Saturday, December 16, 2017

NGORONGORO WAZINDUA KAMPENI YA KUPINGA UKEKETAJI

Wanaharakati wa kupinga ukeketaji wakisikiliza kwa makini mafunzo kabla ya kuanza kampeni ya mwezi mmoja ya kupinga ukeketaji wilayani Ngorongoro. Mafunzo hayo yaliratibiwa na Shrika la UNESCO. Kampeni hiyo inafanywa kwa ushirikiano wa UNESCO, Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro na Baraza la Wazee wa Mila wa Kimaasai (Laigwanan). Kampeni hiyo imeanza Tarehe 5/12/2017 na itaendelea kwa mwezi mzima. Afisa wa UNESCO anayewakilisha miradi ya Ololoswakan Wilayani Ngorongoro Bwana Hamidun Kweka akiwafundisha wanafunzi wa Shule ya Msingi Oloirien wilayani Ngorongoro madhara ya ukeketaji katika uzinduzi wa kampeni ya kupinga ukeketaji wilayani humo. Kampeni hizo zilizinduliwa rasmi Tarehe 5 na zitadumu kwa mwezi mmoja. Ngariba mstaafu akiimba na watoto nyimbo za kupinga ukeketaji baada ya mafunzo ya kuwaelimisha madhara ya ukeketaji katika shule ya msingi Oloirine wilayani Ngorongoro mnamo Tarehe 7, 2017. Wafanyakazi wa UNESCO na Walimu wa Shule ya Msingi Oloirien wakiwa pamoja baada ya uzinduzi wa Kampeni ya Kupinga Ukeketaji wilayani Ngorongoro.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More