Friday, April 29, 2016

CHADEMA Yatangaza Kutoshiriki Kura ya Maoni ya Katiba Mpya

DK. Vincent Mashinji Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (chadema), amesema kuwa Katiba Mpya inayotokana na maoni ya wananchi ndiyo msingi imara pekee unaoweza kuweka mifumo na taasisi kwa ajili ya maendeleo ya kweli yatakayogusa maslahi ya Watanzania wote badala ya nchi kuongozwa na kauli za viongozi.

Kutokana na umuhimu huo wa kuzingatia maoni ya wananchi yanayobeba matakwa yao katika mchakato wa Katiba Mpya, amesema kuwa Chadema hakitashiriki kura ya maoni ya Katiba Mpya Inayopendekezwa ambayo ilipitishwa na Bunge Maalum la Katiba baada ya kubadili na kuondoa mapendekezo yaliyotolewa na wananchi kwenye Rasimu ya Pili ya Katiba Mpya.

Badala yake, Chadema kitaendelea kuweka agenda ya kupigania Katiba Mpya na bora katika vipaumbele vyake, kwa sababu itatibu vidonda na kumaliza makovu yaliyoko katika jamii kutokana na matatizo mbalimbali kama vile ukosefu wa haki, migogoro ya ardhi, wananchi kukosa huduma za msingi za kijamii zikiwemo elimu, maji na afya.

Dkt. Mashinji aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam alipoukaribisha ujumbe wa Chama cha Centre Party cha Norway uliofika ofisini kwake jijini Dar es Salaam kutia saini makubaliano ya ushirikiano kati ya vyama hivyo kwenye Mradi wa Elimu ya Demokrasia awamu ya pili unaofanyika Wilaya ya Mtwara Vijijini.

Dkt. Mashinji pia amekishukuru chama hicho kwa kusaidia kutoa elimu ya uraia kwa Watanzania hususani maeneo ya vijijini katika mradi ambao unahusisha vyama vyote vya siasa vyenye uwakilishi ndani ya Bunge, huku akisisitiza kuwa Chadema kiko tayari kwa ushirikiano unaozingatia maslahi na matakwa ya wananchi hasa katika kukuza uelewa wa kudai haki, demokrasia na uongozi bora ndani ya nchi.

“Suala la Katiba Mpya inayotokana na maoni ya wananchi kama ilivyowasilishwa kwenye rasimu ya pili na Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mpya ni agenda muhimu kwa Watanzania wapenda nchi yao na sisi ni kipaumbele kwa mwaka huu na kuendelea hadi hapo nchi yetu itakapopata Katiba Mpya ya Wananchi.

“Jana na leo tumewasikia baadhi ya viongozi wa serikali wakisema kuwa wanajiandaa kuitisha kura ya maoni…hatutashiriki kura ya maoni ya Katiba Mpya Inayopendekezwa na Bunge Maalum la Katiba. Tunajua Watanzania wengi wanataka Katiba Mpya iliyotokana na maoni yao, si ile iliyochakachuliwa bungeni.

“Katiba Mpya iliweka masuala kuhusu haki za wananchi, kuimarisha misingi na kuweka mifumo ya demokrasia na uongozi bora, walau kwa kuanzia. Hatuwezi kusema sasa tutatumia mikakati gani kuwahamasisha Watanzania kuidai Katiba Mpya…tutajua namna ya kuvuka tukishafika mtoni,” Alisema

Aidha, Katibu Mkuu Dkt. Mashinji alisisitiza kuwa suala la nchi kuwa na misingi na mifumo imara ya demokrasia na uongozi bora ni muhimu kwa Tanzania, katika wakati ambapo nchi inaelekea kwenye uchumi mkubwa wa nishati ya gesi na mafuta, akisema vinginevyo ni hatari iwapo taifa lenye utajiri mkubwa wa rasilimali, litaendelea kuwa na wananchi waliokata tamaa kutokana na mfumo mbovu uliopo.

