Monday, December 18, 2017

VODACOM TANZANIA FOUNDATION, DORIS MOLLEL FOUNDATION WATOA MSAADA WA VIFAA TIBA VYENYE THAMANI YA SH ,MILIONI 24 KWENYE HOSPITALI YA WILAYA YA CHATO, GEITA

Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Afya), Dkt. Mpoki Ulisubisya akipokea moja ya mashine za kusaidia kupumua watoto wanaozaliwa kabla ya wakati (Njiti) kutoka kwa Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Rosalynn Mworia (kushoto) kwa ajili ya Hospitali ya Wilaya ya Chato, Mkoani Geita. Msaada huo umetolewa kwa ushirikiano kati ya Taasisi ya Vodacom Tanzania pamoja na Taasisi ya Doris Mollel. Wanaoshuhudia ni Muasisi wa Taasisi ya Doris Mollel na Balozi wa Watoto Njini nchini, Doris Mollel (wa pili kushoto) na Kushoto ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Chato, Dkt. Ligobert Kalasa.

 Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Afya), Dkt. Mpoki Ulisubisya akizungumza katika hafla ya kukabidhiwa msaada wa vifaa tiba kwa ajili ya kusadia watoto wanaozaliwa kabla ya wakati kwa Hospitali ya Wilaya ya Chato Mkoani Geita, uliotolewa kwa ushirikiano kati ya Taasisi ya Vodacom Tanzania (Vodacom Tanzania Foundation) pamoja na Taasisi ya Doris Mollel (Doris Mollel Foundation). hafla hiyo imefanyika leo katika Hospitali ya Chato, Mkoani Geita.

Baadhi ya vifaa tiba ambavyo vimetolewa kwenye hospitali ya Wilaya ya Chato Mkoani Geita ambavyo vitaweza kuwasaidia watoto ambao wanakuwa bado hawajafikia muda wa kuzaliwa.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Afya), Dkt. Mpoki Ulisubisya akimkabidhi vifaa na  mashine za kusaidia kupumua watoto wanaozaliwa kabla ya wakati (Njiti) katibu tawala wa Wilaya ya Chato kwa ajili ya Hospitali ya Wilaya ya hiyo, Mkoani Geita. Msaada huo umetolewa kwa ushirikiano kati ya Taasisi ya Vodacom Tanzania pamoja na Taasisi ya Doris Mollel. 

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Chato,Dkt. Ligobert Kalasa akitoa maelezo ya namna ambavyo mashine hizo zinatumika.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Afya), Dkt. Mpoki Ulisubisya akiteta jambo na Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Rosalynn Mworia pamoja na Muasisi wa Taasisi ya Doris Mollel na Balozi wa Watoto Njini nchini, Doris Mollel.

 Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Afya), Dkt. Mpoki Ulisubisya akiteta jambo na Mganga mfawidhi wa hospital ya wilaya ya Chato Ligobert Kalasa wakati alipokuwa akielekea kwenye wodi za watoto ambao wamezaliwa kabla ya wakati.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Afya), Dkt. Mpoki Ulisubisya akitoa maelezo juu ya kitanda cha wagonjwa ambacho kilikuwa nje ya hospital.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Afya), Dkt. Mpoki Ulisubisya akimkabidhi zawadi ya Khanga Bi.Lucia  Jamesi pamoja na Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Rosalynn Mworia  aliyekuwa katika Wadi ya Wazazi ya Hospitalini hapo.

Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Rosalynn Mworia akimsalimia mmoja wa watoto waliozaliwa katika Hospitali ya Chato, Mkoani Geita leo.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Afya), Dkt. Mpoki Ulisubisya akiwa pamoja na Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Rosalynn Mworia (katikati) pamoja na Muasisi wa Taasisi ya Doris Mollel na Balozi wa Watoto Njini nchini, Doris Mollel wakipanda mti katika eneo la Hospitali ya Chato ikiwa ni ishara ya mtoto anayezaliwa na kutunzwa katika mazingira bora.

Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Rosalynn Mworia (katikati) pamoja na Muasisi wa Taasisi ya Doris Mollel na Balozi wa Watoto Njini nchini, Doris Mollel  wakiwamwagia maji mti ambao wameupanda.

Picha Zote na Joel Maduka(WA MADUKA ONLINE BLOG)

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More