Wednesday, November 30, 2016

MD KAYOMBO AFANIKISHA MRADI SHULE YA MATOSA

 Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo

Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo amepongezwa na walimu pamoja na wanafunzi wa shule ya sekondari Matosa iliyopo Kata ya Goba , Manispaa ya Ubungo kwa kufanikisha kwa kiasi kikubwa utekelezaji wa mradi wa SEDP II.

Mradi huo unaohusisha ujenzi wa vyumba viwili vya darasa, nyumba za walimu, kisima cha maji, tanki la kuhifadhia maji pamoja na vyoo upo katika hatua nzuri ya kukamailika kutokana na juhudi pamoja na utendaji kazi uliotukuka wa Mkurugenzi Kayombo akishirikiana na watumishi wa Manispaa hiyo.

Akizungumza na mtandao wetu mwalimu Mkuu wa shule hiyo alisema amefurahishwa na juhudi zinazofanywa na Mkurugenzi wa Manispaa hiyo za kuleta maendeleo kwa wananchi na kwenda sambamba na kauli mbiu ya Rais John Pombe Magufuli ya Hapa Kazi Tu.

"Napenda kutoa shukrani Kwa Serikali kwa kuuleta mradi wa SEDP II katika shule yetu, pia napenda kutoa shukrani za dhati kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg. John Lipesi Kayombo kwa juhudi zake anazozifanya mpaka mradi umefika hatua hii, kwa kweli ametusaidia sana, mungu ambariki", alisema Mwalimu mkuu.

Wakati huo huo wanafunzi wanaosoma katika shule hiyo wamempongeza Mkurugenzi Kayombo kwa kazi nzuri aliyofanya mpaka kuweza kufanikisha kupatikana kwa maji pamoja na madarasa, vyoo, tanki la maji na nyumba za walimu.

ESRF YAFANIKISHA MKUTANO WA 5 WA MWAKA, WAJADILI UCHUMI

Imeleezwa kuwa ili kumwezesha kila mwananchi wa Tanzania kupata maendeleo na kuondokana na janga la umaskini, Serikali haina budi kutunga sera ambazo zitamgusa kila mwananchi na kuwa na faida jambo ambalo litawasadia kukuza uchumi wao binafasi na taifa kwa ujumla.

Hayo yamesemwa katika mkutano wa tano wa mwaka wa kujadili sera za jamii na mahusiano yake kwenye mabadiliko ya kiuchumi nchini Tanzania na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Philemon Luhanjo katika mkutano wa siku moja wa kujadili sera za kijamii zinavyoweza kusaidia kubadilisha uchumi wa Tanzania, mkutano ambao uliandaliwa na ESRF.

Luhanjo alisema ni vyema Serikali inapokuwa inatunga sera ihakikishe zinakuwa na faida kwa wananchi ili ziweze kuwasaidia kupata maendeleo na kuboresha maisha yao na hata wakati nchi ikielekea katika uchumi wa kati kila mwananchi ahusike na mabadiliko hayo.

"Sera zipo nyingi, zipo za maendeleo ya jumla, elimu, afya, kilimo, viwanda na kila kitu, sisi tunajaribu kuangalia tunapotengeneza sera mbalimbali tuhakikishe kwamba sera hizo zitamnufaisha binadamu, kwamba chochote unachofanya kiwe nikwa faida ya mwanadamu, mipango na malengo yote yawe yanamlenga binadamu kuondoa matatizo yake,

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dr. Ashatu Kijaji akihutubia katika mkutano wa tano wa mwaka wa ESRF wa kujadili sera za jamii na mahusiano yake kwenye mabadiliko ya kiuchumi nchini Tanzania ulioandaliwa na Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF) jijini Dar es Salaam.(Picha na Said Khalfan wa KVS Blog)

"Serikali inapofanya mipango inatakiwa kupanga mipango ambayo inajaribu kujibu kero za mwananchi, kama ni elimu, kama ni afyaa au kama ni kilimo cha kisasa, tunapotengeneza sera tuwe tunauwianisha, hizo sera zikitekelezeka na mteja wa bidhaa awe ameandaliwa ili mkulima asiwe amepoteza nguvu bure," alisema Luhanjo na kuongeza.

"Tunazungumzia nchi ya viwanda, viwanda gani? na nchi yetu niya kilimo kwahiyo tunatarajia viwanda vingi vitakuwa ni vya kilimo, kwahiyo tunataraji mkulima mdogo aimalishwe ili aweze kuzalisha mazao yanayokwenda kiwandani ni lazima sera ziwe na uwiano mzuri."

