Sunday, July 31, 2016

MBUNGE WA JIMBO LA MAFINGA MJINI COSATO CHUMI AMESAINI MKATABA WA USHIRIKIANO NA NGO YA WORLD SHARE YA NCHINI KOREA


Afisa wa NGO ya world share ya nchini korea Nara Kim na mbunge wa jimbo mafinga mjini Cosato Chumi wakisaini mkataba wa makubaliano ya kazi

BARABARA NI CHANGAMOTO KATIKA USAMBAZAJI WA MADAWA VIJIJI

 
 IMEBAINIKA kuwa ubovu wa miundo mbinu ya barabara, hasa  za vijijini ni changamoto kubwa inayowakabili bohari ya madawa (MSD) wakati wa kusambaza madawa katika vituo vya afya nchi.

Saturday, July 30, 2016

SKY SPORTS YAUNGANA NA STARTIMES KUONYESHA LIGI YA CHINA



Na Dotto Mwaibale

Kituo cha matangazo ya luninga cha Sky Sports cha nchini Uingereza katikati ya wiki hii kilisaini mkataba mnono wa kuonyesha moja kwa moja ligi kuu ya China kwa misimu mitatu ijayo ambayo pia kwa Tanzania inaonekana kupitia visimbuzi vya StarTimes.

SIA PIUS NDIYE WINDHOEK DRAUGHT MISS SINZA 2016

 Windhoek Draught Miss Sinza 2016, Sia Pius (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na mshindi wa pili Catherine Listoni (kushoto) na mshindi wa tatu Hafsa Mahamood baada ya kutangazwa mshindi Hoteli ya Defrance lilikofanyika shindano hilo jana usiku kwa udhamini wa Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spirits Ltd kupitia kinywaji wa Windhoek.

PASTOR DANIEL MOSES KULOLA OF EAGT LUMALA MPYA MWANZA TO VISIT USA.

"Greetings my friend, Again God has given to me a chance to come to America, this time i wont stay in USA for long time it is just for 2 weeks then i come back home Tanzania.

My schedule will be in Boston from 9th to 14th August then 15th August to Dallas, Houston to 22nd, on 23rd to Arizona. my ticket back to Tanzania reads on 25th from Arizona to Boston and Boston to Tanzania.
I thought it is good to let you know so that you can pray for me and also call me for greetings". Pastor Kulola States.

Friday, July 29, 2016

Dk. Kigwangalla akutana na Wakuu wa Idara za Maendeleo ya Jamii, Watoto atoa maagizo

DSC_3248 
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla akipitia madokezo mbalimbali ya Idara za Wizara hiyo muda mfupi kabla ya kukutana na Wakuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii na ile Idara ya Watoto.

HOMA YA INI B NA C KUTOKOMEZWA IFIKAPO MWAKA 2030

 Baadhi ya vijana waliokuwa wakitumia dawa za kulevya wakiwa na mabango yenye ujumbe mbalimbali wa kutokomeza homa ya ini wakielekea kwenye  maadhimisho ya siku ya homa ya ini yaliyofanyika viwanja vya Mwembe Yanga Dar es Salaam leo mchana.

Thursday, July 28, 2016

Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino (SAUT) Chakanusha vyuo vyake kuzuiwa Kudahili

CHUO Kikuu cha Mtakatifu Agustino (SAUT), kimetoa ufafanuzi wa taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii kuwa vyuo vyake vishiriki vimezuiwa na Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU) kufanya udahili wa wanafunzi.

Picha ya Mtanzania anayeteswa na Mchina yampeleka Mwigulu Geita

Waziri wa mambo ya ndani ya nchi, Mwigulu Nchemba amewasili mkoa wa Geita kwa ziara ya kikazi, kubwa ikiwa ni kufuatia taarifa za mateso na mauaji yaliyodaiwa kufanywa na raia wa China wanaomiliki sehemu ya mgodi wa Nyamhuna uliopo Katoro, Geita dhidi ya wafanyakazi/vibarua ambao ni Watanzania.

