Monday, November 30, 2015

Rais Magufuli kaamua Bilioni zilizokua zitumike sherehe za uhuru 9 Dec matumizi yake yawe kama ifuatavyo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameamuru fedha zilizopaswa kutumika kugharamia shamra shamra za siku ya Uhuru ambazo zingefanyika tarehe 09 Desemba 2015, kutumika kufanya upanuzi wa barabara ya Mwenge hadi Morocco jijini Dar es Salaam yenye urefu wa kilometa 4.3 kwa kuongeza njia mbili za barabara za lami. Tayari fedha hizo kiasi cha shilingi bilioni nne zimepelekwa kwa wakala wa barabara hapa nchini TANROADS kwa ajili ya utekelezaji wa agizo hilo, linalopaswa kuanza mara moja Akizungumza na Mtendaji Mkuu wa TANROADS Mhandisi PATRICK MFUGALE Ikulu Jijini Dar es Salaam, Dkt. Magufuli ametaka ujenzi wa barabara hiyo uanze haraka ili kukabiliana na adha ya msongamano wa magari katika barabara...

MBUNGE COSATO CHUMI KUTATUA TATIZO LA MAJI KATIKA MJI WA MAFINGA LILOTUDUMI KWA MUDA MREFU.

 mbunge wa mafinga mjini cosato chumi akikagua chanzo maji cha ikangafu wakati wa ziara yake ya kutembelea vyanzo vya maji na matanki ya kuhifadhia maji  mbunge wa mafinga mjini cosato chumi akikagua moja ya tanki la kuhifadhia maji  mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa mafinga shaibu nnunduma kulia akiwa mbunge cosato chumi wakijali jambo kwenye moja ya matank waliyokuwa wanayakagua. kushoto ni bw uhaula ,bw shaibu nnunduma mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa mafinga wakijadili jambo baada ya kukagua baadi ya vyanzo hivyo vya maji. mbunge wa jimbo la mafinga mjini cosato chumi amefanya ziara ya kuangalia jinsi gani anaweza kutatua tatizo la maji katika jimbo hilo. leo mapema mbunge huyo aliongozana na wataalamu wa...

CCM yakanusha Zilizosambaa Kwamba Imekubali Kumkabidhi Maalim Seif Ikulu

Chama cha Mapinduzi CCM kimekanusha Taarifa iliyozagaa katika Mitandao ya Kijamii kwamba Chama hicho kimeridhia aliyekuwa Mgombea wa Urais wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad akabidhie nchi kuiongoza kwa miaka mitano.  Akikanusha Taarifa hiyo mbele ya Waandishi wa Habari Afisini kwake Kisiwandui Naibu Katibu Mkuu wa CCM Vuai Ali Vuai amesema taarifa hiyo ni uzushi uliotungwa ili kuwatia taharuki WanaCCM na Wananchi kwa Ujumla.  Amesema toka kusambaa kwa Taarifa hiyo Jana amekuwa akipigiwa simu na Watu mbalimbali wa ndani na nje ya nchi kujua ukweli wa Taarifa hiyo hasa ikizingatiwa kuwa ilidaiwa kusainiwa na Naibu huyo. “Huu ni Uzushi Mkubwa na kwamba unafaa kupuuzwa maana hauna lengo jingine zaidi ya kuwagawa WanaCCM” Alismema...

Njia 10 Zinazotumika Kukwepa Kodi Bandari ya Dar es Salaam

Wakati Serikali ikikunjua makucha yake dhidi ya wote waliohusika katika kashfa ya kupitisha makontena 349 kwenye Bandari ya Dar es Salaam bila ya kuyalipia kodi, imefahamika kuwa idadi hiyo ya makontena ni sehemu ndogo tu ya mamia ya mizigo yanayovushwa kinyemela kila uchao na kuikosesha serikali mabilioni ya fedha. Hata hivyo, wakati serikali ya Rais Magufuli na Waziri Mkuu wake, Kassim Majaliwa, ikiendelea kutafuta suluhu ya kudumu kuhusiana na ukwepaji kodi, imebainika kuwa kazi hiyo siyo lelemama kwani zipo njia zaidi ya tisa zinazotumiwa kukwepa kodi katika Bandari ya Dar es Salaam. Mosi, ni kupitia mwanya utokanao na mfumo wa zamani wa malipo usiohusisha ule wa sasa wa kielektroniki, maarufu kama ‘E-Payment’.     Kwamba,...

Sheikh Ponda Aachiwa Huru

Mahakama ya hakimu mkazi Morogoro imemuachia huru Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda aliyekuwa akituhumiwa kwa makosa ya uchochezi baada ya mahakama kutoridhishwa na ushahidi wa upande wa mashtaka na hivyo kuonekana hana hatia  Historia ya kesi ya Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda. Hati ya Mashitaka ya Kesi hiyo ilikuwa na jumla ya Mashitaka matatu  lakini Julai 22 mwaka 2015, Hakimu Mkazi Mary Moyo  alitoa  uamuzi wa kumfutia shitaka la kwanza kwasababu lilishatolewa uamuzi na Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, na hivyo mahakama hiyo ya Morogoro siku hiyo ilitoa uamuzi wa kumuona ana kesi ya kujibu  katika mashitaka mawili yaliyosalia ambalo...

