Thursday, September 29, 2016

ZIMWI LA TEGETA ESCROW LAMTISHA PROFESA TIBAIJUKA, AKATAA KUPOKEA DOLA 300,000 BAADA YA KUPEWA TUZO YA KIMATAIFA

 Mbunge wa Muleba Kusini, Profesa Anna Tibaijuka akionesha tuzo ya kimataifa (UN) ya Maendeleo Endelevu ya Mwana Mfalme Khalifa Bin Salman Al Khalifa aliyotunukiwa hivi karibuni New York Marekani wakati akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo.
 Profesa Anna Tibaijuka akionesha cheti alichokabidhiwa sanjari na tuzo hiyo.
 Profesa Tibaijuka akisisitiza jambo katika mkutano huo na wanahabari. Kulia ni Mratibu wa mkutano huo, Mussa Ally.
 wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
Mkutano na wanahabari ukiendelea.

Na Dotto Mwaibale


MBUNGE wa Muleba Kusini Profesa Anna Tibaijuka amekacha kuchukua dola 300,000 alizopewa baada ya kutunukiwa tuzo ya  Maendeleo Endelevu aliyopewa na Umoja wa Mataifa (UN), kutokana na sakata la fedha za Escrow Tegeta.


Tuzo hiyo aliipokea Septemba 23 mwaka huu New York Marekani ambayo mfadhili wa tuzo hiyo ni wa waziri mkuu wa Bahrain mwana mfalume Khalifa bin Al Khalifa.

MRADI WA URASIMISHAJI ARDHI UBUNGO WAINGIA MIZENGWE WATENDAJI WATISHIA KOGOMA KWA KUKOSA POSHO

Waziri wa Ardhi, William Lukuvi



NaFredy Mgunda

WATENDAJI na vibarua wanaofanya kazi ya kupima ardhi katika mradi wa urasimishaji wa ardhi katika maeneo yaliyojengwa kiholela katika Kata ya Kimara 
wilayani Ubungo umeingia mdudu baada ya kutishia kugoma kutokana na kutolipwa fedha za posho ya kazi hiyo kwa zaidi ya miezi mitatu.

Hatua hiyo imefikiwa baana ya kuona baadhi ya vongozi wanaosimamia mradi huo wa kuanza kujinufaisha wenyewe na kuwanyonya watendaji wakiwemo vibarua 
hao.

Wafanyakazi wa upimaji wa ardhi kutoka wizarani na vibarua hao wakiongea kwa nyakati tofauti na gazeti hili kwa masharti ya kuto andikwa majina yao gazetini 
wamesema  viongozi hao kupitia mradi huo wamejenga mazingira ya  kujinufaisha kupitia fedha zilizotoka Benki ya Dunia kufanya mradi huo.

"Tunachangamoto kubwa ya kupata fedha za malipo kwa kazi tunayoifanya tumefanya kazi miezi minne lakini tumelipwa mwezi mmoja tu na si sisi peke yetu na hata 
watendaji wa wizara wanaofanya kazi hii nao hawajalipwa wakati fedha zipo " alisema mmoja wa vibarua hao.

Kibarua huyo alisema kuwa kuna mmoja wa kiongozi wa wizara hiyo anayesimamia mradi huo ndiye kikwazo kikubwa cha mradi huo na jitihada za makusudi 
zisipochukuliwa mradi huo hautafikia malengo yake.

“Binafsi acha niseme ukweli mradi huu ulianza vizuri lakini sasa utakwama kwani viongozi waliopo pale wizarani wameanza kutumia fedha vibaya na hawataki kutupa
licha ya fedha za mradi kuwepo na tunapowadai wanasema eti Rais John Magufuli hajaidhinisha fedha hizo wakati sio kweli" alisema mtendaji mwingine wa 
mradi huo kutoka wizarani.

Mtendaji huyo alisema changamoto hiyo yakutopewa fedha zao imewapunguzia mori wa kazi hivyo kuingia mashaka kama mradi huo utakwisha.


“Kiukweli ndugu mwandishi hapa watu wanaishi kama ndege wafanyakazi kila kukicha ila hawajalipwa mwezi wa tatu, ukiangalia kwa sasa wanasema eti hela zao 
zimetoka ila wanalipwa siku 20 wakati mwezi unasiku 30 sasa hizo hela zinazobaki za siku 10 viongozi wanazipeleka wapi? kama si wizi wa macho macho" alihoji 
mtendaji huyo.

