Wednesday, May 31, 2017

MAKUMI WAFUNGULIWA KWENYE MKUTANO WA OYES 2017 JIJINI MWANZA.

Makumi ya wakazi wa Jiji la Mwanza na viunga vyake waliohudhuria kwenye mkutano wa Injili wa OYES 2017 (Open Your Eyes and See) jana wamefunguliwa na kumpokea Kristo.

Kabla ya kuanza mkutano huo, Mchungaji Garry White (kushoto) kutoka Marekani alitoa semina kwa akina mama, vijana na wanandoa ambapo tamati ya mkutano huo unaofanyika viunga vya Kanisa la EAGT Lumala Mpya, nyumba ya Soko Kuu la Sabasaba Jijini Mwanza ni jumapili June 04,2017.

Mchungaji Kiongozi wa Kanisa hilo, Dkt.Daniel Kulola, amewasihi watu wote kuhakikisha wanahudhuria mkutano huo uliojaa mahubiri na mafundisho ya neno la Mungu yakilenga kumfungua kila mmoja ili kuuona Ukuu na Utukufu wa Mungu.
#BMGHabari
Mchungaji Garry White kutoka Marekani akihudumu kwenye mkutano wa OYES 2017
Mchungaji Garry White kutoka Marekani akihudumu kwenye mkutano wa OYES 2017
Mchungaji Dkt.Daniel Moses Kulola, akihudumu kwenye mkutano wa OYES 2017
Ibada ya kuabudu ikiendelea
Wakazi wa Jiji la Mwanza wakifuatilia mafundisho kwenye mkutano wa OYES 2017 Kanisa la EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza
Mkutano huu ulianza jumamosi Mei 27 na utafikia tamati jumapili June 04,2017. Muda ni kuanzia saa tisa na nusu mchana isipokuwa jumapili ambapo ibada zitaanza asubuhi.

TBS YAWASHAURI WAZALISHAJI WADOGO WADOGO WA BIDHAA KUTUMIA FURSA YA BURE YA UKAGUZI

Wazalishaji wadogo wadogo wa bidhaa nchini wameshauriwa kutumia fursa ya bure ya ukaguzi wa bidhaa zao inayotolewa na Shirika la Viwango Tanzania TBS.

Hayo yamesemwa na Afisa Masoko Mwandamizi kutoka katika shirika hilo,Gladnes Kaseka pichani kushoto juu wakati akiongea na waandishi wa habari kwenye maonyesho ya tano ya biashara ya Mkoa wa Tanga .

Alisema kuwa licha ya TBS kutoa fursa hiyo lakini bado wazalishaji wadogo na wakati wameshindwa kuitumia fursa hiyo kwa ukamilifu wake na kusababisha kuendelea kuwepo kwa bidhaa ambazo hazina nembo ya ubora.

"Bado wazalishaji wetu wengi hawajaweza kuifikia fursa hiyo ambayo itaweza kuwasaidia kuhakikisha wanazalisha bidhaa zenye ubora lakini wataweza kuingiza bidhaa zao kwa urahisi katika masoko ya ushindani tofauti na sasa" alisema Kaseka.

Aidha alisema kuwa bado wanaendelea na jitihada za kuhakikisha wanaziondosha katika soko bidhaa ambazo ni hafifu kwa kufanya ukaguzi wa Mara kwa Mara katika masoko na maeneo yote yanayohusika na shughuli za uuzaji wa bidhaa.

Nae Mfanyabiashara Aisha Kisoki alisema kuwa changamoto kubwa ni muingiliano wa bidhaa kutoka nje ambazo kwa hapa nchini zinauzwa kwa bei rahisi tofauti na wanazozizalisha.

Alisema kuwa iwapo TBS wataweza kudhibiti uingiaji usio rasmi wa bidhaa kutoka nje utasaidia sana wafanyabiashara wa ndani ya nchi kuona umuhimu wa kuweka nembo bidhaa zao.
Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha.

