Friday, March 6, 2026
VIWANDA MKOANI PWANI VYATAKIWA KUBORESHA MAZINGIRA YA KAZI
Monday, February 23, 2026
KAMPENI YA MAFUNZO KWA WAJASIRIMALI WADOGO YAZINDULIWA KUELEKEA MAADHIMISHO YA WIKI YA USALAMA NA AFYA KAZINI 2026
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na
Mahusiano), Deus Sangu, akiwasilisha hotuba yake ya kufunga mafunzo ya usalama
na afya mahali pa kazi kwa wanachama wa kikundi cha Wanawake Wachimbaji Bukombe
(WAWABU).
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na
Mahusiano), Deus Sangu, akiwasilisha hotuba yake ya kufunga mafunzo ya usalama
na afya mahali pa kazi kwa wanachama wa kikundi cha Wanawake Wachimbaji Bukombe
(WAWABU).
Mtendaji
Mkuu wa OSHA, Bi.Khadija Mwenda, akitoa maelezo ya awali kuhusu mafunzo ya
usalama na afya mahali pa kazi yaliyotolewa na Taasisi yake kwa wanachama wa
kikundi cha Wanawake Wachimbaji Bukombe (WAWABU) katika haflaya kufunga mafunzo
hayo.
Wanachama wa kikundi cha Wanawake Wachimbaji Bukombe
(WAWABU), wakifuatilia nasaha na hotuba za viongozi mbalimbali katika hafla ya
kufunga mafunzo ya usalamana afya mahali pa kazi yaliyotolewa kwao na OSHA
ambapo Waziri wa Nchi, Ofisi yaWaziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Mhe.
Deus Sangu alikuwa Mgeni Rasmi.
Na Fredy Mgunda,Geita
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na
Mahusiano), Deus Sangu,amezindua kampeni ya mafunzo kwa wajasiriamali wadogo
ambayo ni sehemu ya programu za uhamasishaji masuala ya usalama na afya kazini
kuelekea maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi
Aprili 28, 2026.
Kampeni hiyo imeanza kwa kutoa mafunzo kwa wanachama wa
umoja wa Wanawake Wachimbaji Bukombe (WAWABU) wanaofanya shughuli za uchimbaji
madini katika Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita ambayo yametolewa mwishoni mwa
wiki (Februari 21, 2026).
Akifunga mafunzo hayo ya siku moja kwa wanawake zaidi ya
350, Waziri Sangu, mbali na kuwapongeza wakazi wa Bukombe kwa kuwa wachapakazi,
amesisitiza juu ya umuhimu wa kuzingatia masuala ya usalama na afya katika
shughuli za uchimbaji madini hususan kwa wachimbaji wadogo ambao mazingira yao
ya kazi yana vihatarishi vingi na teknolojia yao ni duni.
“Tunafanya mafunzo haya kwa kutambua umuhimu wake kwa
wachimbaji wadogo. Tumekuwa tukipata taarifa za matukio mengi ya ajali hususan
kwa wachimbaji wadogo kufukiwa na vifusi wakiwa wanatekeleza majukumu yao. Hii
ni kutokana na kuwa uchimbaji wenu mara nyingi hautumii teknolojia za kisasa
ambazo ni ghali na upatikanaji wake ni mgumu,” amesema Waziri mwenye Dhamana ya
Masuala ya Kazi na kuongeza:
“Nimefurahi sana kuonana na kundi la wachimbaji wanawake
zaidi ya 350 kwani mara nyingi tumezoea kuona shughuli hizi zinafanywa na
wanaume tu. Hivyo, ninawapongeza sana nasisi tutaendelea kuunga mkono jitahida
zenu kwa kuwawezesha kufanya kazi kwa tija na katika hali ya usalama.”
Amemuagiza Mtendaji Mkuu Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa
Kazi (OSHA), Bi. Khadija Mwenda, kuhakikisha mpango huo wa mafunzo unakuwa
endelevu na kuyafikia makundi mengi zaidi ya wachimbaji wadogo na wajasiriamali
katika sekta nyingine za kiuchumi.