Mtendaji huyo aliongeza kuwa jambo hilo limekuwa ni janga kwani watendaji wa mradi huo wapo zaidi ya 50 sasa anapokatwa siku 10 kila mmoja anapata 
shilingi ngapi hanazikosa na fedha hizo zinapelekwa wapi.

Akizungumzia changamoto hiyo Diwani wa Kata ya Kimara ambapo mradi huo upo, Pascal Manota alikiri kwa watendaji hao kutolipwa fedha hizo na tayari amekwisha 
mjulisha Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi juu ya changamoto hiyo.

"Changamoto kubwa ipo kwa viongozi wa wizara waliopewa kufanyakazi hiyo fedha zipo lakini hawawalipi watendaji hali inayozoofisha mradi huo tunamuomba 
waziri aliangalie suala hilo kwa karibu kabla ya mambo kuharibika" alisema Manota.

Manota alisema watendaji hao wa serikali hivi sasa wapo tu ofisini wakisoma magazeti hawana ari ya kazi hali hii imechangiwa na viongozi hao wasiokwenda na kasi ya Rais wetu Dk. John Magufuli ya hapa kazi tu.

Jitihada za gazeti hili za kumpata mratibu wa urasimishaji wa ardhi wa wizara hiyo ambaye anasimamia mradi huo, Lydia Bagenda zilishindikana baada ya kwenda 
ofisini kwake na kuambiwa alikuwa nje ya ofisi kikazi na hata halipopigiwa simu mara kadhaa simu yake ilikuwa imefungwa.

MCHUNGAJI DKT.DANIEL KULOLA KURINDIMA KWENYE MKUTANO MKUBWA WA INJILI JIJINI MWANZA.


Kanisa la EAGT Posta “B” Mabatini Jijini Mwanza chini ya Mchungaji Lameck Nkumba, linawakaribisha watu wote kwenye mkutano mkubwa wa injili utakaofanyika katika viwanja vya kanisa hilo vinavyotizamana na geti la polisi Mabatini nyuma ya iliyokuwa Orange Tree Hotel.

Mhubiri wa kitaifa na kimataifa ambaye amehubiri mataifa mbalimbali duniani ikiwemo Marekani, Canada, Uingereza, Ireland, Wales , Scotland, Ujerumani, Dernmark, Swirtzland, Afrika Kusini, DRC Congo na mengine mengi, Dkt.Daniel Moses Kulola (pichani), atahudumu kwenye mkutano huo akishirikiana na wahubiri wengine.

Ni wiki moja yenye miujiza na uponyaji wa nguvu ya Mungu, kuanzia jumapili tarehe 9.10.2016 hadi jumapili tarehe 16.10. 2016 muda ni kuanzia saa 9.00 mchana hadi saa 12 jioni, kila siku.

Waimbaji mbalimbali akiwemo Mwanyamaki kutoka Morogoro, Emannuel Mgogo kutoka Dar es salaam pamoja na kwaya zinatotamba Jijii Mwanza kama vile Havillah Gospel Singers kutoka EAGT Lumala Mpya, na kwaya ya EAGT Posta “B” zitahudumu kwenye mkutano huo.

Ewe baba, mama, kaka, dada, ndugu, jamaa na marafiki, fika kwenye mkutano huo ili ukutane na nguvu ya Mungu ambapo wagonjwa mbalimbali, wenye mapepo, mikosi na waliofungwa na vifungo vya ibirisi watafunguliwa kwa jina la Yesu, bila malipo.
Kwa msaada wa Kiroho, piga simu nambari 0784 43 77 82 
Bonyeza HAPA Kusikiliza, Au Bonyeza Play hapo chini .

