Thursday, February 26, 2015

MTOTO MCHANGA AUAWA NA KUTUPWA KICHAKANI MKOANI MOROGORO

Matukio ya kutupa watoto wachanga yameendelea mkoani Morogoro ambapo mtoto mchanga wa siku moja ameuwa na kutupwa vichakani katika eneo la kichangani mjini Morogoro.

Mtoto huyo mwenye jinsi ya kike anaonekana ametupwa kwa saa kadhaa zilizopita ambapo wakizungumzia tukio hilo baadhi ya mashuhuda wamelalamikia kuongezeka kwa matukio ya watoto wachanga kutupwa  ambapo wameomba wazazi kuwahurumia watoto   wasio na hatia huku baadhi ya wakinamama waliokuwepo katika tukio hilo wameonyesha kusikitishwa na kueleza wakati mwingine inatokana na baadhi ya wanaume kukwepa majukumu.
 
Naye mwenyekiti wa mtaa na diwani wa kata ya kichangani John Waziri walioshuhudia tukio hilo wamesema tukio hilo si la kuvumilika na kuomba wananchi kuwafichua wanaowabainika kuzaa na kutupa watoto  kwa lengo la kukwepa majukumu na pia kuomba wananchi kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi ili kufanikisha kupatikana kwa mtuhumiwa.
 
Jeshi la polisi limethibitisha kutokea kwa tukio hilo na wamefika katika eneo la tukio na kuchukua mwili wa mtoto huyo umehifadhiwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Morogoro.

UKAWA WAITAKA SERIKALI KUSITISHA ZOEZI LA UPIGAJI KURA YA MAONI YA KATIBA PENDEKEZWA

Viongozi wa vyama vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi UKAWA umeitaka serikali kusitisha zoezi la upigaji wa kura ya maoni ya katiba kutokana na zoezi hilo kutokidhi vigezo vya kisheria na badala yake ielekeze nguvu na rasilimali fedha katika zoezi la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura ili kuliepusha taifa kuingia katika machafuko.

Viongozi wakuu wa vyama vinavyounda umoja huo wa katiba ya wananchi ukawa wakiongozwa na Profesa Ibrahimu Lipumba wa chama cha wananchi CUF na Freeman Mbowe wa chama cha demokrasia na maendeleo Chadema, chama cha NLD Dr Emmanuel Makaidi, chama cha NCCR mageuzi Mosena Nyambabe wameitoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam mbele ya waandishi wa habari.
 
Mwenyekiti wa CUF Prof Ibrahimu Lipumba amemtaka rais Prof Jakaya Mrisho Kikwete kutoa kauli ya kuusitisha mchakato wa kura za maoni ya katiba pendekezwa kwa kuwa zoezi hilo kwa sasa haliwezi kutekelezeka April 30 ya mwaka huu kama rais alivyotangaza licha ya kutokuwa na mamlaka ya kutangaza tarehe ya kufanyika kwa kura hizo za maoni.
 
Kwa upande wake mwenyekiti wa chama cha demokrasia na maendeleo Chadema Freeman Mbowe ameitaka serikali kuelekeza fedha kidogo zilizopo katika zoezi la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura kwa kuwa zoezi hilo linakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa vifaa vya kutosha na kusitisha kabisa zoezi la kura za maoni ya katiba ili kuiepusha nchi na kile alichodai kuwa ni machafuko yanayowea kuzuilika.
 
Hivi sasa taifa liko katika maandalizi ya kushiriki katika zoezi la kura za maoni ya katiba pendekezwa linalotarajiwa kufanyika alhamis ya April 30, 2015 kama ilivyotangazwa na mh rais wa jamhuri ya mungano wa Tanzania licha ya uwepo wa kauli za kulipinga zoezi hilo kutoka hasa katika vyama vya siasa vya upinzania na baadhi ya vyama vya kiraia kwa sababu kadha wa kadha

JESHI LA POLISI LAPATA AIBU KUBWA, POLISI WAKE AKUTWA AKIFANYA MAPENZI HADHARANI AKIWA AMEVAA SARE ZA JESHI HILO

polise 
 
 
Unakumbuka ile Stori ya askari Asuma Mpaji na Veronica Nazaremo kufukuzwa kazi Mkoani Kagera baada ya picha zao kusambaa mitandaoni wakionekana kupigana mabusu? safari hii nakuletea tena stori inayofanana na hiyo ambayo imetokea Nchini Uingereza.