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII,MHANDISI RAMO MAKANI AFANYA KIKAO NA VIONGOZI WA HIFADHI YA TAIFA YA KISIWA CHA RUBONDO.

Naibu Waziri wa Maliasilili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani ,akiviishwa vazi maalum (Boya) ambalo hutumika kujiokoa wakati uafiri wa maji unatumika.

BENDI 10 MAARUFU ZA MUZIKI WA DANSI KUWASHA MOTO JUMAMOSI VIWANJA VYA LEADERS NI KATIKA TAMASHA KUBWA LA MUZIKI WA DANSI

 Mwanamuzi wa mziki wa dansi, Ali Choki akiwaongoza wenzake kutoa burudani mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda walipofika ofisini kwake leo, kuzungumzia Tamasha la muziki huo litakalofanyika Jumamosi  Viwanja vya Leaders ambalo litashirikisha bendi 10 maarufu za hapa nchini.

Wednesday, July 27, 2016

RAIS MAGUFULI KUZURU MKOA WA SINGIDA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli anayetaraji kuwasili Mkoani humo tarehe 29 mwezi huu.

BREAK NEWS :ASKARI POLISI ALIYEMUUA MWANAHABARI DAUDI MWANGOSI AFUNGWA JELA MIAKA 15

 

 Rais wa klub za wandishi wa habari nchini  DEOGRATIUS NSOKOLO akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kulewa kwa hukumu ya kesi ya mwanahabari daudi mwangosi

MBUNGE WA SEGEREA BONNAH KALUWA AREJESHA KIWANJA KWA WANANCHI WA KATA YA BUGURUNI

 Mbunge wa Jimbo la Segerea,  Bonnah Kaluwa (kulia), akizungumza Dar es Salaam leo na wafanyakazi wa Kampuni ya M/S Yassa General Supplies Limited iliyokodishwa kiwanja kilichopo nyuma ya Kituo cha Polisi Buguruni ambapo ametoa siku tatu waondoke kupisha ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Buguruni. Mapato ya kiwanja hicho kwa zaidi ya miaka 10 yalikuwa hayajulikani yalipokuwa yakienda.

Tuesday, July 26, 2016

KAMPUNI YA MGODI WA GEITA GOLD MINING (GGM) YAFANIKISHA ZOEZI LA KUKUSANYA PESA KWA AJILI YA MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI.

 
Mkuu wa wilaya ya Moshi Kipi Warioba akiongozana na kundi la wapanda mlima Kilimanjaro kutoka kampuni ya Mgodi ya Geita Gold Mining (GGM) waliopanda kwa lengo la kuchangisha fedha za kusaidia taasisi mbalimbali zinazo shughulika na mapambano dhidi ya Ukimwi.

WATEJA WAFURAHIA MICHUANO YA ICC INAYOONEKANA KUPITIA STARTIMES

 Meneja Mauzo wa StarTimes Tanzania, Bw. David Kisaka akizungumza na timu ya StarTimes na maveterani wa uwanja wa Mwembe Yanga – Temeke kabla ya mchezo wa kirafiki uwanjani hapo. StarTimes iliweka kambi uwanjani hapo ikiwa ni uzinduzi wa michuano ya ICC mwaka 2016 iliyokwishaanza kutimua vumbi Julai 22 wiki iliyopita ambapo ilidhamiria kuonyesha mchuano mkali wa ‘Manchester Derby’ uliopaswa kuchezwa jijini Beijing, China lakini kwa bahati mbaya ukaahirisha kutokana na hali ya hewa kuwa mbaya na hivyo wateja wakapewa kutazama marudiano ya mchezo baina ya Manchester United na Borrusia Dortmund ambapo Dortmund waliibamiza United kwa magoli 4 - 1.

Monday, July 25, 2016

Diwani Akwepa Risasi sita akipambana na majambazi Moshi

Diwani wa Kata ya Kiborlon (Chadema) katika Manispaa ya Moshi, Frank Kagoma ameonyesha ujasiri wa hali ya juu alipopambana na majambazi waliokuwa na silaha za moto.