Vijana watakiwa kufanya kazi kwa bidii ili kuondokana na umaskini


Katika kuhakikisha kuwa Tanzania inakuwa nchi yenye maendeleo na iliyo na watu ambao wamefanikiwa kimaisha, vijana nchini wametakiwa kufanya kazi kwa bidii ili kujikomboa na janga la umaskini lakini pia kulisaidia taifa kupata maendeleo.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya HiTech International, Paul Mashauri wakati akizungumza na vijana ambao wanajifunza ujasiriamali na kuwambia ni vyema wakaongeza bidii katika ndoto wanazotamani kuzifikia ambazo pia zitawasaidia kuondokana na umaskini ambao umekithiri nchini.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya HiTech International, Paul Mashauri akizungumza na vijana kuhusu ujasiriamali.
Alisema ili mtu kufanikiwa kimaisha haitaji zaidi elimu ya darasani bali ni muhusika mwenyewe kujiongeza kwa kufanya kazi kwa bidii katika jambo ambalo anatamani kulifikia na akiwatolea mfano yeye mwenyewe kuwa tangu amalize masomo yake katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam hajawahi kurudi chuoni kuchukua cheti chake lakini amefanikiwa kimaisha.
"Mimi simchukii mtu ila nauchukia umaskini alionao, ukiwa na juhudi katika biashara na kujituma hata Rais Magufuli hatakufikia mshahara watu wanaweza kusema unafanya biashara ya kawaida lakini inakulipa sana, ni wewe tu na juhudi zako unazofanya ili ufanikiwe,
"Maisha hayana formula kuwa kufanikiwa ni lazima uwe na masters ndiyo upate mafanikio, masters ya maisha ni kuwa mtaani maisha yakupige alafu uinuke upambane na uyashinde hapo ndiyo umeyashinda maisha, ukitaka kufanikiwa lazima ufanye kazi kwa bidii hata mimi natumia muda wangu mwingi kujifunza ili nizidi kufanikiwa," alisema Mashauri.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya HiTech International, Paul Mashauri akiwaeleza vijana jinsi wanavyoweza kufanikiwa kimaisha kwa kufanya biashara.

Aidha Mashauri aliwataka vijana hao kutumia fursa ambayo inatolewa na kampuni yake ya kuuza vifaa vya viwandani ya HiTech International kwa kuwapatia mkopo wa mashine watu ambao wanatamani kufanya biashara za aina mbalimbali ili waweze kufanikiwa kama matajiri wengine wakubwa nchini wamevyofanikiwa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya HiTech International, Paul Mashauri akiwaonyesha moja ya mashine ambazo Kampuni ya HiTech International inaziuza.
Nae mwendesha mafunzo kwa vijana hao kutoka Shirika la Kazi Duniani (ILO), Benny Mwambela alisema mafunzo hayo yameanzishwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni na Shirika la Kazi Duniani (ILO) ili kuwasaidia vijana kupata mbinu za jinsi gani wanaweza kufanikiwa kibiashara na baada ya mafunzo hayo, wahitimu watakwenda kutoa elimu kwa vijana wengine.
"Tunafundisha walimu ambao watakwenda kufundisha watu wengine kuhusu ujasiriamali, kuna watu wasiopungua 10,000 wamejiandikisha kujifunza ujasiriamali kwahiyo tunawafundisha watu hawa ili wakawafunze na wengine ili na wao wajue jinsi gani wanaweza kufanya biashara,
"Wanafundishwa jinsi ya kubuni wazo la biashara, kuna wengine wana mawazo ya biashara watafundishwa jinsi ya kuanzisha biashara, na kuna wengine wanafanya biashara wanafundishwa jinsi ya kutanua biashara na watafundishwa kuhusu kuanzisha vikundi na jinsi gani ya kutumia fedha," alisema Mwambela.
Na Rabi Hume, MO BLOG
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya HiTech International, Paul Mashauri akiwaeleza vijana jinsi wanavyoweza kuepuka umaskini kwa kufanya kazi kwa bidii.
Baadhi ya vijana walioshiriki semina hiyo.



Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya HiTech International, Paul Mashauri akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, waendeshaji wa mafunzo na washiriki wa mafunzo. (Picha zote na Rabi Hume, MO BLOG)

SSRA YAWATOA HOFU WANANCHI KUHUSU MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII NCHINI

 Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Onorius Njole (kushoto), akitoa ufafanuzi mbalimbali kwenye semina ya siku moja ya wanahabari kuhusu mifuko ya jamii Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkuu wa Idara ya Uhusiano na Uhamasishaji, SSRA, Sarah Kibonde.
 Mkurugenzi wa Tafiti, Sera na Tathmini wa SSRA, Ansgar Mushi akitoa mada katika warsha hiyo.
 Waandishi wa habari wakiwa katika semina hiyo.
 Waandishi wakiwa kwenye semina hiyo
 Semina ikiendelea.
 Waandishi wa habari wakichukua mambo kadhaa kwenye semina hiyo.
 Wanahabari wakiwa makini katika semina hiyo.
 Maswali yakiulizwa.
 Taswira meza kuu katika semina hiyo.

