Thursday, March 31, 2016

Rais Magufuli Azungumzia Uteuzi wa Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi

Rais John Magufuli amewatoa hofu wakuu wa wilaya na wakurugenzi kuhusu uteuzi wao kwa kuwataka kuchapa kazi kwa bidii ili wawe na nafasi nzuri ya kuteuliwa badala ya kufanya kazi kwa wasiwasi jambo ambalo matokeo yake yatakuwa kuondolewa.

Mwanza Yaongoza Kuwa na Watumishi Hewa Wengi Ikifuatiwa na Arusha

Hatimaye  wakuu wa Mikoa yote nchini wametii agizo la Rais John Magufuli lilokuwa linawataka wasilishe ripoti ya idadi ya watumishi hewa kwenye mikoa husika.

Binti Ajinyonga huko Longido Aacha majina ya watu anaowadai na Kuagiza Walipe Kabla Maiti Yake Haijasafirishwa

Binti mmoja anayejulikana kwa jina la Jesca ambaye ni mfanyakazi wa Longido Mountain Lodge amekutwa amejinyonga katika hotel ya Longido Mountain Lodge na kuacha ujumbe kuwa kifo chake kisihusishwe na mtu yeyote

Wednesday, March 30, 2016

IRFA YAUNDA KAMATI ITAKAYO SIMAMIA CHAGUZI MBALIMBALI MKOA WA IRINGA

 
 Ramadhani Mahano
NA RAYMOND MINJA IRINGA.
CHAMA cha mpira wa miguu Mkoa wa Iringa (IRFA) kimetauwa  kamati ya uchaguzi itakayosimamia chaguzi mbalimbali mkoani Iringa.

Auawa Kwa Kuchomwa Kisu Akigombea Mwanamke Baa

Watu  wawili wameuawa mkoani Shinyanga katika matukio mawili tofauti, likiwamo la kijana kuchomwa kisu akigombea mwanamke katika baa ya Matunu mjini Shinyanga.

Watu Wanne Watiwa Mbaroni Kwa Tuhuma za Kutumia Jina la Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Kutapeli

Watu wanne wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wakikabiliwa na tuhuma za kujipatia fedha kwa kutumia jina la Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

Wafanyakazi watatu TANESCO Watiwa Mbaroni Kufuatia Kifo cha Mfanyakazi Mwenzao Aliyenaswa na Umeme Juu ya Nguzo

Wafanyakazi watatu wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) mkoani Morogoro, wanashikiliwa na Polisi wakihojiwa kutokana na kifo cha mfanyakazi mwenzao, Deo Elias (30), mkazi wa Mazimbu, Manispaa ya Morogoro kwa kunaswa na umeme juu ya nguzo.

Waliompiga Daktari Mkoani Mtwara Wakamatwa Wakijiandaa Kutoroka Kwenda Nje ya Nchi

Kufuatia tukio la ndugu wa mgonjwa  kumpiga Daktari Mkoani Mtwara, tayari jeshi la Polisi Mkoani humo linawashikilia watu kadhaa kwa kitendo hicho cha kumpiga Daktari wakati akiwa katika majukumu yake ya kikazi.

Izzo Bizness Apagawisha wakazi wa Mbeya kwenye Tamasha la Pasaka

Msanii Emmanuel Simwinga maarufu “ Izzo Bizness “ akitumbuiza kwenye tamasha la pasaka la home sweet home lililodhaminiwa Tigo jijini Mbeya jumapili iliyopita.

ASKOFU CHARLES GADI NA WACHUNGAJI WENZAKE WALIOMBEA TAIFA LIPATE MVUA

 Askofu  wa Kanisa la God News for all Ministry, Dk. Charles Gadi, akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhu kabla ya kuliombea taifa lipate mvua akiwa na wachungaji mbalimbali. Kulia ni Mchungaji Palemo Masawe.