WAANDISHI WA HABARI ZA KILIMO TANZANIA (TAJF) WAKUTANA MALAIKA BEACH RESORT JIJINI MWANZA KUPANGA MIKAKATI

 Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Kilimo Tanzania (TAJF), Gerald Kitabu (kulia), akizungumza na waandishi wa habari wanachama wa TAJF wakati wa kikao kilichofanyika Ufukwe wa Malaika Beach Resort jijini Mwanza jana kujadili masuala mbalimbali ya chama hicho.

MWENGE WA UHURU KUWASILI WILAYA YA UBUNGO KESHO 31 MEI 2017

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori akisisitiza jambo wakati akizungumza na Waandishi wa habari ofisini kwake Kibamba Chama-Dar es salaam
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori akizungumza na Waandishi wa habari

Mwenge wa Uhuru Mwaka 2017 utawasili kesho Tarehe 31 Mei 2017 katika Wilaya ya Ubungo kuanzia saa moja kamili asubuhi na kuzuru katika Miradi mitano ya Maendeleo.   
     
Akizungumza na Waandishi wa habari ofisini kwake Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori amesema kuwa katika mbio hizo za Mwenge wa Uhuru Mradi mmoja wa kituo cha Polisi Gogoni utawekwa jiwe la msingi.

Alisema kuwa Miradi mingine itakayozinduliwa ni Mradi wa Ujenzi wa Jengo la kutolea huduma za VVU katika Kituo cha afya Mbezi, Uzinduzi wa madarasa nane katika shule ya Msingi Malambamawili iliyopo Kata ya Msigani, Uzinduzi wa Kituo cha mabasi SIMU 2000 Kata ya Sinza na Uzinduzi wa Zahaanti ya Mburahati.

Mhe Makori alisema kuwa Miradi yote hiyo itakayotembelewa na Mwenge wa Uhuru mwaka 2017 itagharibu Bilioni 2,854,647,991.89

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori amewasihi wakazi wa Manispaa ya Ubungo kujitokeza kwa wingi kuulaki Mwenge wa Uhuru ambao utawasili katika eneo la SAISAI Kata ya Gobaukitokea Manispaa ya Kinondoni.

Pia amewasihi wananchi kujitokeza kwa wingi katika Viwanja vya Barafu, Shule ya Msingi Mburahati kwenye mkesha wa Mwenge wa Uhuru.

Imetolewa Na:
Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ubungo

MATUKIO MBALIMBALI KWENYE MAONYESHO YA BIASHARA YA KIMATAIFA JIJINI TANGA

Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu kushoto akitoa elimu kuhusu umuhimu wa wananchi kujiunga na mfuko huo kwa wakazi wa Jiji la Tanga kwenye banda lao lililopo katika eneo la Mwahako Jijini Tanga kunakofanyika maonyesho ya tano ya biashara ya kimataifa
 Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji,Charles Mwijage akiptia kwenye banda la Hifadhi za Taifa Tanzania (Tanapa) wakati alipofungua maonyesho ya kimataifa ya  biashara ya tano yanayofanyika kwenye viwanja vya Mwahako Jijini Tanga
 Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji,Charles Mwijage akisalimiana na mmoja wa watumishi Tanapa wakati wakati alipotembelea banda lao kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella
 Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji,Charles Mwijage akiendelea na shughuli ya kukagua mabanda ya Maonyesho
Afisa Habari za Utalii (TTB William Akile kulia akiongeza na baadhi ya wanafunzi waliotembelea banda lao
 Afisa Habari za Utalii (TTB William Akile kulia akiongeza na baadhi ya wanafunzi waliotembelea banda lao
 Afisa Habari za Utalii (TTB William Akile kulia akiongeza na baadhi ya wanafunzi waliotembelea banda lao

