Friday, November 10, 2017

BARAKA KIMATA NITASHINDA UCHAGUZI WA KATA YA KITWIRU TAREHE 26 MWEZI HUU

MGOMBEA wa udiwani kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Baraka Kimata akiwa jukwaani wakati wa ufunguzi wa kampeni za uchaguzi kata ya Kitwiru

Na Fredy Mgunda

MGOMBEA wa udiwani kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Baraka Kimata amesema kuwa atashinda katika uchaguzi mwa tarehe 26 mwezi huu kutokana na kuendelea kupendwa na wananchi wa kata hiyo kwa kazi aliyofanya akiwa diwani wa chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA)
 
Akizungumza wakati wa kuomba kura kwa wananchi wa kata ya Kitwiru Kimata alisema nimefanya kazi nyingi za kimaendeleo katika kata hii wakati nikiwa diwani wa upande wa pili lakini nimehamia huku CCM naombeni mnipe kura zote kwa faida ya manedeleo ya kata ya Kitwiru.

“Mimi nilishakuwepo pale halmashauri najua vitu vingi ambavyo nilikuwa nanyimwa ila hivi sasa nikirudi nitahakikisha navipata kutokana na umoja wa madiwani wa chama cha mapinduzi najua tufanikiwa kuleta maendeleo katika maeneo ambayo tunayaongoza” alisema Kimata

Kimata alisema kuwa Kitwiru hakuna wapinzani bali kuna watu wanapiga makelele tu kwa wananchi wakati wa mikutano yao hivyo nauhakiki wa kushinda kwa kuwa nipo katika chama ambacho kinamfumo bora wa kuomba kura kwa wananchi.

“Jamani naombeni mnipekura zote maana upande wa pili hawana jipya,mimi mnanifahamu na kazi zangu mnazijua hivyo naombe siku ya tarehe 26 mwezi huu tufanye maajabu kwa kupata kura nyingi na za kishindo ili wapinzani waone aibu” alisema Kimata

Kimata alisema kuwa endapo atachaguliwa atafungua milango ya biashara katika soko la Kitwiru licha ya hujuma zilizofanywa dhidi ya soko hilo na kuwasaidia wafanyabiashara kuuza bidhaa zao kwa manufaa ya wanakitwiru.

Katika kampeni za uchaguzi kata ya Kitwiru Manispaa ya Iringa zimeendelea huku mgombea wake Baraka Kimata akiwaomba wananchi wa eneo hilo kumchagua ili kuendeleza mipango ya maendeleo.

Kampeni za uchaguzi kata ya Kitwiru zinaendelea kwa vyama sita ambavyo vimethibitishwa kuwepo katika uchaguzi utakaofanyika tarehe 26 mwezi huu.

Katika mkutano ulifanyika mtaa wa uyole, Diwani wa kata ya Mshindo, Ibrahim Ngwanda amewataka wapiga kura wa kata hiyo kuupuza madai ya wapinzani wao kwa mgombea wao ambaye awali alikuwa diwani wa kata hiyo kupitia Chadema, kwamba alinunuliwa kabla ya kuhamia CCM.

“Hatujanunua diwani yoyote wa Chadema na wala hatuna mpango wa kufanya hivyo. Iliyoko mdarakani ni serikali ya CCM, Ilani inayotekelezwa ni ya CCM na hata hao wapinzani wanatekeleza Ilani hiyo hiyo, kwanini tununue wapinzani wanaotekeleza pia Ilani yetu?” aliuliza.

Ngwanda alisema kama biashara ya kununua wapinzani ingekuwa inabadili mfumo wa chama hicho na serikali yake katika kutekeleza majukumu yake, basi mtu wa kwanza kununuliwa mjini Iringa angekuwa Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More