Monday, November 6, 2017

HAMPHREY POLEPOLE AKOMBA DIWANI MWINGINE WA CHADEMA MANISPAA YA IRINGA

  Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole akiwa amemshika mkono diwani wa kata ya Kihesa Edgar Mgimwa aliyehamia CCM akitokea chadema
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole akiwatambulisha madiwani wa viti maalum waliohamia CCM wakitokea CHADEMA ambao ni Leah Mleleu na Husna Ngasi

Na Fredy Mgunda,Iringa. 

CHAMA cha Mapinduzi (CCM) Manispaa ya Iringa kimeendelea kuvuna wachama wapya kutoka chama Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika uchaguzi mdogo wa udiwani, kata ya Kitwiru Iringa Mjini ambapo diwani wa kata ya Kihesa Edgar Mgimwa alijiudhuru udiwani wakati na kuhamia CCM.

Hayo yametokea jana katika ufunguzi wa kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani, kata ya Kitwiru ambapo katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa wa chama hicho, Livingstone Lusinde walishuhudia jinsi Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Iringa mjini kinavyozidi kumeguka.


Chadema imepata pigo hilo ikiwa ni miezi kadhaa imepita toka madiwani wengine watatu wakihame chama hicho ambao ni diwani wa kata ya Kitwiru, Baraka Kimata na Leah Mleleu na Husna Ngasi ambao ni madiwani wa viti maalumu.

Akitetea uamuzi wa CCM kumsimamisha tena Kimata kuwania udiwani katika kata hiyo aliyoiongoza kwa miaka miwili akiwa Chadema, Lusinde alisema kwa kuwa Chadema walisema mtu kwanza chama baadae ndio maana tumemrudisha Kimata ili tuone unafiki wao.

Akiwapokea madiwani na wanachama hao, Polepole alisema mwaka 2015 CCM walifanya kosa la kizembe lililosababisha jimbo la Iringa Mjini liende tena kwa Mchungaji Peter Msigwa na wapoteze halmashauri ya manispaa ya Iringa kwa wapinzani wao hao.

“Tukiri tulifanya makosa ya kizembe akapata ubunge, lakini leo nimekuja Iringa kumpa ujumbe mzito Mchungaji Msigwa kwamba ajiandae kurudi kanisani akachunge kondoo wa bwana,” alisema.

Pole pole aliwapongeza wana Chadema wanaojitoa na kujiunga na CCM akisema wanaridhishwa na utekelezaji mzuri wa Ilani ya CCM unaosimamiwa na Rais Dk John Magufuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Taifa.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni za chama cha mapinduzi mbele ya mgeni rasmi Hafrey Polepole, Mgimwa alisema ameamua kukihama chama hicho kutokana na kukiuka maadli ya uongozi na kuwaongozpea wananchi kila wakati.

“Tunawaaminisha wananchi uongo ambao sisi tulikuwa tunajua kuwa uongo hivyo nimeamua kuachana na siasa za maji taka na kuzifuta siasa safi ndani ya chama cha mapinduzi ambako naamini kuna siasa safi” alisema Mgimwa

Mgimwa alisema kuwa CHADEMA manispaa ya Iringa kimepoteza muelekeo kutokana mambo yanayoendelea nadani ya chama ambako kuna migogoro mingi ambayo haina msingi wowote katika kuleta maendeleo ya jimbo la Iringa mjini

“Ndani ya chama kuna migogoro mingi sana ambayo inasababishwa na mbunge na meya wetu kwa kutaka kutuongoza kwa udikteta wanaofanya kwa maslai yao binafsi hivyo mimi nimeamua kuondoka kuwapisha na udikteta wao” alisema 

Aidha Mgimwa alisema kuwa kuna madiwani wengi tu ambao watakihama chama hicho hivi karibuni kutoka na chama hicho kupoteza imani kwa wananchi wa manispaa ya Iringa kwa maslai ya watu wachache ambao ndio wameamua kufanya maamuzi ya kila kitu.

Mgimwa alimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli kwa kazi anayoifanya ya kuleta heshima kwa taifa na kuwafanya wananchi kuacha kuishi kwa mazoezi kama ilivyokuwa miaka ya nyuma.

“Saizi maisha yamekuwa magumu kwa kuwa wananchi wengi walikuwa wanaishi kimazoea na kwa ujanja ujanja hivyo mfumo wa sasa unatutaka wananchi kufanya kazi ili kujipatia kipato” alisema Mgimwa

Polepole na Lusinde waliwataka wapiga kura wa kata hiyo kumchagua Kimata kuwa diwani wa kata hiyo wakisema pamoja na uchache wao katika manispaa ya Iringa, wanaangaliwa kwa jicho kubwa na Rais Dk Magufuli na chama kwa ujumla.

 “CCM tunatambua sehemu ya kata hii kuna tatizo la upatikanaji wa maji, lakini pia kuna tatizo la daraja la Kitwiru. Hiyo ni kazi yetu, ipo ndani ya Ilani yetu hivyo tutaziagiza mamlaka zinazohusika ili zishughulikie,” Polepole alisema.

Naye Kimata alisema kuna kila dalili Mchungaji Msigwa akabaki  pekee yake katika Uchaguzi Mkuu wa 2020 kwa kuwa hataki kuambiwa ukweli.

“Nilipokuwa Chadema nilikuwa na mvutano mkubwa na wa muda mrefu wa kiutendaji na mbunge wa jimbo la Iringa Mjini kwasababu ni mtu asiyeambilika, hataki ukweli na anayeamini anajua kila kitu, nilikuwa pia Katibu Mwenezi wa Chadema Jimbo na hii iliniweka katika mazingira magumu sana. Nimevumilia kulinda heshima ya mbunge na chama lakini ikafikaa mwisho nikasema kuvumilia,” alisema kimata.

Katika hali ya isiyokuwa ya kawaida mgombea ubunge jimbo la Iringa mjini katika uchaguzi wa mwaka 2015 Iringa mjini kupitia CCM Frederik Mwakalebela atikisa kampeni za CCM Iringa mjini.

Mbele  ya katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa wa chama hicho, Livingstone Lusinde, Mwakalebela  alionyesha  kuendelea  kukubalika  zaidi Iringa mjini baada ya wananchi  kupaza  sauti  kumtaka apande  jukwaani wasikie sauti  yake.

Mwakalebela  akiwa  jukwaaani aliwaomba  wananchi wa  Kitwiru  kutopoteza  muda kumchagua mpinzani  katika kata  hiyo na kuwataka  kura  zote  kumpa Baraka  Kimata wa CCM.


“Nawaombeni sana kama  mlivyoonyesha kunikubali  naomba kura  zenu  zote  mpeni Kimata  ili  kwa  kushirikiana na Rais Dkt John Magufuli aweze  kuleta maendeleo” alisema Mwakalebela
Katika uzinduzi wa kampeni hizo, Diwani wa Kata ya Kihesa Iringa Mjini, Edgar Mgimwa (Chadema) na wanachama wengine sita wa Chadema walikihama chama hicho na kujiunga na CCM.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More