Saturday, October 31, 2015

ASKARI WA KIKOSI CHA UPELELEZI AJIUA KWA KUJIPIGA RISASI SHINGONI

  Askari wa kikosi maalumu cha kupambana na ujambazi mkoa wa Iringa Pascal Shila (30) pichani amejiua kwa kujipiga risasi kichwani kutokana na msongo wa mawazo. Askari mwenye namba G.343D/C Pashal James Shila wa Ofisi ya RCO-Kikosi cha Anti Robbery amejiua kwa kujipiga risasi na mwili wake kukutwa kwenye jengo bovu la ghorofa la mjerumani lilipo nyuma ya kituo cha polisi. Akizungumza na mwangaza wa habari blog wakati wa kuaga mwili wa marehemu kwenye kituo kikuu cha polisi Manispaa ya Iringa, Kamanda wa polisi mkoa wa Iringa Ramadhani Mungi alisema tukio hilo lilitokea jana kati ya saa tisa na kumi jioni. Kamanda Mungi alisema askari huyo kutoka ofisi ya upelelezi mkoa wa Iringa (RCO) alichukua silaha...

Jesca: Siwezi kujiuzulu kwa shinikizo la majungu, fitina na vikundi vya uasi...

Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu akizungumza na waandishi wa habari jana.  Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu amesema hawezi kujiuzulu nafasi yake hiyo kwa shinikizo linalotokana na majungu, fitina na vikundi vya uasi vinavyoanzishwa ndani ya chama kwa lengo la kulinda maslai ya watu fulani. “Hizi ni hoja zisizo na mashiko, hivi inawezekaneje mimi na hao wengine wanaowataja katika kipindi chote cha kampeni tufanye kazi ya kukihujumu chama, tuvumiliwe tuendelee na kazi hiyo, halafu tuhuma hizo zije zitolewe sasa baada ya kushindwa uchaguzi?” alisema. Kwa kutumia vikao na taratibu zingine za katiba yake, CCM inapaswa kukaa chini na kufanya tathmini ya kina...

UKAWA Watoa Tamko Zito Lenye Masharti Manne

Viongozi wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), wamesema baada ya kufuatilia mwenendo wa Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar wana taarifa za uhakika kwamba Maalim Seif Sharif Hamad, Mgombea Urais wa Chama cha Wananchi (Cuf) anayeungwa mkono na Umoja huo, ameshinda urais wa Zanzibar. Taarifa iliyotolewa na viongozi hao jana kwa vyombo vya habari imetoa masharti  manne kufuatia kufutwa kwa uchaguzi wa Zanzibar. Sharti la kwanza ni kuzitaka mamlaka zinazosimamia Uchaguzi Mkuu huo kuondoa mara moja tangazo la kuufuta Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar.   Sharti la pili ni kumtangaza Seif kuwa ni mshindi halali wa nafasi ya urais na hivyo aapishwe kuwa Rais wa nchi ya Zanzibar ambayo ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano...

Hali ni Tete Zanzibar....Bomu Lategwa Kituo cha Polisi, JWTZ Waliwahi na Kulilipua

Jeshi la Polisi Zanzibar kwa kushirikiana na Jeshi la Wananchi (JWTZ), limefanikiwa kuteguwa bomu lilitegwa eneo la Mkunazini karibu na kituo cha polisi mjini Zanzibar.   Bomu hilo lilitegwa na watu wasiofahamika na jeshi la polisi lilipata taarifa ya kutegwa kwa bomu hilo kutoka kwa wasamaria wema. Akizungumza na mwandishi wetu, Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar, Hamdani Omar Makame, alisema baada ya kupata taarifa kutoka kwa wananchi kuwa eneo hilo kuna kitu kimetegeshwa, jeshi la polisi lilifanya uchunguzi na kubaini kuwa ni bomu na kufanikiwa kulitegua kwa kuliripua ili kuepusha maafa.   “Ni kweli kulikuwa na kishindo kikubwa baada ya jeshi la polisi kuliripua bomu hilo lakini hakuna madhara yoyote yaliotokea,”...

Friday, October 30, 2015

Lembeli Aeleza Hatma Yake Baada Ya Kushindwa, Ajibu Tetesi Juu Yake

Aliyekuwa mgombea ubunge wa jimbo la Kahama, James Lembeli ameelezea kinachoendelea katika maisha yake ya kisiasa hasa baada ya kushindwa katika uchaguzi wa mwaka huu akiwa ndani ya chama chake kipya cha Chadema. Akiongea katika taarifa rasmi kwa wananchi wa jimbo hilo, Lembeli amesema kuwa hivi sasa atajikita zaidi katika shughuli za chama chake pamoja na shughuli alizokuwa akizifanya kabla ya kuwa mbunge wa jimbo hilo. Alisema kuwa ataendelea kufanya kazi zake na mashirika ya kimataifa kama mjumbe wa Bodi mbalimbali. Pia, ataendelea kufanya kazi ya kusimamia radio yake (Kahama FM) ambayo amedai kuwa taarifa zilizosambazwa kuwa ameiuza kulipa deni la mkopo aliopewa kuendesha kampeni sio za kweli. Pia, Lembeli amewashukuru wananchi...