Askofu Gwajima amjibu Katibu Mkuu wa zamani wa CCM, Yusuf Makamba aliyemuita muongo

Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amemjibu katibu mkuu wa zamani wa CCM, Yusuf Makamba aliyemtuhumu kuwa ni mwongo akisema leseni yake ni ya kuendesha magari makubwa na siyo vibajaji na maguta.

Friday, July 22, 2016

Kesi za Uhujumu Uchumi zaigiza Bilioni 29

Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Harrison Mwakyembe amesema Mahakama Kuu chini ya kitengo kinachosimamia kesi za kuhujumu uchumi imetoa adhabu ya kifungo na kulipa faini ya Sh29 bilioni kwa watu 12 baada ya kutiwa hatiani.

JWTZ yasema wapo tayari kukabiliana na ugaidi Afrika

Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limesema lipo tayari kukabiliana na ugaidi nchini na kwingineko barani Afrika. 

DC WA IKUNGI AFIWA NA MDOGO WAKE MOHAMED MKONONGO MTATURU

Mohamed Mkonongo Mtaturu enzi za uhai wake
 
Asanteni sana kwa faraja zenu kwa msiba wa ghafla wa Mdogo wangu na rafiki yangu Mohamed Mkonongo Mtaturu nilipokea simu leo asubuhi muda wa saa 1:48 ya msamaria mwema akitumia simu ya marehemu akinijulisha amepata ajali daraja la salender akaniita nikamsaidie mdogo wangu, hakika alijua naweza kumsaidia kumbe msaada mkubwa upo kwa mungu aaah inaniuma sana pumzika kwa amani mdogo wangu katika umri wako wa miaka 43 umejitahidi sana kuisaidia jamii,

WANACHAMA WA CUF KUPIGA HODI KWA IGP MANGU ENDAPO ATAENDELEA KUKIFUATILIA CHAMA HICHO

Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Tanzania Bara, Shaweji Mketo, akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam , wakati wa kutoa msimamo wa chama hicho kuhusu mikakati ya Jeshi la Polisi dhidi ya vyama vya siasa hasa cha Cuf. Kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Ulinzi Taifa, Mustafa Wandu na Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Zanzibar, Nassor Ahmed Mazrul.

MOTISHA YA NUNUA, UZA, SHINDA NA KONYAJI YAZINDULIWA KANDA YA ZIWA

Meneja Masoko na Udhaamini wa Kampuni ya TBL, George Kavishe (wa pili kulia), akizungumza katika Uzinduzi wa Motisha Mpya ya Nunua, Uza, Shinda na Konyagi kwa Wasambazaji wa kinywaji cha Konyagi Kanda ya Ziwa ambao ulifanyika jana Jijini Mwanza.

Tuesday, July 19, 2016

DC MTATURU AKUTANA NA WAZEE WA WILAYA YA IKUNGI AWAAHIDI KUFANYA KAZI KWA BIDII

 Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Miraji J. Mtaturu akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wazee waliowawakilisha wazee wengine wilayani humo

Monday, July 18, 2016

RC Makonda afanya uzinduzi wa NAS-DAR AIRCO nchini, kwa kuanza watanzania 60 wapata ajira

Katika kipindi ambacho Tanzania inaendelea kukua kwa kasi kiuchumi na hivyo kuwepo kwa wageni wengi ambao wamekuwa wakiwasili nchini, kampuni ya Mwanza Ground Handling Company (AIRCO) imeungana na kampuni nyingine ya National Aviation Services (NAS) ili kutoa huduma katika Uwanja wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere kwa kuboresha huduma zinazotumia usafiri wa anga kwa kuhudumia abiria, ndege na shughuli za mizigo.

SERIKALI YATOA MSIMAMO WAKE KUHUSU BENKI YA TWIGA BANCORP

 Msajili wa Hazina, Lawrence Mafuru (katikati), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, kuhusu msimamo wa Serikali kuhusu Benki ya Twiga Bancorp. Kulia ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki hiyo, Cosmas Kimario na Mkurugenzi  Rasilimali Watu na Utawala, Amina Lumuli.

