Thursday, November 23, 2017

WAZIRI LUKUVI AFUTA VIWANJA VYA ENEO LA MAWELEWELE MANISPAA YA IRINGA

 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi amefuta viwanja vilikuwa vimepimwa vya eneo la Mawelewele wakati akiwahutubia wananchi wa kata ya Kitwiru katika uchaguzi mdogo wa udiwani kwa kumnadi mgombea wa CCM Baraka Kimata
 baadhi ya wananchi wa kata ya Kitwiru waliokuwa wamejitokeza kumsikiliza Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi alipokuwa akiomba kura za Baraka Kimata ili awe diwani wa kata hiyo
viongozi wa chama cha mapinduzi CCM wakiwa na mtoto ambaye alikuwa kivutio katika kampeni za kumnadi mgombea udiwani wa chama hicho Baraka Kimata 

Na Fredy Mgunda,Iringa.

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi amefuta viwanja vilikuwa vimepimwa vya eneo la Mawelewele pamoja na mchoro wake kutokana kukiuka matumizi yake na kuwataka wananchi walikuwa wamenunua viwanja hivyo waende manispaa wakadai pesa zao.
 
Akizungumza wakati wa kampani za uchaguzi wa kata ya Kitwiru,waziri Lukuvi alisema kuwa amekuwa akipokea malalamiko mengi kuhusu swala la viwanja na mchoro wa Mawelewele hivyo ameamua kufuta rasmi hadi pale serikali itakapopanga matumizi yake.

“Nimefuta mchoro uliokuwa uliokuwa umepima vile viwanja  kwa kuwa manispaa ya Iringa unauhaba wa maeneo ya kufanyia maendeleo kwa kuwa bado wanatafuta ardhi kwa ajili ya kupanga maendeleo hivyo kama kuna mtu alinunua kiwanja kule aende manispaa akadai pesa zake” alisema Lukuvi

Lukuvi alisema kuwa halimashauri ya manispaa ya inauhaba wa ardhi ya kujenga shule na hospital lakini kuna viongozi wanagawana maeneo makubwa hivyo ameamua kufuta kwa faida ya wananchi na vizazi vijavyo kwa kuwa kila siku watu wanaongezeka hivyo vile viwanja ni hazina ya serikali.

“Haiwezekani tunauhaba wa vyumba vya madarasa kwa ajili ya kusomea watoto wetu halafu kuna watu wanachukua ardhi kubwa namna ile kwa ajili ya kujinufaisha wao binafsi haiwezekani na serikali ya awamu ya tano haipo tayari kuona mambo kama hayo yakitoe” alisema Lukuvi

Aidha Lukuvi alisema kuwa serikali ya awamu ya tano ikisikia kero ya wananchi inaifanyia kazi haraka iwezekavyo kwa maslai ya taifa na ndio maana ameamua kuchukua hatua za kufuta viwanja hivyo kwa ajili ya mipango mingine ya halmashauri ya manispaa ya Iringa.

“Nimeisikia kero hilo nimefanya jambo ambalo litawaumiza watu wachache ambao walikuwa wananufaika ndio maana najua itawauma sana lakini hakuna namna lazima kufanya kazi kwa maslai mapana ya taifa sio maslai ya mtu binafsi” alisema Lukuvi

Waziri Lukuvi alimalizia kwa kuwaomba wananchi wa kata ya Kitwiru kupigia kura Baraka Kimata kwa maslai ya maendeleo ya kata hiyo,kwa kuwa anatosha na yupo katika chama ambacho kinampangilio mzuri wa kuafanya maendeleo kwa wananchi wa kata hiyo.

Naombeni mpeni kura za kutosha Baraka kimata anafaa kuwa diwani wa kata hii najua nyie wenyewe mmejionea hali ilivyo kwa wapinzania sasa hawana jipya wanaondoka kila siku uchwao.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More