Polisi wa nchi hiyo ya Uingereza waliamua kumshtaki mwenzao baada ya kufanya kitendo cha kudhalilisha jeshi la nchi la nchi hiyo kwa kufanya tendo la ndoa tena mbele za watu akiwa na sare za kazi.

Kitendo hicho kimemfanya kufukuzwa kazi bila kupewa taarifa za awali haraka baada ya kwenda kwenye shughuli zake za kila siku za usalama na kufanya kitendo hicho huku akijua ni kinyume na sheria tena akiwa amezungukwa na watu.

Msaidizi mkuu wa kituo hicho Russ Middleton alisema wanaamini hatua hiyo itakua fundisho kwa wengine kutokana na kitendo hicho cha udhalilisha.

Kwa upande mwingine polisi mwingine nchini Uruguay naye alikumbwa na mkasa unaofanana na huo baada ya kucheza na mwanamke akiwa uchi katika kituo chake cha kazi.

Picha ya askari huyo zilinaswa na mitandano mbalimbali na kujikuta zikisambaa kwa kasi hali iliyosababisha ashtakiwe kwa kosa hilo.

SERIKALI ISIMAMIE VYEMA HAKI ZA BINADAMU KWA KUSHIRIKIANA NA SEKTA BINAFSI

   waandishi wa habari kutoka mikoa ya nyanda za juu kusini wakipata mafunzo ya kupinga unyanyasaji wa kijinsia yanayoendeshwa na TAMWA

CHAMA cha Waandishi wa habari Wanawake (TAMWA) kimeishauri serikali  kusimamia vyema haki za binadamu, sambamba na kutoa adhabu kali kwa ajili ya kutatua tatizo la unyanyasaji wa kijinsia nchini.

Vilevile waandishi wa habari nchini wametoa ombi kwa baraza la habari Tanzania (MCT) pamoja na TAMWA kufikiria kuziwezesha klabu za waandishi wa habari za mikoani vyombo vya usafiri ili kusaidia kutumia vyombo vya usafiri wa viongozi (sources).

Hayo yalisemwa jana katika semina ya Tamwa iliyofanyika mjini hapa na kuwashirikisha waandishi wa habari kutoka mikoa ya Iringa, Njombe, Mbeya na Ruvuma.

Akizungumza katika semina hiyo, mwezeshaji wa Tamwa, Wence Mushi alisema serikali inapaswa kuchukua hatua kali ikiwa ni pamoja na kutoa adhabu kali kwa ajili ya kuondokana na tatizo la unyanyasaji wa kijinsia hususani kwa watoto, wanawake na watu wenye ulemavu wa ngozi.

 “Kama sheria za haki za binadamu hazitasimamiwa vizuri na maafisa Ustawi wa Jamii bado ukatili wa aina yoyote utaendelea katika mazingira tunayoishi, hadhi ya wanawake na kuonekana kama ni chombo cha starehe itaendelea kwa sababu haki hazisimamiwi ipasavyo,”alisema Mushi.

Mushi aliwataka wanahabari kuendelea kuibua mambo ya kikatili yanayofanywa na baadhi ya watu hasa kwa watoto, wanawake na walemavu wa ngozi ili kuipa elimu jamii na kushinikiza serikali kuchukua hatua katika ukatili huu.

“Kuna taasisi na mashirika yanayojihusisha na kutetea haki za watoto hivyo ni vyema waandishi kila wanapoona matukio kama hayo yanatokea wakayaibua ili kuyatokomeza kwa kuchukuliwa hatua,”alisema Mushi.

Kwa upande wake mwandishi  Geofrey Nilahi kutoka gazeti la Tanzania Daima, Songea alisema kuwa wanahabari ni chachu ya mabadiliko kama tukiibua mambo ya kikatili yanayofanywa na kushinikiza yafanyiwe mabadiliko hasa katika usimamizi wa sheria na kuchukuliwa hatua kwa wahalifu.

“Wanahabari ni chombo muhimu sana na ili kutokomeza ukatili wa aina yoyote ni lazima kalamu zetu zitumike kukemea mambo yasiyostahili kutedwa na kufuata haki za binadamu ili kuleta usawa katika jamii,” alisema.