 Maafisa wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) wakitoa elimu kwa wakazi wa Jiji la Tanga katika Banda lao lililopo kwenye eneo la Mwahako Jijini Tanga kunapofanyika Maonyesho ya Biashara ya Kimataifa ya Tano kutoka kushoto ni Msimamizi wa Ofisi ya Mfuko wa Bima ya Taifa Mkoani Tanga (NHIF) Dinna Mlwilo katikati ni Sabrina Komba ambaye ni Afisa Masoko na Elimu kwa umma makao makuu na kulia ni Afisa matekelezo Macrina Clemens
 kulia ni Sabrina Komba ambaye ni Afisa Masoko na Elimu kwa umma makao makuu Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kulia ni Afisa matekelezo Macrina Clemens wakimsikiliza kwa umakini mkazi wa Jiji la Tanga ambaye alifika kwenye banda lao kupata ufafanuzi kuhusu huduma zinazotolewa na mfuko huo
 Afisa matekelezo wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Macrina Clemens kulia akisitiza jambo kwa mkazi wa Jiji la Tanga kuhusu umuhimu wa kujiunga na mfuko huo ili kuweza kunufaika na huduma mbalimbali muhimu ikiwemo za matibabu kushoto ni Meneja wa Mfuko huo Mkoani Tanga,Ally Mwakababu katikati ni  Msimamizi wa Ofisi ya Mfuko wa Bima ya Taifa Mkoani Tanga (NHIF) Dinna Mlwilo kulia kwake ni Afisa Masoko na Elimu kwa umma makao makuu Sabrina Komba

 Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu kushoto akiwa na maafisa wengine wa mfuko huo wakiwa tayari kutoa elimu kwa wakazi wa Jiji la Tanga kuhusu namna wanavyoweza kunufaika kupitia mfuko huo
 Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu kushoto akitoa elimu kwa mkazi wa Jiji la Tanga ambaye alitembelea banda lao
Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu akizungumza na waandishi wa habari kwenye banda lao kuhusu faida za wakazi wa Jiji la Tanga kujiunga na mfuko huo lakini pia namna walivyojiandaa na ujio wa mradi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga
Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha

Tuesday, May 30, 2017

CHUMI AITAKA WIZARA YA MAMBO YA NJE KUPELEKA MAAFISA KWENYE BALOZI

Mbunge wa Mafinga Mjini Cosato Chumi ameitaka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kuharakisha mchakato wa kupeleka maafisa kwenye Balozi zetu ili kuhakikisha utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi.

Chumi alisema kuwa ili kuelekea uchumi wa viwanda ni muhimu ofisi za Kibalozi zijajengewa uwezo ili kufanya kazi kwa ufanisi. 

'hadi ninapozungumza Balozi kumi na tano hazina Maafisa wa kuwasaidia Mabalozi, hali inayofanya mazingira magumu ya kutekeleza majukumu yao' alisisitiza Mbunge huyo ambaye amewai kufanya kazi katika Wizara hiyo. 

Akifafanua, Chumi alisema kuwa kuwaacha Mabalozi katika nchi kubwa China kufanya kazi bila wasaidizi ni kufifisha jitihada za kuelekea uchumi wa Viwanda kwa kuwa tunategemea tupate wawekezaji kutoka nchi hiyo.

'Ubalozi wa Brussels ambako ni makao makuu ya Jumuiya ya Ulaya kuna mikutano mingi sana, sasa Balozi anapokuwa hana maafisa inamkosesha fursa ya kushiriki mikutano hiyo na hivyo kama Taifa tunajikuta tunakosa fursa nyingi' alisisitiza na kuongeza kuwa

Balozi wetu wa Berlin, Ujerumani anawakilisha zaidi ya nchi saba, anapofanya kazi bila maafisa hawezi kutekeleza majukumu ipasavyo. 

Aidha Mbunge huyo wa Mafinga Mjini alifafanua kuwa unapokosa maafisa ni sawa na ku-down size suala ambalo ni kama ku-down grade mahusiano. 

Wabunge wengine waliochangia hoja hiyo wakiwemo Tundu Lisu, Joseph Kakunda na Dr Faustine Ndungulile walipongeza hatua za kuwarejesha maafisa waliokaa lakini wakaeleza kuwa hatua hiyo lazima iendane na kuwapeleka haraka maafisa katika Balozi zetu. 

Akijibu hoja hiyo Naibu Waziri Dk. Suzan Kolimba alikiri kuwa hoja ya Chumi ni ya Msingi na kwamba tayari fedha zimetingwa kuwapeleka maafisa katika mwaka huu wa fedha.