Kwa upande wake ujumbe huo uliokuwa ukiongozwa na Katibu Mkuu wa Centre Party, Knut Olsen, ulisema kuwa chama hicho kinashukuru kwa mradi huo kuingia katika hatua ya pili kuanzia mwaka 2016-2019 huku hatua ya kwanza ikiwa na mafanikio makubwa katika jamii ya wananchi wa maeneo ya pembezoni.

“Kama unavyojua, mradi huu kupitia TCD unahusisha vyama vyote vyenye uwakilishi ndani ya bunge, na lengo letu ni kuwajengea uwezo viongozi wa vyama hasa wanawake na vijana katika ngazi ya jamii kwenye vitongoji, vijiji, kata na bunge ili waweze kushiriki mchakato wa maamuzi. Tunatarajia kuendelea kupata ushirikiano katika hatua ya pili,” alisema Inger Bigum, ambaye ni Meneja wa Mradi hapa nchini.

Wengine waliokuwa katika ujumbe huo wa Centre Party ni pamoja na Vijana Sara Hamre Katibu Mkuu wa, Katibu Mkuu wa Wanawake, Eline Stokstad-Oslan na Kristin Madsen Katibu Mkuu wa Wazee.

Mradi huo wa Elimu ya Demokrasia katika Wilaya ya Mtwara Vijijini unaohusisha vyama vyenye uwakilishi bungeni kupitia Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) chini ya ufadhili wa chama hicho, katika awamu ya kwanza ulihusisha kata za Msangamkuu, Nanyamba, Ziwani na Mbembaleo na katika sasa awamu ya pili utakuwa katika kata za Mkunwa, Tangazo, Mayanga na Madimbwa.

Trump Achekwa Baada Ya Kushindwa Kulitamka Jina la Nchi yetu Tanzania

Mgombea wa urais kupitia chama cha Republican nchini Marekani ambaye amekuwa akiongoza kwenye kinyang’anyiro hicho, Donald Trump amejikuta akikosolewa vikali kuhusu upeo wake juu ya sera za nje pale aliposhindwa kulitamka bayana jina la Tanzania.

Naibu Spika Achafua Hali ya Hewa Bungeni Baada ya Kumwita Mbunge BWEGE

Naibu Spika Tulia Ackson, ambaye katika vikao vya Bunge anatakiwa kusimamia mijadala kwenye chombo hicho cha kutunga sheria, jana alizua kizaazaa baada ya kumuelezea mbunge wa Kilwa Kusini (CUF), Selemani Said Bungara kuwa ni bwege, akimtaka aache kuonyesha hali hiyo.

Mfanyabiashara Auawa gesti Kwa Kuchomwa Kisu

 
Mfanyabiashara wa mazao, Eliusta Peter(40),   amefariki dunia baada ya kuchomwa na kitu chenye ncha kali shingoni akiwa katika  nyumba ya kulala wageni wilayani Kilombero.

MWANAHABARI MTOTO NA MWANAMAZINGIRA WA UN, GETRUDE CLEMENT AWASILI JIJINI MWANZA.

Shujaa Wetu, Mwanahabari Mtoto, Mwanamazingira Balozi wa Umoja wa Mataifa UN kutoka Mwanza Tz, Getrude Clement (16) jana amewasili nyumbani Jijini Mwanza majira ya saa tatu usiku na kupokelewa kwa shangwe na ndugu, jamaa na marafiki katika Uwanja wa Ndege Mwanza.

Thursday, April 28, 2016

Sakata la UDA Laitikisa Serikali

Wakati Serikali ikiendelea kuchunguza mikataba kati ya Shirika la Usafiri Dar es Salaam (Uda) na Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka Dar es Salaam (Dart) kuhusu Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka (BRT), Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ametia pilipili kidonda kwa kuibua udanganyifu unaolizunguka shirika hilo.

Watakaolipa mishahara HEWA kuburuzwa Mahakamani

Serikali imesema vigogo wa juu katika utumishi wa umma, watakaobainika kuhusika kwa namna moja au nyingine katika kufanikisha ulipaji wa mishahara hewa, watafunguliwa kesi ya jinai.

