
DK.
Vincent Mashinji Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(chadema), amesema kuwa Katiba Mpya inayotokana na maoni ya wananchi
ndiyo msingi imara pekee unaoweza kuweka mifumo na taasisi kwa ajili ya
maendeleo ya kweli yatakayogusa maslahi ya Watanzania wote badala ya
nchi kuongozwa na kauli za viongozi.
Kutokana
na umuhimu huo wa kuzingatia maoni ya wananchi yanayobeba matakwa yao
katika mchakato wa Katiba Mpya, amesema kuwa Chadema hakitashiriki kura
ya maoni ya Katiba Mpya Inayopendekezwa ambayo ilipitishwa na Bunge
Maalum la Katiba baada ya kubadili na kuondoa mapendekezo yaliyotolewa
na wananchi kwenye Rasimu ya Pili ya Katiba Mpya.
Badala
yake, Chadema kitaendelea kuweka agenda ya kupigania Katiba...