Dr. Magufuli Akabidhiwa Rasmi CHETI Cha Ushindi wa Kiti cha Urais

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Mstaafu Damian Lubuva amemkabidhi cheti cha ushindi wa kiti cha urais, Dk John Pombe Magufuli  na  mgombea  mwenza  wake  Samia  Suluhu  katika  Ukumbi wa Diamond Jubilee  asubuhi  hii. Katika  tukio  hilo, Wagombea urais wa Chadema Edward Lowassa na Hashim Rungwe wa Chauma wamesusia sherehe hizi  za kukabidhiwa cheti cha ushindi Dk John Magufuli wa C...

KAMPUNI YA NDEGE YA FASTJET KUISAFIRISHA TIMU YA TAIFA STARS KWENDA ALGERIA

 Ofisa Habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Baraka Kizuguto (kulia), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, kuhusu timu ya taifa Taifa Stars kwenda nchini, Algeria kwa mchezo utakaofanyika Novemba 17 mwaka huu. Katibu wa Kamati ya Timu ya Taifa Stars, Teddy Mapunda (katikati), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, kuhusu timu hiyo kwenda nchini Algeria kushiriki  mchezo wa marudiano utakaofanyika Novemba 17  mwaka huu. Kampuni ya Ndege ya Fastjet imedhamini safari hiyo kwa kutoa ndege yake kwa kwenda na kurudi. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Fastjet Afrika Mashariki, Jimmy Kibati na Kushoto ni Mkuu wa Masoko wa Fastjet, Jan Petrie.  Mkurugenzi...

UN TANZANIA STATEMENT ON TANZANIA GENERAL ELECTIONS

UN Resident Coordinator, Alvaro Rodriguez. Dar es Salaam, 29 October 2015: The United Nations is following very closely the Tanzanian general elections of 25 October and congratulates the president elect. We congratulate Tanzanians for exercising their democratic rights in a peaceful manner. We take note of the international observers statement (Commonwealth, AU, SADC and EU) of today that indicates they are pleased that the voting and counting took place in an environment of peace. However, the observer missions as well as the US Embassy and UK High Commission have also shared their great concern with the statement issued by the Chairman of the Zanzibar Electoral Commission in which he nullified the Zanzibar elections. We call on political...

Vyama 6 Yyamtaka Mwenyekiti ZEC Ajiuzulu......Maalim Seif atoa Wito kwa Rais Kikwete Na Dk Shein

Mgombea wa Urais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad amemuomba Rais Jakaya Kikwete na Rais Ali Mohamed Shein kubeba dhamana ya uongozi katika siku hizi chache zilizobaki za uongozi wao kwa kusimamia katiba na sheria za nchi. Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mtendeni Maalim Seif amesema marais hao wawili kuheshimu maamuzi ya Wazanzibari waliyoyafanya tarehe 25 Oktoba na kuwataka washirikiane nae katika kuinusuru Zanzibar. “Nawaomba sana Rais Kikwete na Rais Shein kukwepa matumizi ya nguvu na badala yake tushirikiane kutunza amani na haki za wananchi. Mimi niko tayari kushirikiana nao kama ambavyo nimekuwa nikifanya mara zote. Tushirikiane kuiepushia Zanzibar na Tanzania fedheha ya kimataifa”. Alisema Maalim...

Rais Kikwete Alivyomkaribisha Kumpongeza Dk. Magufuli Baada ya Matokeo ya Urais Kutangazwa

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza kwa furaha mshindi wa kinyang'anyiro cha Urais kwa tiketi ya CCM na Rais Mteule Dkt John Pombe Joseph Magufuli wakifurahia matokeo mara baada ya Mwenyekiti wa  Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Damian Lubuva  kutangaza kutangaza rasmi matokeo ya uchaguzi mkuu Ikulu jijini Dar es salaam ambako walifuatilia kwa pamoja matangazo hayo ya moja kwa moja kupitia vituo vya televisheni  jana  jioni Oktoba 29, 2015 Mama Salma Kikwete akimpongeza mshindi wa kinyang'anyiro cha Urais kwa tiketi ya CCM na Rais Mteule Dkt John Pombe Joseph Magufuli mara baada ya Mwenyekiti wa Tais kutangaza matokeo ya uchaguzi mkuu Ikulu jijini Dar es salaam ambako walifuatilia kwa pamoja matangazo...