Picha ya pamoja waandishi wa habari na maofisa wa SSRA.


Na Dotto Mwaibale

MAMLAKA ya Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii nchini (SSRA), imewataka Watanzania kuondoa hofu iliyojengeka kwenye jamii kuwa mifuko ya hifadhi ya jamii ina hali mbaya kifedha.

Akizungumza katika warsha maalum ya siku moja ya waandishi wa habari, iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi wa SSRA, Ansgar Mushi alisema kuwa mifuko hiyo haina hali mbaya kama wanavyodhani watu katika jamii kwani ina fedha za kutosha.

“Watanzania wamekuwa wakiambizana kuwa mifuko hii ina hali mbaya kifedha, napenda kuwahakikishia kuwa ina fedha za kutosha kwani tumekuwa tukifanya ukaguzi wa mara kwa mara. Katika kaguzi zetu za mara kwa mara hakuna mfuko tuliobaini kuwa una kasoro au upungufu wowote,” alisema Mushi.

Aidha, Mushi alisema kwa mwaka mifuko hiyo ya pensheni imekuwa ikikusanya jumla ya sh trilioni 1.692 wakati mfuko wa bima ya afya (NHIF) unakusanya sh bilioni 88.5 ambapo jumla ya makusanyo yote ni sh trilioni 1.78.

Kwa upande wa fao la kujitoa, Mushi alisema licha ya kutawaliwa na sintofahamu, fao hilo lilifutwa na Serikali kuanzia mwaka 2012 na kwa sasa SSRA imeanzisha mchakato wa kuratibu uanzishwaji wa fao la upotevu wa ajira.

Mushi alisema kuwa fao hilo lilipofutwa, bado kulikuwa na mifuko iliyoendelea kuruhusu kujitoa lakini kwa sasa wameamua waanzishe mchakato wa fao la kupoteza ajira, ambalo ni mahususi kwa ajili ya kuwanufaisha waathirika.

“Fao la Upotevu wa ajira litakuwa mahsusi kwa ajili ya wale waliopoteza ajira zao, huku wakiwa wamechangia mifuko ya hifadhi kwa kipindi cha miezi zaidi ya 18. Hawa watalipwa asilimia 33 ya mshahara wa mwisho kwa kipindi cha miezi 6,”

“Kipindi hicho cha miezi 6 kikiisha, mtu huyo kama hajapata ajira atawekwa katika hatua nyingine ambapo ataruhusiwa kuchukua nusu ya fedha alizochangia katika kipindi chake cha ajira,” alisema Mushi.

Akizungumzia wale waliopoteza ajira zao wakiwa hawajafikisha kipindi cha miezi 18, Mushi alisema kuwa wataruhusiwa kuchukua asilimia 100 ya fedha walizochangia kipindi chote walipokuwa kwenye ajira.

“Watu hao wataruhusiwa kuchukua fedha zao kwa asilimia 100 ambazo walichangia kipindi wakiwa waajiriwa. Hata hivyo, napenda kuwaambia Watanzania kuendelea kuichangia mifuko hiyo kwani ina manufaa zaidi nyakati za uzeeni baada ya kustaafu,” alisema Mushi.

TAARIFA YA KATIBU MKUU JUU YA UPATIKANAJI WA DAWA


Wednesday, September 28, 2016

22 Watiwa Mbaroni kwa tuhuma za Kutaka Kuchoma Moto Ofisi za CUF Dar es Salaam

Ikiwa zimepita siku kadhaa tangu Kamati ya Uongozi wa Chama cha Wananchi (CUF) kutuhumu baadhi ya viongozi wake waliosimamishwa uanachama kupanga njama za utekaji viongozi wa chama hicho, Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam linawashikiliwa wanachama wa CUF 22 kwa tuhuma za kupanga njama za kufanya fujo na kuchoma mali za ofisi za chama hicho.

Ikumbukwe kuwa, Septemba 16,2016 CUF kupitia Kurugenzi yake ya Habari na Uenezi ilitoa taarifa ya jaribio la utekaji wa Mkurugenzi wa Uchumi na Fedha CUF, Joran Bashange ambapo chama hicho kiliwatuhumu Magdalena Sakaya, Abdul Kambaya na Profesa Ibrahim Lipumba kuwa walinzi wao walijaribu kufanya tukio hilo.

