Monday, December 18, 2017

Magufuli: Wapinzani Mtaisoma Namba

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri wa Muungano Dkt. John Pombe Magufuli amefunguka na kutangaza kuuvuruga upinzani Tanzania kwa kupokea Mbunge mmoja kutoka chama cha upinzani na madiwani wengine saba.

Magufuli amesema hayo leo kwenye Mkutano Mkuu wa 9 wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambao umefanyika leo Disemba 18, 2017 mjini Dodoma na kuhudhuriwa na wajumbe mbalimbali wakiwepo marais wastaafu.

"Nimepokea majina mengine ya viongozi wa upinzani ambao wanataka kurudi Chama Cha Mapinduzi (CCM) wasaidizi wangu wameniambia yupo Mbunge mmoja anataka kurudi na ameniambia kuwa anataka kuja na madiwani saba kwenye jimbo lake, nasema hiki ni kimbunga na wataisoma namba kweli kweli" alisisitiza Rais Magufuli

Aidha Magufuli amewataka viongozi wapya wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuhakikisha wanafanya kazi ya kuongeza wanachama wapya katika chama hicho na kuongeza wafuasi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Mbali na hilo Rais Magufuli amesema kuwa wataendelea kupokea na kuwatangaza watu ambao wanahamia kwenye chama hicho, na kusema kuwa lazima kwanza wajiridhishe ili wasije kupokea na watu wengine ambao hawana mpango mzuri kwa CCM.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More