Nae Naibu Waziri wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji alisema Serikali inafahamu kuwa nchi haiwezi kupiga hatua bila kuhusisha mwananchi mmoja mmoja na inachofanya kwa sasa na kuwashawishi watu wenye viwanda kutumia malighafi ambazo zinazalishwa nchini ili wakulima nchini wafaidike na uwepo wa viwanda nchini.

"Tunaamini hatuwezi kuwa na uchumi unaokua kama hali ya kijamii ya wananchi haikui na hata Rais Magufuli alikuwa akisema tangu akiwa katika kampeni kwamba Tanzania ya Magufuli niya viwanda, na viwanda hivi ni kwa ajili ya watu wetu,

Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini wa ESRF, Philemon Luhanjo, akizungumza katika mkutano wa tano wa mwaka wa kujadili sera za jamii na mahusiano yake kwenye mabadiliko ya kiuchumi nchini Tanzania ulioandaliwa na ESRF.

"Kwenye mpango wetu wa miaka mitano tumesisitiza maendeleo ya viwanda lakini vinavyotumia malighafi zinazozalishwa hapa nchini katika kilimo chetu, kwahiyo hatuwezi kuwa na viwanda kama kilimo hakijaendelea, hatuwezi kuwa maendelo ya kijamii kama kilimo chetu hakijaendelea, kilimo ndiyo uti wa mgongo wa taifa letu, kwahiyo tumejadili hilo ili kuona wananchi wetu wananufaika vipi," alisema Kijaji. Kwa upande wa Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF, Dk. Tausi Kida alizungumza kuhusu mkutano huo ambao umedhaminiwa na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) na kusema,"ESRF kwasasa hivi tupo kwenye mchakato wa kutengeneza Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu ya mwaka 2017, "Katika hiyo ripoti tumeweza kutaharisha ripoti 11 ambazo zitachangia katika utayarishishaji wa hiyo ripoti na dhumuni kubwa ni kuweza kuzijadili hizo ripoti na kupata uelewa mpana ni kwa kiasi gani sera za kijamii zina mchango mkubwa katika kuleta mageuzi ya kiuchumi hapa Tanzania."
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF), Dk. Tausi Kida akitoa maelezo kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi katika mkutano huo.
Mkuu wa Programu, Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa UNDP, Amon Manyama akizungumza katika mkutano wa tano wa mwaka wa kujadili sera za jamii na mahusiano yake kwenye mabadiliko ya kiuchumi nchini Tanzania.
Mtafiti mshiriki mwandamizi wa ESRF, na mashauri wa ufundi wa mradi wa THDR Profesa Marc Wuyts, akiwasilisha mada Situating social policy transformation: A conceptual framework, kwenye mkutano wa tano wa mwaka wa kujadili sera za jamii na mahusiano yake kwenye mabadiliko ya kiuchumi nchini Tanzania.
Mhadhiri wa Masuala ya Afrika na Maendeleo katika Chuo Kikuu cha Edinburgh, Shule ya Sayansi ya Siasa nchini Uingereza Dk.Hazel Gray, akiwasilisha mada yake kuhusu mabadiliko katika sera za kijamii kwenye mkutano wa tano wa mwaka wa ESRF.
Mchokoza mada kutoka taasisi ya Daima na Mtafiti mwandamizi mshiriki ESRF, Profesa Samwel Wangwe, akitoa maelezo yake kuhusu mada iliyowasilishwa mezani kwa wajumbe.
Profesa wa uchumi DoE, Chuo kikuu cha Dar es Salaam Profesa Humphrey Mushi, akiwasilisha mada kuhusu historia ya sera ya jamii katika mkutano huo.
Mgeni rasmi Dk. Kijaji, (wa pili kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF, Dk. Tausi Kida, (wa kwanza kushoto), Bi Anna, na mwenyekiti wa bodi ya udhamini ya ESRF, Bw Philemon Luhanjo, Mkurugenzi wa Kupunguza Umaskini na Kuinua Uchumi kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Anna Mwasha (wa pili kulia) wakipongeza wakati wa mkutano huo.
Wageni waalikwa wakifuatilia mada mbalimbali kwa makini katika mkutano wa tano wa mwaka wa ESRF wa kujadili sera za jamii na mahusiano yake kwenye mabadiliko ya kiuchumi nchini Tanzania
Picha ya pamoja ya washiriki, wakuu ESRF, wakiwa na mgeni wa heshima Dk. Kijaji.

