Monday, November 27, 2017

TAASISI YA LEVEDE YATOA MAFUNZO YA KUIMARISHA VIKUNDI VYA VIKOBA JIMBO LA MAFINGA MJINI


Taasisi  ya LEVEDE iliyoandaa  mafunzo  ya  wanachama  wa vikoba  katika  Halmashauri  ya  Mji  wa Mafinga  ambayo  yaliudhuriwa  na  washiriki  270  kati  ya  376 ambao  walikusudiwa, Mafunzo  haya  yalilenga  kuimarisha  vikundi  na  kukabiliana  na  changamoto  mbalimbali.

 Mafunzo  haya yameendeshwa  na  Evance Chipindi  ambaye  ni  miongoni  mwa  wadau  wakubwa  wa  vikoba Tanzania. 

 Katika  mafunzo  haya  wanavikundi  wamejifunza  maswala  ya  Uongozi, Utunzaji  wa kumbukumbu,  sharia  za vikundi,  Utatuzi  wa  migogoro  na  Utunzaji  wa  fedha. Wanavikundi waliohudhuria  wamefuraishwa  na  mafunzo  hasa  kutokana  na  kupata  ufumbuzi  wa  changamoto ambazo  zimekuwa  zikiwakabili.  

Katika  mafunzo  haya  viongozi  bora  walipewa  zawadi, wanachama  bora , mwezeshaji  bora  na  kikundi  chenye  hamasa . Katibu  wa  mbunge  wa  jimbo  la Mafinga  Mjini  naye  alitoa  salamu  kutoka  kwa  Mhe Mbunge  Cosato  chumi  ambaye  aliombwa kuwa  mgeni  rasmi  lakini  alishindwa  kutokana  na  majukumu  mengineyo  ya  kikazi.  Kauli  mbiu  ya  mwaka  huu  Mafinga
VICOBA  UKIIPENDA  ITAKUTOA 

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More