Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na
Mahusiano), Deus Sangu, akiwasilisha hotuba yake ya kufunga mafunzo ya usalama
na afya mahali pa kazi kwa wanachama wa kikundi cha Wanawake Wachimbaji Bukombe
(WAWABU).
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na
Mahusiano), Deus Sangu, akiwasilisha hotuba yake ya kufunga mafunzo ya usalama
na afya mahali pa kazi kwa wanachama wa kikundi cha Wanawake Wachimbaji Bukombe
(WAWABU).
Mtendaji
Mkuu wa OSHA, Bi.Khadija Mwenda, akitoa maelezo ya awali kuhusu mafunzo ya
usalama na afya mahali pa kazi yaliyotolewa na Taasisi yake kwa wanachama wa
kikundi cha Wanawake Wachimbaji Bukombe (WAWABU) katika haflaya kufunga mafunzo
hayo.
Wanachama wa kikundi cha Wanawake Wachimbaji Bukombe
(WAWABU), wakifuatilia nasaha na hotuba za viongozi mbalimbali katika hafla ya
kufunga mafunzo ya usalamana afya mahali pa kazi yaliyotolewa kwao na OSHA
ambapo Waziri wa Nchi, Ofisi yaWaziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Mhe.
Deus Sangu alikuwa Mgeni Rasmi.
Na Fredy Mgunda,Geita
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na
Mahusiano), Deus Sangu,amezindua kampeni ya mafunzo kwa wajasiriamali wadogo
ambayo ni sehemu ya programu za uhamasishaji masuala ya usalama na afya kazini
kuelekea maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi
Aprili 28, 2026.
Kampeni hiyo imeanza kwa kutoa mafunzo kwa wanachama wa
umoja wa Wanawake Wachimbaji Bukombe (WAWABU) wanaofanya shughuli za uchimbaji
madini katika Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita ambayo yametolewa mwishoni mwa
wiki (Februari 21, 2026).
Akifunga mafunzo hayo ya siku moja kwa wanawake zaidi ya
350, Waziri Sangu, mbali na kuwapongeza wakazi wa Bukombe kwa kuwa wachapakazi,
amesisitiza juu ya umuhimu wa kuzingatia masuala ya usalama na afya katika
shughuli za uchimbaji madini hususan kwa wachimbaji wadogo ambao mazingira yao
ya kazi yana vihatarishi vingi na teknolojia yao ni duni.
“Tunafanya mafunzo haya kwa kutambua umuhimu wake kwa
wachimbaji wadogo. Tumekuwa tukipata taarifa za matukio mengi ya ajali hususan
kwa wachimbaji wadogo kufukiwa na vifusi wakiwa wanatekeleza majukumu yao. Hii
ni kutokana na kuwa uchimbaji wenu mara nyingi hautumii teknolojia za kisasa
ambazo ni ghali na upatikanaji wake ni mgumu,” amesema Waziri mwenye Dhamana ya
Masuala ya Kazi na kuongeza:
“Nimefurahi sana kuonana na kundi la wachimbaji wanawake
zaidi ya 350 kwani mara nyingi tumezoea kuona shughuli hizi zinafanywa na
wanaume tu. Hivyo, ninawapongeza sana nasisi tutaendelea kuunga mkono jitahida
zenu kwa kuwawezesha kufanya kazi kwa tija na katika hali ya usalama.”
Amemuagiza Mtendaji Mkuu Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa
Kazi (OSHA), Bi. Khadija Mwenda, kuhakikisha mpango huo wa mafunzo unakuwa
endelevu na kuyafikia makundi mengi zaidi ya wachimbaji wadogo na wajasiriamali
katika sekta nyingine za kiuchumi.
Aidha, Waziri Sangu, ametoa rai kwa wachimbaji wadogo
kuzingatia masuala mbalimbali waliyofundishwa katika mafunzo hayo ikiwa ni
pamoja na matumizi endelevu ya vifaa kinga ambavyo baadhi vimetolewa na OSHA
kupitia programu hiyo.
Akizungumza nje ya ukumbi wa mafunzo, Mtendaji Mkuu wa OSHA,
Bi.Khadija Mwenda, amesema lengo la programu ya mafunzo kwa makundi mbalimbali
ya wajasiriamali wadogo ni kuwatambua na kuwajengea uelewa wa masuala ya
usalama na afya ili kuongeza kiwango cha uzingatiaji (compliance level) wa
kanuni bora za usalama na afya nchini.
Aidha, ameahidi kuhakikisha kwamba mpango huo wa mafunzo
unakuwa endelevu kwa mujibu wa maelekezo ya serikali yaliyotolewa na Waziri
mwenye Dhamana ya Masuala ya Kazi nchini.
Kwa upande wao washiriki wa mafunzo hayo akiwemo Mwenyekiti
wa WAWABU, Bi. Regina Kabogo, wameishukuru serikali kwa uwezeshaji waliopata wa
mafunzo na vifaa kinga huku wakiiomba serikali kuwafanyia upembuzi yakinifu wa
hali ya upatikanaji wa dhahabu katika vitalu 13 vinavyomilikiwa na umoja huo.
“OSHA wametufundisha vitu vingi sana kuhusiana na usalama na
afya katika shughuli zetu za uchimbaji madini na wametupatia baadhi ya vifaa
kinga vya muhimu jambo ambalo litatuhamasisha kufanya kazi kwa bidii ili
kujiongezea kipato binafsi pamoja na mapato ya serikali,” ameeleza Bi. Regina
Kabogo.
Mafunzo yalitolewa na OSHA kwa wanachama wa WAWABU
yamehusisha mada mbalimbali zikiwemo dhana ya usalama na afya mahali pa kazi,
vihatarishi vya usalama na afya katika sekta ya madini, sheria ya usalama na
afya mahali pa kazi pamoja na misingi ya huduma ya kwanza mahali pa kazi kwa
nadharia na vitendo.






Monday, February 23, 2026
mwangaza wa hbari
































%20NACHINGWEA,%20AHAIDI%20PIKIPIKI%20MPYA%20NA%20UJEN.webp)
%20NACHINGWEA,%20AHAIDI%20PIKIPIKI%20MPYA%20NA%20UJEN%20(1).webp)
%20NACHINGWEA,%20AHAIDI%20PIKIPIKI%20MPYA%20NA%20UJEN%20(2).webp)