UN NA EU YAWANOA MABALOZI 50 WA MALENGO YA DUNIA IRINGA

UMOJA wa Ulaya (EU) na Umoja wa Mataifa (UN) wameweka nguvu ya pamoja kuendesha kampeni ya uelewa wa malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) nchini Tanzania. Wakiwa Mkoani Iringa wamepata nafasi ya kuzungumza na wanachuo 1,000 kutoka vyuo vikuu vya Iringa na Ruaha kwenye semina iliyoelezea malengo ya dunia ambayo ni sehemu ya ajenda 2030 ya maendeleo endelevu duniani ambapo kati ya hao, vijana 50 wamepata semina ya mwongozo wa kuwa mabalozi wa malengo hayo (Global Goals Champions). Kampeni hiyo imelenga kuwafanya vijana waelewe malengo 17 ya dunia ambayo kwa sasa yana mwaka mmoja tangu yapitishwe na kuwatanabaisha wajibu wao katika kufanikisha utekelezaji wake ndani ya mazingira ya Tanzania. 
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akimkabidhi Ripoti ya Umoja wa Mataifa ya mpango wa misaada ya maendeleo UNDAP II 2016-2021 Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU) Iringa, Dr. Cephas Mgimwa alipomtembelea ofisini kwake mjini Iringa.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akifafanua jambo juu ya ripoti ya Umoja wa Mataifa ya Mpango wa misaada ya Maendeleo 2016-2021 (UNDAP II) kwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU) Iringa, Dr. Cephas Mgimwa alipomtembelea ofisini kwake mjini Iringa
Mwanasheria wa Chuo Kikuu cha Ruaha Iringa, Martin Noel akiwa ameongozana Mtaalam wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa nchini, Hoyce Temu kuelekea kwenye ukumbi wa mikutano chuoni hapo sambamba Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez aliyeambatana na Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akiendesha semina ya malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) kwa vijana 50 kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha ambao watakuwa ni mabalozi wa malengo hayo ya dunia huku lengo la UN ni kuwaelimisha vijana zaidi ya 30,000 ifikapo mwaka ujao kuhusu malengo hayo ya dunia.

Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro akielezea fursa za ufadhili wa masomo nje ya nchi katika tovuti ya Umoja wa Ulaya Tanzania wakati wa semina ya malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) kwa vijana 50 kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha ambao watakuwa ni mabalozi wa malengo hayo ya dunia (Global Goals Champions) huku lengo la UN ni kuwaelimisha vijana zaidi ya 30,000 ifikapo mwaka ujao kuhusu malengo hayo ya dunia iliyofadhiliwa na EU.
Mkufunzi wa Malengo ya Dunia ambaye pia ni Mtaalam wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa nchini, Hoyce Temu akiwapiga msasa vijana 50 kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha ambao watakuwa ni mabalozi wa malengo hayo ya dunia (Global Goals Champions) huku lengo la UN ni kuwaelimisha vijana zaidi ya 30,000 ifikapo mwaka ujao kuhusu malengo hayo ya dunia kwenye semina hiyo iliyofadhiliwa na EU.
Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini ambaye pia ni Afisa Miradi, Anna Muro akiwa amejumuika na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha wakati wa semina ya malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) kwa vijana 50 ambao watakuwa ni mabalozi wa malengo hayo ya dunia (Global Goals Champions) huku lengo la UN ni kuwaelimisha vijana zaidi ya 30,000 ifikapo mwaka ujao kuhusu malengo hayo ya dunia ambapo semina hiyo imefadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU) nchini.
Pichani juu na chini ni vijana 50 kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha walioshiriki semina maalum ya kuwa mabalozi wa malengo ya dunia (Global Goals Champions) iliyoandaliwa na UN na kufadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU) mjini Iringa.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez (kulia) akimkabidhi cheti Rais wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU) Iringa Athman Waziri aliyehitimu kuwa balozi wa Malengo ya Dunia (Global Goals Champion).
Picha juu na chini Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez akiendelea na zoezi la kutunuku vyeti kwa mabalozi wa malengo ya dunia kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha.


Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez katika picha ya pamoja na Mabalozi wa Malengo ya Dunia (Global Goals Champions) baada ya kuhitimisha semina maalum iliyoshirikisha vijana 50 kutoka Chuo Kikuu cha Iringa na Ruaha.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez katika picha ya pamoja na Mwanasheria wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU) Iringa, Martin Noel baada ya kuhitimisha semina ya malengo ya dunia mjini Iringa.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez katika picha ya pamoja na Afisa Habari wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU), Muazarau Matola
Baadhi ya Global Goals Champions katika picha ya kumbukumbu na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez na Mtaalam wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa nchini, Hoyce Temu.
Mkufunzi wa Malengo ya Dunia ambaye pia ni Mtaalam wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa nchini, Hoyce Temu akibadilishana mawazo na wahitimu wa semina malengo ya dunia (Global Goals Champions) mara baada ya kuhitimisha semina hiyo iliyofanyika katika Chuo Kikuu cha Ruaha mjini Iringa ambapo imefadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU).

FAHAMU JINSI FEDHA ZA TETEMEKO LA ARDHI MKOANI KAGERA ZILIVYOTUMIKA


Na Mathias Canal


Ndugu zangu kama ambavyo tunakumbuka Tarehe 10/09/2016 majira ya saa 9 na dakika 27 Alasiri maeneo ya Kanda ya ziwa hasa Mkoani Kagera kulitokea tetemeko la ardhi linalokadiriwa kuwa na ukubwa wa 5.9 katika vipimo vya Richter ambapo Kitovu cha tetemeko hilo ni kwenye makutano ya latitudo 10 06’ na longitudo 31055’ eneo ambalo ni kilomita 20 kaskazini mashariki mwa kijiji cha Nsunga na kilomita 42 kaskazini magharibi mwa mji wa Bukoba na Kitovu hicho kilikuwa kilomita 10 chini ya ardhi kwenye eneo hilo.

Tetemeko hilo la ardhi liliacha familia kadhaa zikiwa na huzuni kubwa kwa kuwapoteza ndugu, jamaa na rafiki zao ambapo idadi ya watu waliofariki walikuwa ni 17 huku watu 560 wakipatiwa matibabu kutokana na majeraha waliyoyapata sambamba na kukutikana kwa uharibifu wa makazi na miundombinu ya umma na watu binafsi.

Kwa Mujibu wa Mtendaji Mkuu, Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST) alieleza sababu za kutokea kwa Tetemeko hilo la ardhi kuwa ilikuwa ni kutokana na kitovu cha tetemeko hilo kuwa kiko chini sana ya ardhi (Km 10) na kwa kutafasiri umbile la mawimbi ya tetemeko hilo yaliyonakiliwa na vituo vya kupimia matetemeko ya ardhi inaonekana kuwa tetemeko hilo limetokana na misuguano ya mapange makubwa ya ardhi iliyopasuliwa na mipasuko ya ardhi mithili ya mipasuko kwenye bonde la ufa. 

Kwa kuwa eneo lililokumbwa na tetemeko la ardhi liko karibu na mkondo wa magharibi wa bonde la ufa la Afrika Mashariki inakisiwa kuwa mtetemo huo ulisababishwa na kuteleza na kusiguana kwa mapande ya miamba juu ya mipasuko ya ardhi ya bonde hilo la ufa.

Katika siku za karibuni kumekuwepo na taarifa mbalimbali katika mitandao ya kijamii ikiwemo facebook, Twitter, Blogs, Instagram na Makundi mbalimbali ya Watsup jambo ambalo lilinilazimu kufunga safari na kuweka kambi ya takribani siku nne Mkoani Kagera ili kubaini ukweli wa namna fedha zilizopatikana na zilivyotumika ikiwa ni pamoja na mahitaji mengine jinsi yalivyopatikana na namna yalivyoelekezwa.