Aidha, Waziri Sangu, ametoa rai kwa wachimbaji wadogo
kuzingatia masuala mbalimbali waliyofundishwa katika mafunzo hayo ikiwa ni
pamoja na matumizi endelevu ya vifaa kinga ambavyo baadhi vimetolewa na OSHA
kupitia programu hiyo.
Akizungumza nje ya ukumbi wa mafunzo, Mtendaji Mkuu wa OSHA,
Bi.Khadija Mwenda, amesema lengo la programu ya mafunzo kwa makundi mbalimbali
ya wajasiriamali wadogo ni kuwatambua na kuwajengea uelewa wa masuala ya
usalama na afya ili kuongeza kiwango cha uzingatiaji (compliance level) wa
kanuni bora za usalama na afya nchini.
Aidha, ameahidi kuhakikisha kwamba mpango huo wa mafunzo
unakuwa endelevu kwa mujibu wa maelekezo ya serikali yaliyotolewa na Waziri
mwenye Dhamana ya Masuala ya Kazi nchini.
Kwa upande wao washiriki wa mafunzo hayo akiwemo Mwenyekiti
wa WAWABU, Bi. Regina Kabogo, wameishukuru serikali kwa uwezeshaji waliopata wa
mafunzo na vifaa kinga huku wakiiomba serikali kuwafanyia upembuzi yakinifu wa
hali ya upatikanaji wa dhahabu katika vitalu 13 vinavyomilikiwa na umoja huo.
“OSHA wametufundisha vitu vingi sana kuhusiana na usalama na
afya katika shughuli zetu za uchimbaji madini na wametupatia baadhi ya vifaa
kinga vya muhimu jambo ambalo litatuhamasisha kufanya kazi kwa bidii ili
kujiongezea kipato binafsi pamoja na mapato ya serikali,” ameeleza Bi. Regina
Kabogo.
Mafunzo yalitolewa na OSHA kwa wanachama wa WAWABU
yamehusisha mada mbalimbali zikiwemo dhana ya usalama na afya mahali pa kazi,
vihatarishi vya usalama na afya katika sekta ya madini, sheria ya usalama na
afya mahali pa kazi pamoja na misingi ya huduma ya kwanza mahali pa kazi kwa
nadharia na vitendo.
MIGODI MIKUBWA NCHINI IMETAKIWA KUWEZESHA WACHIMBAJI WADOGO
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Deus Sangu, akiagana na Mkurugenzi Mtendaji wa Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGML), Bw. Ashraf Suryaningrat, mara baada ya kuhitimisha ziara ya kufuatilia utekelezaji wa Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi na Sheria nyingine za kazi katika Mgodi huo.Na Fredy Mgunda,Geita
Wednesday, February 11, 2026
OSHA YAJA NA MPANGO WA KUWEZESHA BIASHARA NA UWEKEZAJI NCHINI
Washiriki wa kikao kazi baina ya OSHA na Maafisa Biashara wa Mikoa na Wilaya za Kanda ya Kaskazini wakifuatilia mawasilisho toka kwa wataalam wa OSHA kuhusu Sheria na Usalama na Afya Mahali pa Kazi pamoja na utekelezaji wa majukumu ya OSHA kwa ujumla.Monday, January 12, 2026
WANAFUNZI VYUO VIKUU WAMETAKIWA KUJIEPUSHA NA NDOA ZA REJAREJA, DKT MSOWOYA
Dkt. Msowoya aliwahimiza wanafunzi kuipenda nchi yao, kusoma kwa bidii na kuepuka makundi yenye viashiria hasi katika masomo na maisha kwa ujumla.
Sunday, January 11, 2026
USHIRIKI WA WANANCHI WAIMARISHA UPANDAJI MITI SAO HILL
Wananchi wanaozunguka Shamba la Miti Sao Hill wameendelea kunufaika kielimu na kiuchumi kupitia ushiriki wao katika shughuli za uchukuaji miche ya miti zinazofanyika katika bustani za miche zilizopo Tarafa ya Kwanza Irundi na Tarafa ya Tatu Ihalimba.