Friday, May 26, 2017

DC UBUNGO MHE KISARE AAGIZA KUAZNZA MCHAKATO WA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI KATA YA KIMARA

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Matiku Makori akizungumza na wananchi mara baada ya kuzuru kukagua eneo litakalojengwa Shule ya Sekondari ya Kata ya Kimara Jijini Dar es salaam. Leo Mei 26, 2017
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Matiku Makori (Kulia), Diwani wa Kata ya Kimara Mhe Manota wakikagua eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa shule ya Sekondari ya Kata ya Kimara Jijini Dar es salaam. Leo Mei 26, 2017
Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Kimara wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Matiku Makori wakati akizungumza nao mara baada ya kuzuru kukagua eneo litakalojengwa Shule ya Sekondari ya Kata ya Kimara Jijini Dar es salaam. Leo Mei 26, 2017
Diwani wa Kata ya Kimara Mhe Manota akizungumza na wananchi wa Kata hiyo kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Matiku Makori kuzungumza na wananchi mara baada ya kuzuru kukagua eneo litakalojengwa Shule ya Sekondari ya Kata ya Kimara Jijini Dar es salaam. Leo Mei 26, 2017
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Matiku Makori akiwaongoza wananchi kukagua eneo litakalojengwa Shule ya Sekondari ya Kata ya Kimara Jijini Dar es salaam. Leo Mei 26, 2017
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Matiku Makori akikagua ukarabati wa Zahanati ya Mavurunza mara baada ya kuzuru kukagua eneo litakalojengwa Shule ya Sekondari ya Kata ya Kimara Jijini Dar es salaam. Leo Mei 26, 2017 ambapo ameahidi kusaidia kukamilika haraka kwa ujenzi huo.
 Hali ya ukarabati wa Zahanati ya Mavurunza iliyopo katika Mtaa wa Mavurunza Kata ya KImara
Diwani wa Kata ya Kimara Mhe Manota akimuongoza Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Matiku Makori kukagua ukarabati wa Zahanati ya Mavurunza mara baada ya kuzuru kukagua eneo hilo. Leo Mei 26, 2017 ambapo ameahidi kusaidia kukamilika haraka kwa ujenzi huo.
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Matiku Makori akizungumza na wananchi mara baada ya kuzuru kukagua eneo litakalojengwa Shule ya Sekondari ya Kata ya Kimara Jijini Dar es salaam. Leo Mei 26, 2017
Katibu Tawala wa Wilaya ya Ubungo Ndg James Mkumbo akizungumza na wananchi wa Mtaa wa Mavurunza Kata ya Kimara Jijini Dar es salaam muda mchache kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Wilaya ya Ubungo kuzungumza na wananchi wa Kata hiyo. Leo Mei 26, 2017
Wananchi wa Kata ya Kimara wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Matiku Makori mara baada ya kuzuru kujionea eneo litakalojengwa Shule ya Sekondari ya Kata hiyo Jijini Dar es salaam. Leo Mei 26, 2017
Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Kimara wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Matiku Makori wakati akizungumza nao mara baada ya kuzuru kukagua eneo litakalojengwa Shule ya Sekondari ya Kata ya Kimara Jijini Dar es salaam. Leo Mei 26, 2017
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Matiku Makori akizungumza na wananchi mara baada ya kuzuru kukagua eneo litakalojengwa Shule ya Sekondari ya Kata ya Kimara Jijini Dar es salaam. Leo Mei 26, 2017


Na Mathias Canal, Dar es salaam

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Matiku Makori Leo Mei 26, 2017 ameiagiza Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo inayoongozwa na Ndg John Lipesi Kayombo kuanza haraka ujenzi wa Shule ya Sekondari kwa ajili ya Kata ya Kimara Jijini Dar es salaam.

Agizo hilo amelitoa wakati akizungumza na wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya shule ya Msingi Mvurunza mara baada ya kufanya ziara ya kikazi katika Kata hiyo ili kujionea hali ya maendeleo ya elimu sambamba na kubaini changamoto zinazowakabili wananchi katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Ubungo na hatimaye kuzitatua.

Katika ziara hiyo ya Mkuu wa Wilaya ya Ubungo imehudhuriwa pia na Katibu Tawala wa Wilaya ya Ubungo, Afisa Tarafa ya Kibamba, Afisa Elimu Sekondari Manispaa ya Ubungo, Diwani wa Kata ya Kimara, Mtendaji Kata ya Kimara, Wenyeviti na Watendaji wa Mitaa sambamba na Baadhi ya Wananchi wa eneo hilo.