COSATO CHUMI KESHO KUTIMIZA KAULI MBIU YA HAPA KAZI TU KATIKA JIMBO LA MAFINGA MJINI

 hivi ni baadhi ya vifaa atakavyokabidhi mbuge wa jimbo hilo cosato chumi katika jimbo la mafinga mjini siku ya kesho.  hili ni gari likishusha vifaa hivyo na baadhi ya watumishi wakisaidia kuvishusha   huyu ni mmoja ya wafanyakzi katika hospitali ya mafinga akiwa ameshusha kiti cha wagonjwa akipeleka sehemu inayotakiwa. Mbunge wa jimbo la mafinga mjini cosato chumi ameanza kutimiza ahadi zake alizo waahidi wakazi wa jimbo hilo na kutekeleza kauli mbiu ya rais wa jamhuri ya muungano ya Tanzania dr john pombe magufuli ya hapa kazi tu. Akizungumza na blog hii mbunge huyo amesema kesho anatarajia kutoa vifaa ya hospitali ili viweze kuwasaidia wakazi wa jimbo na kuboresha afya za wananchi wake kwa kuwa usipokuwa...

Chadema Yateua Meya Manispaa ya Kinondoni

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Mkoa wa Konondoni, kimempitisha Diwani mteule wa Ubungo, Boniface Jacob (Chadema), kuwa mgombea umeya wa Manispaa ya Kinondoni, huku akiwakilisha mwamvuli wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa). Mgombea huyo alikuwa akiwania nafasi hiyo huku akipambana na diwani mwenzake mteule wa Kata ya Mbweni, Abdunel Elibariki (Chadema) ambaye alishindwa kutamba. Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo jana jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa uchaguzi huo Venus Kimei ,  alisema Jacob alishinda kwa kura 20 kati ya kura 28 zilizopigwa. “Wagombea walikuwa wanne lakini watatu ndio ambao walikidhi vigezo, hata hivyo waliopigiwa kura ni wawili kutokana na mgombea mmoja Ndeshukurwa Tungaraza...

Lowassa, Mbowe Watua Alipouawa Alphonce Mawazo

Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe  na aliyekuwa mgombea urais wa chama hicho Mhe. Edward Lowassa pamoja na viongozi mbalimbali wakitazama eneo ambalo Alphonce Mawazo alifanyiwa kitendo ya kinyama cha kukatwakatwa mapanga na watu wanaosemekana ni wafuasi wa CCM ikiwa ni umbali mchache kutoka kutuo cha polisi na ofisi za CCM katika barabara kuu inayoelekea Geita kutokea Busanda. Umati mkubwa wa wakazi wa Jimbo la Busanda waliojitokeza kutoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa mgombea ubunge na M/kiti wa Mkoa wa Geita, Alphonce Mawazo. Mwili wa Marehemu Alphonce mawazo ukipokelewa na wakazi wa jimbo la Busanda ambako alikuwa akiwania Ubunge katika jimbo hilo ...

Waziri Mkuu: Tumedhamiria Kuwatumikia Watanzania...Tutahakikisha Mapato Ya Taifa Yanatumika Kwa Maslahi ya Watanzania Wote

WAZIRI MKUU Majaliwa Kassim Majaliwa amesema Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kuhakikisha kila kinachokusanywa kama mapato ya nchi kinatumika kwa maslahi ya Watanzania wote na si kwa manufaa ya wachache. Alitoa kauli hiyo jana mchana (Jumapili, Novemba 29, 2015) wakati akifunga maadhimisho ya miaka 20 ya Dayosisi ya Pwani ya Kanisa la African Inland Church Tanzania (AICT) kwenye ukumbi wa PTA, viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam. “Serikali imeanza kukabiliana na upotevu wa mapato ya Serikali na kuepuka matumizi yasiyo ya lazima ya fedha za umma. Nia yetu ni kuhakikisha kila kinachopaswa kukusanywa kama mapato ya nchi, kikusanywe na kitumike kwa masuala ya msingi kwa ustawi wa Watanzania wote na si kwa watu wachache,”...

Magazeti ya Leo Jumatatu ya Leo Tarehe 30 Novemba

...

Sunday, November 29, 2015

HAPA KAZI TU” YAWAWEKA SAWA WAFANYAKAZI WA DAWASCO.

 Ofisa Mtendaji wa Mkuu wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka (Dawasco), Mhandisi Cyprian Luhemeja, akizungumza katika mkutano na wafanyakazi uliofanyika hivi karibuni Makao Makuu ya Dawasco jijini Dar es Salaam kuhusu utendaji kazi wa kazi.  Wafanyakazi wa Dawasco wakimsikiliza Ofisa Mtendaji  Mkuu wao. Na Mwandishi, Maalumu Ule usemi maaarufu wa Hapa kazi tu”  unaendelea kuimbwa na kufanyiwa kazi na watanzazia wengi hususani watumishi wa Umma na serikali ili kuendana na kasi ya awamu ya Tano ya Raisi Magufuli. Kauli mbiu hiyo imekumbushwa tena na Afisa Mtendaji Mkuu wa Dawasco Eng Cyprian Luhemeja wakati wa kikao cha pamoja na  wafanyakazi wa shirika hilo mapema wiki hii. “lazima tuendane na...

Katibu Wa Wizara ambaye ni Goigoi Ajiondoe Mapema

Joto la utawala wa Rais John Magufuli limebadili utendaji kazi wa makatibu wakuu wa wizara mbalimbali waliozoea kukaa ofisini na sasa wanafanya kazi nje ya ofisi na kusikiliza kero za wananchi kwenye maeneo yao. Wakati hilo likifanyika, Ikulu jijini Dar es Salaam imesema katibu mkuu au mtumishi yeyote wa umma atakayeshindwa kwenda na kasi na mabadiliko ya utendaji kazi katika serikali ya awamu ya tano ajiondoe. Tamko hilo linalotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, alipohojiwa jana  kuhusu kutokuwapo kwa makatibu wakuu wa wizara kadhaa kwenye ofisini zao wiki iliyopita.    Makatibu wakuu wa Wizara kadhaa wamelazimika kuzifunga ofisi zao na kuelekea mikoani kusikiliza kero za wananchi. Hali ...

Page 1 of 69412345Next
Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More