Thursday, November 19, 2015

MWANALIBENEKE YUSKISS KISIBA ATIMIZA MIAKA KADHAA YA KUZALIWA KWAKE.


Anaitwa Yusuph Kisiba a.k.a Yuskiss Kisiba ambae ni Blogger @Lake Zone Media & Kisibasharesky Media, Graphics Desiner & Video Editor @Shafineys Film Production Jijini Mwanza.
Na:George Binagi-GB Pazzo wa Binagi Media Group
Tarehe kama ya leo (Nevemba 19) miaka kadhaa iliyopita alizaliwa hivyo hii leo anafurahia siku yake ya kuzaliwa na ndugu, jamaa na Marafiki. Nasi tunamtakia maisha mema katika kuzaliwa kwake.

"Novemba 19 ni tarehe ambayo Mwenyezi Mungu aliweza kuniruhusu kutoka katika tumbo la mama yangu kipenzi na kuuona ulimwengu huu. Na hapo ndipo safari yangu ilipoanzia na ikawa ndiyo chanzo cha kufahamiana na wewe hivi sasa. Novemba 19 ni siku ambayo huwa ya kipekee sana kwangu katika huzuni na furaha kutokana na kuishi mazingira haya ya ulimwengu uliojaa kila aina ya uzuri na ubaya wake.Ukiwa kama ndugu/rafiki yangu sina budi kukukumbusha kuungana nami kufanya ibada ikiwa na lengo moja la kumuomba  Mungu atusamehe makosa yetu. Kwa yeyote niliewahi kumkosea sina budi kukuomba radhi katika siku hii". Anasema Kisiba.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More