Agizo la Mkuu wa Wilaya ya Ubungo linakuja zikiwa ni siku chache zimepita tangu kutoa maagizo kama hayo katika Shule ya Msingi Ubungo Plaza, Shule ya Msingi Kawawa na Shule ya Sekondari Mburahati ambapo kote huko ameelekeza kuanza haraka ujenzi wa Madarasa sambamba na Vyoo kwa ajili ya wanafunzi na walimu.

Mhe Makori alisema kuwa madarasa anayoagiza yaanze kujengwa yatapunguza kadhia ya mbanano wa wanafunzi darasani ambapo pia amewaahidi wananchi hao kujengwa madarasa kwa viwango vya kisasa.

Naye Moses Mzakwe na Deogratius Stephano ambao ni wakazi wa Mtaa wa Mavurunza wameomuomba Mkuu wa Wilaya kutilia mkazo swala la upimaji wa viwanja ili wananchi waweze kumiliki ardhi huku wakimpongeza kwa kuzuru katika eneo hilo kwani ameonyesha uwezo wa kujali wananchi anaowaongoza.

Awali akizungumza kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Wilaya kuzungumza na wananchi hao Diwani wa Kata ya Kimara Mhe Manota alimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli kwa kutekeleza sera na kuisimamia ilani ya uchaguzi ya mwaka 2015/2020 na kuwaomba watanzania wote kwa kauli moja pasina itikadi za vyama kumuunga mkono kwani atakuwa imara na madhubuti zaidi katika utendaji wake iwapo ataungwa mkono na watanzania wote.

Alisema kuwa Rais Magufuli anapaswa kutilia mkazo zaidi kwa kuwawekea kufuli watu waliokuwa wanalihujumu Taifa kwa wizi na ufisadi katika sekta mbalimbali nchini.

Mhe Manota alisema kuwa tayari zimetolewa jumla ya shilingi milioni mia moja kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Shule hiyo ambapo mara baada ya kukamilika itawarahisishia wanafunzi kupata elimu bora pasina mateso wanayoyapata sasa kutokana na ukosefu wa shule ya serikali ya Sekondari katika Kata nzima ya Kimara.

MWISHO

CCM YAMPONGEZA JPM SAKATA LA MCHANGA WA MADINI, YALAANI VIKALI MAUAJI MKOANI PWANI

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi CCM, Itikadi na Uenezi Ndg Humprey Polepole akizungumza na Waandishi wa Habari katika ukumbi wa Mikutano Ofisi ndogo ya CCM Lumumba Jijini Dar es salaam. Picha Zote na Mathias Canal
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi CCM, Itikadi na Uenezi Ndg Humprey Polepole akisisitiza jambo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari katika ukumbi wa Mikutano Ofisi ndogo ya CCM Lumumba Jijini Dar es salaam.

Waandishi wa habari wakimsikiliza Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi CCM, Itikadi na Uenezi Ndg Humprey Polepole wakati wa Mkutano wake na Waandishi wa Habari katika ukumbi wa Mikutano Ofisi ndogo ya CCM Lumumba Jijini Dar es salaam.
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi CCM, Itikadi na Uenezi Ndg Humprey Polepole akizungumza na Waandishi wa Habari katika ukumbi wa Mikutano Ofisi ndogo ya CCM Lumumba Jijini Dar es salaam.

Na Mathias Canal, Dar es salaam

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Taifa kwa kutekeleza sera na kuisimamia ilani ya ushindi ya CCM ya mwaka 2015/2020 na kuwaomba watanzania wote kwa kauli moja pasina itikadi za vyama kumuunga mkono kwani atakuwa imara na madhubuti zaidi katika utendaji wake iwapo ataungwa mkono na watanzania wote.