KAMATI YA BUNGE YA HUDUMA ZA JAMII YATEMBELEA BOHARI YA DAWA MSD JIJINI DAR ES SALAAM

 Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii, Peter Serukamba (kushoto), Wajumbe wa kamati hiyo na Mkurugenzi wa Bohari ya Dawa (MSD), Laurean Banakunu (kulia), wakitembea wakati kamati hiyo ilipotembelea MSD Makao Makuu Keko Dar es Salaam.

Tuesday, March 29, 2016

COSATO CHUMI APONGEZWA NA WANANCHI WA JIMBO LA MAFINGA MJINI


mbunge wa jimbo la Mafinga mjini mkoani Iringa  Cosato Chumi akiwa na balozi wa korea  mh Geum-young song wakipata picha ya pamoja baada ya maongezi ya muda mrefu.

Wafuasi Zaidi ya 600 wa UKAWA Wakiongozwa na Freeman Mbowe Wafanya Tukio Kubwa Nyumbani Kwa Lowassa

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),Freeman Mbowe, amewashauri Watanzania wasife moyo kwa matokeo mabaya ya uchaguzi yaliyopinduliwa; na kwamba matokeo hayo yawe chachu ya kufanya  vizuri zaidi katika uchaguzi ujao.

Serikali ya Tanzania kujenga bomba la mafuta kutoka Tanga hadi Uganda.

Serikali za Tanzania na Uganda zinatarajia kuanzisha mradi wa uwekezaji wa ujenzi wa mradi wa bomba la mafuta unaolenga kuongeza pato la taifa na uchumi wa nchi hizo.

Utafiti: Wanawake Wanne Kati ya 10 Wanaofanya Biashara ya Ngono Wana UKIMWI

Utafiti uliofanywa na Shirika lisilo la kiserikali linalojihusisha na upimaji wa virusi vya Ukimwi la MATUMAINI, unaonyesha kuwa kati ya wanawake kumi wanaofanya biashara ya ngono wanaopima wanne kati yao wanakutwa na virusi vya Ukimwi.

Monday, March 28, 2016

Watu sita wamefariki dunia na wengine zaidi ya 38 kujeruhiwa na kulazwa kwenye hospitali ya rufaa mkoa wa Iringa

 Askari   polisi na  wasamaria  wema  wakisaidia  kutoa maiti  kutoka katika  basi la Lupondije Express namba T 798 AKV kutoka Mwanza - Iringa baada ya  kupinduka  eneo la Mteremko wa Ipogolo mjini Iringa. 

20 Watiwa Mbaroni Wakituhumiwa Kumpiga Mawe Ofisa wa JWTZ

Polisi mkoani Ruvuma inawashikilia waendesha bodaboda 20 Manispaa ya Songea wanaodaiwa kumshambulia askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Kikosi cha 411 KJ Ruhuwiko, kwa kupiga mawe gari alilokuwa akiendesha baada ya kumgonga mtembea kwa miguu.

AJALI YA BASI LA LUPONDIJE EXPRESS KUTOKA MWANZA - IRINGA YAUA HAPA MKOANI IRINGA

 Askari   polisi na  wasamaria  wema  wakisaidia  kutoa maiti  kutoka katika  basi la Lupondije Express namba T 798 AKV kutoka Mwanza - Iringa baada ya  kupinduka  eneo la Mteremko wa Ipogolo mjini Iringa.

Sunday, March 27, 2016

Ajali ya Lori Yaua watu 7 na Kujeruhi 10

WATU saba wamekufa na wengine 10  k u j e r u h i w a baada ya gari walilokuwa wanasafiri nalo aina ya Mitsubishi Fuso kupasuka tairi la mbele na kugonga kingo za barabara katika barabara kuu ya Igunga-Singida.

Mtoto wa Siku Moja Aibwa Hospitali ya Rufaa ya Bugando

Mtoto wa siku moja ameibwa katika mazingira ya kutatanisha katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando, akiwa pembeni mwa mama yake aliyekuwa amelala, mwenye umri wa miaka 16.

Madereva Watatu wa Malori Wajeruhiwa Kwa Risasi na Mlinzi wa Hoteli

Madereva watatu wa malori yaendayo mikoani na wasaidizi wao watatu, wamenusurika kifo baada ya kupigwa risasi sehemu mbalimbali za mwilini na mlinzi wa nyumba moja ya wageni iliyopo Ubena, Chalinze mkoani Pwani.

