Monday, April 27, 2015

Frank kibiki awaokoa watoto waliofanyiwa ukatili wa kijinsia mkoa wa iringa

 mwanahabari frank kibiki  , aliyewahi kuwa katibu wa umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi (uvccm) ngazi ya wilaya kwa zaidi ya miaka 10 na ambaye ni mjumbe wa nec akiwa na  watoto waliofanyiwa ukaliti wa kijisia pamoja mkuu wa kituo cha matumaini centre
mwandishi wa habari wa gazeti la mzalendo na uhuru TUMAINI MSOWOYA KIBIKI akiwa na watoto waliofanyiwa ukatili wa kijinsia
mwandishi wa habari wa gazeti la mzalendo na uhuru TUMAINI MSOWOYA KIBIKI akiwa na watoto waliofanyiwa ukatili wa kijinsia pamoja na mkuu wa kituo cha matumaini centre.

na fredy mgunda,iringa

Ukatili wa kijinsia kwa watoto wa kike ndio inaonekana kuwa sababu  ya mkoa wa iringa kuzalisha wafanyakazi wengi wa kazi za ndani

akizungumza na blog hii mwanahabari frank kibiki  , aliyewahi kuwa katibu wa umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi (uvccm) ngazi ya wilaya kwa zaidi ya miaka 10 na ambaye ni mjumbe wa nec.amesema kuwa watoto wengi wa kike hawapewi nafasi ya kwenda kusoma kutokana na tamaduni potofu hivyo waandishi wa habari tunatakiwa kuungana kuwapigania watoto hawa.

Aidha KIBIKI amewataka wananchi wa mkoa wa iringa kushirikiana na mkuu wa kituo cha matumaini centre ili kuwasaidia watoto wa kike ambao wanaishi katika kituo hicho.

lakini KIBIKI amewaomba viongozi mbalimbali na waandishi wa habari kupaza sauti zetu ili kukomeshakabisha suala la ukatili wa kijinsia ambao bado unaendelea hapa mkoani kwetu.

Wananchi mkoani iringa wametakiwa kuwathamini na kuwapa elimu watoto wa kike ili kupunguza unyanyasaji wa kijinsia unaoendelea kwa sasa.

Kwa upande wake mkurugenzi kituo cha matumaini centre HELLEN NKUNDA amesema kuwa amekuwa akipokea watoto wengi wa kike ambao wamefanyiwa ukatili wa kijinsia  na amekuwa akiwapokea na kuwapa elimu ya ufundi.

Lakini NKUNDA amewataka watoto hao kuwa makini na waaminifu katika maisha yao ili wasirudie yale ambayo yalimtokea hapo awali na wasikubari kudanganywa tena.

NKUNDA ameitaka serikali  kutoa elimu kuanzia shule ya msingi juu madhara ya ukatili ili kujenga jamii ambayo itakuwa na elimu juu ya unyanyasaji na ukatili wa kijinsi hasa kwa watoto wa kike.

Alimalizia kwa kumshukuru mwandishi wa habari frank kibiki kwa kutoa msaada wake kwa mtoto ambaye aliyekuwa amefanyiwa ukatili wa kijinsia.