Kamishna wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamanda Simon Sirro jana alisema wanachama hao walikamatwa na zana za kufanyia uhalifu yakiwemo mapanga, Jambia, visu na chupa za kupulizia 10 zikiwa kwenye boksi lenye maandishi ya lugha ya kichina.

Watuhumiwa hao walikamatwa Septemba 25,2016 maeneo ya Mwananyamala katika gari ya abiria ambayo ruti yake inapitia njia ya Buguruni-Mwananyamala.

Kamanda Sirro alisema watuhumiwa hao walikamatwa baada ya askari kupata taarifa kwamba wamekuja Dar es Salaam wakitokea visiwani Unguja kutoka katika matawi mbalimbali ya chama hicho kwa lengo la kufanya fujo.

Aidha, Sirro alisema baada ya watuhumiwa hao kuhojiwa, walieleza kuwa wamekuja kutokana na maelekezo ya kiongozi wa CUF Nassoro Ahmad Mazrui ambaye ni Naibu Katibu mkuu wa chama hicho aliyewataka kuungana na walinzi wenzao waliopo katika makao makuu ya chama hicho yaliyopo Buguruni.

Hata hivyo, baada ya taarifa za watuhumiwa hao kukamatwa kuenea katika mitandao ya kijamii, baadhi ya watu walimhusisha aliyekuwa mwenyekiti wa kamati ya uongozi wa CUF kwa muda Julias Mtatiro kuhusika katika mipango ya njama hizo.

Lakini Kamanda Sirro alieleza kuwa hadi sasa hajapokea taarifa hiyo ya kuhusika kwa Mtatiro na kwamba taarifa hizo si za kweli.

DC KONGWA AMTUMBUA MENEJA WA MAMLAKA YA MAJI

Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Mhe Deogratius Ndejembi akizungumza wakati wa kikao cha Kumng'oa Meneja wa Mamlaka ya Maji safi na salama Wilyani humo
Watumishi wa Mamlaka ya Maji safi na salama WIlayani Kongwa wakizunguza na Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe Deogratius Ndejembi

Tuesday, September 27, 2016

MAONYESHO YA FILAMU ZA BEIJING 2016 CHACHU KWA UKUAJI WA SANAA NCHINI


 Washindi wa kwanza hadi wa tatu wa mashindano ya sauti waliopatikana katika shindano hilo na kujipatia fursa ya kwenda kufanya kazi katika ofisi za makao makuu ya StarTimes yaliyopo jijini Beijing, China wakionesha tuzo baada ya kukabidhiwa na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Anastazia Wambura katika hafla iliyofanyika Dar es Salaam leo. Washiriki 10 walishinda mashindano hayo. Kutoka kushoto ni Hilda Malecela, Safiya Ahmed na Sadiq Kututwa.


Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Anastazia Wambura akisalimiana na mmoja wa washindi 10 wa mashindano ya vipaji vya sauti, Abraham Richard, ambao watakakwenda kufanya kazi makao makuu ya StarTimes jijini Beijing, China wakati wa hafla fupi ya Maonyesho ya Matangazo ya Tamthiliya za Runinga na Filamu za Beijing 2016.

 Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo,  Anastazia Wambura akizungumza na washindi hao.

 Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo,. Anastazia Wambura akiwasisitizia jambo mshindi wa kwanza hadi wa tatu baada ya kuwakabidhi tuzo zao.
 Washindi 10 wa mashindano ya vipaji vya sauti, Abraham Richard, ambao watakakwenda kufanya kazi makao makuu ya StarTimes jijini Beijing, China wakiwa katika picha ya pamoja na kutoka (kushoto) Muwakilishi wa Mamlaka ya Halmashauri ya Beijing, Yang Peili,  Meneja Mkuu wa Shirika la Utangazaji la Taifa, Dk. Ayoub Riyoba, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Anastazia Wambura, Muwakilishi wa Ubalozi wa China nchini,  Guo HaoDong, Makamu wa Rais wa Makampuni ya StarTimes,  Guo ZiQi na Kansela wa Utamaduni katika Ubalozi wa China nchini Tanzania, Gao Wei wakati wa hafla fupi ya Maonyesho ya Matangazo ya Tamthiliya za Runinga na Filamu za Beijing 2016.
 Washindi hao 10 wakifurahia baada ya kukabidhiwa  tuzo.