Msajili wa Hazina amaliza maneno kuhusu Twiga Bancorp, asema itaendelea kuhudumia wateja kama kawaida

Msajili wa Hazina amaliza maneno kuhusu Twiga Bancorp, asema itaendelea kuhudumia wateja kama kawaida

Kumekuwepo na maneno mengi ambayo yamekuwa yakizungumzwa kuhusu benki ya Twiga Bancorp, tangu Rais John Magufuli alipoiagiza Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kuchukua hatua kwa benki zote ambazo zimekuwa hazifanya vizuri ikiwepo benki ya Twiga na hivyo wananchi wengi wakawa wakiamini kuwa benki hiyo itafutwa

LAPF YATOA MSAADA WA MASHUKA 375 KWA HOSPITALI YA WILAYA YA KISARAWE MKOANI PWANI

 Mganga wa Hospitali ya Wilaya ya Kisarawe, Elizabeth Oming'o (kulia), akitoa historia fupi ya hospitali hiyo kabla ya kumkaribisha Mbunge wa Kisarawe ambaye pia ni Naibu Waziri wa Tamisemi, Suleiman Jaffo (wa pili kulia), kupokea msaada wa mashuka 375 yenye thamani ya sh.milioni nane kutoka Mfuko wa Pensheni wa LAPF katika hafla ya makabidhiano yaliyofanyika juzi hospitalini hapo. Kutoka kushoto ni Katibu wa Madiwani wa Halmshauri hiyo, Jnady Chakachaka na Mwenyekiti wa Huduma za Jamii wa Kisarawe, Abel Mudo.

Askofu Gwajima Aibuka.

KIONGOZI wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Askofu Josephat Gwajima, amefunguka kwa kuelezea safari yake aliyoifanya nje ya nchi hivi karibuni, baada ya taarifa mbalimbali kudai kuwa alilikimbia Jeshi la Polisi.

Chenge Akaidi Agizo la Jeshi la Polisi

Agizo la Jeshi la Polisi nchini la kusitisha kufanyika kwa mikutano ya hadhara ya kisiasa imeonekana kutoathiri ratiba za Mbunge wa Bariadi, John Chenge ambaye ameendelea na mikutano ya hadhara jimboni kwake.

KONGAMANO LA VIJANA WAJASIRIAMALI NA WAWEKEZAJI MKOANI MWANZA LAFANYA

Mgeni Rasmi, Meneja wa Shirika la kuhudumia Viwanda Vidogo SIDO mkoani Mwanza, Damian John Changa, akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Biashara, Viwanda na Uwekezaji, katika ufungaji wa Kongamano la Vijana Wajasiriamali na Wawekezaji mkoani Mwanza lililohitimishwa jana katika Viwanja vya Gandh Hall Jijini Mwanza. 

UNESCO YAKUTANISHA WADAU KUJADILI USAFI WA MAJI, HALI YA USALAMA BADO SI NZURI

Mkurugenzi Msaidizi wa Rasilimali za Maji kutoka Wizara ya Maji na Umwagiliaji, George Lugomela akitoa hotuba kwa niaba ya serikali katika kongamano hilo. (Picha na Modewjiblog)
"Kongamano hili linaangalia kuhusu vijidudu vilivyo katika maji ambavyo kwa asilimia kubwa yanachafuka kutokana na usafi ambao anaufanya binadamu na ukiangalia kwa nchi zetu inaonyesha bado uhifadhi wa hizo taka kama kinyesi ambacho baadae huathiri vyanzo vya maji ni mdogo," alisema Lugomela.

WANAHABARI JIJINI MWANZA WAMLILIA MAREHEMU MWALIMU SOKORO, ALIEKUWA MHARIRI WA BARMEDAS TV.