Chama cha Mapinduzi (CCM) Kimetoa pongezi hizo kutokana na maamuzi yaliyofanywa na Rais Magufuli mara baada ya kupokea Ripoti ya kamati iliyokuwa inachunguza Hatma ya mchanga wa madini iliyoundwa na Rais Magufuli Machi 29 mwaka huu ikiwajumuisha Profesa Abdulkarim Hamisi Mruma (Mwenyekiti), Profesa Justiania Rwezaura Ikingula, Profesa Joseph Bushweshaiga, Dokta Yusuph Ngenya, Dokta Joseph Yoweza Phili, Dokta Ambrose Itika, Mohamed Zengo Makongoro na Hery Issa Gombela.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi CCM, Itikadi na Uenezi Ndg Humprey Polepole wakati akizungumza na Waandishi wa Habari katika ukumbi wa Mikutano Ofisi ndogo ya CCM Lumumba Jijini Dar es salaam.

Polepole alisema kuwa uamuzi wa kuundwa kwa kamati hiyo ulitokana na kukamatwa kwa makontena 277 ya mchanga huo katika bandari ya Dar es salaam Machi 23 Mwaka huu baada ya Rais kufanya ziara ya kushitukiza katika bandari hiyo na kukuta makontena 20 yakiwa mbioni kusafirishwa kinyume cha maelekezo yake ya Machi 2 ya kuzuia kusafirisha mchanga huo nje ya nchi.

Alisema kuwa huu sio wakati wa kulumbana na kutofautiana kisa itikadi za vyama bali ni wakati wa kusimama pamoja na kuikabili vita ya kiuchumi kwani kwa kuzingatia taarifa iliyosomwa na Profesa Mruma mbele ya Rais Magufuli imebainisha jinsi Taifa lilivyopata hasara ya mabilioni ya fedha kwa kuwa makontena yaliyozuiliwa bandarini yana thamani ya madini yaliyomo kwa kiwango cha wastani wa shilingi Bilioni 829.4 na kiwango cha juu ni Shilingi Trioni 1.4

"Tumeibiwa na kudhulumiwa sana mali zetu ambazo tumezirithi kutoka kwa babu zetu lakini awamu ya Tano ikiongozwa na Rais Magufuli imeamua kwa dhati kabisa kutilia mkazo Vita dhidi ya Rushwa, Uhujumu uchumi, Udhalimu wa kila namna, sambamba na wizi na ufisadi kwa maslahi mapana ya Taifa la Tanzania na Watanzania wote" Alisema Polepole

Akizungumzia Mauaji yanayotokea katika maeneo mbalimbali nchini hususani Mkoani Pwani katika Wilaya ya Kibiti, Rufiji na Mkuranga alisema kuwa kipindi hiki kigumu kwa kuwapoteza ndugu zetu vyama vya siasa vilipaswa kushikamana kwa pamoja pasina kujali itikadi zao badala yake vimeanza kutumia misiba hiyo kwa maslahi ya kiuongozi kuliko maslahi ya Taifa.

Polepole alisema kuwa vyombo vyote vya serikali vinavyoshughulikia ulinzi vinapaswa kutumia Rasilimali zao, Weledi na Utendaji wao, na kuweka umaalumu katika kuyakabili matukio ya mauaji na kuyakomesha kabisa.

"Hakuna dini yoyote Duniani inayoamini katika kutoa uhai wa mtu ambapo pia kuua mtu ni kinyume na Katiba ya  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hivyo Tunataka amani ya wananchi wetu inarudi" 

"Tunatambua kuwa wananchi wetu wanapita katika wakati mgumu kutokana na kukatishwa kinyama maisha ya Wananchi wenzao, Viongozi, Askari, Watendaji wa serikali, Wanachama wa CCM si kwa sababu ya mapenzi ya Mungu Bali kwa sababu yamekatishwa katika namna inayokiuka ubinadamu kwa kuuawa kikatili na watu wasio na Utu, Hisia na Imani ya Dini" Alisema Polepole

Polepole ametilia msisitizo wananchi kutoa taarifa kwa jeshi la Polisi kuhusu watu wanaofanya mauaji hayo kwani ushirikiano huo utasaidia kufichua uovu wa wadhalimu wanaokatisha maisha ya watanzania.

