Friday, October 23, 2015

VIJANA WATAKIWA KUWAKWEPA WANASIASA WANAOTAKA KUWATUMIA KAMA MADARAJA



KATIBU wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mufindi Gimson Mhagama amewataka  vijana kuwaepuka na kuwakwepa wanasiasa uchwara wanaotaka kuwatumia kama madaraja ya kupitia ili kutimiza malengo yao kwa  kwa kuwahamasisha kufanya   vurugu  kwenye vituo vya kupiga kura siku ya uchaguzi  kwani watu hao hawana nia njema na taifa hili bali wanatakakuvuruga amani ya nchii hii

Alisema kuwa amani ambayo tunajivunia ipo siku itatoweka na iwapo vyama vya siasa vitaacha kufanya kazi yake ya kisiasa kwa kunadi sera za vyama vyao na kueneza chuki dhidi ya serikali kama ilivyo hivi sasa kwa baadhi ya vyama kuendesha siasa za chuki na kuwatumia vijana kuvuruga amani yetu.

Akizungumza katika kampeni  za kuwanadi mgombea udiwani na mbunge katika kata ya mbagala wilayani Mufindi mkoani Iringa Mhagama ilisema kuwa kumekuwa na wasasiasa wasio na nia njema na vijana na kuamua kuwalisha viroba na bangi na kuwamuru kwenda kufanya fujo katika
mikutano ya ccm jambo ambalo ni kuvuruga amani ili yopo kwani wanamufindi walizoeya kufanya kampeni za kistarabu lakini sasa
inaonekana kama vita kutokana na watu wachache wanaotaka madaraka kwa
mabavu badala ya sera za chama chake

“Ndugu zangu  na vijana wenzangu sisi bado umri wetu unadai tusikubali kushawishiwa na watu wachache eti kwa kuwa alikupa elifu kumi na viroba uende kufanya fujo kwenye kampeni za ccm au kwenda kufanya vurugvu kwenye vituo vya kupigia kura nawambia  anawapotosha na matokeo yake utakubwa na matatizo na kuanza kulaumu serekali ,hawa
watu wasitufanye hatuna akili wewe piga kura rudui zako nyumbani kwa ustarabu hakuna atayekugusa  kama kulinda mwambie alinde yeye “

Alisema katika jimbo lake la mafinga mjini kuna vijana wengi wameingia kwa makundi makundi  kwa awamu tofauti kutoka katika mikoa ya Arusha ,Mbeya na Morogoro  na lengo la vijana hao wanaosemekana kudhaminiwa na mgombea ubunge wa jimbo la Mafinga mjini Wille Mungai ni kwa ajili
ya kufanya vurugu siku ya uchaguzi na wengine wamekuwa wakisambazwa
katika mikutano ya ccm na kufanya vurugu za kupiga watu na kufunga barabara  ili wanaccm wasipite kwenda kufanya kampeni

Aliwaeleza kuwa nchi hii inaongozwa kwa misingi ya sheria za nchi hivyo kila mmoja anapaswa kuziheshimu na kuzifuata kwa kuwa wako watu wanaojifanya wako juu ya sheria na kuwataka watu wote kujitokeza kwenda kupiga kura kwa kuwa jeshi la polisi liko kwa ajili ya kulinda raia na mali zaa hivyo kila mmoja anapaswa kwenda kutimiza haki yake ya msingi ya kupiga kura

“Kuna watu humu jimboni mwetu wamezoeya jela na wengine walikuwa wanakesi lakini walitoka kiujanja unjanja  na ndio  anaotusumbua kwa kupiga wanachama wetu sasa tusubiri tu Mh John Magufuli aingie
madarakani baada ya ninyi wanachi kumpa ridha kuna watu wataona hii nchi chungu kwa maaovu waliofanya ndio mana wanamuogopa na mimi ninaamni huu ndio mwaka wa mabadiliko na tutashinda kwa kishindio ndio
na wale waliotoka kiujanja ujanta wataisoma nambaa

Kwa upande wake Gift Mwachanga aliyekuwa kada maarufu wa chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) na hatimaye kujiunga na chama cha mapinduzi ccm  alisema sio jambo la busara wanasiasa  kutumia majukwaa
yao ya siasa vibaya kwa kuwatuma watu kufanya vurugu katika mikutano ya kampeni na wengine kuwahadaa kuwa wakalinde kura katika vituo   ila hali wao na  watoto wao watakuwa majumbani kwao mamepumzika huku wakila bata

Mwachanga alisema jambo kubwa liliomfanya kuondoka ndani ya chama hicho ni kukiukwa kwa misingi ya demokraisa ndani ya chama hicho kwani watu wachache ndio wenye sauti ndani ya chama huku wengine wakiwa  ni
bendera fuata upepo hivyo akamua kujiengua ili kusiadia kuleta maendeleo katika jimbo hilo kupitia ccm  tofauti naapo  awalia ambapo
alikuwa akipinga kila kitu hata kama ni kizuri ili mradi tu kimesemwa na mtu kutoka chama cha mapinduzi( CCM)

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More