Shughuli hizo ni sehemu ya mpango endelevu wa upandaji miti unaotekelezwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kwa lengo la kuendeleza misitu ya kupandwa, kuongeza uzalishaji wa rasilimali za misitu na kuimarisha uhifadhi wa mazingira.
Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Msaidizi wa Mhifadhi Mkuu wa Shamba la Miti Sao Hill, PCO Said Singano, alisema uchukuaji wa miche unafanyika kwa kuzingatia taratibu na kanuni za kitaalamu ili kulinda ubora wa miche.
“Tunasisitiza miche ichukuliwe kwa uangalifu mkubwa ili isiharibu mizizi, kwa sababu ubora wa miche ndiyo msingi wa mafanikio ya upandaji miti mashambani,” alisema Singano.
Shughuli hizo pia zimeongeza uelewa wa wananchi kuhusu mchango wa Shamba la Miti Sao Hill katika uhifadhi wa mazingira, mapambano dhidi ya mabadiliko ya tabianchi na upatikanaji endelevu wa mazao ya misitu kwa manufaa ya Taifa.
Mmoja wa wananchi walioshiriki zoezi hilo, Bw. Joshua Ng'umbi kutoka Kijiji cha Igowole Wilaya ya Mufindi, alisema ushiriki wake umemsaidia kuongeza kipato na kupata ujuzi mpya katika shughuli za misitu.
“Mbali na kupata ajira, nimejifunza kuchagua miche bora na namna sahihi ya kupanda miti ili iweze kuota vizuri na kukua kwa ubora unaoweza kuleta kipato kizuri wakati wa uvunaji,” alisema Bw. Joshua.
Kwa ujumla, zoezi la uchukuaji miche katika Tarafa za Irundi na Ihalimba limeendelea kuleta manufaa makubwa kwa Shamba la Miti Sao Hill na wananchi kwa kuimarisha juhudi za upandaji miti, kutoa ajira na kukuza uelewa wa masuala ya misitu na uhifadhi wa mazingira.
Wednesday, December 31, 2025
RUNALI YATATUA CHANGAMOTO YA MAJI KITUO CHA AFYA MARAMBO
Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa Hassan Ngoma aliyemwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea katika hafla ya kukabidhi kisima cha maji kilichojengwa na RUNALI katika kituo cha afya Marambo kwa uongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Nachingwea
Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa Hassan Ngoma aliyemwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea akifungua maji wakati hafla ya kukabidhi kisima cha maji kilichojengwa na RUNALI katika kituo cha afya Marambo kwa uongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Nachingwea Na Fredy Mgunda, Nachingwea
Chama Kikuu cha Ushirika RUNALI kimetatua changamoto ya upatikanaji wa maji katika Kituo cha Afya Marambo, changamoto iliyodumu kwa miaka mingi na kusababisha baadhi ya huduma kushindwa kutolewa ipasavyo katika kituo hicho.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kisima hicho cha maji, Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Ushirika RUNALI, Odas Mpunga, alisema kuwa lengo kuu la mradi huo ni kusogeza huduma muhimu kwa jamii inayohudumiwa na Kituo cha Afya Marambo.
Mpunga alisema chama hicho kilipokea maombi ya kusaidia kutatua changamoto ya maji katika kituo hicho cha afya, hali iliyopelekea RUNALI kuchukua jukumu hilo kwa dhamira ya kuisaidia jamii.
Aliongeza kuwa kisima hicho kimekamilika na kuanza kutoa huduma, hivyo ni jukumu la wananchi pamoja na viongozi wa eneo hilo kuhakikisha wanakitunza ili kiwe mradi endelevu wenye manufaa ya muda mrefu.
Kwa upande wake, Meneja wa RUNALI, Jahida Hassan, alisema kuwa utekelezaji wa mradi huo ni sehemu ya kutimiza msingi wa saba (7) wa vyama vya ushirika, unaohimiza vyama hivyo kurudisha mchango kwa jamii inayowazunguka.