Msajili wa Vyama Avikaba Koo Vyama 21 Vya Siasa Ambavyo Havijakaguliwa.

Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi ametoa miezi mitatu kwa vyama 21 ambavyo havijakaguliwa kuwasilisha hesabu zake.

Wafanyakazi 8,000 Hawajawasilishiwa Michango ya NSSF

Wafanyakazi takriban 8,000 ambao ni wanachama wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) hawajawasilishiwa michango kutoka kwa waajiri wao yenye thamani ya Sh bilioni 21.4.

Korea Kuleta Walimu wa Sayansi na Hisabati ili Kupunguza Uhaba wa Walimu Nchini

SerikaliI ya Korea imepanga kuleta nchini walimu wa masomo ya hisabati na sayansi kwa shule za sekondari, kusaidia kupunguza uhaba wa walimu wa masomo hayo.

Halmashauri ya Rombo Hatarini Kufutwa

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Saidi Meck Sadiki amesema Halmashauri Wilaya ya Rombo iko hatarini kufutwa kutokana na kushindwa kufikia lengo la Serikali la kukusanya mapato kutoka kwenye vyanzo vyake.

Serikali Kununua Magari Mengi Zaidi ya Polisi

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga amesema katika bajeti ya mwaka huu Serikali imepanga kununua magari mengi na kuyasambaza katika vituo vya polisi vyenye shida ya vitendea kazi.

Madiwani wa Chadema Wilayani Hai Wasusa Kuhudhuria Kikao cha Mkuu wa Mkoa Said Meck Sadiki

Madiwani  wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai wakiongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Helga Mchomvu, wamesusa kuhudhuria kikao cha Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Said Meck Sadiki wakati akizungumza na viongozi wa vitongoji, vijiji, kata, viongozi wa taasisi za serikali na dini.

Wabunge MABUBU Kubanwa Bungeni.

Kiti cha Spika wa Bunge kimesema ipo haja ya kufanya marekebisho ya Sheria pamoja na Kanuni ili kila mbunge apate posho kulingana na kazi aliyofanya bungeni, badala ya utaratibu wa sasa wa kuangalia mahudhurio pekee. 

Wednesday, April 27, 2016

Rais Magufuli Asamehe Wafungwa 3,551

Rais John Magufuli ametoa msamaha kwa wafungwa 3,551, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 52 ya Muungano wa Tanzania.

Mwenyekiti Aweka Majina HEWA Mradi wa Kuokoa kaya Masikini (TASAF )

Wananchi wamemkataa mwenyekiti wa kitongoji cha Mwanogi kijiji cha Bulima, Kata ya Nyashimo wilayani Busega katika Mkoa wa Simiyu, wakimtuhumu kuweka majina hewa katika mradi wa kuokoa kaya masikini unaosimamiwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (Tasaf).

Mwanafunzi Amkaanga kortini polisi anayedaiwa kumbaka katika kibanda cha ulinzi cha benki.

Mwanafunzi wa kidato cha tatu, juzi alimkaanga askari polisi anayedaiwa kumbaka kwa kuieleza Mahakama jinsi alivyotendewa kitendo hicho katika kibanda cha ulinzi cha benki.

Ripoti ya CAG Yawaweka Kikaangoni Vigogo wa Bohari Kuu ya Dawa (MSD)

Ripoti iliyotolewa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Profesa Musa Juma Assad imezichanganya Hospitali ya Taifa Muhimbili na Bohari ya Dawa (MSD), huku Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akihitaji maelezo ya kina kuhusu mkanganyiko huo. 

Tuesday, April 26, 2016

Wananchi wa Kigogo wanufaika na upimaji bure wa afya kutoka Fazel Foundation na TAHMEF

DSC_0039
Na Rabi Hume, MoDewjiBlog
Kwa kuhakikisha jamii inakuwa katika hali ya usalama wa kiafya, Taasii ya Fazel Foundation kwa kushirikiana na Taasisi ya Elimu ya Afya na Madawa (TAHMEF) wametoa huduma ya upimaji wa magonjwa mbalimbali kwa wananchi wa Kigogo, Dar es Salaam.