Saturday, March 26, 2016

Maalim Seif Sharif Hamadi Arejea Zanzibar Baada ya Kukaa Mapumzikoni Serena Hoteli Kwa Siku 17

Siku chache baada ya Rais wa Zanzibar Dr Ali Mohamed Shein kuapishwa baada ya kushinda uchaguzi wa marudio uliosusiwa na baadhi ya vyama vya upinzani, Katibu mkuu wa chama cha wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, amerejea Zanzibar.

Polisi Amtandika Risasi Dereva wa Daladala Baada ya Kupishana Kauli

Polisi mmoja anadaiwa kumpiga risasi dereva daladala, Pistus Ngowi baada ya kutofautiana kauli.

Tukio hilo lililotokea juzi saa tatu usiku, Kariakoo jijini Dar es Sallam  lilisababisha madereva wenzake wanaofanya wote safari za Tandika pamoja na wa Temeke kugoma kwa zaidi ya saa tano wakidai kwamba licha ya kushambuliwa, amebambikiwa kesi katika Kituo cha Polisi cha Msimbazi.

Waliokula mishahara HEWA Singida kusherehekea siku ya Wajinga Rumande

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mathew Mtigumwe ameagiza mamlaka zinazohusika kuwakamata na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria watu watakaobainika kutafuna fedha za mishahara hewa kabla ya mwezi huu kumalizika.

Sakata la Tumbili 61 Waliokamatwa Uwanja wa Ndege Lachukua sura Mpya

Serikali imeunda kikosi kazi kinachohusisha taasisi nyeti nchini kuchunguza sakata la kukamatwa kwa raia wawili wa Uholanzi wakiwa katika harakati za kusafirisha tumbili 61 kwenda nchini Albania.

MAJAMBAZI YAUA NA KUJERUHI JIJINI MWANZA.

Kamanda wa Polisi Mkoani Mwanza, SACP Justus Mamugisha, akitoa taarifa kwa wanahabari.

Watu wawili wameuawa Jijini Mwanza kwa kupigwa risasi na Majambazi, huku Wengine saba wakijeruhiwa katika tukio la uvamizi wa duka lililokuwa likitoa huduma mbalimbali za kifedha.
Habari Zaidi BONYEZA HAPA.

Friday, March 25, 2016

Zitto Kabwe Ahojiwa TAKUKURU

Siku tatu baada ya kuibuka kwa kashfa ya rushwa miongoni mwa wajumbe wa Kamati za Kudumu za Bunge, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imemuita Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe kumhoji.

Muda mfupi baada ya taarifa za kashfa hiyo kuwa wazi, Zitto na mwenzake wa Nzega Mjini, Hussein Bashe ambao ni wajumbe wa Kamati ya Huduma za Jamii, walimuandikia barua Spika wa Bunge, Job Ndugai kujiondoa kwenye nafasi zao ili kupisha uchunguzi dhidi ya tuhuma hizo.

Kamati ya Bunge yashindwa kujadili Deni la taifa

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) imeshindwa kujadili Deni la Taifa na kuagiza kukutana na idara na taasisi sita, zinazohusika na deni hilo.

Polisi Arusha Yamnusuru Na Kipigo Meneja Wa Kiwanda Cha Best Pack .

Jeshi la polisi mkoani Arusha jana lilifanikiwa kumnusuru meneja wa kiwanda cha kutengeneza bidha za plastiki  cha Best Pack kilichopo jijini Arusha,Vijay Kumar raia wa India baada ya kunusurika kupigwa na baadhi ya wafanyakazi wa kiwanda hicho.

Thursday, March 24, 2016

BODABODA MKOANI MWANZA WAADHIA KUANZISHWA KWA UMOJA WA KITAIFA WA BODABODA.

Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mkoani Mwanza Baraka Konisaga (Mtumishi wa Mungu) akuzungumza katika Mkutano Mkuu Muhura wa Kwanza wa mwaka 2016 wa Umoja wa Waendesha Bodaboda Mkoa wa Mwanza uliofanyika Jumamosi Machi 19,2016 katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Pamba Jijini Mwanza. Kushoto kwake ni viongozi wa bodaboda Mkoa wa Mwanza.

Wabunge Waanza Kuhojiwa TAKUKURU Kwa Tuhuma za Rushwa....Zitto Kabwe Apongeza

Siku mbili baada ya baadhi ya wabunge kudaiwa kuhusika katika vitendo vya rushwa, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru), Valentino Mlowola amesema taasisi yake inawahoji wote waliotajwa kuhusika na tuhuma hizo.

Hukumu ya Kutoa Lugha Chafu Inayomkabili Mbunge Saed Kubenea Itatolewa April 13

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu inatarajia kutoa hukumu ya kesi ya kutoa lugha chafu dhidi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda inayomkabili Mbunge wa Ubungo (Chadema), Saed Kubenea, Aprili 13, mwaka huu.

Walinzi Watatu wa Suma JKT Watiwa Mbaroni Kwa Wizi wa Kompyuta 50 Chuo Kikuu

Walinzi watatu wa Suma JKT na askari mmoja wa Kituo  Kikuu cha Polisi Mkoa wa Dodoma, wametiwa mbaroni kwa tuhuma za wizi wa kompyuta zinazokadiriwa kufikia 50 mali ya Chuo Kikuu Dodoma (Udom).

Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) Laridhishwa na Serikali ya Magufuli Katika Mapambano ya Rushwa

Ujumbe wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) umeridhishwa na juhudi zinazofanywa na Serikali ya Rais John Magufuli katika kuongeza juhudi za kupambana na rushwa. 

MSTAHIKI MEYA MANISPAA YA KINONDONI AZINDUA RASMI UGAWAJI WA FEDHA ZA MIKOPO KWA WANAWAKE NA VIJANA

meya wa Kinondoni 
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Mh. Boniface Jacob akizindua rasmi ugawaji wa fedha za Mikopo ya Mfuko wa wanawake na vijana katika Kata 6, kati ya Kata 34 Manispaa hiyo ya Kinondoni

KAMPUNI YA MABIBO BEER YADHAMINI BONANZA LITAFANYIKA LEADERS CLUB JUMAMOSI JIJINI DAR ES SALAAM

 Mwonekano wa chupa ya bia ya Windhoek inayosambazwa hapa nchini na kampuni ya Mabibo Beer Wine and Spirits Ltd.

Wednesday, March 23, 2016

TAMWA WAENDESHA MAFUNZO YA SIKU MOJA YA WADAU WA MRADI WA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA

DSC_7648
Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA, Bi. Eda Sanga akifungua mkutano huo wa siku moja jinsi ya kutoa huduma kwa wahanga wa ukatili wa kijinsia unaosababishwa na unywaji wa pombe kupita kiasi

Binti wa Miaka 17 Ajifungulia Mtoto Chooni Hospitali ya Amana Dar

Msichana wa umri wa miaka 17 ambaye alikuwa katika machungu ya uzazi, amejikuta akijifungulia mtoto chooni baada ya muuguzi mmoja wa Hospitali ya Amana jijini Dar es Salaam kumtaka aende kuoga na kubadilisha nguo bila ya kujali hali yake.

Utata Wagubika Waliokufa Kwa Kunyongwa Gesti.

Hatimaye kitendawili cha watu watatu walionyongwa kisha kuchomwa moto kwenye Gesti ya Mexico mjini Kyela, kimetenguliwa baada ya ndugu kujitokeza na kuwataja kwa majina halisi.

CUF haitashiriki uchaguzi wowote chini ya Tume ya Jecha Salim Jecha

SIKU mbili tangu kufanyika kwa uchaguzi wa marudio Zanzibar, na siku moja kabla ya kuapishwa Dk Ali Mohamed Shein, Maalim Seif Shariff Hamad, Mgombea wa Urais wa Zanzibar katika uchaguzi wa Oktoba 25 mwaka jana kupitia Chama cha Wananchi (CUF), amesema CUF haitashiriki uchaguzi wowote chini ya Tume ya Jecha Salim Jecha.