Jahida aliongeza kuwa kisima hicho ni kirefu na kina maji ya kutosha, hivyo kinapaswa kutumika kwa malengo yaliyokusudiwa, hususan kuhudumia Kituo cha Afya Marambo.
Alisema kuwa RUNALI imetumia zaidi ya shilingi milioni 15 kuchimba kisima hicho hadi kukamilika kwake na kuanza kutoa huduma za maji katika kituo hicho cha afya.
Naye mgeni rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, akimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Hassan Ngoma, aliwataka wananchi na viongozi wa eneo hilo kuhakikisha wanauhudumia na kuutunza mradi huo ili uwe na manufaa ya kudumu kwa jamii na serikali kwa ujumla.
Ngoma alisema kuwa fedha nyingi zimewekezwa katika mradi huo wa kisima cha maji kwa lengo la kutatua kero ya maji kwa wagonjwa, wahudumu wa afya pamoja na wananchi wanaohudumiwa na kituo hicho, hivyo ni muhimu kulinda na kuutunza uwekezaji huo.
Aidha, aliwahimiza wananchi na wakulima ambao bado hawajajiunga na vyama vya ushirika kufanya hivyo kwa ajili ya maendeleo yao binafsi na maendeleo ya taifa kwa ujumla.
Monday, December 22, 2025
SERIKALI YATOA SIKU 90 KWA WAMILIKI WA MAENEO YA KAZI KUJISAJILI OSHA
Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda, akimkabidhi Waziri wa Nchi, Ofisi yaWaziri Mkuu-Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, vifaa kinga (Personal Protective Equipment-PPEs) ambavyo atakuwa anavitumia anapotembelea maeneo yakazi kwa ajili ya ukaguzi wa mifumo ya usalama na afya
Sunday, December 21, 2025
OSHA YATAJWA KUWA NA NAFASI MUHIMU KATIKA KUWEZESHA SHUGHULI ZA UZALISHAJI – KATIBU MKUU
Wajumbe wa Baraza la OSHA wakiimba wimbo wa mshikamano (solidarity) wakati wa kikao cha Tano cha Baraza la Tano la wafanyakazi wa OSHA kilichofanyika katika Ofisi za OSHA Jijini Dodoma Desemba, 20, 2025Wajumbe wa Baraza la OSHA wakifuatilia majadiliano mbalimbali yaliowasilishwa katika kikaocha Tano cha Baraza la Tano la wafanyakazi wa OSHA kilichofanyika katika Ofisi za OSHA Jijini Dodoma.Desemba, 20, 2025.Na Fredy Mgunda
Katibu Mkuu katika Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano ya Kazi), Bi. Mary Maganga, amesema Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) ni taasisi yenye umuhimu mkubwa katika kuwezesha shughuli za uzalishaji kufanyika kwa tija na ufanisi.
Bi. Maganga ametoa kauli hiyo wakati akifungua Kikao cha Tano cha Baraza la Tano la Wafanyakazi wa OSHA kilichofanyika leo, Desemba 20, 2025, jijini Dodoma, ambapo alikuwa mgeni rasmi.
Amesema OSHA ina jukumu muhimu la kusimamia utekelezaji wa Sheria ya Afya na Usalama Mahali pa Kazi, huku akiipongeza taasisi hiyo kwa kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi. Aidha, amewasisitiza watumishi kuendelea kufanya kazi kwa weledi, kuzingatia kanuni za utumishi wa umma na kuimarisha ushirikiano kazini.
“Kabla ya kufungua rasmi kikao hiki, napenda kusisitiza umuhimu wa kufanya kazi kwa weledi. Mara nyingi tumekuwa tukiamini kuwa wito unawahusu zaidi viongozi wa dini, lakini hata kazi zetu hizi ni wito, kwani kuna wananchi wengi wanaotegemea huduma zetu,” amesema Bi. Maganga.