MWISHO

BURUDANI ZA GULIO LA MTAA KUTOKA LAKE FM MWANZA ZAANZA KWA KISHINDO

DJ Buster kutoka Lake Fm akisababisha burudani kweny Gulio la katika Mnada wa Nyakato National Jijini Mwanza.

102.5 Lake FM Mwanza, #RahaYaRockCity #RedioYaWananzengo leo Mei 26,2017 imezindua rasmi burudani za Gulio la Mtaa kupitia kampeni yeke ya usafi ya Ng'arisha Nzengo Uchafu Nuksi.

Burudani leo iko katika mnada wa Nyakato National Jijini Mwanza kisha itahamia kwenye minada yote Jijini Mwanza ambapo kuna makumi ya wasanii watakaoshusha burudani kali balaa.

Kupitia burudani, Lake Fm inahamasisha suala la usafi minadani na mkoani Mwanza kwa ujumla. Pia kila mnada atatafutwa Mama Lishe Bora, Balozi Imara na Mwananzengo Hodari ambapo watajipatia zawadi.

Burudani za Gulio la Mtaa zimepewa nguvu na Pepsi, Tigo, Busy Bee, Barmedas Tv, Genic Studio, Mama Salakika Deco, Lake Zone Tents & Supply, Mamba Entertainment, CF Hospital, Gerusalem Sound na BMG.
Wanyakazi wa Lake Fm
Wanyakazi wa Lake Fm
Mwananzengo katika ubora wake
Raha ya Rock City
Burudani
Wanyakazi wa Lake Fm, kulia ni Tatu Jabu na kushoto Fatuma Sinda
Vester JTZ kutoka Lake Fm Mwanza
Morice kutoka Lake Fm akihost burudani ya Gulio la Mtaa, Mnada wa Nyakato
Haroun Tambwe kutoka Lake Fm
Amina Swedy kutoka Lake Fm
Eve kutoka Lake Fm
Amos kutoka Lake Fm
Mtangazaji wa kipindi cha Kijiji Pub kutoka Lake Fm
Washereheshaji kutoka Barmedas Tv Mwanza
Stage ya Gulio la Mtaa
Wananzengo kwenye ubora wao
Katikati ni Mkurugenzi wa Lake Fm, Doreen Noni, akiteta jambo kwenye Gulio la Mtaa
Zawadi za tisheti kwa Wananzengo
Wananzengo kwenye Gulio la Mtaa
Back Stage, Wasanii watakaoshambulia jukwaa la Gulio la Mtaa
Back Stage, Wasanii watakaoshambulia jukwaa la Gulio la Mtaa
Back Stage, Wasanii watakaoshambulia jukwaa la Gulio la Mtaa
Back Stage, Wasanii watakaoshambulia jukwaa la Gulio la Mtaa
Back Stage, Wasanii watakaoshambulia jukwaa la Gulio la Mtaa
Back Stage, Wasanii watakaoshambulia jukwaa la Gulio la Mtaa
Back Stage, Wasanii watakaoshambulia jukwaa la Gulio la Mtaa
Back Stage, Wasanii watakaoshambulia jukwaa la Gulio la Mtaa na Wananzengo wa Lake Fm
Back Stage, Wasanii watakaoshambulia jukwaa la Gulio la Mtaa
Back Stage, Wananzengo na Wasanii watakaoshambulia jukwaa la Gulio la Mtaa
Back Stage, Wananzengo na Wasanii watakaoshambulia jukwaa la Gulio la Mtaa
Back Stage, Wananzengo na Wasanii watakaoshambulia jukwaa la Gulio la Mtaa
Back Stage, Wananzengo na Wasanii watakaoshambulia jukwaa la Gulio la Mtaa
Shukurani sana Tigo, Jaza Ujaziwe
Wananzengo tayari kwenye Gulio la Mtaa
Wananzengo wako tayari kwenye Gulio la Mtaa
Wananzengo wako tayari kwenye Gulio la Mtaa
Wananzengo wako tayari kwenye Gulio la Mtaa
Burudani zimeanza kwa kasi
Sogea Mnada wa Nyakato National upate burudani za Gulio la Mtaa kutoka 102.5 Lake Fm Mwanza #RahaYaRockCity #RedioYaWananzengo

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More