Friday, October 28, 2016

AKAUNTI ZA LAKE FM MWANZA NA WAFANYAKAZI WAKE ZATOWEKA HEWANI

Ikiwa yamebaki masaa machache kuelekea kwenye show ya Usiku wa Mshike Mshike iliyoandaliwa na Lake Fm redio ya Jijini Mwanza, akaunti ya Instagram ya redio hiyo imevamiwa na watu wanaosadikika kuwa ni wahuni wa mtandaoni.

"Siku hizi mitandao ya kijamii ina nguvu sana hususani kwenye kusambaza habari, hivyo nadhani wameamua kuingilia akaunti yetu baada ya kuona namna ambavyo tunaitangaza show ya Usiku wa Mshike Mshike inayofanyika leo". Uongozi wa Lake Fm umefafanua na kuongeza;

"Tunapenda kuwaambia Wananzengo wetu kwamba show hiyo itafanyika kama kawaida na tayari Khadija Omar Kopa amewasili Jijini Mwanza kwa ajili ya kuwapa burudani hivyo wasishtuke kutoona posts zetu kwenye mtandao wa Instagram kwani tunapatikana Facebook na Twitter @lakefmmwanza".

Mbali na akaunti ya redio kuibiwa, pia akaunti za Instagram za wafanyakazi wa redio hiyo pamoja na wasikilizaji wake waliokuwa wakipost kuhusu show ya Mshike Mshike zimeibiwa.

Show ya Mshike Mshike inafanyika leo alhamisi Oktoba 27,2016 katika kiwanja cha nyumbani Villa Park Rerort kuanzia saa moja jioni kwa kiingilio cha shilingi 7,000 kabla ya saa tano usiku na shilingi elfu kumi baada ya saa tano usiku ambapo bendi ya Ogopa Kopa Classic pamoja na wasanii mbalimbali akiwemo Fatina Khamis kutoka bendi ya Big Star watakuwepo.
Na BMG
Bonyeza HAPA Kujua Zaidi

TAARIFA YA HOSPITALI KWA NAIBU WAZIRI – WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO MHE. DKT HAMISI KIGWANGALLA (MB) OKTOBA 27, 2016 KATIKA HAFLA YA UZINDUZI WA BODI YA HOSPITALI YA TAIFA YA MAGONJWA YA KUAMBUKIZA – KIBONG'OTO



Mhe. Naibu Waziri Dkt Hamisi  Kigwangalla (MB) – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,
Mhe.  Ndugu Onesmo Buswelu, Mkuu wa Wilaya (SIHA)
Dr Said Egwaga, Mwenyekiti wa Bodi ya Hospitali ya Magonjwa ya Kuambukiza Kibong'oto
Dr Best Magoma, Mganga Mkuu wa Mkoa.
Bwana Saimon Msuya, Katibu wa Mkoa (TUGHE)
Wadau wa Maendeleo (WHO, USAID, CDC-EGPAF, KNCV) mliopo hapa
Viongozi kutoka KCMC, Chuo Kikuu cha Nelson Mandela na CEDHA
Mwenyekiti wa CCM (Wilaya) na viongozi wote wa chama Tawala na Serikali
Viongozi wa vyama vya upinzani
Wageni waalikwa
Wanahabari
Mabibi na Mabwana


Mhe. Mgeni Rasmi, 
Awali ya yote kwa niaba ya Wafanyakazi wa Taasisi ya Magonjwa ya Kuambukiza ya Kibong'oto napenda kukukaribisha wewe pamoja na wageni wote mliopo hapa katika viwanja hivi vya Taasisi. Tunashukuru sana kwa kutenga muda wako adhimu kukubali na kuhudhuria hafla hii muhimu kwa Taifa letu na safari ya kuboresha sekta ya Afya nchini.