UKWELI WA MAMBO

Kufuatia tathmini zilizofanyika kupitia wataalamu mbalimbali, makadirio ya awali yalibaini kuwa kiasi cha jumla ya shilingi Bilioni 104.9 zinahitajika katika kukabiliana na kurejesha hali katika Mkoa wa Kagera kufuatia maafa hayo. Ambapo gharama hizi zinajumuisha:

a) Ujenzi wa makazi ya muda kwa waathirika wa nyumba zipatazo 16,667 zilizoharibika katika viwango tofauti, ambapo kiasi cha Shilingi Bilioni 41.7 zitahitajika.

b) Kiasi cha shilingi 1.92 kwa ajili ya kodi ya miezi sita kwa wapangaji waliokuwa wakiishi kwenye nyumba zilizoharibiwa.

c) Ukarabati wa shule za msingi 163 kwa gharama ya shilingi Bilioni 12.7, sekondari 57 kwa gharama ya shilingi Bilioni 45.65, vituo vya afya na zahanati 32 kwa gharama ya shilingi milioni 772 na Majengo ya taasisi nyingine 20 kwa shilingi Bilioni 1.3

MISAADA ILIYOTOLEWA

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Katibu Mkuu (WAZIRI MKUU NA BUNGE) Ndg Uledi A. Mussa ilibainisha kuwa hadi kufikia Tarehe 13 Novemba, 2016 serikali ilikuwa imepokea misaada ya vifaa, Chakula, Fedha na ahadi mbalimbali zenye thamani ya shilingi Bilioni 15.19 kutoka kwa wadau mbalimbali, washirika wa Maendeleo, Balozi wan chi marafiki ambapo tayari misaada hiyo imeshagawiwa na inaendelea kusambazwa kwa walengwa. 

Msaada ya misaada iliyopokelewa ni kama ifuatavyo:

 Fedha taslimu kiasi cha shilingi Bilioni 5,412,934.82 kimeshapelekwa Benki.


 Kiasi cha shilingi milioni 17,579,427.00 kupitia mitandao ya simu

 Ahadi za shilingi Bilioni 6,703,000,000 Hivyo jumla ya ahadi na fedha taslimu hadi sasa ni Shilingi Bilioni 12,133,564,361.82

 Serikali pia imepokea misaada mingine yenye thamani ya shilingi Bilioni 2.25 kama ifuatavyo: Unga Tani 58.12, Sukari Mifuko 1,150, Mchele Tani 133.96, Maharagwe Tani 19.666. Mahindi Tani 70.1, Majani ya Chai Tani 3, Maji Katoni 1,570, Mafuta lita 6,022, Sabuni Katoni 443, Shuka 495, Blanketi 6,125, Vyandarua 2,821, Magodoro 1,146, Mahema 367 n Turubai 6,237 vilipokelewa. 

Aidha serikali ilipokea vifaa vya ujenzi vikiwemo Saruji mifuko 24,433, Bati 20,933, Misumari kilo 1475, Nondo vipande 725, Kofia za bati 150 na mbao 250.

Lakini ifahamike kuwa baadhi ya waaliotoa ahadi kama serikali ya Uingereza wameahidi kutekeleza ahadi zao kwa kujikita moja kwa moja katika ujenzi wa Shule, Mara baada ya wakala wa majengo kuainisha viwango na gharama.

HATUA ILIYOCHUKULIWA NA SERIKALI KATIKA KUKABILIANA NA MAAFA 

Katika siku za hivi karibuni kumekuwepo na juhudi za kujaribu kufanya upotoshaji kuhusu hatua zilizochukuliwa na zinazoendelea kuchukuliwa katika kukabiliana na maafa haya, Ukweli ni kwamba serikali kwa kushirikiana na wadau imechukua hatua kubwa za kuwasaidia waathirika ambapo miongoni mwao yafuatayo yameshafanyika:

 Kutoa matibabu bure kwa majeruhi wote 560, kuandaa na kugharamia mazishi ya watu 17 waliofariki ambapo Mheshimiwa Waziri Mkuu alihudhuria, Aidha serikali kwa kushirikiana na wadau ilitoa mkono wa pole wa Shilingi Milioni 1.8 kwa kila familia iliyopatwa na msiba.

 Kuendelea kutoa misaada mbalimbali ya kibindamu ikiwemo chakula, Madawa, Nguo, Makazi ya muda, Huduma za tiba, Vifaa vya shule na huduma ya ushauri wa kisaikolojia kwa waathirika katika Wilaya zote za Mkoa wa Kagera zilizopata athari.

 Kushirikiana na Ofisi ya Mwakilishi Mkazi mmoja wa Mataifa na wadau mbalimbali wakiwemo Msalaba Mwekundu, Plan International (T), BRAC (T), World Vision, CARITAS, Save the Childre, JH Piego na Benki ya Dunia kufanya tathmini ya pamoja ya mahitaji ya haraka ya athari za Tetemeko la ardhi ili kubaini maeneo zaidi ya kuwasaidia wananchi.

