Sunday, October 18, 2015

Wafuasi wa CCM na CHADEMA Wachomana Visu Tunduma.......Watu wawili Wapoteza Maisha


Watu wawili wamefariki  dunia  baada  ya  vurugu  kubwa  kutokea kati  ya wafuasi  wa  CCM  na  CHADEMA  katika  mji  mdogo  wa  Tunduma  Mkoani  Mbeya.

Vurugu  hizo  zimetokea  baada  ya  wanachama wa CCM kuweka mawe barabarani ili wafuasi wa CHADEMA wasipite  kuhudhuria  mkutano  wa  Lowassa. 
Hali  hiyo  iliwafanya  wafuasi  wa   CHADEMA kushuka  ili kutoa mawe hayo, ndipo akatokea kijana  mmoja wa CCM na kumchoma kisu kijana mmoja wa CHADEMA  ambaye  alifariki  dunia  papo hapo.

Baada  ya  tukio  hilo, vijana wa CHADEMA nao walijibu mapigo kwa  kumshambulia  na  kumuua kijana huyo.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More