Thursday, November 30, 2017

MHE MWANJELWA AMUAGIZA MKURUGENZI KUMSIMAMISHA KAZI MSIMAMIZI WA ZAO LA PARETO KUPISHA UCHUNGUZI

Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa  akizungumza wakati wa Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Jojo Kata ya Santilya akiwa kwenye ziara ya kikazi Katika Mikoa ya Nyanda za Juu kusini Kwa Tanzania, Jana Novemba 29, 2017. Picha zote Na Mathias Canal
 Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa  akisisitiza jambo wakati wa Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Jojo Kata ya Santilya akiwa kwenye ziara ya kikazi Katika Mikoa ya Nyanda za Juu kusini Kwa Tanzania, Jana Novemba 29, 2017.
 Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa  akizungumza wakati wa Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Jojo Kata ya Santilya akiwa kwenye ziara ya kikazi Katika Mikoa ya Nyanda za Juu kusini Kwa Tanzania, Jana Novemba 29, 2017.
 Baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Jojo Kata ya Santilya wakimsikilkiza Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akitoa maelekezo ya serikali kuhusu zao la Pareo akiwa kwenye ziara ya kikazi Katika Mikoa ya Nyanda za Juu kusini Kwa Tanzania, Jana Novemba 29, 2017.
 Mbunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini Mhe Oran Njeza akizungumza katika mkutano huo kufikisha kilio cha wananchi mbele ya Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwwa kuhusu zao la Pareto na matatizo la wafanyabiashara kujaza Lumbesa kwenye uuzaji wa mazao mbalimbali likiwemo zao la viazi wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika Kijijini Jojo Kata ya Santilya, Jana Novemba 29, 2017.
Baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Jojo Kata ya Santilya wakimsikilkiza Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akitoa maelekezo ya serikali kuhusu zao la Pareo akiwa kwenye ziara ya kikazi Katika Mikoa ya Nyanda za Juu kusini Kwa Tanzania, Jana Novemba 29, 2017.

Na Mathias Canal, Mbeya

Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa Jana Novemba 29, 2017 amemuagiza Mkurugenzi Wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya kumsimamisha kazi Afisa Kilimo Wilaya ya Mbeya anayesimamia zao la Pareto Ndg Emmanuel Halinga ili kupisha uchunguzi.

Mhe Naibu Waziri ametoa agizo hilo wakati wa Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Jojo Kata ya Santilya akiwa kwenye ziara ya kikazi Katika Mikoa ya Nyanda za Juu kusini mwa Tanzania mara baada ya Mhe Mbunge wa Jimbo hilo Mhe Oran Njeza na Wananchi wote waliokuwepo kwenye mkutano huo wa hadhara kumrushia shutuma nzito na kumkataa mtaalamu huyo wa kilimo mbele ya Naibu Waziri.

Alisema kuwa pamoja na zao hilo la Pareto kuwa la kwanza kwa uzalishaji katika nchi za Afrika huku likiwa zao la pili kwa uzalishaji Duniani lakini bado halijamkomboa Mkulima nchini jambo ambalo linaonyesha namna ambavyo baadhi ya wataalamu Wa Kilimo wameshindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

Alisema kuwa wataalamu wa kilimo walipaswa kusimamia kwa kiasi kikubwa zao hilo kwani Pato lake ni wastani wa tani 2000 kwa mwaka sawa na Bilioni 12 mpaka 14 ambapo katika kipindi hili bei ya kuanzia Mkulima analipwa shilingi 2300 kwa kilo lakini inapanda mpaka shilingi 3300 kulingana na ubora wa zao hilo ambalo mkulima amelima.

Alisema kuwa serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Mhe Rais Wa Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli inaamini katika kazi ambazo matokeo yake yanapaswa kuonekana hivyo Mkulima kushindwa kunufaika na mazao ya Kilimo ni uzembe wa baadhi ya wataalamu Wa Kilimo unaosababishwa na kufanya kazi kwa mazoea.