HATUA ZA KUREJESHA HALI

Tangu kutokea kwa maafa haya serikali imeendelea kufanyia kazi masuala muhimu yaliyoainishwa katika tathmini ya Tetemeko ambapo hadi kufikia tarehe 13 Novemba, 2016 licha ya kuendelea kuwapatia wananchi mahitaji muhimu kama Chakula, Dawa na Misaada ya kujikimu katika makazi ya muda, kiasi cha shilingi Milioni 969,238,326.35, Mifuko ya saruji 17,423, Bati 5,348 na Misumari Kilo 1,107 vilitumika kwa kufanya ukarabati mkubwa na mdogo wa shule za msingi na Sekondari, Juhudi ambazo ziliwezesha wanafunzi wa shule hizo waliokuwa katika hatari ya kukosa masomo kuendelea na masomo yao.

Gharama hizo pia zimejumuisha ukarabati wa zahanati katika Halmashauri za Mkoa wa Kagera na kuanza kwa ujenzi wa kituo kipya cha afya (Ishozi/Kabyaile) kitakachojumuisha chumba cha upasuaji wa wodi ya kina mama na watoto kwa faida ya wananchi wote wa maeneo hayo. Pia serikali imegharamia urejeshwaji wa miundombinu ya barabara, maji na umeme katika maeneo kadhaa yaliyoathiriwa na tetemeko.

Shirika la World Vision kwa kushirikiana na serikali mkoani Kagera, tayari limetoa jumla ya mifuko ya saruji 2300 yenye thamani ya shilingi milioni 39,000,000 kwa kaya 460 zilizobomolewa nyumba na zilizoonekana kuwa na uhitaji zaidi ambapo katika awamu ya kwanza kila kaya ilipaa mifuko mitano ya saruji na kwa sasa utekelezaji wa awamu ya pili umeanza ambapo inatarajiwa kugawiwa mifuko ya saruji 10,645 yenye thamani ya shilingi Milioni 164,997,000.00 kwa kaya 2,129.

Aidha tayari serikali imeainisha kaya nyingine zilizoathirika zaidi zipatazo 370 za watu waliomo kwenye makundi maalumu (Wazee, Wajane na Walemavu) ambao watapatiwa vifaa vya ujenzi (Mabati 20 na mifuko 5 ya saruji kwa kila kaya) kwa ajili ya kukarabati nyumba zao. Ugawaji kwa awamu ya kwanza umeanza.

HITIMISHO

Haya ndio niliyoyabaini katika ziara yangu nilipozuru Mkoani Kagera naishauri Serikali kuchukua hatua kali dhidi ya wale wate waliokuwa wanapotosha watanzania dhidi ya matumizi ya fedha hizi kwa makusudi kwa madai kwamba zimeliwa na serikali.

Lakini niwapongeze wananchi wote Mkoani Kagera ambao waliitikia wito wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuitikia wito wa kuanza ujenzi wa nyumba zao wao wenyewe huku serikali ikiunga mkono katika maeneo baadhi kama ambavyo nimeeleza katika makala yangu.

Jamii inapaswa kutambua kuwa hakuna serikali duniani ambayo inapanga Tetemeko la ardhi litokee ili liwauwe wananchi wake bali ni majanga ya asili ambayo kwa namna moja ama nyingine hayazuiliki.

Kwa wale wasomaji wa Biblia Takatifu Ukisoma Mathayo 3:2 inasema ”Tubuni, Kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribi” Nami nawasihi WATUBU wale wote waliokuwa wanapotosha kuwa hela za rambi rambi zimeliwa tena walipotosha bila kuwa hata na Data wala Taarifa sahihi za Matumizi ya fedha hizo.

Wakati Mwema...!
Mathias Canal
0756413465
Mwanza

SBL yatoa saruji ya 10m/- kwa waathirika wa tetemeko Kagera

Meneja Usalama wa SBL, Sebastian Kalugulu  akimkabidhi  Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu baadhi ya mifuko ya saruji 500 yenye thamani ya shilingi milioni 10 kwa wahanga wa janga la tetemeko la ardhi lililotoa mkoani Kagera.Makabidhiano hayo yalifanyika  Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera mjini Bukoba mapema leo.
Meneja Usalama wa SBL, Sebastian Kalugulu  akitoa maelezo kwa mkuu wa mkoa wa Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu mara baada ya makabidhiano ya mifuko ya saruji 500 yenye thamani ya shilingi milioni 10 kwa wahanga wa janga la tetemeko la ardhi lililotoa mkoani Kagera.Makabidhiano hayo yalifanyika  Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera mjini Bukoba mapema leo.


Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu akifurahi jambo na  Meneja Usalama wa SBL, Sebastian Kalugul    mara baada ya makabidhiano ya mifuko ya saruji 500 yenye thamani ya shilingi milioni 10 kwa wahanga wa janga la tetemeko la ardhi lililotoa mkoani Kagera.Makabidhiano hayo yalifanyika  Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera mjini Bukoba mapema leo.




Waandishi wa habari wakichukua matukio wakati wa makabidhiano ya msaada wa mifuko ya mifuko ya saruji 500 yenye thamani ya shilingi milioni 10 kwa wahanga wa janga la tetemeko la ardhi lililotoa mkoani Kagera.Makabidhiano hayo yalifanyika  Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera mjini Bukoba mapema leo.


Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu akiongea na wafanyakazi wa SBL waliowakilisha katika kutoa msaada wa mifuko ya mifuko ya saruji 500 yenye thamani ya shilingi milioni 10 kwa wahanga wa janga la tetemeko la ardhi lililotoa mkoani Kagera.Makabidhiano hayo yalifanyika  Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera mjini Bukoba mapema leo.




Bukoba, Novemba 29, 2016-Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) leo imetoa msaada  mifuko ya saruji 500 yenye thamani ya shilingi milioni 10 kwa wahanga wa janga la tetemeko la ardhi lililotoa mkoani Kagera. Msaada huo ni kuitikia wito wa serikali  kwa mashirika, watu binafsi  na watu wenye mapenzi mema wa kujitoa kusaidia wahanga wa tukio hilo.

Akizungumza katika tukio la kukabidhi msaada huo katika Ofisi ya Mkuuu wa Mkoa wa Kagera mjini Bukoba, Meneja Usalama wa SBL, Sebastian Kalugulu  aliwapa pole  wahanga wa tetemeko hilo  kwa kuwahakikishia kwamba SBL  kila mara iko tayari kusaidia  pindi inapohitajiwa na jamii.

 “”Tunatoa pole ya dhati na masikitiko yetu kwa wahanga wa  tetemeko la ardhi  na tunawaombea majeruhi wote wapone haraka,” alisema Kalugulu, na kuongeza kwamba SBL  inaungana na watu wengine wenye mapenzi mema kutoa msaada wa kibinadamu kwa ajili ya kuwasaidia  kuhimili kadhia iliyowapata  na kurudi katika shughuli zao kawaida.

Kalugulu alithibitisha tena kwamba kampuni hiyo ya bia  imejikita katika kuunga mkono  serikali  na watu binafsi wenye mapenzi mema, mashirika  na makampuni  katika kuisaidia jamii katika maeneo SBL inapoendesha shughuli zake.

 “Ni matumaini yetu kwamba msaada huu utachangia katika michango  iliyokwishatolewa na wasamaria wengine  na kwamba itawawezesha  wahanga hao kujenga  miundombinu iliyoharibika  na hata kuboresha maisha yao.”

 Akizungumzia mchango uliotolewa na SBL, Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu alisema kwamba msaada huo unachangia katika michango  mingine  kutoka kwa watu wenye mapenzi mema kutoka ndani, mikoani  na kimataifa  ambao kmwa ukarimu waliitikia wito wa serikali wa kusaidia.

Mkuu huyo wa mkoa alisema kuwa atahakikisha kuwa  msaada huo unaenda kwenye lengo lililokusudiwa  na kutoa wito  kwa watu zaidi  kuendelea kuwasaidia wahanga.

Mwisho

MADAKTARI NCHINI WAMETAKIWA KUITISHA MIKUTANO YA KIJAMII ILI KUJADILI MAGONJWA


Katibu Mtendaji wa Chama cha Afya ya Jamii Tanzania (TPHA), Fabian Magoma  (kulia), akizungumza katika Kongamano la 33 la siku tano la Chama cha Afya ya Jamii Tanzania (TPHA) linaloendelea Hoteli ya Kebby Mwenge jijini Dar es Salaam leo asubuhi. Kushoto ni  Mwenyekiti wa TPHA anayemaliza muda wake, Daktari Bingwa  Elihuruma Nangawe.
Dk. Manase Frank akitoa mada kwenye kongamano hilo.

