Tuesday, June 30, 2015

Dkt MUSA MDEDE apata Baraka za kuwa mbunge wa jimbo la kalenga kutoka kwa vijana wa kikatoliki wa jimbo hilo.

 Dkt  MUSA LEONARD MDEDE akitoa neno katika kongamano la vijana wa katoliki 
 baadhi ya vijana wakimsikiza mdede katika kongamano hilo.
 baadhi ya viongozi wa vijana hao wakiwa makini kumsikiliza mdede




mdede akiingia katika ukumbi uliokuwa unafanyika sherehe

na fredy mgunda,iringa.

Vijana kikatoliki waliokuwa kwenye kongamano lililofanyika katika kijiji cha ulete wamewataka wananchi wa jimbo la kalenga kuelekeza macho na masikio yao kuhakikisha wanamchagua kijana mwenzao ambaye ameonekana kuwa na uwezo wa kuwa kiongozi bora na kuwaletea maendeleo katika jimbo hilo.

Wakizungumza katika kongamano hilo vijana hao walisema kuwa hawajapata kuona kijana anayejiamini na kuonesha wazi mbinu za kulikomboa jimbo katika nyanja ya kimaendeleo.

“Jimbo la kalenga linawasomi wengi lakini jimbo hilo bado halina maendeleo ya kuridhisha licha ya kuwa na vitega uchumi vingi ambavyo vingeweza kuiongezea mapato na kukuza uchumi wa jimbo hilo,kwa mipango na mbinu ambazo mose madede amezionyesha zinatufaa kabisa wananchi wa jimbo la kalenga”. walisema vijana hao.

Lakini waliongeza kwa kuwataka vijana na wananchi wa jimbo la kalenga  kutofanya makosa katika uchaguzi wa mwaka huu kwa kumchagua kiongozi anayewafaa na kujiamini kwa kuwaletea maendeleo na kuwatetea wananchi wake.

Nao viongozi wa vikalia tosamaganga walimsifu kijina moses kwa kujiamina na kuwaonyenyesha vijana wenzao kwa maneno na ujumbe wa kuwapa njia muhimu za kufikia malengo yao katika maisha.

Waliongeza kwa kusema kuwa baadhi ya vijana waliokosa hutuba ya moses mdede wamekosa kitu cha muhimu sana lakini akawaomba vijana hao wakirudi nyumbani kwao basi wafikishe ujumbe kwa wananchi na vijana waliokosa kongamano hilo kwa kuwa wao ndio mabadiliko ya sasa.

“Vijana mbadilike msiwe kama vijana wa zamani nchi hii inahitaji viongozi wenye weledi wa kuwaongoza wananchi na kuwalete maendeleo  mdede anafaa na anasifa zote za kuwa kiongozi kwa kuwa anasifa zote za kuwaongoza wanachi wa jimbo la kalenga hivyo wananchi msifanye makosa”.walisema  viongozi hao.

Kwa upande wake sister kiliana sanga wa ulete alisema kuwa hajawahi kukutana na kijana mwenye uwezo mkubwa wa kifikra na mipango madhubuti ya kuleta maendeleo ya jimbo la kalenga.

Naye moses mdede aliwataka vijana kujitambua na kushemu maamuzi yao wakati wananfanya kitu sahihi kwa wakati sahihi kuwataka wasikubali kuchaguliwa kiongozi katika uchaguzi wa mwaka huu.

“Sasa ifike wakati vijana muwe na maamuzi ya kujichagulia viongozi sahihi vijana ni taifa la leo sio la kesho hivyo ukimchagua kiongozi kwa kununuliwa ujue kuwa atakapo ingia madarakani atawaongoza anavyowataka yeye na sio kuwaletea maendeleo kwa kuwa ameingia madarakani kwa kuwanunua”.alisema mdede

mdede aliwataka vijana kuacha kulalamika kila wakati na badala yake wafanye kazi kwa kujituma ili wajiletee maendeleo na kuacha tabia ya kufaata mkumbo katika kutafuta maisha bora.