Aidha, Mhe Mwanjelwa ametoa siku saba kwa Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya Pareto nchini Ndg Lucas Ayo kutoa sababu za kwanini mnunuzi ni mmoja wa zao hilo jambo ambalo linaonyesha kuwa na harufu ya rushwa au kupelekea kudumaza solo la zao hilo kwa kuwa na mnunuzi mmoja asiyekuwa na ushindani.

Ili kuongeza ufanisi wa zao hilo Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa ameelekeza wakulima Kuanzisha vikundi vya vyama vya ushirika vya msingi ambavyo vitakuwa na usajili serikalini kwani vitasaidia kuwa na mjadala wa jinsi ya kuwa na ubora wa zao la pareto jambo litakalopekea kuanzisha viwanda vidogo ambavyo ni ishara ya kuunga mkono juhudi za Rais Magufuli kuwa na Tanzania ya Viwanda.

"Mkishaanzisha tu vikundi vya vyama vya ushirika mtoe taarifa mapema iwezekanavyo na serikali kupitia mrajisi itatoa Elimu ya ushirika" Alikaririwa Mhe Mwanjelwa

Ameagiza zao la Pareto kuwa huru ili mkulima awe huru kuuza kwa mnunuzi anayemtaka kwani kwa sasa kuna mnunuzi mmoja tu ambaye anajipangia mwenyewe namna ya kununua zao hilo kwa gharama atakazo pasina kupingwa.

Pia alielekeza wakulima Kuingia kwenye Kilimo cha mkataba kati yao na Chama cha msingi (AMCOS) jambo litakalorahisisha kupata mikopo ya Kilimo kupitia Benki ya Kilimo nchini (TADB).

Kuhusu Lumbesa, aliwataka wafanyabiashara wa wanaojaza Lumbesa badala ya kujazwa kilo 100 kwa gunia lakini linajazwa mpaka kilo 120 kuacha haraka tabia hiyo kwani wanakwenda kinyume na sheria hivyo kwa yeyote atakayebainika atachukuliwa hatua Kali za kisheria.

TANESCO: HITILAFU KWENYE GRIDI YA TAIFA ASUBUHI HII

MAJIRA ya saa 7:20 leo hii Alhamisi Novemba 30, imetokea hitilafu kwenye Gridi ya Taifa na hivyo kusababisha umeme kukatika takriban kwenye mikoa yote iliyounganishwa kwenye Gridi hiyo.


Kwa mujibu wa Kaimu Meneja Uhusiano wa TANESCO, Bi. Leila Muhaji, mafundi na wataalamu wa Shirika la Umeme Tanzania TANESCO wameanza kufuatilia kujua chanzo chake hasa ni nini na taarifa Zaidi zitatolewa kila baada ya muda ili kuufahamisha umma na watuamiaji wa umeme.

Wednesday, November 29, 2017

MHE MWANJELWA AWATAKA WAJUMBE WA JUMUIYA ZA CCM KUCHAGUA VIONGOZI WAADILIFU NA WACHAPA KAZI

Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa, Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa Akizungumza kwenye Mkutano Mkuu Maalumu wa Umoja wa Wanawake wa CCM Mkoa wa Mbeya uliofanyika katika Ukumbi wa Shule ya Kutwa ya Mbeya, Jana Novemba 28, 2017.
Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa Akisakata rumba kwenye Mkutano Mkuu Maalumu wa Umoja wa Wanawake wa CCM Mkoa wa Mbeya uliofanyika katika Ukumbi wa Shule ya Kutwa ya Mbeya, Jana Novemba 28, 2017.
Makada wa CCM Mkoani Mbeya wakimlaki Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa Wakati akiondoka kwenye Mkutano Mkuu Maalumu wa Umoja wa Wanawake wa CCM Mkoa wa Mbeya uliofanyika katika Ukumbi wa Shule ya Kutwa ya Mbeya, Jana Novemba 28, 2017.
Makada wa CCM Mkoani Mbeya wakimlaki Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa Wakati akiondoka kwenye Mkutano Mkuu Maalumu wa Umoja wa Wanawake wa CCM Mkoa wa Mbeya uliofanyika katika Ukumbi wa Shule ya Kutwa ya Mbeya, Jana Novemba 28, 2017.