Zitto Kabwe: Magufuli Hajagusa KANSA Ya Ufisadi

Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe amemtaka Rais John Magufuli kukabiliana na vikundi vya mafisadi vinavyoiba mabilioni ya fedha za umma kupitia mikataba mibovu waliyoingia badala ya kuishia kutumbua majipu.

CAG Aviumbua Vyama vya Siasa ni chama cha CUF Pekee Kilichopeleka Hesabu zake Kukaguliwa

Kati ya vyama 22 vya siasa vyenye usajili wa kudumu, ni chama kimoja tukilichopeleka hesabu zake kukaguliwa kwa kipindi cha miezi sita ya mwanzoni mwaka 2015. 

Polisi Dar Yakamata Ombaomba 45 Dar, 17 Wapelekwa gerezani

Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, wamewakamata na kuwaondoa ombaomba 45 na 17 wamewapeleka gerezani. 

Ofisa wa TRA na Mfanyakazi Mmoja wa Yono Auction Mart Wafikishwa Mahakamani Kwa Rushwa

Ofisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Amani Mkwizu na mfanyakazi wa kampuni ya udalali ya Yono Auction Mart, Edward Magobela wamepandishwa kortini jana wakikabiliwa na mashtaka matatu ya rushwa. 

Deni la Taifa Lazidi Kupaa

Deni la Taifa limeongezeka kwa Sh7.05 trilioni, kutoka Sh26.49 trilioni Juni 30, 2014, hadi Sh33.54 trilioni sawa na ongezeko la asilimia 27. 

Mchina Ahukumiwa Miaka Mitatu Jela Kwa Kuuza Bidhaa Bila Kutoa Risiti

Mahakama ya Wilaya ya Ilala imemhukumu kifungo cha miaka mitatu jela au kulipa faini ya Sh4.5 milioni, mfanyabiashara Huifang Ma baada ya kupatikana na hatia ya kuuza bidhaa na kushindwa kutoa risiti kwa kutumia mashine ya kieletroniki. 

Monday, April 25, 2016

Bomba la Mafuta Kutoka Uganda kuingiza Bilioni 4.8 Kila Siku

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo amesema kuwa mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Hoima, Uganda hadi Tanga ukikamilika utaliingizia Taifa Sh4.8 bilioni kila siku.

TAKUKURU Yaanza Kuchunguza Mabilioni ya Kikwete

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), imeanza kuchunguza fedha za uwezeshaji maarufu kama ‘Mabilioni ya JK’ ambazo hazikurejeshwa na wakopaji nchi nzima.

Nape Ataja Majipu Manne Katika Sanaa Nchini,aahidi Kuyatumbua

Waziri wa Habari,Utamaduni,sanaa na michezo nchini,Nape Nnauye ametaja mambo manne ambayo ni vikwazo ndani ya sekta ya sanaa ya filamu nchini na kuyaita kwamba ni majipu huku akisisistiza kwamba serikali itakwenda kutunga sera ya sekta hiyo katika mwaka wa fedha 2016/17.

CAG Kuanika Mafisadi Bungeni Leo Wakati Akiwasilisha Ripoti Yake

Mdhibiti  na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) leo anawasilisha bungeni ripoti ya mwisho ya ukaguzi wa hesabu za serikali ya mwaka 2014/15.

Kigogo mbaroni kwa kuhifadhi wahamiaji haramu nyumbani

MWENYEKITI wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibondo, Simon Kagoli amefikishwa mahakamani kwa kosa la kuhifadhi wahamiaji haramu nyumbani kwake na kuwatumikisha mashambani.