“Viongozi wa dini  nyie mnaka mara kwa mara na waumini wenu hiyo mnapaswa kuwapa elimu ya maisha na kuwajua viongozi wazuri kwa kuwa nyie mnakaramu hiyo,mfano leo hii mmekaa na vijana hao na kuwapa mafunzo mbalimbali hivyo mnapaswa kuwaambia ukweli juu ya mstakabadhi wa serikali yetu ambayo imepoteza matumaini”.alisema mdede.

Lakini  MDEDE aliwataka vijana kuwa mstari wa mbele katika kuinua uchumi wa nchi.

MDEDE aliyasema katika kongamano la vijana wa katoliki katika kata ya ulete Iringa vijijini ambapo amewataka vijana kutambua umuhimu wao katika jamii ili kuleta madadiliko chanya kwa taifa .


Aidha Dkt MUSA amesema kuwa wazee ni hazina kwa taifa kwa ushauri wa mambo mbali mbali ya kiuongozi   lakini nguvu ya vijana inahitajika ili kulikwamua taifa kutoka hapa lilipo na kusonga mbele.

Friday, June 12, 2015

BALOZI DKT. DIODORUS BUBERWA MGENI RASMI KATIKA UTOWAJI WA ZAWADI KWA WASHINDI WA ‘NA MIMI NIPO- ONLINE ARTS & SCIENCE COMPETITION LILILO ANDALIWA NA FASDO.

Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji, Dr. Diodorus Buberwa akizungumza wakati wa sherehe hiyo.
Meza Kuu, kuanzia kushoto ni Mratibu Mkuu wa FASDO nchini, Joyce Msigwa,  Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji, Dr. Diodorus Buberwa, Mkurugenzi wa Kituo cha Utamaduni cha Urusi nchini, Alexander Tsykunov na mwisho ni Mkurugenzi Mtendaji wa FASDO, Tedvan Chande. 
 Mkurugenzi Mtendaji wa FASDO, Tedvan Chande akizungumza jambo wakati wa sherehe hizo
Mratibu wa shindano hilo, Joyce Msigwa akizungumza jambo.
Mshereheshaji wa sherehe hizo ambaye pia ni Mratibu Msaidizi, Tunukiwa Daudi akifafanua jambo.
Mzee Nabora Akizungumza Jambo wakati wa Sherehe hizo
Baadhi ya  washindi wakiwa wanakabidhiwa zawadi zao
 Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji, Dr. Diodorus Buberwa akitazama baadhi ya kazi ambazo wamefanya vijana hao.
Burudani ya sanaa ikiendelea.
 Baadhi ya washiriki wachoraji wakiendelea na Mafunzo
 Kushoto ni mwanafunzi kutoka Chuokikuu cha Mzumbe ambaye pia ni mbunifu mavazi akitoa somo kwa baadhi ya washiriki
 Mmoja ya washiriki akiwa anaendelea kuchora wakati wa Sherehe hizo
 Picha ya Pamoja

Shirika la FASDO (Faru Arts and Sports Develepment Organization) leo hii limetoa zawadi kwa washindi wa shindano la Na Mimi Nipo- Online Arts and Science Competition katika ukumbi wa  kituo cha utamaduni cha Urusi nchini (Russian Tanzania Cultural Center).

Shindano hilo linalohusisha vipaji vya uchoraji, sanaa za mikono na ubunifu wa kisayansi lililozinduliwa mwezi Februari mwaka huu kwa lengo la kutambua vipaji vya vijana wenye umri kati ya miaka 12 hadi 24 limefikia kilele chake leo hii kwa kuwapata washindi sita, wawiliwawili kutoka katika fani za Uchoraji, Sanaa za Mikono na Ubunifu wa Kisayansi. 

Zoezi la kutoa zawadi kwa washindi hao lilihudhuriwa na Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji, Dr. Diodorus Buberwa, Mkurugenzi wa Kituo cha utamaduni cha Urusi nchini hapa, Alexander Tsykunov na wageni waalikwa.