 Profesa Andrew Swai akitoa mada.
 Wadau wa sekta ya afya wakifuatilia kwa karibu mada zilizokuwa zikitolewa katika kongamano hilo.
 Kongamano likiendelea.
 Dk. Andronicus Aloyce Rwelamila kutoka Hospitali ya Tumbi Kibaha (kushoto) na Muuguzi wa Hospitali hiyo, Mary Gowele wakiwa kwenye kongamano hilo.
 Kongamano likiendelea

Usikivu katika kongamano hilo. Kushoto ni Mwenyekiti wa TPHA, Dk. Elihuruma Nangawe

 Profesa Japhet Kileo (kulia), akiuliza maswali kwenye 
kongamano hilo.
 Dk. Mwanahamisi Magwangwara (kushoto), akizungumza wakati akijibu maswali mbalimbali kutoka kwa wadau wa sekta ya afya katika kongamano la 33 la siku tano la Chama cha Afya ya Jamii Tanzania (TPHA) linaloendelea Hoteli ya Kebby Mwenge jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni mtoa mada, Profesa Andrew Swai. 
Dk.Chilolo Edward (katikati), akijibu maswali kuhusu changamoto ya waendesha bodaboda. Kushoto ni Profesa Andrew Swai na Dk. Manase Frank. 
Mkurugenzi wa Shirika la Wanawake katika Jitihada za Maendeleo (WAJIKI), Janeth Mawinza akielezea changamoto ya matumizi ya pombe katika Manispaa ya Kinondoni.

Na Dotto Mwaibale

MADAKTARI nchini wametakiwa kufanya mikutano ya kijamii au wananchi ili kuwapa fursa ya kujua magonjwa yanayo wakabili.

Hayo yalielezwa na Dk. Manase Frank wakati akitoa mada katika kongamano la 33 la siku tano la Chama cha Afya ya Jamii Tanzania (TPHA) linaloendelea Hoteli ya Kebby Mwenge jijini Dar es Salaam leo asubuhi.

"Changamoto kubwa tuliyonayo ni wananchi wengi kutojua magonjwa yanayowasumbua hivyo ni muhimu kwa madakatari kuitisha mikutano itakayowakutanisha na wananchi ili kuondoa changamoto hiyo" alisema Dk. Frank.

Alisema wagonjwa wengi wamekuwa wakikata tamaa kwa kuchangiwa na kauli za baadhi ya madaktari ambao wanashindwa kujua tatizo la mgonjwa husika hivyo wakati umefika wa madaktari kushirikiana kwa karibu na jamii, viongozi wa dini  ili kuondoa changamoto hiyo.

Akitolea mfano wa kijana mmoja ambaye alifiwa na ndugu zake wote wa karibu kutokana na ugonjwa wa ukimwi na kuishi kwa kunyanyapaliwa lakini baadaye afya yake ilikuja kuimarika kufuatia ushauri uliotolewa na daktari kwa  jamii iliyokuwa ikimzunguka wakati wa ugonjwa wake.

Mtoa mada mwingine Profesa Andrew Swai aliomba serikali wakati wa siku ya Jumamosi na Jumapili kufunga baadhi ya barabara ili zitumike kwa wananchi kufanya mazoezi ya kutembea ili kujenga afya za miili yako na kuepukana na magonjwa kama kisukari.

Akizungumzia changamoto ya matumizi ya bodaboda Dk.Chilolo Edward alisema kwa mwaka jana katika Hospitali za mikoa ya  Morogoro, Tumbi Pwani na Shinyanga kulikuwa na ajali 895 huku majeruhi wakiwa 4813.

Alisema majeruhi waliolazwa katika hospitali hizo walikuwa ni 4525, waliopewa rufaa kwenda hospitali za Bugando na Muhimbili walikuwa 71 na waliolazwa ni 702.

Alisema vifo vilikuwa 81 hivyo vilitokea baada ya kufikishwa Hospitalini ni 70 na vilivyotokea eneo la ajali vilikuwa 11.

Dk.Chilolo alisema ili kupunguza changamoto hiyo inapaswa watoa huduma za afya kutoa elimu kwa waendesha boda boda pale wanapofikishwa mahospitali kuhusu umuhimu wao katika familia na taifa kwa ujumla hivyo kuwa makini wanapoendesha vyombo hivyo vya moto badala ya kuacha kazi hiyo kufanywa na polisi au Sumatra.

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More