Tunakupongeza kwa dhati kwa juhudi zako ambazo zinaonekana wazi tangu ulipokabidhiwa Wizara hiikwa kubuni njia mbali mbali ambazo zimeendelea kuboresha utoaji wa huduma za Afya nchini likiwemo suala la uhakiki ubora wa vituo vya kutolea huduma za afya nchini. Hongera sana

UTANGULIZI:
Hospitali Maalumu ya Taifa ya kutibu Magonjwa ya Kuambukiza ya Kibong'oto (zamani Hospitali ya Taifa ya Kifua Kikuu Kibong'oto) ilianzishwa mwaka 1926 na Dr Norman Davis (Mwingereza) ikiwa ni Kituo cha kutunza wagonjwa - waliogunduliwa kuwa na Kifua Kikuu (Sanatorium) wakati dunia ilikuwa bado haina dawa za kutibu vimelea vinavyosababisha Kifua Kikuu. Mwaka 1952 hospitali ilizinduliwa rasmi kama kituo cha kutibu Kifua Kikuu nchini Tanganyika pamoja na  nchi zingine za Afrika Mashariki, Somalia, Eritrea na Ethiopia.

Mhe. Mgeni Rasmi,
Mwaka 2009 Hospitali ilipewa hadhi ya kuwa Kituo Bora cha utoaji wa Huduma za Kifua Kikuu Sugu nchini – yaani “Center of Excellence for Management of Drug Resistant TB in Tanzania” ikiwa na jukumu la kutibu wagonjwa wote wanaogunduliwa na kifua kikuu sugu kitaifa. 
Tarehe 12 Novemba 2010, Serikali ilitangaza rasmi kupitia tangazo la Gazeti la Serikali namba.828 kuwa Kibong'oto imekuwa Hospitali  Maalumu ya Taifa ya Kutibu Magonjwa ya Kuambukiza (Super specialized Infectious Diseases Hospital – Kibong'oto).  Aidha hospitali ilikamilisha mpango Mkakati wa wa muda mfupi na mrefu mwaka 2013 kwa kushirikiana  na Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Watu wa Marekani (USAID).

Mhe. Mgeni Rasmi,
Kuanzia Mwaka 2013, Hospitali ilianza kutekeleza malengo yaliyomo kwenye mpango mkakati wa Hospitali. Juhudi kubwa imeelekekezwa kutekeleza lengo linalohusu kuimarisha utawala bora katika hospitali kwa kuimarisha mifumo ya uendeshaji wa Hospitali ikiwemo kuunda upya  mfumo wa utawala (organizational structure), kuanzishwa Bodi ya Udhamini, Kamati za Uendeshaji (Executive Management Committee), Kamati ya ukaguzi wa ndani (Internal Audit committee), vitengo mbalimbali kama vile kudhibiti ubora, usimamizi shirikishi, mifumo ya taarifa na kitengo cha mwanasheria wa taasisi. 

Aidha, katika kipindi hicho, Hospitali kwa kushirikiana na Wizara  na wadau wengine iliandaa andiko la kusaidia kupata mchakato wa Kisheria wa kuanzishwa kwa Taasisi hii. Tuna imani kuwa andiko hilo litakamilika katika siku za karibuni.

Napenda kuchukua nafasi hii kukushukuru Mgeni Rasmi kwa kuwa leo hii utakamilisha na kuhitimisha moja ya nguzo muhimu katika maendeleo na ustawi wa Taasisi yetu ambayo ni utawala bora “Good governance” kwa kuzindua rasmi Bodi ya Udhamini.
 


Mhe. Mgeni Rasmi,
Nichukue nafasi hii kukuarifu kuwa, utekelezaji wa malengo mengine yaliyomo katika mpango mkakati unaendelea katika ngazi tofauti  zinazoridhisha. 

Lengo namba moja linaeleza kuwa “Taasisi ya Magonjwa ya Kuambukiza itaendelea kuchangia katika juhudi za taifa za kuboresha tiba kwa magonjwa ya kuambukiza kama vile Kifua Kikuu Sugu, UKIMWI na magonjwa mengine. Kuanzia mwaka 2009 hospitali imetibu wagonjwa zaidi ya 582 wa Kifua Kikuu Sugu kati yao asilimia 40 wakiwa na maambukizi ya UKIMWI.  Matibabu yao kwa sasa yanaanza ndani ya masaa 24. Matibabu yanachukua miezi 18 – 24. Tunafurahi kukutaarifu kuwa asilimia 75 ya wagonjwa hawa wanatibiwa na kupona kabisa kiwango ambacho ni juu ya kiwango cha asilimia 70 kichowekwa na Shirika la Afya Duniani (WHO).  Mpango wa kati ni kufupisha tiba kutoka miezi 18 – 24 na kuwa miezi 9 – 11 huku wataalam wakiendelea kusimamia tiba hiyo ili kuhakikisha matokeo mazuri yanapatikana.