Na Mwandishi Wetu, Mbeya

Wajumbe wa Jumuiya mbalimbali za Chama Cha Mapinduzi (CCM) wametakiwa kuchagua viongozi waadilifu, weledi na wenye maono ya kuziongoza Jumuiya hizo ila kuendana na kasi ya Mwenyekiti wa CCM Taifa ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Akizungumza wakati wa Mkutano Mkuu Maalumu wa Umoja wa Wanawake wa CCM Mkoa wa Mbeya uliokuwa na Ajenda ya uchaguzi wa viongozi wa Jumuiya hiyo Mkoa na Taifa, Mhe Mwanjelwa ambaye ni mjumbe Halmashauri kuu ya CCM Taifa, Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa aliwasisitiza wajumbe hao kutochagua viongozi kwa matakwa ya urafiki na kujuana Bali kuchagua viongozi wa kazi watakaoisaidia jumuiya kuendana na mtazamo mpya wa CCM Mpya na Tanzania Mpya.

Mbali na kuwashukuru makada hao kwa kumchagua kuwa Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mbeya jambo lililopelekea Mhe Rais John Pombe Magufuli kumteua kuhudumu nafasi muhimu ya Kuwa Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mhe Mwanjelwa alisema kuwa serikali ya awamu ya tano ni ya kazi hivyo uchaguzi huo ni vyema kumalizika kwa kuwapata viongozi wachapakazi.

"Tunaelekea kwenye Mbeya Mpya, CCM Mpya, UWT Mpya na Tanzania Mpya hivyo msichague viongozi kutokana na makundi au watakaoendeleza makundi baada ya uchaguzi Bali chagueni viongozi shupavu na wachapakazi" Alikaririwa Mhe Mwanjelwa
Mhe Mwanjelwa (MNEC), alisema kuwa atafanya ziara katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Mbeya ili kuangalia jinsi utekelezaji wa ilani ya CCM inavyotekelezwa.

Mkutano huo Maalumu ulimalizika kwa salama hapo Jana Novemba 28, 2017 katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Mbeya ambapo viongozi mbalimbali walichaguliwa katika ngazi ya Mkoa na Taifa.

MWISHO

KENANI KIHONGOSI MWENYEKITI MPYA WA UVCCM MKOANI IRINGA

Mwenyekiti mpya wa umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi (UVCCM) mkoa wa Iringa Kenani Kihongosi akitangazwa na msimamizi mkuu wa uchaguzi huo uliofanyika katika manispaa ya Iringa.
 katibu wa chama cha mapinduzi (CCM) manispaa ya Iringa Marco Mbaga akimpongeza Mwenyekiti mpya wa umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi (UVCCM) mkoa wa Iringa Kenani Kihongosi kwa ushindi mkubwa aliupata na kuwa kiongozi wa jumuiya hiyo.
 Viongozi mbalimbali walimpongeza mwenyekiti mpya wa umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi (UVCCM) mkoa wa Iringa Kenani Kihongosi kwa kupata kura za kishindo na kuonyesha kuwa anakubalika na vijana wa chama hicho.

Na Fredy Mgunda,Iringa.

Hatimaye umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi (UVCCM) mkoa wa Iringa umempata mwenyekiti mpya bwana Kenani Kihongosi alichaguliwa kwa kura nyingi za kishindo na kurudisha matumaini mapya ya kuanza safari ya kuijenga CCM mpya kwa vijana wa mkoa huu wa Iringa.

