Thursday, April 28, 2016

Serikali Kununua Magari Mengi Zaidi ya Polisi

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga amesema katika bajeti ya mwaka huu Serikali imepanga kununua magari mengi na kuyasambaza katika vituo vya polisi vyenye shida ya vitendea kazi.

Kitwanga alisema hayo bungeni jana alipokuwa akijibu swali Mbunge wa Igalula, Musa Ntimizi (CCM), aliyetaka kujua kama wizara haioni umuhimu wa kuvipatia vituo vya polisi magari ambavyo havina katika jimbo hilo ili kurahisisha utendaji kazi.

Mbunge huyo pia alitaka kujua kama Serikali itakuwa tayari kumalizia ujenzi wa kituo cha polisi katika Kata ya Loya katika Halmashauri ya Tabora (Uyui) ambapo kwa sasa wananchi wameishiwa nguvu ya kuendeleza ujenzi huo. 

“Serikali inatambua kazi kubwa inayofanywa na wananchi katika kuchangia maendeleo, naomba mbunge uwasiliane na wizara ili tuweze kuona namna ya kusaidia kumalizia ujenzi wa kituo hicho,” alisema Kitwanga.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More