Mhe.Mgeni Rasmi,
Lengo la pili ni kuongeza ushiriki  wa jamii katika mapambano dhidi ya magonjwa ya kuambukiza kwa kuiongezea uelewa, kuzuia unyanyapaa pamoja na kuimarisha masuala yanayohusu jinsia.  Baada ya kubaini ongezeko la TB katika mazingira hatarishi hasa katika mgodi wa uchimbaji madini ya Tanzanite – Mererani, Hospitali ilianzisha huduma za vikoba kwa kutumia idara ya Afya ya Jamii kuelimisha wachimbaji wadogo wadogo wa Tanzanite. Mpaka sasa wachimbaji wadogo wadogo zaidi ya 2,000 wameechunguzwa afya zao. Kati ya hao asilimia 4.5 wamekutwa na maambukizi ya TB na walipatiwa matibabu. Aidha hospitali imeshiriki katika mazungumzo kati ya wamiliki wa migodi pamoja na wizara ya Nishati na Madini ili kuboresha mazingira ya utendaji kazi kwa kutumia maji kwenye mashimo ili kuzuia vumbi inayowaathiri wachimbaji na kuathiri mapafu (Pneumoconiosis).
Mhe. Mgeni Rasmi,
Lengo la tatu la Mpango Mkakati wa Hospitali ni kujenga uwezo wa watumishi kutoa huduma za hali ya juu za tiba kwa wagonjwa pamoja na kuwafuatilia wale wote waliopo kwenye tiba. Serikali imeongeza idadi ya watumishi kwa kuajiri  na mpaka sasa watumishi waliopo ni 253; Miongoni mwao Madaktari wapo 15, mmoja ana shahada ya uzamivu katika eneo la magonjwa ya kuambukiza,5 wana shahada za uzamili katika utaalam mbalimbali, 3 wanaendelea na masomo ya uzamili katika taaluma mbalimbali (Microbiologia, Mionzi na magonjwa ya ndani). Pia tuna wauguzi 67, kumi kati yao ni maafisa wauguzi, Wafamasia wawili, Wataalam wa maabara ni 12, sita kati yao ni wataalamu wa teknologia maabara (Lab scientists), Makatibu wa Afya 2, wahasibu 3, Afisa manunuzi 2 na wengineo. 

Mhe. Mgeni rasmi,
Lengo la nne ni kuanzisha kituo cha mafunzo cha kutibu magonjwa ya kuambukiza katika ngazi ya uzamili (Post graduate courses) na fellowship programu. Kwa kuanza, tumetoa mafunzo kwa watumishi zaidi ya  1,000 kutoka hospitali mbalimbali nchini juu ya tiba sahihi ya Kifua Kikuu Sugu. Lengo ni kuwawezesha kusimamia  tiba ya kifua kikuu sugu kwa wagonjwa wanaotoka hospitali ya Kibong'oto. 
Pia kuna mazungumzo yanaendelea baina yaChuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela ili Hospitali iwe kituo cha mafunzo kwa wanafunzi wa shahada ya uzamili katika sayansi ya magonjwa ya binadamu.
Aidha tulianzisha mafunzo ya muda mfupi ya Mawasiliano Bora kwa wagonjwa na watumishi wa Afya “Health Communication skills” kwa kuwajengea uwezo wa kuwasiliana vizuri na wagonjwa ili kuimarisha mahusiano na ufuasi wa dawa za Kifua Kikuu  Sugu ambayo tiba ni ya muda mrefu
Matokeo ya hili lengo ni kuwa na wataalamu bingwa katika Nyanja ya magonjwa ya Kuambukiza


Mhe. Mgeni Rasmi, 
Lengo la tano ni kuanzisha kituo cha utafiti wa magonjwa ya kuambukiza Kibong'oto. Hospitali –ikishirikiana na wadau kama NIMR, KCMC, Chuo Kikuu cha Virginia (USA) na Shirika la Afya Duniani kitengo cha utafiti magonjwa ya nchi joto (WHO – TDR kufanya tafiti mbalimbali zenye kuimarisha utambuzi wa magonjwa ya TB na magonjwa mengine ya kuambukiza. Aidha kuna machapisho ya kisayansi yamefanyika kutokana na tafiti hizi.