Akizungumza mara baada ya kutangazwa kuwa ndiye msingi katika uchaguzi huo Kihongosi alisema kuwa atahakikisha jumuiya zote za umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi zinarudi na kufanya kazi kwa ushirikiano mkubwa na kuhakikisha wanapata wanachama wapya ambao itakuja kuwa nguzo ya chama hicho hapo baadae.

“Sasa ni wakati wa kufanya kazi kwa pamoja na kuhakikisha kila kitu kinaenda kama kilivyokusubiwa na kuhakikisha chama kinapata matokeo chanya kutoka kwetu vijana hivyo naomba mniunge mkono kuhikikisha tunakuwa wamoja” alisema Kihongosi

Kihongosi aliwataka vijana kufanya kazi na kuhakikisha wanaendelea kumuunga mkono Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuijenga CCM na Tanzania mpya.

“Sisi ndio vijana ambao tunatakiwa kuonyesha mfano kwa kufanya kazi na kuonyesha wapinzani wa mkoa wa Iringa kuwa sasa kuna UVCCM ambavyo inania ya kuhaikisha inaumaliza upinzani uliopo hapa mkoana na CCM ikachukua jimbo la Iringa Mjini” alisema Kihongosi

Aidha Kihongosi aliwashukuru wanachama wote wa umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi (UVCCM) mkoani Iringa kwa kumpigia kura za kuwa na imani naye na kuhakikisha anakuwa mwenyekiti wa umoja huo.

“Bila kura zenu mimi nisingekuwa mwenyekiti hivyo naona nitoe shukrani zangu za dhati kwenu wote kwa kunipa ushindi huu niweze kuwaongoza hivyo naomba mnipe ushirikiano wa kutosha ili tujenge UVCCM mpya hapa mkoani Iringa” alisema Kihongosi

DAWA ZA SARATANI ZAPATIKANA KWA ASILIMIA 80 % KUTOKA ASILIMIA 4%

  Mkurugenzi Mkuu wa MSD,  Laurean Bwanakunu (kulia), akizungumza na maofisa wa Hospitali ya Rufaa ya Amana wakati wa ziara yake ya kikazi ya siku moja Dar es Salaam leo ya kujua changamoto za upatikanaji wa dawa katika hospitali hiyo na kuzitafutia ufumbuzi. Kushoto ni Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Amana, Meshack Shimwela.
 Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Amana, Meshack Shimwela, akisisitiza jambo katika mkutano huo.
 Maofisa wa Hospitali ya Rufaa ya Amana wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa MSD,Laurean Bwanakunu.
 Meneja wa MSD Kanda ya Dar es Salaam , Celestine Haule akichangia jambo wakaz8i akizungumza na maofisa wa Hospitali ya Rufaa ya Amana.
 Mfamasia wa Hospitali ya Rufaa ya Amana, Anna Kajiru (kulia), akisisitiza jambo kwenye mkutano huo.
 Mkurugenzi Mkuu wa MSD,  Laurean Bwanakunu (wa sita kushoto), akiwa katika picha ya pamoja na maofisa wa Hospitali ya Rufaa ya Amana. 
 Mkutano ukiendelea.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road Dk. Julius Mwaiselage akizungumza katika mkutano huo.
 Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laurean Bwanakunu akisisitiza jambo wakati akizungumza na maofisa wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road katika ziara hiyo ya siku moja.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road Dk. Julius Mwaiselage ( kulia), akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laurean Bwanakunu wakati wa ziara hiyo.
Mkurugenzi Mkuu wa MSD,  Laurean Bwanakunu (wa tano kulia), akiwa katika picha ya pamoja na maofisa wa Taasisi ya Saratani Ocean. 

Na Dotto Mwaibale

TAASISI ya Saratani ya Ocean Road wameipongeza Bohari ya Dawa (MSD), kwa usambazaji wa dawa katika taasisi hiyo na maeneo mengine nchini.