MADAKTARI BINGWA WA MAGONJWA SUGU NA MAGONJWA MBALIMBALI WANATARAJIA KUTUA MKOANI IRINGA

 
Dokta Abdull Maulid Abdull akimpima Miwani ya kuonea Mwananchi Chale Muumin Fumu mkaazi wa Kijiji cha Matemwe Tunda ngaa katika matibabu yalio fanyika skuli ya matemwe mkoa wa Kaskazini unguja.Dokta Rajab Mohd(picha kutoka maktaba)

Sunday, April 24, 2016

Kilimanjaro: Watumishi HEWA Wakopa Mamilioni ya Pesa Benki

Msako ulioanzishwa na Rais John Magufuli wa kutokomeza tatizo la wafanyakazi hewa katika utumishi wa umma, umeendelea kuibua mazito, ambapo mkoani Kilimanjaro, Benki ya CRDB imejikuta ikitoa mkopo kwa waliokuwa wafanyakazi hewa.

Serikali Yapangua Hoja Moja ya UKAWA

SIKU moja baada ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kususa kuchangia hotuba za bajeti, Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, Florence Mwanri, amesema serikali haikukosea kuipa Wizara ya Ujenzi fedha zaidi ya zilizokuwa zimeidhinishwa na Bunge.

Serikali yawakalia Kooni Watumishi wazembe na wabadhilifu

 
Serikali imesema kuanzia sasa mtumishi wa umma atakayeshindwa kusimamia rasilimali za umma, achague moja kati ya mawili, kuacha kazi au atumbuliwe.

Maalim Seif Aendelea Kummwagia Lawama Rais Mstaafu Jakaya Kikwete Kwa Kupindua Matokeo ya Uchaguzi Mkuu Zanzibar

Katibu Mkuu wa CUF, Seif Sharif Hamad ameendelea kumtupia lawama Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete akidai kuwa alitumia dola ‘kupindua’ demokrasia ili kuinusuru CCM iliyokuwa imebwagwa kwenye Uchaguzi Mkuu uliopita.

Wednesday, April 20, 2016

JUNAYSATY kuwasha moto siku ya Mkwawa Talent Search(MTS) linatarajiwa kufanyika april 30 mwaka huu mkoani Iringa




NA RAYMOND MINJA IRINGA

Lile Shindano la kusaka na kuibua  vipaji vya uimbaji lijulikanalo kama Mkwawa Talent Search(MTS) lenye washiriki zaidi  72 linatarajiwa kufanyika april 30 mwaka huu mkoani Iringa na kuhudhuriwa na wasani mbalimbali toka nyanda za juu kusini

Waziri Kitwanga Aikana Kampuni ya Lugumi

Wakati sakata la Kampuni ya Lugumi kudaiwa kushindwa kutekeleza mradi wa utambuzi wa vidole kwenye vituo vya polisi likianza kudaliwa na  Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga amesema hana uhusiano wowote na kampuni hiyo kama watu wanavyodai. 

Wachina Kizimbani kwa Kukwepa Kodi

Wafanyabiashara wawili raia wa China wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala kujibu shtaka la kuuza bidhaa bila kutoa stakabadhi za kodi za kieletroniki (EFD).

DENMARK YATOA MSAADA WA VIFAA VYA MUZIKI KWA TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBA)

 Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Sanaa  Wizara ya Habari ,Utamaduni, Sanaa,na Michezo Leah Kihimbi akizindua mradi wa vyombo vya muziki kati ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBA)  na Kituo cha Utamaduni na Maendeleo cha Watu wa Denmark (CKU), uzinduzi huo ulifanyika katika Chuo cha Sanaa mjini  Bagamoyo mkoani Pwani jana.

Tuesday, April 19, 2016

MULTICHOICE TANZANIA WATANGAZA WASHINDI WA "JISHINDIE NA DSTV"


bmn2.0-620x308 
Afisa Masoko wa Multichoice Tanzania, Furaha Samalu akizungumza kwa waandishi wa habari (Hawapo pichani) juu ya droo hiyo pamoja na ofa mbalimbali zinazoendelea kutolewa kwa wateja wa DSTV

VICHAKA HATARISHI KATIKA KITUO CHA AFYA BUZURUGA JIJINI MWANZA VYAFYEKWA.