Mhe. Mgeni Rasmi, 
Lengo la sita ni kuendeleza Hospitali ya Magonjwa ya Kuambukiza Kibong'oto kuwa Taasisi Bora katika kutibu magonjwa ya Kuambukiza na kufanya iwe ya mfano nchini. 
Katika lengo hili hospitali imeendelea kutoa ushauri kwa vituo vilivyogatua huduma hizi na kuvifanyia usimamizi shirikishi katika mikoa yote ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Pia Hospitali imeendekea kufanya vikao vya robo mwaka kwa wataalam  wa Tiba ya Kifua Kikuu Sugu ili kujua ufanisi wa tiba baada ya wagonjwa kuruhusiwa, lengo likiwa ni kuendelea kufuatilia ubora wa huduma zinazotolewa kwa kuzingatia viwango na miongozo ya Taifa. Hospitali inashirikiana na vituo hivi kutatua changamoto zinazowakabili watoa huduma.

Pamoja na huduma za moja kwa moja, Hospitali imeendelea kusambaza dawa za za kifua kikuu sugu kwa wagonjwa wote ambao wanaendelea na matibabu  katika vituo vya tiba nchi nzima.


Mhe. Mgeni Rasmi,
Lengo la saba la mpango mkakati ni kuanzisha na kuboresha mifumo ya utawa bora katika Hospitali hii likiwa na shabaha ya kuifanya taasisi. Uwepo wa Bodi ya Wadhamini, mfumo wa utawala wa Taasisi pamoja na usimamizi wa kazi zinazotekelezwa lilishakamilika kwa kuandika nyaraka mbali mbali. Lengo hili limekamilika kwa ushirikiano mkubwa sana na wadau wa Kimaendeleo USAID. Leo hii tunajivunia kuzindua Bodi ya Hospitali.
Mhe. Mgeni Rasmi,
Lengo la nane la mpango mkakati ni kuboresha miundo mbinu ya majengo ili kuwezesha shughuli za Tiba, Mafunzo pamoja na tafiti ziweze kufanikiwa. Katika lengo hili tunaishukuru Serikali kwa kufanya uwekezaji mkubwa katika kuboresha majengo kuanzia mwaka 2004. Mwaka 2010, kazi ziliongezeka katika Hospitali na kusababisha wao kufanya utafiti  na kujua uhitaji mkubwa uliopo wa majengo.
 
Majengo haya yanajumuisha upanuzi wa maabara iwe ya kisasa kwa ajili ya ugunduzi wa magonjwa ya kuambukiza na kufuatilia mwenendo wa magonjwa, Hosteli kwa wanafunzi wa fellowship, Kumbi za mikutano na sehemu za kufundishia (Resource center) pamoja na nyumba za watumishi. 

Mipango yetu ni kuendelea kutafuta njia mbadala ya kuingia ubia na mashirika kama vile Shirika la Nyumba la Taifa, Mifuko ya Hifadhi ya Jamii na mengine ili kuweza kujenga majengo ambayo yatafanyiwa tathmini ya uwekezaji (RETURN ON INVESTMENT). 

Andiko (business plan) limeshafikishwa kwa mchumi wa Wizara ili afanye tathmini ya kichumi juu ya suala la uwekezaji katika majengo.


