Monday, December 18, 2017

Takukuru yamwachia Mukoba

Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini imemuachia aliyekuwa Rais wa Chama cha walimu (CWT)  Gratius Mukoba bila kumfikisha mahakamani.

Kamanda wa Takukuru mkoa wa Dodoma Emma Kuhanga  amesema Mukoba hakupelekwa mahakamani kama ilivyotakiwa.

"Hapana hatujampeleka mahakamani, tulishamuachia,....ni hivyo kwamba mahakamani hakupelekwa," amesema Kuhanga

Mwishoni mwa wiki Takukuru ikimkamata Mukoba kwa madai ya kujihusisha na ugawaji wa rushwa kwa wajumbe na alitarajia kufikishwa mahakamani leo.

Alipoulizwa iwapo Rais huyo wa zamani wa CWT ataitwa tena ama taasisi yake imeona hana hatia, Kamanda Kuhangwa amesema "wewe elewa kuwa hatujampeleka mahakamani lakini tumemwachia,"

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More