Pongezi hizo zimetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road Dk. Julius Mwaiselage wakati akizungumza na watendaji wa MSD ambao walifanya ziara ya kikazi ya kujua changamoto mbalimbali za usambazaji dawa katika taasisi hiyo wakiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laurean Bwanakunu.

Katika hatua nyingine  upatikanaji wa dawa za saratani,vifaa tiba na vitendanishi  vya maabara katika taasisi hiyo ni asilimia 80  kutoka asilimia nne mwaka 2015.

Kutokana na hatua hiyo taasisi hiyo imesema ipo haja jamii kutambua mchango mkubwa unaotolewa na Bohari ya Dawa MSD katika kupunguza changamoto za huduma za saratani ambapo ilikuwa kero miaka miwili iliyopita.

 Mwaiselage alisema hapo awali  upatikanaji wa dawa vifaa tiba na vitendanishi ilikuwa ni changamoto kubwa katika utendaji.

"2015 taasisi hiyo ilikuwa ikipata dawa,vifaa tiba na vitendanishi asilimia nne sasa ni asilimia 80 haya ni matokeo mazuri ya utendaji wa kazi wa MSD," alisema.

Alisema bajeti ya taasisi hiyo mwaka 2015 ilikuwa ni sh.milioni 790 na sasa ni sh.bilioni saba jambo ambalo linatia faraja.

Mkurugenzi Mkuu wa MSD,  Laurean Bwanakunu alisema taasisi hiyo inatambua kuwa dawa za kansa ni gharama lakini atahakikisha zinaendelea kupatikana kwa wakati ili kuokoa maisha ya watanzania.

Alisema suala la vifaa vya maabara ni tatizo linalohitaji mpango wa kitaifa wa manunuzi.

"Nawahakikishia Ocean Road ni mteja muhimu hivyo nipo tayari muda wote kuwahudumia leteni orodha ya mahitaji ya dharura hata leo," alisema.

Mfamasia wa Hospitali ya Rufaa ya Amana, Anna Kajiru alisema katika Hospitali hiyo upatikanaji wa dawa kutoka MSD ni asilimia 80 na kuwa hali hiyo imetokana na ushirikiano mzuri baina yao.

"Hivi sasa hali ya upatikanaji wa dawa ambazo zinahitajika sana na wananchi ni mkubwa mkubwa tofauti na zamani na hii inatokana na kazi nzuri inayofanywa na ninyi MSD" alisema Kajiru.

Mkurugenzi wa MSD, Laurean Bwanakunu na maofisa wake yupo katika ziara ya kikazi ya kutembelea Hospitali za Mkoa wa Dar es Salaam ambapo leo alitembelea Hospitali ya Rufaa ya Amana na Saratani ya Ocean Road na kesho atazitembelea Hospitali ya Taifa ya  Muhimbili, Vijibweni na Temeke.


MAMBO 10 UNAYOTAKIWA KUYAFAHAMU KUHUSU UKIMWI

Na Jumia Travel Tanzania

Wakati dunia ikielekea kuadhimisha siku ya UKIMWI kila ifikapo Desemba mosi ya kila mwaka, bado Virusi Vya UKIMWI (VVU) na ugonjwa huo unabaki kuwa ni changamoto muhimu ya kiafya ndani ya jamii hususani kwenye nchi zenye kipato cha chini na kati.

Kutokana na maendeleo yaliyofikiwa sasa katika upatikanaji wa tiba ya mchanganyiko wa dawa zinazotumika kuzuia VVU kuongezeka mwilini (antiretroviral therapy - ART), watu waliogundulika kuwa na VVU wanaishi kwa muda mrefu na maisha yenye afya. Kwa kuongezea, imethibitishwa kwamba dawa hizo zinazuia kuendelea kuongezeka kwa VVU.