Mhe. Mgeni Rasmi,
Lengo la tisa ni Kutafuta vyanzo vya fedha ambavyo ndiyo vitakavyotumika kufanikisha malengo mengine nane. 
Vyanzo vikubwa vya raslimali fedha katika Hospitali hii ni Serikali (fedha za uendeshaji, miradi ya maendeleo, fedha ya uchangiaji huduma za afya), Wadau wa maendeleo (Mfuko wa Dunia , East Africa Public Health Laboratory Network Project , Shirika la Kimataifa lisilo la Kiserikali  Norway – LHL International, CDC, USAID pamoja na WHO – TDR).
Kwa kipindi chote, hospitali imekuwa ikitegemea fedha ya uendeshaji wa Hospitali kutoka Serikali Kuu ambapo kwa miaka minne mfululizo fedha hizi zimekuwa hazitoshi kuendesha shughuli za Hospitali hata kutishia wadau wa maendeleo kutokuamini kuwa fedha wanayotoa inaweza kutumika kufanya shughuli nyingine tofauti na malengo halisi yaliyowekwa. Pamoja na mafanikio makubwa yaliyopatikana ndani ya muda mfupi wa kutekeleza Mpango Mkakati wa Taasisi ambao umezingatia Mpango Mkakati wa tatu na sasa wa nne wa  Wizara, Matokeo makubwa sasa na Sera nyingine za Wizara, bado tuna changamoto mbalimbali ambazo tunaamini kwa kushirikiana na Bodi ya Hospitali tutaendelea kupunguza na hatimaye kuondoka kabisa. Nazo ni:
Madeni mbali mbali ya watumishi na wazabuni waliotoa huduma kuanzia mwaka 2010 mpaka Juni 2016 yanafikia Bilioni 1.068
Upatikanaji wa sheria ya kuanzisha Taasisi
Masuala yanayohusu maslahi ya watumishi kama vile upandishwaji vyeo, malimbikizo ya mishahara pamoja na ubadilishwaji wa kada za watumishi waliojiendeleza
Kuhuishwa kwa muundo wa Taasisi
Mhe. Mgeni Rasmi napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa kukubali mwaliko wetu wa kuja kuzindua Bodi ya Hospitali ya Magonjwa  Ambukizi Kibong'oto.  
Tumefarijika sana.
Imeandaliwa na Uongozi wa Hospitali na kusomwa kwenu na


Dkt. Riziki Michael Kisonga
KAIMU MGANGA MKUU
HOSPITALI YA MAGONJWA YA KUAMBUKIZA KIBONG'OTO

MAMLAKA YA MAJI SAFI NA USAFI WA MAZINGIRA MJINI MOSHI (MUWSA) YAONGEZA VYANZO VIWILI VYA MAJI

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya maji safi na usafi wa Mazingira mjini Moshi,Prof Faustine Bee (kushoto) akimuongoza Waziri wa Maji na Umwagiliaji ,Mhandisi Gerson Lwenge kuelekea katika chanz cha Mkashilingi kilichopo wilyani Hai kwa ajili ya uzinduzi, kulia kwa Waziri ni Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA).Joyce Msiru.
Waziri wa Maji na Uwagiliaji ,Mhandisi Gerson Lwenge akizungumza wakati wa uzinduzi wa chanzo cha maji cha Mkashilingi kilichopo  wilayani Hai mkoani Kilimanjaro.
Baadhi ya wananchi waliohudhuria uzinduzi huo wakimsilikiliza Waziri wa Maji na Umwagiliaji (hayupo pichani) wakati wa uzinduzi wa chanzo cha Mkashilingi.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Said Meck Sadiki akizungumza katika uzinduzi huo.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA) Joyce Msiru akimueleza jambo Waziri wa Maji na Umwagiliaji ,Mhandisi Gerson Lwenge mara baada ya kujionea chanzo cha maji cha Mkashilingi.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji ,Mhandisi Gerson Lwenge akiwasili atika chanzo kingine cha Kaloleni kwa ajili ya uzinduzi rasmi ,kulia kwake ni Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA) Joyce Msiru.
Chanzo cha Maji cha Kaloleni.
Chumba maalumu kwa ajili ya matibabu ya maji.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi,(MUWSA) Joyce Msiru akisoma taarifa ya mradi wa ujenzi wa chanzo cha maji cha Kaloleni.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji ,Mhandisi Gerson Lwenge akizindua mradi wa maji wa Kaloleni.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji,Mhandisi Gerson Lwenge akiotesha mti katika chanzo cha maji cha Kaloleni mjini Moshi.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Meck Sadiki akiotesha mti katika chanzo cha maji cha Kaloleni.
Mwenyekiti wa Bodiya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA) Prof Faustine Bee akiotesha mti katika chanzo hicho.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa MAzingira mjini Moshi (MUWSA) Joyce Msiru akiotesha mti katika chanzo cha maji cha Kaloleni.
Mkuu wa wilaya ya Moshi ,Kippi Warioba akiotesha mti katika chanzo cha maji cha Kaloleni. 

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

Saturday, October 22, 2016

KONGAMANO LA SAUTI YA MWANAMKE KUWAWEKA PAMOJA WANAWAKE JIJINI MWANZA KUJIFUNZA NA KUPATA BURUDANI.

Kongamano la Sauti ya Mwanamke ambalo limeandaliwa na Kampuni ya CHOCOLATE PRINCES inayoandaa kipindi cha THE MBONI SHOW chini ya mtangazaji wake Mboni Masimba, kinachoruka TBC1, litawakutanisha wanawake wengi Jijini Mwanza kupata elimu ya kujikwamua kiuchumi pamoja na kupata burudani.