Aliekuwa Mhariri wa miaka mingi wa Barmedas Tv ya Jijini Mwanza, Mwalimu Charles Sokoro, enzi za uhai wake. Marehemu Sokoro alifariki dunia jumamosi julai 16,2016 majira ya saa mbili usiku katika hospitali ya Rufaa Bugando alikokuwa amelazwa kwa siku kadhaa.

Saturday, July 16, 2016

DC MTATURU AKABIDHI OFISI YA CCM MKOA WA MWANZA

Dc Mtaturu (kushoto) akikabidhi nyaraka za ofisi ya ccm mkoa wa mwanza kwa katibu wa CCM Wilaya ya Nyamagana Elias Mpanda

Friday, July 15, 2016

ASKOFU DK. CHARLES GADI KUONGOZA MKUTANO MKUBWA WA KUOMBEA TAIFA VIWANJA VYA BIAFRA JIJINI DAR ES SALAAM

 Mwenyekiti wa Good News for All Ministtry (Great Vition 2000), Askofu Dk.Charles Gadi (wa pili kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi kuhusu mkutano mkubwa wa kuombea Taifa kila Jumanne kwa siku 1001 utakaofanyika kuanzia Julai 19, 2016 viwanja vya Biafra jijini Dar es Salaam. Kutoka kulia ni Mchungaji James Manyama, Palemo Massawe na Mchungaji Leonard Kajuna.

Sitta ahamishwa nyumba ya Serikali,Awamu ya tano yagoma kumlipia kodi ya pango, Ahamia Mtaa wa Manzese

ALIYEKUWA Spika wa Bunge la tisa, Samuel Sitta, ameondolewa kwenye nyumba aliyokuwa akiishi baada ya Serikali kugoma kumlipia kodi ya pango.

KUTANA NA STAA WA MTAA MWENYE NDOTO ZA KUWA STAA WA KIMATAIFA.

Kutana na kijana Biela Alex kutoka Mtaa wa Mji Mwema Mkudi, Kata ya Isamilo Jijini Mwanza. Anasema yeye ni staa wa mtaa wao na ndoto yake kubwa kwa sasa ni kuwa staa mkubwa wa muziki na maigizo kimataifa zaidi.

Wednesday, July 13, 2016

WAZAZI WATAKIWA KUWA MAKINI NA MARAFIKI WA WATOTO WAO

Mkurugenzi wa Shule ya Watoto ya O'Jays Kiddies Zone, Usia Nkhoma Ledama (kushoto) akizungumza na mmoja wa wazazi Bw. Ally Msoya alipowasili kwenye mahafali ya nne ya shule hiyo yaliyofanyika katika ukumbi wa Msasani Tower jijini Dar es Salaam.(Picha zote na Modewjiblog)

Vinara wa Kutengeneza nyaraka bandia za Serikali watiwa mbaroni

Watu watatu wanaosadikiwa kuwa vinara wa kutengeneza vyeti bandia pamoja na nyaraka mbalimbali za Serikali wamekamatwa eneo la Buguruni wakiwa na mitambo yao. 

Kukamatwa kwao kulitokana na msako mkali uliofanywa na Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam hivi karibuni na hatimaye watuhumiwa walinaswa wakiwa nyumbani wanakoishi eneo la Buguruni Ghana wakitengeneza nyaraka bandia.

Mfanyabiashara Anayedaiwa Kujipatia Milioni 7 Kwa Dakika Afikishwa Mahakamani Na Kusomewa Mashitaka 199

Mfanyabiashara Mohamed Mustapha (anayeongea na simu) na wenzake, wakiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam jana kukabiliana na tuhuma za kuibia Serikali kodi ya Sh milioni 7 kwa kila dakika kwa kipindi kirefu.

NYOTA YA WAPANCRASS KUTOKA KANDA YA ZIWA YAZIDI KUNG'ARA.

Baada ya wimbo wao uitwao Chausiku kufanya vizuri sokoni, Wasanii Payus (kushoto) na Mecrass (kulia) kutoka Jijini Mwanza ambao wanaunda kundi la Wapancrass, nyota yao imezidi kung'ara zaidi katika muziki.