Katika kukupatia elimu zaidi juu ya ugonjwa huu, Jumia Travel ingependa kukufahamisha juu ya mambo yafuatayo ambayo yamebainishwa na Shirika la Afya Duniani (WHO), ambalo huunga mkono nchi mbalimbali katika kuunda na kutekeleza sera na programu ili kuboresha na kuongeza jitihada za kuzuia VVU, matibabu, huduma na kutoa msaada kwa watu wote wanaohitaji msaada.

Taafirifa hizi zinatoa takwimu zilizopo sasa kuhusu ugonjwa huu pamoja na njia za kuuzia na kuutibu:

VVU huambukiza seli za kwenye mfumo wa kinga za mwili. Maambukizi husababisha kuendelea kuzorota kwa mfumo wa kinga ya mwili, huvunja uwezo wa mwili kuweza kuepuka baadhi ya maambukizi na magonjwa. UKIMWI hujulikana kuwa ni hatua ya juu kabisa ya VVU ambapo hujipambanua kwa kujitokeza kwa maambukizi kati ya zaidi ya 20 au saratani zinahusiana na virusi hivyo.   

VVU vinaweza kuambukizwa kwa njia kadhaa. VVU vinaweza kuambukizwa kupitia: kujihusisha na ngono isiyo salama; kuhamishiwa damu au bidhaa inayohusiana na damu au kufanyiwa upandikizaji ambao sio salama; kushirikiana kutumia vifaa vya kutobolea mwili (sindano) na vimiminika au vya kuchorea michoro mwilini (tattoo); kutumia vifaa vya upasuaji na vinginevyo vyenye ncha kali; na maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto mchanga wakati wa ujauzito, kujifungua na kunyonyesha.   
Zipo njia kadhaa za kuzuia maambukizi ya VVU. Njia muhimu za kuzuia maambukizi ya VVU ni: kufanya ngono salama kama vile kutumia kondomu; kupima na kupatiwa matibabu kwa magonjwa yaliyoambukizwa kupitia ngono, ikiwemo VVU ili kuzuia maambukizi kuendelea; hakikisha kwamba damu au bidhaa yoyote inayohusiana na damu unayotaka kuitumia imepimwa VVU; chagua njia salama ya kimatibabu wakati wa tohara endapo unatoka katika nchi ambazo huchangia vifaa; kama una VVU anza mara moja kutumia dawa za kusaidia kupunguza virusi kuongezeka mwilini kwa manufaa yako na pia kuzuia kuambukiza VVU kwa mwenza au mtoto wako (kama ni mjamzito au unanyonyesha).  
Watu milioni 36.7 duniani wanaishi na VVU. Duniani kote, inakadiriwa kuwa watu milioni 36.7 (milioni 34.0 - 39.8) walikuwa wanaishi na VVU mwaka 2015, na kati ya hawa milioni 1.8 (milioni 1.5 - 2.0) walikuwa ni watoto. Idadi kubwa ya watu wanaoishi na VVU wanapatikana kwenye nchi zenye kipato cha chini na kati. Inakadiriwa watu milioni 2.1 (milioni 1.8 - 2.4) walipata maambukizi mapya ya VVU mwaka 2015. Inakadiriwa watu milioni 35 mpaka sasa wamefariki kutokana na VVU, wakiwemo milioni 1.1 (940,000 mpaka milioni 1.3) mwaka 2015.    
Mchanganyiko wa dawa za ART huzuia virusi hivyo kuongezeka mwilini. Endapo kuzaliana kwa VVU kukikoma, basi seli za kinga za mwili zitaweza kuishi kwa muda mrefu na kuupatia mwili kinga dhidi ya maambukizi. Ufanisi wa dawa za ART hupelekea kupungua kwa virusi, kiasi cha virusi mwilini, kwa kiasi kikubwa hupunguza kuambukiza virusi kwa watu walio kwenye mahusiano ya kimapenzi. Endapo mmojawapo wa wapenzi kwenye mahusiano anatumia dawa za ART ipasavyo, kuna uwezekano wa maambukizi ya njia ya ngono kwa mwenza ambaye hana VVU kupungua kwa kiasi cha takribani 96%. Kupanua wigo wa matibabu ya VVU kunachangia katika jitihada za kuzuia VVU.   
Katikati ya mwaka 2016, watu milioni 18.2 duniani walipokea dawa za kusaidia kuzuia VVU kuongezeka mwilini. Kati ya hawa zaidi ya milioni 16 wanaishi kwenye nchi zenye kipato cha chini na kati. Mwaka 2016, WHO ilitoa toleo la pili la “Miongozo juu ya matumizi ya dawa za kusaidia kuzuia kuongezeka VVU mwilini ili kutibu na kuzuia maambukizi ya VVU.” miongozo hii imetoa mapendekezo kadhaa, ikiwemo pendekezo la kutoa dawa za kusaidia kuzuia VVU kuongezeka mwilini kwa watoto kwa kipindi chote cha maisha yao, vijana na watu wazima, wakiwemo wanawake wajawazito na wanaonyonyesha waishio na VVU, licha ya idadi ya CD4 walizonazo mara baada tu baada ya kugundulika.          

