikali imetoa pesa za kutosha, hivyo kila mtu awajibike kwa nafasi yake ili miradi iweze kukamilika kwa wakati,

 Makufwe amewata wasimamizi hao wa miradi kutunza vifaa vyote ambavyo vimenunuliwa kwaajili ya ujenzi.

Hata hivyo, amewasisitiza watumishi hao kuhakikisha wanafuata utaratibu katika ufanyaji wa manunuzi ili kutoingia katika matatizo na serikali, ikiwa ni pamoja na kufanya manunuzi kwa idhini ya wahusika hususani kitengo cha manunuzi.

“hakikisheni mnashindanisha bei za bidhaa ambazo mnataka kuzinunua ili mpate bei ambazo zinaeleweka, sio kwasababu una mahusiano na mdau fulani basi unampa tenda”.

Kwa upande mwingine, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha nyingi katika kuendeleza miradi ambayo inawagusa wananchi moja kwa moja kama vile , Elimu na Afya ili kuhakikisha watanzania wanapata huduma stahiki na bora.

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More