Na Dotto Mwaibale

STARTIMES  imefanya Maonyesho ya Michezo ya Kuigiza ya Runinga na Filamu za Beijing ya mwaka 2016 kwa mara ya pili jijini Dar es Salaam kwa lengo lakuendelea kukuza ushirikiano wa iutamaduni baina ya China na Tanzania.

Akizungumza wakati wa maonyesho hayo yaliyofanyika katika hoteli ya Hyatt Regency Kilimanjaro jijini Dar es Salaam leo asubuhi, mgeni rasmi Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Anastazia Wambura amesema kuwa kwa muda mrefu serikali ya China na Tanzania zimekuwa na 
mahusiano mazuri katika Nyanja za kiuchumi, kisiasa na kiutamaduni.

“Mahusiano mazuri ya kiutamaduni ndiyo yaliyopelekea serikali hizi mbili kuendelea kushirikiana na kuwa marafiki mpaka hivi leo. Uhusiano huo si tu unatunufaisha katika masuala ya kiuchumi bali pia kijamii. 

Kupitia kazi za sanaa kam vile tamthiliya za michezo ya kuigiza na filamu watu huweza kujua na kujifunza tamaduni za kila upande. 

Nawapongeza StarTimes kwa kushirikiana na ubalozi wa China nchini Tanzania kwa kutuletea maonyesho haya ambayo nina hakika yatakuwa na manufaa makubwa kwa tasnia yetu.” Alisema . Wambura

“Pia ningependa kuwapongeza StarTimes kwa juhudi zao za dhati katika kukuza utamaduni wetu kuipa nafasi lugha ya Kiswahili kuwa mojawapo inayotumika kutafsiri filamu na tamthiliya hizi za 
michezo ya kuigiza. Nimesikia mlifanya shindano la vipaji vya sauti ambapo watanzania kumi walipatikana na watakwenda kufanya kazi katika makao yenu makuu yaliyopo Beijing. 

Hii ni hatua nzuri na jambo la kuigwa kwa kukipa Kiswahili nafasi kubwa. Ninegependa kumalizia kwa kutoa wito kwa washindi waliopatikana kwenda huko China kutuwakilisha vema kama mabalozi wetu na kukifanya Kiswahili kiendelee kutambulika zaidi.” alisema Wambura

Akielezea umuhimu wa maonyesho hayo Makamu wa Rais wa Makampuni ya StarTimes,. Guo ZiQi amebainisha kuwa kihistoria China imedumisha kwa dhati urafiki na mataifa ya Afrika na kushirikisha tamaduni ndio njia madhubuti itakayoenzi mahusiano hayo.

‘’Utofauti ndio unaofanya dunia pawe mahala pazuri pa kuishi na China na Tanzania kwa muda mrefu zimedumisha utamaduni wao unaovutia zaidi. Katika kilele cha mkutano wa jukwaa la ushirikiano baina ya China na Afrika uliofanyika mwaka 2015, Rais wa Jamhuri ya watu wa China, 

 Xi Jinping alionesha nia ya kujizatiti katika kudumisha mahusiano mazuri ya kiutamaduni, kuimarish mafunzo baina ya China na Afrika ili kusonga mbele kwa pamoja na vilevile kuhakikisha mustakabali wa ukuaji wa urafiki baina ya China na Afrika.’’Alisema  ZiQi

‘’Kwa kuendelea kukua kwa mahusiano ya maingiliano ya kiutamaduni baina ya watu wa China na Waafrika, michezo ya kuigiza ya runinga na filamu za Kichina imezidi kujizolea umaarufu na kuwa kichocheo muhimu katika kujenga mahusiano baina ya pande hizo mbili. Kwa hivi sasa Beijing inaongoza China katika uzalishaji wa michezo ya kuigiza ya runinga na filamu. 

Mpaka hivi sasa ina taasisi takribani 3,400 zilizojikita katika uzalishaji wa filamu na vipindi vya uninga na uendeshaji, vikiwa tayari vimekwishazalisha zaidi ya mfululizo wa vipindi vya runinga 3,000 na karibuni filamu 300 kwa mwaka.’’ alisema ZiQi

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Teknolojia na Ufundi ambaye alizungumza kwa niaba ya Ofisa Mtendaji Mkuu wa StarTimes Tanzania, Wang Xiabo alisema kuwa,‘’mnamo mwaka 2014, Halmashauri ya Mamlaka ya Uandishi wa Habari, Uchapishaji, Redio, Filamu na Runinga ya Beijing ilishirikiana na StarTimes kuzindua msimu wa Maonyesho ya Michezo ya Kuigiza ya Runinga na 
Filamu za Beijing katika nchi za Kiafrika. Lengo kubwa lilikuwa ni kuleta simulizi nyingi za Kichina barani Afrika na kukuza uhusiano katika tasnia za filamu na runinga baina ya pande mbili.’’