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, ANGELINE MABULA AFUNGUA MKUTANO WA WADAU WA UENDELEZAJI MILKI JIJINI DAR ES SALAAM LEO

 Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angeline Mabula (kushoto), akihutubia wakati akifungua mkutano wa wadau wa uendelezaji milki uliofanyika Makao Makuu ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Upanga jijini Dar es Salaam leo asubuhi. Kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Usimamizi Milki, Hamad Abdallah, Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Nehemia Mchechu, Mkurugenzi wa Nyumba wa wizara hiyo, Charles Mafuru na Mkurugenzi wa Fedha wa NHC, Felix Maaly. Mkutano huo uliandaliwa na NHC.

JE MAFUNDI CHEREHANI WOTE, MWALIMU WAO NI MMOJA?

Na BMG
Nalazimika kuyaandika haya baada ya jana kusikia mteja mmoja akimlalamikia fundi wake wa nguo (fundi cherehani japo kiuhalisia yeye ni mshonaji wa ngu), kutokana na fundi huyo kutokamilisha ushonaji wa nguo yake ambayo alitarajia kuivaa kwenye shughuli (Send Off) kwa wakati.

Sunday, July 10, 2016

Jeshi la Polisi Latoa ONYO Kali Kwa Vyama vya Siasa.

ONYO limetolewa kwa vyama vya siasa vinavyojaribu kusuguana na Jeshi la Polisi kukumbuka kuwa hilo ni jeshi, ambalo liko tayari kutumia nguvu na rasilimali zote, kuhakikisha raia na mali zao ni salama.

Viongozi Watatu wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha) Watiwa mbaroni Mkoani Dodoma


JESHI la Polisi mkoani Dodoma linawashikilia viongozi watatu wa Baraza la Vijana la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Bavicha) Taifa, kwa uchochezi na kuikashifu serikali.

Mtatiro Amtaka Profesa Lipumba Apumzike Uongozi.

ALIYEKUWA Naibu Katibu Mkuu wa CUF (Bara), Julius Mtatiro amesema hana mpango wa kugombea nafasi ya Uenyekiti wa chama hicho, licha ya kuwepo kwa msukumo mkubwa wa kumtaka agombee.

Wanawake walia Magufuli ‘kuwabania’ katika uteuzi

Mashirika yanayotetea haki za wanawake na usawa wa kijinsi nchini yamesema uteuzi wa nafasi muhimu za uongozi serikalini unaofanywa na Rais John Magufuli, hauzingatii hali halisi ya uwakilishi wa kijinsia. 

Lowassa Awapa Chadema ‘ukweli mchungu'


Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa amewataka viongozi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kutokatishwa tamaa na hali ya kisiasa nchini hususan marufuku za mikutano yao ya kisiasa pamoja na misukosuko mingine wanayopitia.

MBUNGE VENANCE MWAMOTO AKABIDHI MABATI YENYE THAMANI YA SHILINGI MIL.MOJA NA LAKI MBILI

 mbunge wa jimbo la kiloloVenance Mwamoto akikabidhi mabati 57 yenye zaidi ya Mil.moja kwa uongozi wa kata ya nyanzwa
Na fredy mgunda,Kilolo

WANANCHI wa  kata ya Nyanzwa iliyopo katika kijiji cha Nyanzwa Wilaya ya Kilolo Mkoani Iringa wamemuomba mbunge wa Jimbo hilo Venance Mwamoto kuwasaidia kumalizia ujenzi wa Nyumba za walimu zilizopo kwenye kata hiyo ili kuondokana na changamoto ya walimu kuishi mbali na eneo la shule.

Friday, July 8, 2016

WAZIRI MKUU APIGA STOP UVUNAJI MITI/MBAO KATIKA MISITU YAKE

Moja kati ya Mashamba makubwa ya mbao.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ametangaza rasmi kusitisha utoaji  wa vibali vya uvunaji wa mbao kutoka katika mashamba nane ya miti ya kupandwa yanayosimamiwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS).

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More