Ni Jumapili tarehe 06.11.2016 katika Ukumbi wa Gold Crest Hotel kuanzia majira ya saa kumi alasiri kwa kiingilio cha shilingi elfu arobaini pamoja na chakula.

HUDUMA YA MCHUNGAJI DANIEL KULOLA WA KANISA LA EAGT LUMALA MPYA JIJINI MWANZA YAFANA MKOANI DODOMA.

Huduma ya injili iliyofanywa na mchungaji kiongozi wa Kanisa la "EAGT Lumala Mpya Internationa Church " lililopo Sabsaba Ilemela Jijini Mwanza, Dkt.Daniel Moses Kulola (pichani), mkoani Dodoma imekuwa ya kufaana na watu wengi wameokoka na kubarikiwa.

Ni katika mkutano wa injili ulioandaliwa na kanisa la Siloam EAGT Ipagala mkoani Dodoma kwa juma zima ambapo unatariwa kufikia tamati kesho Oktoba 23, 2016.
Picha na Jorum Samwel
Mchungaji Dkt.Daniel Kulola, akiendelea na huduma ya maombezi mkoani Dodoma
Wengi waliponywa na wanaendelea kuponywa kwa jina la Yesu, vifungo vilivyowatesa kwa muda mrefu.
Mchungaji Dkt.Daniel Kulola, akifanya maombezi mkoani Dodoma.

PIKIPIKI YAZUA HOFU BAADA YA KUTELEKEZWA MWAKA MZIMA JIJINI DAR ES SALAAM, UKIIKARIBIA, IKIIGUSA INAJIWASHA POLISI WAGWAYA KUIPELEKA KITUONI

 Mwananchi akipita kwa kuikwepa pikipiki yenye namba za usajili T 684 CJZ aina ya Fokon iliyotelekezwa kwa zaidi ya mwaka mmoja katika Kituo cha waendesha bodaboda cha Maganga Veterinary Dar es Salaam.
 Mwonekano wa pikipiki hiyo kwa nyuma.
Pikipiki hiyo ikiwa katika kijiwe hicho cha  Veterinary Maganga Temeke jijini Dar es Salaam.

Na Dotto Mwaibale

PIKIPIKI yenye namba za usajili T 684 CJZ aina ya Fokon iliyotelekezwa kwa zaidi ya mwaka mmoja katika kituo cha waendesha bodaboda cha Maganga Veterinary Temeke jijini Dar es Salaam inazua hofu kwa wananchi na hata kwa askari polisi ambao wameshindwa kuipeleka kituoni.

Imeelezwa kwamba pikipiki hiyo iliegeshwa katika eneo hilo na mtu mmoja ambaye alifika nayo akiwa akiiendesha mwishoni mwa mwaka jana.

Akizungumza jana na mtandao wa www. habari za jamii.com mmoja wa waendesha bodaboda wa kituo hicho ambaye hakupenda kujitambulisha jina lake alisema pikipiki hiyo inawapa hofu wananchi wa eneo hilo na hata waendesha bodaboda.

"Hata sisi wenyewe tuna hofu na pikipiki hii ndio maana tunaegesha mbalimbali na pikipiki zetu na ndio maana sitaki kutaja jina langu" alisema mwendesha bodaboda huyo.

Aliongeza kuwa awali baada ya pikipiki hiyo kutelekezwa katika kituo hicho mtu yeyote alipokuwa akiisogelea au kuigusa ilikuwa ikijiwasha yenyewe lakini baada ya kupita mwezi mmoja iliacha kujiwasha jambo ambalo limeongeza hofu kwa wananchi.

Mkazi mwingine wa eneo hilo aliyejitambulisha kwa jina moja la Ismail alisema hata walipotoa taarifa kituo cha polisi cha Maganga walishindwa kuichukua pikipiki hiyo kutokana na tabia ya kujiwasha.

Alisema aaskari wa kituo hicho ambacho kipo mita 10 na eneo ambalo ipo pikipiki hiyo walitoa taarifa kwa wenzao wa kituo cha Chang'ombe ambao nao wameshindwa kuichukua na kwenda nayo kituoni kwa ajili ya kumtambua mmiliki wa pikipiki hiyo kupitia namba zake za usajili.

