Monday, November 30, 2015

COSATO CHUMI KESHO KUTIMIZA KAULI MBIU YA HAPA KAZI TU KATIKA JIMBO LA MAFINGA MJINI

 hivi ni baadhi ya vifaa atakavyokabidhi mbuge wa jimbo hilo cosato chumi katika jimbo la mafinga mjini siku ya kesho.
 hili ni gari likishusha vifaa hivyo na baadhi ya watumishi wakisaidia kuvishusha 
 huyu ni mmoja ya wafanyakzi katika hospitali ya mafinga akiwa ameshusha kiti cha wagonjwa akipeleka sehemu inayotakiwa.

Mbunge wa jimbo la mafinga mjini cosato chumi ameanza kutimiza ahadi zake alizo waahidi wakazi wa jimbo hilo na kutekeleza kauli mbiu ya rais wa jamhuri ya muungano ya Tanzania dr john pombe magufuli ya hapa kazi tu.

Akizungumza na blog hii mbunge huyo amesema kesho anatarajia kutoa vifaa ya hospitali ili viweze kuwasaidia wakazi wa jimbo na kuboresha afya za wananchi wake kwa kuwa usipokuwa na afya huwezi kufanya kazi na kutimiza malengo ya kuleta maendeleo kwa kasi kubwa.

“Unajua afya ni kila kitu katika maisha ya binadamu hivyo lazima nitekeleze ahadi zangu nilizotoa wakati wa kampeni na wanachi lazima tufanye kazi kwa kujituma ili tumuunge mkono rais wetu ambaye ananiaya ya kutuletea maendeleo “aliyasema hayo wakati akiwashukuru wananchi wake mapema tu baada ya kutangazwa kuwa ni mshindi katika uchaguzi huu.

chumi amewaomba wananchi wa jimbo hilo kuunga mkono kwa kufanya kazi kwa nguvu zote ili walete maendeleo kwa pamoja maana akifanya kazi pekee yake bila wao hawezi kuleta maendeleo pekee yake.

Viongozi wa serikali katika ngazi mbalimbali wametakiwa kujituma kufanya kazi kwa bidii ili kutimiza azma yao ya kuleta maendeleo katika jimbo hilo.


Kesho natajia kukabidhi vifaa ambavyo vitawasaidia wagonjwa kupata huduma inayostahili.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More