Awali, akimkaribisha Katibu Mkuu kufungua kikao hicho, Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda, amesema kikao hicho kinalenga kutathmini utendaji wa taasisi kwa kipindi kilichopita na cha sasa, pamoja na kuweka mwelekeo wa maendeleo ya OSHA kwa kipindi kijacho.
Amesema kikao hicho kinatazama utekelezaji wa shughuli za mwaka wa fedha 2024/2025 pamoja na tathmini ya utendaji katika miezi mitano ya mwaka wa fedha 2025/2026, ikiwa ni maandalizi ya bajeti ya mwaka wa fedha 2026/2027.
Bi. Mwenda ameongeza kuwa kikao hicho kilitanguliwa na mafunzo kwa watumishi wote wa OSHA yaliyohusu maadili ya utumishi wa umma, mpango mkakati wa taasisi wa miaka mitano ijayo (2026/2027–2030/2031), masuala ya afya ya akili na itifaki.
Kwa upande wake, akitoa salamu za wafanyakazi, Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya (TUGHE), Bw. Rugemalila Rutatina, ameipongeza OSHA kwa kuzingatia ushirikishwaji wa watumishi wote bila ubaguzi katika kufanya maamuzi yanayohusu utendaji wa taasisi hiyo.
Saturday, December 20, 2025
BWANKU ASHAURI MELI MPYA YA MV MWANZA KUPITA BANDARI YA KEMONDO NA KUPUNGUZA NAULI
Na Fredy Mgunda.
Afisa Tarafa ya Katerero, Bwanku M. Bwanku, ameshauri Meli mpya ya MV Mwanza kupitishwa katika Bandari ya Kemondo na nauli zake kupunguzwa ili wananchi wengi waweze kunufaika na uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali ya Tanzania.
Bwanku alitoa ushauri huo umetolewa wakati wa kikao cha wadau wa bandari za Kagera kilichowakutanisha Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), Kampuni ya Meli Tanzania (TASHICO) pamoja na wadau mbalimbali wa sekta ya usafiri wa majini.
Kikao hicho kililenga kupokea na kujadili maoni ya wadau kuhusu nauli za Meli mpya ya MV Mwanza, kikao kilichofanyika katika Hoteli ya ELCT mjini Bukoba.
Meli ya MV Mwanza ni meli kubwa na ya kisasa iliyojengwa kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 120, ikiwa na uwezo wa kubeba tani 400 za mizigo pamoja na abiria 1,200 kwa safari moja. Meli hiyo inatarajiwa kuanza safari zake rasmi katika Ziwa Victoria, ikihudumia mikoa ya Mwanza, Kagera na maeneo mengine ya ukanda wa Ziwa hivi karibuni.
Akizungumza katika kikao hicho, Bwanku alieleza kuwa licha ya mapendekezo ya awali ya TASAC na TASHICO kuwa meli hiyo itafanya safari kati ya Mwanza na Bukoba pekee, ni muhimu pia ipitie Bandari ya Kemondo ili kuongeza fursa za kiuchumi kwa wananchi wa maeneo ya jirani.
Aidha, alisisitiza umuhimu wa kupunguza nauli za meli hiyo ili wananchi wa kawaida waweze kumudu gharama za usafiri na hivyo kunufaika moja kwa moja na uwekezaji huo wa Serikali.
Kikao hicho kilifunguliwa na Mkuu wa Mkoa wa Kagera kupitia kwa Mkuu wa Wilaya ya Missenyi, Kanali (Mst) Hamis Maiga, ambaye aliwataka wadau kutoa maoni yao kwa lengo la kuboresha huduma za usafiri wa majini katika Ziwa Victoria.
Thursday, December 18, 2025
WAHIFADHI TFS SAO HILL WAJENGEWA UELEWA WA AFYA
Na Fredy Mgunda, Mufindi Iringa
Wahifadhi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kutoka Shamba la Miti Sao Hill wamepatiwa mafunzo maalumu kuhusu masuala ya afya, yakilenga kuongeza uelewa juu ya maambukizi ya Virusi vya Ukimwi (VVU) pamoja na magonjwa yasiyoambukiza, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuboresha ustawi wao na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya uhifadhi wa misitu.