‘’Maonyesho haya yamefanyika kwa mafanikio makubwa kwa miaka ya 2014 na 2015 mfululizo. Filamu maarufu za Kichina na mfululizo wa michezo ya kuigiza ya runinga  ambayo imeingizwa sauti kwa lugha ya Kiingereza, Kifaransa na lugha nyinginezo tano za Kiafrika zilionyeshwa na StarTimes kwa miaka hiyo iliyopita,’’ alisema Wang Xiabo kuwa,‘’Katika kipindi hiko tamthiliya kama zilipata mapokezi makubwa sana kutoka kwa hadhira ya barani Afrika.


Meneja Mkuu wa Shirika la Utangazaji waTaifa (TBC),  Ayoub Riyoba, ambao ni washirika wa kampuni ya StarTimes katika urushaji wa matangazo ya dijitali nchini Tanzania amebainisha umuhimu wa filamu hizo hususani katika ukuzaji wa tamaduni baina ya nchi hizo mbili.

‘’Tanzania na China zina historia ndefu ya mahusiano tangu enzi hizo za waasisi wa mataifa haya. Nchi hizi mbili zimekuwa zikishirikiana kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni. Sisi kama chombo cha habari cha taifa tumekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha kuwa tunasaidia jitihada za 
serikali kukuza na kuutangaza utamaduni wetu hususani lugha ya Kiswahili. Kwa takribani miaka miwili iliyopita TBC imekuwa ikionyesha tamthiliya za Kichina zilizoingiziwa sauti kwa lugha ya Kiswahili. 

Kwa kufanya hivyo hivyo tamthiliya hizo zimeonyesha kupokewa vizuri na kupendwa sana na watanzania kwani wamekuwa wakielewa kinachoonekana.’’ alisema Riyoba

‘’Mbali na kukuza lugha yetu ya Kiswahili nchini na nje yanchi, hii pia ni fursa kwa tasnia yetu ya filamu kujifunza kutoka kwa wenzetu ambao wamepiga hatua zaidi. Tasnia yetu bado ni change na inahitaji mengi ya kujifunza ili kusonga mbele na kufikia pale walipo wenzetu na kuwa inazalisha kazi nyingi zaidi za sanaa. 

Ningependa kuchukua fursa hii kuipongeza na kuishukuru serikali ya China kwa jitihada zao wanazozionyesha katika kukuza filamu na lugha yetu ya Kiswahili. Na ningependa kuwaahidi kutokana na ushirikiano huu watazamaji wa TBC wataendelea kupata burudani ya tamthiliya 

na filamu nzuri zaidi ya zilizopita.’’  alisema Meneja Mkuuwa TBC katika maonyesho hayo Ubalozi wa China nchini Tanzania pia ulikabidhi mfano wa hati za makubaliano ya kwenda kufanya kazi 
jijini Beijing kwa washindi 10 waliopatikana katika shindano la vipaji vya sauti lililofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita jijini Dar es Salaam.

Washindi hao 10 waliopatikana ni; Hilda Malecela(DSM), Safiya Ahmed(ZNZ), Saiq Kututwa(ZNZ), Mathew Philip Mgeni(Arusha), Maisala Abdul(DSM), Rukia Hamdan(ZNZ), Richard Rusasa (DSM), Happiness Stanslaus - Nyamayao (DSM), Jamila Hassan(DSM) na Abraham Richard (DSM).

CHADEMA IRINGA YASAIDIA ZAIDI YA WANAFUNZI MIA MBILI (200) KUENDELEA NA MASOMO


 Diwani wa   viti maalum CHADEMA Sara Mwajeka na
Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Igumbilo, Fredrick Asenga wakionyesha mfano wa sare za wanafunzi walizotoa msaada
 Naibu Meya wa manispaa ya Iringa Joseph Lyata na Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Igumbilo, Fredrick Asenga wakiwa tayari kukabidhi sare kwa wanafunzi
Hawa ni baadhi ya wanafunzi mia mbili (200) wanaoishi katika mazingira magumu wanatarajiwa kusaidiwa msaada wa pesa kwa ajili ya kununulia sabuni,nauli kila wiki na sare za shule ya msingi.
 