MNUSO WA UZINDUZI WA SHAMRA SHAMRA ZA MIAKA 70 YA UMOJA WA MATAIFA WAFANA JIJINI DAR

DSC_0351
Cake maalum iliyoandaliwa kwenye sherehe za uzinduzi wa shamra shamra za miaka 70 ya Umoja wa Mataifa uliofanyika mwishoni mwa juma kwenye hoteli ya White Sands jijini Dar es Salaam.
DSC_0354
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (katikati) akiteta jambo na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la UN Women nchini Tanzania, Anna Collins kabla ya zoezi la kuwasha mishuma 70 kwenye cake hiyo ikiwa ni uzinduzi wa shamra shamra za miaka 70 ya Umoja wa Mataifa. Kushoto ni Mshehereshaji wa sherehe hizo Afisa Habari wa kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Usia Nkhoma Ledama.
DSC_0382
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (wa pili kulia) na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la UN Women nchini Tanzania, Anna Collins wakiwa wamejumuika na wafanyakazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa kwenye mnuso huo.
DSC_0361
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (wa pili kushoto) akiwasha nakshi nakshi zilizowekwa kwenye cake maalum ya uzinduzi wa shamra shamra za miaka 70 ya Umoja wa Mataifa nchini. Anayemkingia upepo ni walioandaa Cake hiyo kutoka kampuni ya M.E Gift Wraps and Delivery huku Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la UN Women nchini Tanzania, Anna Collins naye akijianda kufanya zoezi hilo.
DSC_0372
Wafanyakazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini wakishiriki kuwasha mishumaa 70 iliyowekwa kwenye cake hiyo.
DSC_0380
IMG_0162
DSC_0388
Wafanyakazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa wakikata cake kwa niaba ya wafanyakazi wenzao.
DSC_0396
DSC_0404
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (kulia) akila kipande cha cake kwenye mnuso huo.
DSC_0407
Wafanyakazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini Tanzania wakilishana cake kabla ya kupata chakula cha usiku wakati wa shamra shamra za uzinduzi wa miaka 70 ya Umoja wa Mataifa.
DSC_0412
Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce Temu (kushoto) akibadilishana mawazo na wafanyakazi wenzake.
IMG_0172
Pichani juu na chini ni wafanyakazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini wakijumuika kwenye chakula cha usiku wakati wa sherehe za uzinduzi wa shamra shamra za miaka 70 ya Umoja wa Mataifa Tanzania.
IMG_0179
IMG_0188
IMG_0225
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akifuatiwa na Afisa Habari wa UNIC, Usia Nkhoma Ledama wakipakua chakula cha jioni kwenye mnuso huo.
IMG_0190
IMG_0193
Pichani juu na chini ni wafanyakazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa wakijisevia nyama choma ndani ya hoteli ya White Sands.
IMG_0220
IMG_0197
IMG_0202
IMG_0213
IMG_0207
IMG_0222
BAADA YA KUPATA BUFEE LA NGUVU ULIWADIA ULE WASAA WAKUFANYA DIGESTION YA CHAKULA KWA KUSAKATA RHUMBA...
IMG_0253
Wafanyakazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa wakisakta rhumba kwenye hafla ya uzinduzi wa shamra shamra za miaka 70 ya Umoja wa Mataifa nchini.
IMG_0303
Wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa wakionyesha ufundi wa kusakata rhumba kwenye mnuso huo.
DSC_0502
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (mwenye shati ya kijivu) naye hakubaki nyuma alionyesha umahiri wake.
DSC_0493
Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la UN Women nchini Tanzania, Anna Collins naye alionyesha ufundi wake kama anavyoonekana pichani.
DSC_0484
Usia Nkhoma Ledama naye akasema hata wasinichezee hawa.... akajibu mapigo.
DSC_0487
Burudani ikiendelea kwa furaha na amani.
DSC_0533

Thursday, April 23, 2015

KATIBU WA CCM MKOA WA IRINGA HASSAN MTENGA AENDELEA KUVURUNGA MIPANGO YA WAPINZANI KATIKA JIMBO LA ISMANI

 katibu wa CCM mkoa wa iringa HASSAN MTENGA akiwahutubia wananchi wa tarafa ya pawaga.
 katibu wa CCM mkoa wa iringa HASSAN MTENGA akijibu maswali ya wananchi wa tarafa ya pawaga.
katibu wa CCM mkoa wa iringa HASSAN MTENGA akiwapa vifaa vya michezo wananchi wa tarafa ya pawaga

na fredy mgunda,iringa

katibu wa chama cha mapinduzi  mkoa wa iringa hassani mtenga  amewataka wananchi wa tarafa ya pawaga katika jimbo la isimani kuendelea kumwamini mbunge wa jimbo hilo kwa kuwa anawatendea haki kwa kuwaletea maendeleo.

akizungumza katika mkutano huu  katibu wa chama hicho MTENGA  amewataka wananchi kuendelea kukiamini chama hicho kutokana na kutekeza ahadi zao ambazo wanakuwa wanaziahidi kwa wananchi.

Kwa upande wao wananchi kijiji cha boliboli kilichopo tarafa ya pawaga wilaya ya iringa vijijini  wanakabiriwa na matatizo ya kiafya pamoja na migogoro ya aridhi baina ya wafugaji na wakulima hayo yamebaini katika mkutano ulifanyika katika kijiji hicho.

wakizungunza wakati wa mkutano huo wananchi hao wamesema kuwa  kijiji hicho hakina mganga wa kutoa huduma katika zahanati yao na kuongeza kuwa tatizo la migogolo ya aridhi limekuwa kubwa.