Akizungumza na washiriki pamoja na wageni waalikwa katika Sherehe hizo Balozi wa Tanzania Nchini Ubelgiji aliwapongeza sana vijana kwa kuwa na vipaji vya hali ya juu na kusisitiza kuwa eneo hili la sanaa ya Uchoraji linatakiwa kupewa kipaumbele, aliongeza kuwa Tanzania sasa inatakiwa kuwa na maeneo zaidi kwa ajili ya kukuza sanaa hizi, na katika kuendeleza na kusapoti sanaa , Mh.Balozi Buberwa amechangia Tsh 1,000,000.

Washiriki walikuwa 27 lakini waliopata zawadi walikuwa ni washiriki 6 ambao walizingatia umri kati ya miaka 12 hadi 24 na washindi hao ni pamoja na Thomas Mwakilima, Anhony Tendwa, Primus Mapunda, Philipo Frolian, Cornelio Malya na Anderson Msangi washindi wote wamepata zawadi Dola 300.

1 of 77 CHUMBA CHA HABARI CHA GAZETI LA JAMBO LEO NA STAA SPOTI CHAZIZIMA KWA HUZUNI BAADA YA KUFIWA NA MENEJA WAO MZEE RAMADHANI KIBANIKE

 Marehemu  Ramadhani Kibanike enzi za uhai wake.
 Mhariri Mkuu wa Gazeti la Jambo Leo, Julian Msacky na Mwandishi wa Habari, Stela Kessy (kulia), wakiendelea na kazi huku wakiwa na hudhuni baada ya kupokea taarifa ya kifo cha Kibanike leo jioni.
 Mwanahabari Celina Mathew akilia kwa uchungu baada ya kupokea taarifa hiyo.
 Ofisa Matangazo, Kinai akiwa amepigwa butwaa kutokana na  kifo hicho.
 Wanahabari Nyendo Mohamed (katikati), Edith Msuya (kulia) na  Magendela Hamisi wakiwa katika hali ya huzuni kufuatia kifo hicho.
 Mwanahabari Magendela Hamisi akitafakari juu ya kifo hicho.
 Msanifu kurasa wa gazeti la Jambo Leo, Elizabeth Mkeleja alishindwa kujizuia kulia.
 Dereva wa Ramadhani Kibanike akiwa katika huzuni baada ya kupokea taarifa ya kifo hicho.
Mwanahabari Grace Gurisha akisaidiwa na wenzake baada ya kuishiwa nguvu muda mfupi baada ya kupata taarifa hizo za kifo cha Meneja  Ramadhani Kibanike.

Na Dotto Mwaibale

KAMPUNI ya JL Comunications inayochapisha magazeti ya Jambo Leo, Staa Spoti, imepata pigo baada ya aliyekuwa Meneja wake Mkuu Ramadhani Kibanike kufariki.

Kibanike amefariki dunia leo mchana nyumbani kwake Tabata Kimanga jijini Dar es Salaam, baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Akitoa taarifa ya kifo hicho kwa wafanyakazi wa Kampuni hiyo, Mkurugenzi wa Kampuni hiyo Theophil Makunga alisema Kibanike alikumbwa na mauti leo mchana.

Taarifa hiyo ambayo iliwashtua wafanyakazi wa Kampuni hiyo na hata kupelekea baadhi yao kupoteza fahamu, ilisababisha pia kusimama kwa muda kwa shughuli za Kampuni hiyo.


Mipango ya mazishi bado inapangwa, na msiba upo nyumbani kwa marehemu Tabata Jijini Dar es Salaam.

MBUNGE WA JIMBO LA MUFNDI KASIKAZINI MAHAMOD MGIMWA ANOGESHA ZAWADI ZA MSHINDI WA KOMBE LA MUUNGANO.





naibu waziri wa maliasili na utalii mahamod mgimwa ambye pia mbunge wa jimbo la mufindi kasikazini.

 hapa mabingwa wa kombe hilo wakishangia ushindi pamoja na mgeni rasmi pamoja na viongozi mbalimbali.





mratibu wa mashindano hayo aliyetangaza kustahafu kuratibu mashindano hayo.

na fredy mgunda,iringa

akizungumza wakati wa kufunga mashindano ya kombe la muungano mratibu wa kombe hilo DAUDI YASSIN alimpongeza mbunge wa mufindi wa jimbo la mufindi kasikazini ambaye pia ni naibu waziri wa maliasili na utalii MAHAMOD MGIMWA kwa kisaidia kutoa zawadi.