CCM na CUF Watwangana Ngumi Pemba Wakati Wakisherehekea Ushindi wa Dr. Shein

Jeshi la Polisi jana walitumia mabomu ya machozi kurejesha hali ya amani baada ya wananchi kuanza kupigana kwa sababu za kisiasa wakati wakisherehekea ushindi wa Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein, katika kijiji cha Mjini Wingwi Wilaya ya Micheweni, Pemba.

Watumishi HEWA Anzeni Kujiondoa

Mkuu  mpya  wa  Mkoa  wa  Kagera,Meja  Jenerali Mstaafu, Salum Kijuu amewaagiza  watumishi  wasio  na  sifa za  kuajiriwa kujiondoa  kabla  ya March  31  mwaka  huu.

Tuesday, March 22, 2016

UKAWA Washinda Umeya wa jiji la Dar es Salaam.

Hatimaye uchaguzi wa Meya wa jiji la Dar es Salaam umekamilika leo katika ukumbi wa Karimjee, na kushuhudia Isaya Mwita wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) akitangazwa kuwa mshindi wa uchaguzi huo.

Zitto Kabwe Atangaza Kujiuzulu Ujumbe Kamati ya Huduma Za Jamii Baada ya Wajumbe wake Kutuhumiwa Kwa Rushwa


Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi wa chama cha ACT-Wazalendo, ameishtumu Kamati ya Huduma za Jamii anayohudumu kuwa kuna baadhi ya Wajumbe wammepokea rushwa.

Mahakama Yatupilia Mbali Maombi ya Kuzuia Uchaguzi wa Meya wa Jiji la Dar Es Salaam.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imeamuru uchaguzi wa meya na naibu meya wa Jiji la Dar es Salaam, kufanyika leo kama ilivyopangwa.

Mwandishi wa Habari Salma Said Asimulia Alivyotekwa

Mwandishi wa habari wa Kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL) na DW, Salma Said amedai alitekwa na wanaume wawili baada ya kumkamata na kumuingiza kwenye gari lao kisha kuondoka naye na kumpeleka kusikojulikana.

MKUU WA WILAYA YA IRAMBA LUCY MAYENGA AJISALIMISHA KWA RAIS

AWakati Taifa likisubiri uteuzi wa wakuu wa wilaya huku wanaoshikilia nafasi hizo wakiwa katika chekeche kwa kuzingatia vigezo vitano, Mkuu wa Wilaya Iramba, mkoani Singida, Lucy Mayenga amemuomba Rais John Magufuli asimjumuishe kwenye orodha ya wakuu hao anayotarajia kuitangaza wakati wowote.

NAIBU SPIKA WA BUNGE AHUDHURIA VIKAO VYA KAMATI ZA BUNGE KATIKA KUMBI ZA BENKI KUU JIJINI DAR ES SALAAM

  Naibu Spika wa Bunge, Tulia Mwansasu (kushoto) akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Sheria Ndogo alipohudhuria kikao cha kamati hiyo kilichoketi katika Kumbi za Benki Kuu (BoT Dar es Salaam leo.Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa  kamati hiyo, William Ngeleja.

KIPINDUPINDU CHAENDELEA KUUA MKOANI IRINGA


NA RAYMOND MINJA IRINGA 
Idadi ya waliokufa kutokana na ugonjwa wa kipindupindu katika tarafa ya Pawaga, wilaya ya Iringa  mkoani Iringa imeongezeka na kufikia watano baada ya mgonjwa wengine kufariki na kuzikwa jana kijiji cha Luganga.

Monday, March 21, 2016

Maalim Seif Afunguka wakati Wazanzibar wakipiga Kura.

Aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad ambaye alitangaza kususia uchaguzi wa marudio licha ya jina lake kujumuishwa kwenye makaratasi ya kura, amesema ameiachia CCM kuamua hatma ya nchi hiyo.

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More