Akijibu maswali ya wananchi hao katibu wa ccm mkoa wa iringa hassani mtenga  amewata  viongozi wa chama hicho kufanya mikutano ya mara kwa mara na kupokea kero za wananchi na kuzitatua mapema ili kuendelea kukijengea imani chama chao.

Viongozi wengi wamekuwa hawawajali wananchi wao ambao wamewaweka matarakani na ndio imekuwa sababu ya matatizo mengi na migogolo mikubwa katika vijijini.

Lakini MTENGA amesema swala mfureji,tatizo la mganga,walimu kuwa walevi na mgogoro wa mbomipa anayachukua na kwenda kuyafanyia kazi na kuwaahidi kuwa matatizo yote waliomweleza yatatulika.

“Alimalizia kwa kuwaomba wananchi kuipigia kura katiba inayopendekezwa ili waweze kupata katiba ya wananchi na kuwaambia wananchi wa eneo hilo kuitumia fursa ya kuijiandikisha katika daftari la kudumu la kupigia kura ambalo iringa litaanza tarehe 29 mwezi huu” alisema HASSAN MTENGA.

mwisho.

Friday, April 17, 2015

VIJANA WA CCM IRINGA WAMPA NGUVU KATIBU WA MKOA HASSAN MTENGA KUKOMBOA JIMBO, LA IRINGA MJINI.

Mtenga katika kikao na baadhi ya vijana hao




KIU ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Manispaa ya Iringa kukomboa jimbo la Iringa Mjini katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu inazidi kuongezeka, baada ya umoja wake wa vijana (UVCCM Manispaa ya Iringa) kuahidi kuongeza nguvu ili kuufanikisha mkakati huo.

CCM ililipoteza jimbo hilo katika Uchaguzi Mkuu wa 2010 kwa Mchungaji Msigwa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) anayekaribia kumaliza muda wake.

Katika kikao kilichozikutanisha sekretarieti za umoja huo kutoka katika kata zote 18 za manispaa ya Iringa, Mwenyekiti wa UVCCM wa manispaa hiyo, Kaunda Mwaipyana alisema; “katika kukisaidia chama kushinda uchaguzi huo, kauli mbiu yetu ni chama kwanza mtu baadaye.”

“Tutapita katika matawi na kata zetu zote, tutafanya vikao, mikutano ya hadhara na kuwakumbusha vijana wajibu wa kukipigania chama chao ili mkakati wa kulikomboa jimbo ufanikiwe,” alisema.

Katibu wa CCM wa Mkoa wa Iringa, Hassan Mtenga aliwaongezea hamasa vijana hao kwa kuwapa seti 60 za jezi na mipira watakazozitumia kuwahamasisha vijana hao kupitia mchezo wa soka.

“CCM ina vijana wengi sana katika jimbo hili, mnahitaji kukutana na kujipanga, tumieni mbinu zote za kukutana, iwe  vikao, mikutano na hata michezo na ndio maana nimewapa msaada huu,” alisema.

Aliwataka vijana wa chama hicho kujitokeza kwenye vikao visivyo rasmi vya maeneo yao wanayoishi na kuitetea CCM kwasababu majibu ya hoja nyingi za wapinzani wanayo.

Akiwakabidhi jezi hizo, Mwenyekiti wa Umoja wa Wazazi wa CCM Mkoa wa Iringa, Ephraim Mhekwa alisema  CCM inayo nafasi ya kulikomboa jimbo hilo kama itajipanga vizuri.

“Pamoja na kwamba wapinzani walipata viti 65 katika uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka jana, wasisahau kwamba CCM ilipata viti 126; hesabu hiyo inadhihirisha chama chetu kinaungwa mkono mara mbili yao,” alisema.

Aliwataka vijana hao kuweka bendera za chama hicho kila panapostahili katika mitaa yote na akawasihi wasikubali kutumika na kukigawa chama kwa maslai ya wachache.

Naye Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, Mahamudu Madenge alisema CCM itaendelea kuwepo hata kama watu wasiotaka kufuata utaratibu wataondoka.

“Wameondoka wengi, wengine hii leo ni viongozi wa vyama vikubwa vya siasa. Pamoja na kuondoka kwao CCM ipo pale pale na inaendelea kupata wanachama,” alisema

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More