YASSIN alisema kuwa tulipungukiwa baadhi ya zawadi kutokana na kombe hilo kufanyika bila ya kuwa na mdhamini wa kudumu hivyo aliamua kumtafuta mbunge huyo na kumuomba awasaidie baadhi ya zawadi kutokana na kukwama kwake.

"niliamua kumtafuta mbunge wetu ili atusaidie kwa kuwa tulikuwa tumepungukiwa kwenye upande wa zawadi hivyo mgunge huyo naye hakusita akatusaidia" alisema DAUDI YASSIN
baada ya hapo nilisikia minong'ono ya wananchi waliokuwepo  uwanja hapo walimsifia mbunge huyo kwa kijitolea na kuwasaidia waandaaji wa mashindano hayo kutokana na waandaaji kuto kamilisha baadhi ya zawadi.

lakini wananchi hao ambao ni wapenzi wa michezo waliendelea kumuongea mbunge wao kwa kusema amekuwa akitolea mara kwa mara katika matatizo mbalimbali ya wananchi wa jimbo hilo kwa kuwa bado ana wajali na kuwapenda.

hata hivyo baadhi ya wananchi waoshabikia chama cha demokrasia na maendeleo(CHADEMA)walisema kuwa licha ya wao kuwa katika chama hicho lakini bado wanaukubali na kuupokea mchango wa mbunge huyo ambaye amekuwa akisaidia maendeleo katika jimbo hilo.

niliamua kutafuta mbuge huyo kwa njia ya cm ili kujua kwanini ameamua kuwasidia wananchi wake kipindi hiki cha uchaguzi alijibu hivi "hiyo sio mara ya kwanza kufanya hivyo nimekuwa nikifanya mara kwa mara kwa lengo la kuleta maendeleo ya katika jimbo hilo"alisema mgimwa

MGIMWA aliwaomba wananchi wa jimbo hilo kuendelea kumuunga mkono wakati wa kuleta maendeleo na kuacha na itikadi ya vyama,inatakiwa tukae pamoja ili tuweze kuleta maendeleo kwa kuwa akifanya pekee yake ataweza kuleta maendeleo hivyo ushirikiano kwa pamoja ndio njia sahihi ya kuleta maendeleo katika jimbo hilo.

 

Thursday, June 11, 2015

MKUU WA WILAYA YA KINONDONI PAUL MAKONDA APIGA MARUFUKU UCHIMBAJI MCHANGA MTO MBEZI NA KAWE

 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda akizungumza na wakazi wa Mbezi na Kawe Ukwamani ambao nyumba zao zilibomoka kutokana na mmomonyoko wa ardhi uliosababishwa na shughuli za kibinadamu kama vile uchimbaji wa mchanga katika mto huo hali iliyosababisha kingo za mto huo kupanuka hadi kwenye makazi ya watu. Makonda aliwatembelea wakazi hao Dar es Salaam jana.
 DC Makonda akiwa ameongozana na viongozi mbalimbali wakati alipo watembelea waathiriwa hao.
 Wananchi wakiwa katika maeneo hayo yaliyoathiriwa na mmomonyoko huo.
 Baadhi ya nyumba zilizobomoka kutokana na mmomonyoko huo.
Na Dotto Mwaibale

MKUU wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda amepiga marufuku uchimbaji mchanga katika mto Mbezi na Kawe Ukwamani kutokana na uharibifu wa mazingira ambao umesababisha nyumba zilizo kando ya mto huo kubomoka kutokana na mmomonyoko wa ardhi.