Festo Sikagonamo mwakilishi wa ITV Mbeya alisema kuwa endapo wanahabari wakiwezeshwa na  TAMWA kufuatilia habari  juu ya ukatili wa kijinsia pamoja na mauaji ya watu wenye ulemavu hakika mabadiliko yatakuja kupitia kalamu zetu.

Waandishi wa habari walioshiriki mafunzo hayo, waliiomba Tamwa kuwawezesha vyombo vya usafiri vyama vya waandishi wa habari za mikoani (Press Clubs) kwa ajili ya kufuatilia habari katika maeneo ya vijijini ambako wanaamini ndiko habari nyingi zinapopatika.

“Tukiwezeshwa usafiri tunaamini tutaleta habari za kuelimisha jamii, tutaibua mambo mbalimbali na baadaye kuyapatia ufumbuzi kupitia viongozi husika,” alisema George Tarimo mwandishi wa habari Nipashe Iringa.

Wednesday, February 25, 2015

FFU watumia mabomu kutuliZa vurugu Ilula ,magari yachomwa moto ,mahabusu waachiwa silaha zaporwa



KIJANA WA KITANZANIA AUNDA REDIO STESHENI

 - SHUJAAZ! Shujaaz Banner
DJ Tee (19) ni kijana mwenye ndoto kubwa katika maisha yake. Baada ya kuona mahangaiko ya vijana kuelekea kwenye mafanikio, wengi wakiwa wamemaliza shule na vyuo bila kupata kazi, ameamua kuunda redio stesheni ghetoni kwake aliyoipa jina la Shujaaz, ili aweze kushea ideas na vijana wote nchini Tanzania kuhusu mbinu mbalimbali za kuingiza pesa, kuwapa stori za vijana wanaochakarika katika maisha yao pamoja na kuwaburudisha.
"Nimeamua kuiita Shujaaz kwa sababu, naamini kuwa kijana ambaye anajituma na kuweka mfano bora kwenye jamii ni shujaa". Alisema DJ Tee. "Ndoto zangu zinakaribia kuwa kweli".
Story ya kijana huyu inapatikana kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi kupitia kijarida cha Shujaaz, kitakachokuwa kinasambazwa kupitia gazeti la Mwanaspoti, kuanzia JUMAMOSI HII ya tarehe 28. Kwenye kijarida hicho, utapata ideas mbali mbali ambazo vijana wanaweza kuzifuata na kujiingizia kipato. Pia, kutakuwa na stori za vijana wengine kama Pendo, Semeni na Pepe ambao ni mashabiki wakubwa wa DJ Tee na redio show yake ya Shujaaz.
DJ Tee akiwa studio
DJ Tee akiwa studio.
Kijana huyu ameamua kujiita DJ Tee ili asijulikane na watu wake wa karibu, kwa kuwa ana-hack airwaves za redio stesheni ili aweze kusikika. Sikiliza redio stesheni uipendayo kuanzia wiki ijayo, huwezi jua, inawezekana DJ Tee akawa hewani!
Wewe pia USIKOSE kuwa sehemu ya mafanikio na harakati za kijana huyu kwa kujiunga naye. Pata nakala yako ya Shujaaz kuanzia Jumamosi hii (28/02/2015) kupitia gazeti la Mwanaspoti. Pia, jiunge naye kwenye ukurasa wake wa Facebook kwa jina DJTee255 ili upige naye story na wewe uweze kushea idea zako za hustle. Unaweza pia ukampata Instagram na Twitter kwa jina @djtee255
Studio
Studio.

WATANZANIA WAASWA KUTHAMINI BIDHAA ZINAZOZALISHWA NDANI YA NCHI



KAIMU MENEJA WA SIDO MKOA WA IRINGA, MR NIKO MAHINYA AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI OFINI KWAKE
KAIMU MENEJA WA SIDO MKOANI IRINGA, NIKO MAHINYA AKIWA NA MHANDISI WA KARAKANA YA SIDO IRINGA, MICHAEL MATONYA WAKATI WAKITEMBELEA UTENDAJI KAZI WA KARAKANA HIYO
FUNDI WA KARAKANA YA SIDO ELAYSON TARIMO AKIANGALIA MASHINE YA KUNOA VYUMA, AMBAYO ILIKUWA IKINOA MAJEMBE YA KUKATIA CHAI
MSIMAMIZI WA KARAKANA YA KUTENGENEZEA MASHINE MBALIMBALI YA SIDO MKOANI IRINGA, LEONARD LUMATO AKIENDELEA NA KAZI KATIKA KARAKANA HIYO
KIJANA AKIENDELEA NA KAZI NDANI YA KARAKANA

NA FRANK KIBIKI, IRINGA


SHIRIKA la kuhudumia viwanda vidogo (SIDO), mkoani Iringa limewataka watanzania kujenga utamaduni wa kupenda bidhaa zinazotengenezwa ndani, badala ya zile zinazoingizwa kutoka nje ili kukuza uchumi wan chi.
 