Ismail alisema inawezekana pikipiki hiyo ilifungwa kifaa maalumu cha utambuzi iwapo kama imeibiwa na ndio maana ilipokuwa ikiguswa au kusogelewa inajiwasha yenyewe licha ya baadhi ya watu wanahusisha kujiwasha kwake na imani za ushirikina.

Imeelezwa kuwa pikipiki hiyo wakati inatelekezwa ilikuwa katika hali ya upya lakini hivi sasa imeanza kupoteza upya wake kwa kukosa huduma ya matunzo.

Jitihada za mtandao huu kumpata Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa huo wa Maganga ili kuzungumzia suala hilo zimeshindika baada ya kuelekezwa alikuwa Manispaa ya Temeke kwenye mkutano.

WANAFUNZI WALIOHITIMU DARASA LA SABA 1993 SHULE YA MSINGI NYAKATO JIJINI MWANZA WAIKUMBUKA SHULE YAO.

Baadhi ya Wanafunzi waliohitimu darasa la saba mwaka 1993 (1987-1993) Shule ya Msingi Nyakato Jijini Mwanza (kushoto), wakimkabidhi Afisa Mtendaji wa Kata ya Muhandu ilipo shule hiyo, vifaa mbalimbali vya kurudufu taarifa ambavyo ni printa pamoja na kompyuta walivyovitoa kwa ajili ya shule yao hii leo. 

Mbali na vifaa hivyo, pia wanafunzi hao ambao miongoni mwao ni wafanyabiashara na watumishi wa taasisi mbalimbali za serikali na binafsi, wametoa vifaa vya michezo kwa ajili ya wanafunzi wa shule hiyo ikiwemo mipira na jezi, pamoja na zawadi mbalimbali kwa ikiwemo kompyuka kwa baadhi ya waliokuwa waalimu wao kipindi hicho.
Na BMG
Baadhi ya Wanafunzi waliohitimu mwaka 1993 (1987-1993) Shule ya Msingi Nyakato Jijini Mwanza (kushoto), wakiwakabidhi baadhi ya waalimu pamoja na kamati ya shule hiyo, vifaa mbalimbali vya kurudufu taarifa ambavyo ni printa pamoja na kompyuta walivyovitoa kwa ajili ya shule yao hii leo. 
Baadhi ya Wanafunzi waliohitimu mwaka 1993 (1987-1993) Shule ya Msingi Nyakato Jijini Mwanza (kushoto), wakikabidhi vifaa mbalimbali vya kurudufu taarifa ambavyo ni printa pamoja na kompyuta walivyovitoa kwa ajili ya shule yao hii leo. 
Baadhi ya Wanafunzi waliohitimu mwaka 1993 (1987-1993) Shule ya Msingi Nyakato Jijini Mwanza, wakiwakabidhi vifaa vya michezo wanafunzi wa shule hiyo walivyovitoa kwa ajili ya shule yao hii leo. 
Baadhi ya Wanafunzi waliohitimu mwaka 1993 (1987-1993) Shule ya Msingi Nyakato Jijini Mwanza, wakiwakabidhi vifaa vya michezo wanafunzi wa shule hiyo walivyovitoa kwa ajili ya shule yao hii leo. 
Baadhi ya Wanafunzi waliohitimu mwaka 1993 (1987-1993) Shule ya Msingi Nyakato Jijini Mwanza, wakiwakabidhi vifaa vya michezo wanafunzi wa shule hiyo walivyovitoa kwa ajili ya shule yao hii leo. 
Baadhi ya Wanafunzi waliohitimu mwaka 1993 (1987-1993) Shule ya Msingi Nyakato Jijini Mwanza (kulia), wakimkabidhi zawadi ya kompyuta aliyekuwa mwalimu wao, Mwalimu Nicholaus Magashi (kushoto).
Baadhi ya Wanafunzi waliohitimu mwaka 1993 (1987-1993) Shule ya Msingi Nyakato Jijini Mwanza (kushoto), wakimkabidhi zawadi mmoja wa aliyekuwa mwalimu wao, Mwalimu Elizabeth Makonda (kulia).
Kaimu Mkuu wa shule ya Msingi Nyakato Jijini Mwanza, Florence Sam, akisoma taarifa ya shule hiyo kwa wanafunzi waliohitimu shuleni hapo mwaka 1993 walipoitembelea na kutoa vifaa mbalimbali ikiwemo kompyuta pamoja na printa.
Mwalimu Benadetha Athanasi, akitoa taarifa fupi kwa niaba ya wanafunzi waliohitimu shule ya msingi Nyakato Jijini Mwanza mwaka 1993.
Atley Kuni akizungumza kwa niaba ya wanafunzi waliohitimu shule ya msingi Nyakato Jijini Mwanza mwaka 1993, namna wazo kusaidia shule ya msingi waliyosoma lilivyoanza kwenye mitandao ya kijamii (kundi la whatsupp).
Baadhi ya Waalimu wa shule ya msingi Nyakato Jijini Mwanza, kamati ya shule pamoja na baadhi ya waaliohitimu darasa la saba mwaka 1993 katika shule hiyo.
Baadhi ya Waalimu wa shule ya msingi Nyakato Jijini Mwanza, kamati ya shule pamoja na baadhi ya waaliohitimu darasa la saba mwaka 1993 katika shule hiyo, wakiimba wimbo wa Taifa.
Mmoja wa wanafunzi waliohitimu darasa la saba mwaka 1993 katika shule ya msingi Nyakato Jijini Mwanza akijitambulisha.
Mmoja wa wanafunzi waliohitimu darasa la saba mwaka 1993 katika shule ya msingi Nyakato Jijini Mwanza akijitambulisha.
Mmoja wa wanafunzi waliohitimu darasa la saba mwaka 1993 katika shule ya msingi Nyakato Jijini Mwanza akijitambulisha.
Mwalimu Nicholaus Magashi, aliyekuwa mwalimu wa shule ya msingi Nyakato Jijini Mwanza akijitambulisha
Mwalimu Elizabeth Makonda, aliyekuwa mwalimu wa shule ya msingi Nyakato Jijini Mwanza akisalimia
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Nyakato Jijini Mwanza, 2016
Moja ya darasa walilosoma wanafunzi waliohitimu darasa la saba mwaka 1993 katika shule ya msingi Nyakato Jijini Mwnza.
Moja ya darasa walilosoma wanafunzi waliohitimu darasa la saba mwaka 1993 katika shule ya msingi Nyakato Jijini Mwnza.
Picha ya pamoja kati ya wanafunzi waliohitimu darsa la saba shule ya Nyakato Jijini Mwanza, pamoja na waalimu wa shule hiyo.