Kupima VVU kunasaidia kuhakikisha matibabu kwa watu wenye uhitaji. Upatikanaji wa huduma ya kupima VVU na madawa unatakiwa kuongezeka kwa kasi ili kufikia lengo la kutokuwa na ugonjwa wa UKIMWI kufikia mwaka 2030. Upimaji wa VVU bado ni mdogo, ambapo inakadiriwa kwamba 40% ya watu wenye VVU au zaidi ya watu milioni 14 bado hawajatambulika na hawafahamu hali ya maambukizi yao. WHO inapendekeza ubunifu kwenye mbinu za kujipima wenyewe VVU na wenza wao ili kuongeza huduma za kupima VVU kwa watu ambao hawajagundulika.    
Inakadiriwa watoto milioni 1.8 duniani wanaishi na VVU. Kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2015, wengi wa watoto hawa wanaishi katika nchi zilizopo kusini mwa jangwa la Sahara na waliambukizwa kutoka kwa mama zao wenye VVU wakati wa ujauzito, wakati wa kuzaliwa au kunyonyeshwa. Karibu watoto 150,000 (110,000 - 190,000) walipata maambukizi mapya ya VVU mwaka 2015.
Kuondoa maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto inawezekana. Ufikiwaji wa hatua za kuzuia maambukizi ya VVU umekuwa ni mdogo kwenye nchi zenye kipato cha chini na kati. Lakini jitihada zimeendelea kufanyika kwenye baadhi ya maeneo tofauti kama vile kuzuia maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto pamoja na kuokoa maisha ya akina mama. Mwaka 2015, karibu wajawazito 8 kati ya 10 wanaoishi na VVU au sawa na wanawake milioni 1.1 walipokea dawa za kuzuia VVU kuongezeka mwilini. Mwaka 2015, Cuba ilikuwa ni nchi ya kwanza kutangazwa na WHO kufanikiwa kuzuia maambukizi ya VVU na Kaswende kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto. Mwaka 2016, nchi zingine tatu: Armenia, Belarus na Thailand nazo zilithibitishwa kulifanikisha hilo.        
VVU ni sababu kubwa inayopelekea kupata ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB). Katika mwaka 2015, inakadiriwa kuwa watu milioni 1.2 (11%) kati ya watu milioni 10.4 duniani waliopata TB walikuwa ni waathirika wa VVU pia. Mwaka huohuo takribani vifo 390,000 vilivyotokana na TB vilitokea miongoni mwa watu waliokuwa wanaishi na VVU. Nchi za Kiafrika ambazo zilizo chini ya WHO zilizidi karibu 75% ya idadi ya vifo vilivyokuwa vinahusiana kati ya TB na VVU.
UKIMWI ni janga ambalo linaikumba dunia nzima Tanzania ikiwemo, licha ya ugonjwa huu kutzungumziwa kwenye kampeni tunazozisikia lakini ukweli ni kwamba bado upo, ni tatizo, unaathiri na kuua nguvu kubwa ya taifa. Katika kuelekea kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani, Jumia Travel ingependa kuikumbusha jamii inapaswa kutambua kwamba jukumu la kuupiga vita ugonjwa huo bila ya kutegemea taasisi binafsi au mashirika ya nje.   