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Iringa, Kaimu meneja wa SIDO mkoani Iringa, Niko Mahinya alisema ikiwa watanzania wataenzi bidhaa zinazotengenezwa ndani itakuwa rahisi kuinua uchumi wa nchi, na mtu mmoja mmoja.
Alisema shirika hilo limekuwa likitengeneza bidhaa nyingi, zikiwemo mashine na pembejeo za kilimo lakini, kutokana na dhana ya kununua bidhaa za nje wamekuwa wakikabiliana na tatizo kubwa la soko.
 
“Tunazalisha mashine mbalimbali, zikiwemo zana za kilimo kama vile, mashine za kusagia nafaka, kuchujia mafuta ya alizeti, kukamulia asali na nyingine nyingi lakini changamoto kubwa ni soko la bidhaa za ndani,”alisema
 
Aidha alisema itakuwa vyema kama serikali itaweka utaratibu au sera itakayofanya watu wajenge tabia ya kuheshimu, kupenda na  kutumia bidhaa za ndani.
 
Kwa upande wao baadhi ya wajasiriamali na wakulima walisema kuwa mara nyingi wamekuwa wakinunua mashine za kichina kutokana na bei yake kuwa chini ingawa hazina ubora.
 
“Bidhaa za nje ni bei ndogo kuliko zile zinazotengenezwa ndani, hii ndiyo sababu inayofanya wengi tutumie bidhaa za kichina ambazo hata hivyo hazidumu kwa muda mrefu,”alisema LeoniKA Sanga, mmilikiwa kiwanda cha kukamua mafuta ya alizeti, mjini Iringa.
 
Aliiomba serikali kutoa ruzuku kwa SIDO ili bidhaa zinazotengenezwa zishushwe bei yake na kuweza kuwahudumia wajasiriamali na wakulima wadogo.

Tuesday, February 24, 2015

CHAMA CHA ALBINO KUMSHITAKI RAIS KIKWETE UMOJA WA MATAIFA.


Msemaji wa Chama cha Albino Tanzania (TAS), Josephat Torner
Msemaji wa Chama cha Albino Tanzania (TAS), Josephat Torner
CHAMA cha Albino Tanzania (TAS), kimetoa miezi mitatu kwa Rais Jakaya Kikwete kuingilia kati vitendo vya mauaji ya albino yanayoendelea nchini. Akishindwa kuchukua hatua, watamshitaki Umoja wa Mataifa (UN).
Akizungumza Afisa Habari wa TAS, Josephat Torner amesema, wamechoshwa na vitendo vya mauaji ya albino vinavyoendelea huku Rais Kikwete akiwa kimya.
Torner amesema Rais Kikwete ni rais wa Watanzania wote hivyo analazimika kukomesha mauaji ya albino na akishindwa kuchukua hatua katika kipindi hicho walichompa watapeleka malalamiko yao UN.
Alisema watalazimika kufika huko kwani chama chao kimesajiliwa chini ya UN hivyo wakishindwa kusaidia wa Rais Kikwete watalazimika kukimbilia huko ambako wana imani watasaidiwa.
Msemaji huyo alisema kabla ya kupeleka malalamiko yao UN watafanya maandamano makubwa Machi 2, 2015 nchini nzima, na kwa upande wa Dar es Salaam wataanzia Ocean Road na kumalizikia Ikulu ambapo wamepanga kumuona Rais Kikwete na kumpa malalamiko yao.
“Maandamano hayo ya amani yatakuwa na kauli mbiu ‘MAUAJI YA ALBINO SASA BASI’. Mikoani Albino wataandamana kwenda ofisi za wakuu wa mikoa kupeleka vilio vyao,” alisema Torner.
Tangu mwaka 2006 zaidi ya Albino 76 wameuawa, na majeruhi waliopo ni zaidi ya 56 na makaburi 18 yamefukuliwa na kuchukuliwa miili ya waliozikwa huku walioachwa na ulemavu wa kudumu ni 11, hakuna muuaji hata mmoja aliyekamatwa.