NA FREDY MGUNDA,Iringa

ZAIDI ya wanafunzi mia mbili (200) wanaoishi katika mazingira magumu wanatarajiwa kusaidiwa msaada wa pesa kwa ajili ya kununulia sabuni na nauli kila wiki na wanawake walionda timu maalum ya kutoa msaada kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Msaada huo unatarajiwa kutolewa kwa wanafunzi wanaoishi katika mazingira magumu kutoka kata nne zilizoko manispaa ya Iringa ambazo ni Miyomboni, Igumbilo, Kitanzani na Ruaha na kugharimu zaidi ya shilingi milioni 3.5
 
Akizungumza wakati wa kuwakabidhi msaada wa sare za shule,viatu na soksi wanafunzi hao, katika hafla fupi ya iliyofanyika katika shule ya msingi ya Igumbulo, Diwani wa   viti maalum CHADEMA Sara Mwajeka alisema kuwa wameamua kuwasaidia wanafunzi hao kwa lengo la kuwapatia elimu bora japo kuwa misaada hiyo haiwezi kumaliza shida zao.
Mwajeka aliongeza kuwa wanafunzi wenye mazingira magumu wanatakiwa kusoma ili taifa lipate wasomi wengi wenye tija ya kuisaidai nchi yao kuendelea kiuchumi.
“Mimi kama mama napata uchungu kuona wanafunzi wenye mazingira magumu wanasoma kwa taabu huku wana uwezo mkubwa darasani,hivyo tunajitaidi na kujikuna pale tunapoweza kuwasaidia wanafunzi nawaomba watu wenye uwezo kuwasaidia wanafunzi wote wenye mazingira magumu” alisema Mwajeka.

Kwa upande wake Naibu Meya wa manispaa ya Iringa Joseph Lyata aliwapongeza timu ya wanawake wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) manispaa ya Iringa kwa kutoa msaada huo ambao ni mkubwa kwa maisha ya wanafunzi wanaoishi kwenye mazingira magumu.
“Tanzania yetu kuna matajiri wengi sana lakini wanashindwa kuwasaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu lakini wakimama hawa wamejitoa kwa kile walicho nacho kuwasaidia wanafunzi hao hivyo nami naunga mkono kuendelea kuchangia watoto hawa” alisema Lyata

Aidha Lyata aliwataka viongozi wa nchi kuwaangalia wanafunzi wanaoishi katika mazingira magumu ili kufuata na kumuenzi Mwalimu Nyerere kwa vitendo kwani alikuwa anapenda sana elimu ili wananchi waweze kuongeza ufahamu na kujua mbinu za kujitegemea na sio kuomba omba kila siku.
“Jamani kusaidia wanafunzi wenye mazingira magumu hawana idikadi ya vyama,dini wala makabila tunatakiwa kuwasaidia kutokana na uwezo wetu wa kifedha,mm nimekuwa mwalimu kwa muda mrefu na nayajua matatizo ya wanafunzi wenye mazingira  wanavyosoma kwa taabu ni aibu kwa taifa kama Tanzania kuwa wanafunzi wanaoteseka kama hawa” alisema Lyata.
Naye Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Igumbilo, Fredrick Asenga aliwashukuru timu ya wanawake wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Naibu Meya, Joseph Lyata kuwa kuwasaidia wanafunzi wa shule hiyo kwani wamewapunguzia na kuwaondolea aibu iliyokuwa inawakumba kutokana na umasikini wao.

“Wanafunzi hawa walikuwa wanavaa sare ambazo zilikuwa zimechanika na ilikuwa aibu kwa wanafunzi wengine lakini kwa msaada huu mmefanya wajisikie nao ni matajiri na najua sasa watasoma kwa bidii bila kujiangalia  wamekaaje hongereni sana na karibuni tena kuendelea kuwasaidia wanafunzi hawa” alisema Asenga.


Misaada hiyo imetolewa na timu ya wanawake wa chama cha demokrasia na maendeleo(CHADEMA) manispaa ya Iringa kwa lengo la kuwasaidia watoto wenye mazingira magumu wasome wakiwa na furaha kwa kuwa nao ni binadamu kama binadamu wengine.

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More