Makonda alipiga marufuku wakati akizungumza na wananchi walioathiriwa na mmomonyoko huo alipofika kuwapa pole na kuona jinsi ya kuwasaidia Dar es Salaam jana.

"Wakati tunaangalia namna ya kuwasaidi naomba kuanzisha leo shughuli za uchimbaji wa mchanga katika mto Mbezi ukome na mtu atakaye bainika anaendelea kuchimba mchanga atachukuliwa hatua za kisheria" alisema DC Makonda.

Makonda alisema wataalamu wa Manispaa hiyo watafika katika eneo hilo ili kuona nini kifanyike kupunguza tatizo hilo kwa siku za mbele kama walivyofanya maeneo ya Tegeta yaliyokumbwa na mafuriko ambapo kutajengwa karavati kubwa ili maji yaweze kupita.

Katika eneo hilo nyumba zaidi ya 100 zimebomoka kutokana na kusombwa na maji wakati wa mvua za maisha huku zikiwaacha wakazi wa maeneo hayo wakiishi katika chumba kimoja na wengine wakikosa makazi. 

MASHINDANO YA MUUNGANO YAMEFIKIA MWISHO KWA MAFANIKIO MAKUBWA SANA,HUKU DAUDI YASSINI AKING’ATUKA

 DAUDI YASSINI AKIMKARIBISHA MKUU WA WILAYA YA MUFINDI MBONI MAHITA KATIKA UWANJA WA WAMBI MJINI MAFINGA
 MKUU WA WILAYA MBONI MAHITA AKIKAGUA TIMU KABLA YA MCHEZO
 MSIMAMIZI DAUDI YASINI NA MGENI RASMI MBONI MAHITA WAKIWA KATIKA PICHA MOJA NA MABINGWA  WA MUFINDI CUP TIMU YA MKOBA
  MSIMAMIZI DAUDI YASINI NA MGENI RASMI MBONI MAHITA WAKIWA KATIKA PICHA MOJA NA  TIMU YA DODOMA ACADEMY
 SEHEMU YA MASHABIKI WA WALIOJITOKEZA KATIKA MCHEZO HUO WA FAINALI
 SEHEMU YA MASHABIKI WA WALIOJITOKEZA KATIKA MCHEZO HUO WA FAINALI

 na fredy mgunda,iringa


mashindano ya muungano cup yafikia tamati hapo jana kwa mafanikio makubwa huku timu ya mukoba ikishinda  na kuwa bingwa mpya kwa kumfunga timu ya dodoma academy goli mbili bila.

katika mchezo ulikuwa na mashabiki wengi katika uwanja wa wambi uliopo mafinga mjini na kuchezeshwa na marefa wenye weledi wa kazi yao na kuuchezesha mchezo kwa hali ya juu kiasi ambacho mashabiki walifurahia uwepo wa marefa hao katika mchezo huo.

mchezo huu ulikuwa wa vuta nikuvute kutokana na timu zote mbili kuwa katika kiwango bora katika mchezo huo hali iliyokuwa ikiwapa raha mashabiki kila muda kutokana na burudani ilikuwa ikitolewa uwanjani na wachezaji wa timu zote mbili.

kwa upande wake msimamizi wa mashindano hayo DAUDI YASINI alisema kuwa ni kazi ngumu sana kufanikisha mashindano hayo kutokana na kukosa wadhamini wa kudumu hivyo juhudi zake binafsi ndio zilizosababisha mashindano hayo kufanyika kwa mafanikio kipindi chote wakati akiwa msimamizi wa mashindano hayo.

baada ya mashindano hayo kumalizika katika uwanja wa wambi DAUDI YASINI alisimama mbeli ya maelfu ya mashabiki waliokuwa wamejitokeza na kuwaambia kuwa amejuudhuru rasmi kuendelea kusimamia mashindano hayo ambayo amekuwa akisimamia kwa miaka kadha iliyopita.

DAUDI YASSINI aliwapondeza wadau mbalimbali waliokuwa wakimuunga mkono katika harakati zote za kuandana mashindano hayo na kuwaomba waendelee kuwaunga mkono  wasimamizi wengine watakao kuwa wakisimamia hapo baadae.