Mafunzo hayo yamelenga kuwaelimisha wahifadhi kuhusu hali halisi ya maambukizi ya VVU, njia za kujikinga, umuhimu wa upimaji wa hiari na wa siri, pamoja na kuondoa dhana potofu zinazokwamisha juhudi za kudhibiti maambukizi. Washiriki walikumbushwa kuzingatia maadili, kujilinda na kuchukua tahadhari stahiki katika maisha ya kila siku.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Mhifadhi Mkuu wa Shamba la Miti Sao Hill, PCO Tebby Yoramu, amesema mafunzo hayo hutolewa kila mwaka kama sehemu ya mafunzo endelevu kwa watumishi wa TFS, yakilenga kuwajengea uwezo wa kujikinga na magonjwa yanayoathiri afya na kushusha kasi ya utendaji kazi.
“Afya njema ni mtaji muhimu katika kulinda rasilimali za misitu, kwani kazi ya uhifadhi inahitaji nguvu, umakini na utayari wa mwili na akili. Ni muhimu kuzingatia maelekezo ya wataalamu ili kujikinga na magonjwa mbalimbali,” amesema PCO Yoramu.
Katika mafunzo hayo, mada za magonjwa yasiyoambukiza yakiwemo shinikizo la damu, kisukari, magonjwa ya moyo na saratani zilijadiliwa kwa kina. Wahifadhi walielimishwa kuhusu dalili za awali, visababishi na athari za magonjwa hayo kwa afya na ufanisi wa kazi.
Washiriki walihimizwa kubadili mtindo wa maisha kwa kuzingatia lishe bora, kufanya mazoezi ya mara kwa mara, kudhibiti msongo wa mawazo na kuepuka matumizi ya pombe kupita kiasi pamoja na uvutaji wa sigara, ambavyo vimetajwa kuwa miongoni mwa vyanzo vikuu vya magonjwa yasiyoambukiza.
Naye Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji wa Mafinga, Dkt. Bonaventura Chitopela, amesema kila mmoja ana wajibu wa kulinda afya yake kwa kupima afya mapema na kufuata ushauri wa wataalamu ili kupata matibabu kwa wakati.
“Tumia fursa hizi kupima afya zenu mara kwa mara ili kujua hali za kiafya mapema, hatua itakayowezesha kupata matibabu na ushauri kwa wakati,” amesema Dkt. Chitopela.
Kwa upande wake, Mkufunzi kutoka TACAIDS na Meneja wa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Bw. Emmanuel Petro, amewataka wahifadhi kutumia kikamilifu elimu waliyoipata kwa kuchukua hatua za mapema dhidi ya changamoto za kiafya, akisisitiza kuwa uzingatiaji wa maelekezo ya wataalamu ni msingi wa kuzuia madhara ya kiafya.
Mafunzo hayo ni sehemu ya jitihada za TFS kuhakikisha wahifadhi na watumishi wake wanakuwa na afya bora, nidhamu na uwajibikaji. Wahifadhi walioshiriki wameahidi kuzingatia elimu waliyoipata na kuwa mabalozi wa afya njema katika maeneo yao ya kazi na jamii zinazowazunguka.
MBUNGE LIWAKA KUWANUNULIA KOFIA NGUMU BODABODA ZAIDI YA 300.






Friday, March 06, 2026
mwangaza wa hbari
































%20NACHINGWEA,%20AHAIDI%20PIKIPIKI%20MPYA%20NA%20UJEN.webp)
%20NACHINGWEA,%20AHAIDI%20PIKIPIKI%20MPYA%20NA%20UJEN%20(1).webp)
%20NACHINGWEA,%20AHAIDI%20PIKIPIKI%20MPYA%20NA%20UJEN%20(2).webp)