Na George Binagi-GB Pazzo
Wadau wa elimu mkoani Mwanza wametakiwa kushirikiana na serikali katika kutatua baadhi ya changamoto ikiwemo uhaba wa vyumba vya madarasa pamoja na nyumba za waalimu katika shule ya msingi Nyakato Jijini Mwanza.

Kaimu Mkuu wa shule hiyo, Florence Sam, ametoa rai hiyo wakati wa hafla ya kupokea vifaa mbalimbali ikiwemo kompyuta pamoja na printa, vilivyotolewa na wanafunzi waliohitimu darasa la saba katika shule hiyo mwaka 1993.

Mwalimu Sam amesema shule hiyo ina wanafunzi zaidi ya 1,800 huku vyumba vilivyopo vikiwa ni 18 hali inayosababisha kuwa na upungufu wa vyumba 32 ambapo ametumia fursa hiyo kuwaasa wadau mbalimbali kusaidia kukabiliana na changamoto hiyo.

Akizungumza kwa niaba ya wanafunzi waliohitimu darasa la saba mwaka 1993 katika shule hiyo, Mwalimu Benadetha Athanasi, amesema wanafunzi hao wameamua kusaidia kutatua baadhi ya changamoto za shule hiyo ili kutoa mwamko kwa wadau wengine kusaidia utatuzi wa changamoto za elimu nchini.

Vifaa vilivyotolewa na wanafunzi hao ni pamoja na vifaa vya michezo kwa wanafunzi, kompyuta pamoja na printa ambavyo vimegharimu Zaidi ya shilingi Milioni Mbili.

BENKI YA NMB MLIMANI CITY YATOA SEMINA FUPI KWA WATEJA WAKE KUHUSU HUDUMA WAZITOAZO

Wafanyakazi wa Benki ya NMB Tawi la Mlimani City wakijitambulisha kabla ya kuanza kwa semina hiyo.

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More