Tuesday, June 2, 2015

UTAFITI WA KISIASA ULIOFANYWA NDANI YA MANISPAA YA IRINGA WAMBEBA FRANK KIBIKI

        frank kibiki akiongea na wananchi stand kuu ya mabas iringa
 
wananchi wakimsikiza frank kibiki  alipokuwa maeneo ya stand kuu
na fredy mgunda,iringa
MATOKEO ya utafiti uliofanywa na taasisi ya Southern Highland Zone Election Research (SHZER), katika jimbo la Iringa mjini umeonyesha kuwa nyota ya Mwanahabari ,  Frank Kibiki aliyetangaza nia kuwania Ubunge jimbo la Iringa mjini (CCM) inazidi kung’ara baada ya kuongoza huku akichuana vikali na Mbunge wa sasa Mchungaji Peter Msigwa(CDM).
Utafiti huo uliofanywa kwa miezi minne tangu, kuwepo kwa wimbi la watu wengi kutangaza nia ya kuwania ubunge katika jimbo la Iringa mjini, wakiwemo makada lukuki wa CCM unaonyesha kuwa Nyota ya Frank Kibiki inazidi kung’ara kutokana na kuungwa mkono na makundi mengi ya kijamii hasa vijana,  wanawake, walemavu na wazee.
Akizungumza na mtandao huu, Mtafiti mkuu wa SHZER,  Patson William alisema utafiti huo umefanywa katika kata 14 za jimbo la Iringa mjini huku wagombea vijana wakiwa ndio wanaoongoza kupendwa ikilinganishwa na wagombea wenye umri kuanzia miaka 50 na kuendelea.
Kibiki anaongoza kwa asilimia 40.7, Mchungaji Msigwa 20.9, Jesca Msambatavangu 11.7, Dr Yahaya Msigwa 7.6, Fredrick Mwakalebela 2.8, John Kiteve 2.4, Mahamoud Madenge 1.2 na wengine waliobaki wanagawana asilimia 12.7.
Utafiti huo unaonyesha kuwa, kinachomfanya Kibiki kuendelea kung’ara ni siasa zake za kistaarabu, taaluma ya uana habari, uwezo mkubwa wa kujenga na kujibu hoja anazokumbana nazo sambamba na uzoefu katika utendaji wake wakati akiwa Katibu wa UVCCM katika wilaya mbalimbali alizowahi kufanya kazi.
Alisema utafiti huo umefanywa kwa njia ya madodoso ambapo watu 400 walijibu na maswali ya papo kwa papo ambapo watu 1000 waliyajibu.
Alitaja kata zilizohusishwa kuwa ni Makorongoni, Miyomboni/kitanzini, Kihesa, Kwakilosa, Mlandege, Mivingeni, Gangilonga, Kitwiru, Igumbilo, Nduli, Ruaha, Mkwawa, Mtwivila na Isakalilo.
Mambo ya msingi ambayo utafiti huo uliangalia ili kutafuta majibu ni Changamoto za jimbo la Iringa mjini kwa sasa,sifa za Mbunge anayetakiwa kukabiliana na changamoto hizo, mapendekezo ya jina la atakayesimamia vizuri changamoto hizo na mazingira ya siasa za sasa za jimbo la Iringa mjini.
Hata hivyo CCM na Chadema ndiyo vyama pekee vinavyochuana kwa kasi katika jimbo la Iringa mjini, tangu CDM iliponyakua jimbo hilo mwaka 2010.
Hata hivyo utafiti huo unaonyesha kuwa CCM itakuwa na wakati mgumu ikiwa watateua jina la mtu asiyechaguo la wananchi jambo ambalo, litampa Mchungaji Msigwa ushindi usio na jasho.
“Utafiti huu unaonyesha kuwa CCM inanafasi nzuri ya kuchukua jimbo la Iringa mjini ikiwa tu watafuata nini wana Iringa wanasema vinginevyo, nafasi ya Msigwa kuendelea itakuwa kubwa,”anasema

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More