RITTA KABATI AKABIDHI MIFUKO 50 YA SARUJI KWA SHULE YA SEKONDARI YA IRINGA GIRLS

 MBUNGE wa viti maalum mkoa wa Iringa kwa tiketi ya chama cha mapinduzi  CCM Ritta Kabati akikabidhi mifuko ya sumenti kwa mwalimu wa shule ya Iringa Girls akiwa sambamba na diwani wa Kata ya Nduli Bashir Mtove
MBUNGE wa viti maalum mkoa wa Iringa kwa tiketi ya chama cha mapinduzi  CCM Ritta Kabati akikabidhi mifuko ya sumenti kwa wanafunzi wa shule ya Iringa Girls akiwa sambamba na diwani wa Kata ya Nduli Bashir Mtove

Na Fredy Mgunda,Iringa. 

MBUNGE wa viti maalum mkoa wa Iringa kwa tiketi ya chama cha mapinduzi CCM Ritta Kabati amechangia kiasi cha mifuko ya saruji 50 kwa shule ya sekondari ya Iringa Girls iliyoko katika manispaa ya Iringa kutokana na uhaba wa baadhi ya majengo ya shule hiyo.

Akizungumza na walimu na wanafunzi wa shule ya sekondari ya Iringa Girls Kabati alisema kuwa ameamua kujitolea kutoka kwenye posho yake kuhakikisha elimu kwa wanafunzi wa shule zilizopo mkoani Iringa wanasoma na wanapa elimu iliyo bora kutokana na ubora wa miundombinu iliyopo.

“ Nimetembelea shule nyingi mkoani kwetu hasa za msingi kuweza kuangalia miundo mbinu na majengo yake kwa kweli hali inatisha na majengo mengi yamekuwa chakavu hivyo nitajitahidi kwa kushirikiana na wadau wa elimu kuweza kukarabati yaendane na hali ya sasa ya kuwa bora zaidi” alisema Kabati

Hadi sasa Kabati amekwisha fanya ukarabati kwa shule za msingi za Azimio, Kihesa,Mtwivira na shule ya Kibwabwa ambazo alizitembelea na kubaini uchakavu mkubwa wa majengo na miundo mbinu mibaya na shule nyingine alizoahidi kuzifanyia ukarabati ni shule ya msingi Gangilonga.

Kwa upande wake mwalimu wa shule hiyo Bazila Kondo alimushukuru mbunge huyo kwa msaada wake alioutoa kwa kuwa utawasidia kujenga majengo ya mabweni ya wanafunzi hapa ambayo imekuwa ikiwasumbua na kuongeza mlundikano kwa wanafunzi mabwenini.

“Tulikuwa tunasherekea jubilee ya shule hivyo mgeni rasmi alikuwa Mheshimiwa Joyce Ndalichako  Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi  na Katika ziara hiyo aliongzana na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe  Amina Masenza, Katibu Tawala wa mkoa wa Iringa Bi wamoja Ayoub, Wakuu wa wilaya ya Mufindi Mheshimiwa Jamhuri David na Iringa Mheshimiwa Richard Kasesela,Pia wabunge waheshimiwa, Ritta Kabati, Zainab Mwamwindi na Mch Peter Msigwa hivyo mbunge kabati ametimiza ahadi yake”alisema Kondo

Kondo alisema lengo la shule ni kuhakikisha wanajenga jingo la bweni jipya la wanafunzi pamoja na kujenga vyoo viwili vya wanafunzi wenye mahitaji maalum

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More