Mambo Yaliyombeba Dr. Magufuli Kushinda Urais Wa Tanzania

Tanzania  imeandika historia mpya, ambapo jana imempata Rais Mteule wa Awamu ya Tano, Dk John Pombe Magufuli, ambaye alikuwa mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Uchaguzi Mkuu uliohitimishwa Jumapili ya Oktoba 25, mwaka huu. Dk Magufuli ambaye katika kampeni ya kuwania urais alikuwa na kauli mbiu ya Hapa Kazi Tu, si mgeni katika safu za uongozi wa Tanzania kwa kuwa amekuwa serikalini kwa miaka 20, akishika majukumu mbalimbali ambayo yalitumiwa na Watanzania kumpima. Moja ya sifa yake kubwa tangu alipotangaza nia ya kugombea urais kupitia chama hicho mwishoni mwa Mei mwaka huu, ni uadilifu katika utendaji kazi wake katika majukumu tofauti aliyokabidhiwa Rais huyo mteule wa Awamu ya Tano, anatajwa kuwa katika...

Thursday, October 29, 2015

Ubalozi wa Uingereza nchini Tanzania pamoja na Ireland Kaskazini Wapinga Uchaguzi Mkuu Kufutwa Zanzibar

Ubalozi wa Uingereza nchini Tanzania pamoja na Ireland Kaskazini umetoa taarifa ukipinga kufutiliwa mbali kwa matokeo ya Uchaguzi kisiwani Zanzibar.   Ubalozi huo umesema kuwa hauoni sababu za kufutiliwa mbali kwa matokeo hayo ilhali waangalizi walifurahishwa na vile uchaguzi huo ulivyofanyika kwa amani.   Wameitaka tume ya uchaguzi Kiswani Zanzibar kuorodhesha matokeo hayo bila kuchelewa. ---------------------------- PRESS STATEMENT Thursday 29 October, 2015 United Kingdom statement on Zanzibar elections The United Kingdom of Great Britain and Northern Ireland is deeply concerned by the announcement of the Chairman of the Zanzibar Electoral Commission to nullify the elections. We note that all the international...

Tamko la Edward Lowassa Baada ya NEC Kumtangaza Dr Magufuli Kuwa Mshindi wa Kiti cha Urais

Watanzania wenzangu! Leo tarehe 29 October 2015, kwa kupitia Mgombea Mwenza wangu, Mh. Juma Duni Haji nimewasilisha rasmi malalamiko yetu kuhusu mwenendo mzima wa uchaguzi mkuu wa 2015 kwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi. Tumeainisha kwenye malalamiko yetu, kutokuridhishwa kwetu na mwenendo na matukio mbalimbali, hususani, utangazaji wa matokeo batili, yasiyo akisi matokeo halisi yaliyopatikana kwenye vituo vya kupiga kura, kama ifuatavyo. • Upunguzwaji wa kura zangu • Kuongeza kura kwa mgombea wa CCM •Tunaendelea kukataa dhuluma hii dhidi ya matakwa ya wananchi, na jaribio la kutaka kubakwa kwa Demokrasia kunakooneka wazi kutokana na mwenendo wa Tume kuendelea kutangaza matokeo ya kura yasiyo ya kweli kwa kupoka...

Breaking News: Dr John Pombe Magufuli Atangazwa Rasmi Kuwa Mshindi Wa Kiti cha Urais wa Tanzania kwa Asilimia 58.46

Tume ya uchaguzi ya Tanzania Bara (NEC) kupitia Mwenyekiti wake Jaji Damian Lubuva   imemtangaza  Rasmi  mgombea  Urais  wa  CCM, Dr John Pombe  Magufuli  kuwa  mshindi  halali  wa  kiti  cha  Urais  katika uchaguzi mkuu uliofanyika siku ya jumapili wiki iliyopita.   Kwa  Mujibu  wa  jaji  Lubuva, Dr  magufuli  amepata  ushindi  wa  kura Milioni 8 ( 8,882,935  ) sawa  na  asilimia  58.46%  huku  akimwacha  kwa  mbali  mpinzani  wake  wa  karibu , Edward  Lowassa (Chadema )  ambaye  amepata  jumla  ya  kura ...

TULINDE AMANI TUNAPOENDELEA KUPOKEA MATOKEO YA UCHAGUZI MKUU

Ndugu watanzania wenzetu, tunapenda kuwapongeza kwa kumaliza mchakato wa kampeni za vyama vya siasa na wagombea  kwa amani na utulivu.  Vile vile tunawapongeza kwa kupiga kura kwa kwa amani na utulivu, kwani pamoja na kujitokeza kwa wingi tulipiga kura kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu za uchaguzi ukiachilia mbali kasoro ndogo ndogo zilizojitokeza katika zoezi hilo.  Ndugu watanzania wenzetu,  tangu juzi jumapili 25 Oktoba tulianza kupokea matokeo.  Hiyo ni hatua muhimu sana kwa taifa letu, demokrasia yetu na amani ya nchi yetu. Wote tutakubaliana kwamba nchi nyingi za kiafrika zimeingia katika machafuko ya kisiasa na kuvuruga amani ya nchi hizo katika kipindi cha kupokea matokeo. Nchi...

Page 1 of 69412345Next
Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More