MTANDAO WA HAKI ZA BINADAMU WATOA TAMKO JUU YA KUTEKWA NA KUTESWA KWA KIONGOZI WA WAHITIMU JKT

9
Mwenyekiti wa JKT Tanzania, Bw. George Mgoba akiwa wodini.

TAMWA YATOA MAFUNZO KWA WANAHABARI WA MIKOA YA NYANDA ZA JUU KUSINI JUU YA KUPAMBANA NA UNYANYASAJI WA KIJINSIA

WENCE AKITOA ELIMU KWA WANAHABARI WALIOKUTANA MKOANI IRINGA
WANAHABARI NWAKIWA MAKINI KUMSIKILIZA MTOA ELIMU
MWANAHABARI FRANK KIBIKI AKIWA MAKINI KUFUATILIA NINI KINACHOENDELEA KWENYE MAFUNZO HAYO

 na fredy mgunda,iringa

Waandishi wa habari wametakiwa kuandika zaidi habari zinazohusu unyanyasaji wa kijinsia hususan dhidi ya wanawake na watoto ili kuiamsha zaidi jamii inayowafanyiwa vitendo hivyo na mamlaka husika ziweze kuchukua hatua za kisheria dhidi ya vitendo hivyo.

Msisitizo huo ulitolewa na chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (Tamwa) kwa waandishi wa habari wa mikoa ya nyanda za juu kusini (IRINGA,MBEYA,SONGEA NA NJOMBE) ambapo wanahabari wameombwa kuendelea kufichua habari hizo hususan kwa wanaofanyiwa vitendo hivyo ili waweze kuelewa kwamba sheria dhidi ya ukatili huo zipo na kwamba kuna taasisi za kuwatetea.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo mwanahabari wa siku nyingi WENCE MUSHI alisema dhahiri kuwa vitendo vya unanyanyasaji vimepungua kutokana na wanaofanya ukatili huo kuelewa, na watendewa pia kuzidi kuamka, juhudi zaidi zilitakiwa kujipenyeza zaidi dhidi ya imani za kimila ambazo bado zinashikiliwa katika sehemu mbalimbali za nchi.

“Endeleeni kutumia kalamu zenu na vifaa vyenu vyote kupiga vita vitendo vyote vinavyotokana na manyanyaso ya kijinsia ambayo hasa hutokana na mfumo dume,” alisema wence akiwaomba wahabari kufanya hivyo kwa ajili ya kuendeleza juhudi za kutokomeza kabisa suala la unyanyasaji wa kijinsia.

Wence alisema jicho la waandishi wa habari linasaidia kuwaelimisha wananchi juu ya mambo mbalimbali yanafanywa kinyume cha seria,kuwaomba wanahabari kufanya habari za kichunguzi juu ya ukatili wa kijinsia pamoja na unyanyasaji wake.

Pia aliongeza kwa kusema kuwa kwa sasa TAMWA imekijita katika kufuatilia habari juu ya ukatili wa kijinsia pamoja na mauwaji ya watu wenye ulemavu na kulenga hasa habari za kichunguzi ambazo zitaleta mabadiliko kwa jamii yetu.

Kwa upande wa waandishi wa habari wa nyanda za juu kusini walioshiriki warsha hiyo wamesema kuwa wanafanya kazi hiyo katika mazingira magumu,hivyo kuwaomba TAMWA kuwasaidia chombo cha usafiri kila mkoa ili waweze kuwafikia wananchi waliopo vijijini na kupata taarifa zao.

Lakini wakawataka wanahabri wengine kufanya kazi kwa kufuta weledi wao kutokana na elimu walioipata wakiwa darasa na kwenye mafunzo mbalimbali.

Friday, February 20, 2015

JAY Z NA MTOTO NJE YA NDOA

jay z son
Skendo haziko mbali  na kivuli cha staa, hii iko duniani kote na safari hii imemkuta jamaa ambaye wengi wanaofanya Hip Hop wanamuangalia kama model wao, kutokana na nguvu yake kubwa kwenye muziki huo, leo zimeanza kusikika za upande wa pili ambazo huenda hattukuwahi kuzisikia siku za nyuma.
Shawn Corey Carter ama Jay Z tunajua kuwa ana ndoa na mpenzi wake ambaye ni Beyonce na wana mtoto mmoja,

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More