Hali ya Usalama katika Kituo cha Afya cha Kata ya Buzuruga kilichopo Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza imeimarika, baada ya Wakazi wa Kata hiyo wanaounda Kikundi cha Kijamii cha “Ulipo Tupo” kufyeka vichaka vilivyokuwa katika kituo hicho ambavyo vilikuwa vikitumiwa na wahalifu kama maficho yao.

MWAMOTO ATAKA MAJI YA MTO RUAHA MDOGO YAMALIZE TATIZO LA MAJI MJI WA ILULA


MBUNGE wa Jimbo la Kilolo, Venance Mwamoto akiongea neno mbele ya kamati ya maji

SERIKALI KUCHUNGUZA MKATABA WA JENGO LA MACHINGA COMPLEX

 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaa, Paul Makonda (kulia), akikagua vizimba katika Jengo la Machinga Complex Dar es Salaam jana, baada ya kufanyika kikao cha kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa kilichoketi jana kujadili uendeshaji wa biashara wa katika jengo hilo pamoja na kamati ya mkoa iliyoundwa kuchunguza mkataba wa jengo.

MBUNGE WA VITI MAALUMU MKOA WA IRINGA RITHA KABATI AAPISHWA HII LEO MBUNGENI NA KUWA MBUNGE KAMILI.

 mbunge wa jimbo la iringa mjini mch Petter Msigwa akimpongeza mbunge wa viti maalum Ritha Kabati mara baada ya kuapishwa sambamba na watu wengi walimpongeza mbunge huyo kama wanavyoonekana kwenye picha.

Sera Ya Rais Magufuli ya Kubana Matumizi Yawaliza Wafanyabiashara Dodoma

Sera ya Rais John Magufuli ya kubana matumizi serikalini imekuwa majanga kwa wafanyabiashara wa Mkoa wa Dodoma, huku wizara nazo zikionja cha moto. 

Wabunge Wabanwa, Sasa Kusajiliwa Kwa Kuchukuliwa Alama za Vidole 10

Bunge  linaanza rasmi usajili wa wabunge na watumishi wa Bunge hilo pamoja na wageni mbalimbali, wanaoingia bungeni kwa kutumia mfumo wa kisasa wa kuchukua alama za vidole.

Monday, April 18, 2016

Kampuni ya Ivori Iringa,Wanayo hii Taarifa


Kama wewe ni mmoja kati ya watu ambao umekua ukikutana na Chocolate inayotoka nje ya Nchi yenye nembo inayofananishwa na Chocolate ya Ivori Iringa ukahisi labda wamebadilisha muonekano wa nembo yao sasa Uongozi wa Kampuni ya IVORI IRINGA inayo majibu yake kwenye hizi sentensi 5 na inabidi uzingatie pia unapoenda dukani kununua.

Rais Magufuli Amteua Mathias Chikawe kuwa Balozi wa Tanzania nchini Japan.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Mheshimiwa Mathias Meinrad Chikawe kuwa Balozi wa Tanzania  nchini Japan.

Vigogo Jiji la Dar es Salaam Wakalia Kuti Kavu.

Kamati maalumu ya uchunguzi iliyoundwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda imefichua madudu na harufu ya ufisadi katika utekelezwaji wa mikataba mitatu, inayohusu maeneo ya ukusanyaji mapato ya Stendi Kuu ya Mabasi Yaendayo Mikoani ya Ubungo na kodi ya uegeshaji magari katikati ya mji.

Kampuni binafsi zaongoza kuajiri wahamiaji haramu

Ofisa Uhamiaji Mkoa wa Shinyanga, Anamaria Yondani ameeleza kuwa kipindi cha miezi mitatu wamekamata wahamiaji haramu 283, huku kampuni binafsi zikiongoza kwa kuajiri watu hao kinyume cha utaratibu.

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More