Thursday, February 1, 2018

UWT MKOA WA IRINGA WAMETOA MSAADA WA VIFAA TIBA VYENYE GHARAMA YA SH 8,385,000 KATIKA HOSPITAL YA RUFAA IRINGA

Mwenyekiti wa umoja wa wanawake wa chama cha mapinduzi (UWT) mkoa wa Iringa Nikolina Lulandala akiongea na waandishi wa habari wakati wa kukabidhi vifaa tiba kwa uongozi wa Hospitali ya rufaa ya mkoa wa Iringa akiwa sambamba na viongozi wengine wa umoja huo
 Mwenyekiti wa umoja wa wanawake wa chama cha mapinduzi (UWT) mkoa wa Iringa Nikolina Lulandala akimkabidhi vifaa tiba afisa muuguzi msaidizi wa hospital hiyo Victory Ntara 
 Baadhi ya makada wa chama cha mapinduzi (CCM) mkoani Iringa wakielekea hodini kukawa zawadi kwa wagonjwa 
Mwenyekiti wa umoja wa wanawake wa chama cha mapinduzi (UWT) mkoa wa Iringa Nikolina Lulandala akiongea na waandishi wa habari wakati wa kukabidhi vifaa tiba kwa uongozi wa Hospitali ya rufaa ya mkoa wa Iringa akiwa sambamba na viongozi wengine wa umoja huo


Na Fredy Mgunda,Iringa.


UMOJA wa wanawake wa chama cha mapinduzi (UWT) mkoa wa Iringa wametoa msaada wa vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi milioni nane laki tatu na themanini na tano (8,385,000) katika hospital ya rufaa ya mkoa wa Iringa kwa lengo la kusaidia kutatua changamoto za afya.

 
Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa tiba mwenyekiti wa umoja huo Nikolina Lulandala alisema kuwa wameamua kutoa msaada wa vifaa tiba kutokana na upungufu uliopo katika hospital hiyo.

“Tumeamua kufanya hivi kwa lengo la kuboresha sekta ya afya kwa kuwa tumegundua kuwa hapa kuna changamoto nyingi hivyo sisi ni wanawake ndio maana tumeamua kutafuta wadau watusaidie kwa kuokoa maisha ya wagonjwa wanaokuja kutibiwa hapa” alisema Lulandala

Lulandala alisema kuwa walifanya utafiti kwanza kabla ya kununua vifaa tiba ambavyo wamevitoa msaada ili kuweza kutatua changamoto kwenye maeneo ambayo ndio yanakumbana na changamoto husika.

“Nashukuru tulikuja hapa kimya kimya na tulifanya utafiti na ndio tukaenda kwa wadau mbalimbali ambao wametusaidia na kutuwezesha kutoa msadaa huu ambao utachangia kuokoa maisha ya watanzania wanaotibiwa katika hospital yetu hii” alisema Lulandala

Alivitaja vifaa tiba ambavyo wamekabidhi hospitalini hapo kuwa ni Injection Gentramicin,  boksi 1000, Nabulaiza 1, Injection Ampiliciline vipande 1000,Suction Mashine 2, box za sabuni, mafuta ya kupaka watoto na biskuti.


lulandala alisema kuwa anaishukuru serikali ya awamu ya tano kwa kufanya kazi kwa kuwafikia wananchi wa chini hasa wale wanyonge kwa kutimiza kile ambacho kilikuwa kimeahidiwa wakati wa kuomba kura za kuongoza nchi.

“Kiukweli naomba nichukue nafasi hii kumpongeza sana  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli kwa kuwa anafanya kazi kubwa sana kuhakikisha kuwa Tanzania inapiga hatua ya kimaendeleo hivyo ni lazima tuonge mkono juhudi hizi” alisema lulandala

lulandala alisema kuwa serikali imefanikisha kuleta mabadiliko ya haraka katika sekta ya afya tofauti na hali ilivyokuwa hapo awali hivyo wananchi wanatakiwa kuendelea kufanya kazi kwa kujituma ili kuunga mkono juhudi hizi.

“Najua kuwa mnaona kwa macho yenu kiasi gani serikali ya wamu ya tano jinsi gani huduma za afya zilivyo boreshwa na lazima tujivunie hiki kinachofanywa na Rais wetu,mimi binafsi naunga mkono juhudi hizi na ninaomba wananchi nao waunge mkono juhudi hizi” alisema lulandala

lulandala alisema kuwa kuongezaka kwa hospital za rufaa kwenye mikoa,vituo vya afya kwenye kata au tarafa, zahanati kwenye vijiji na mitaa ni hatua kubwa ya kimaendeleo hivyo ndio serikali ya awamu hii inavyotekeleza vilivyo ilani ya chama cha mapinduzi ya mwaka 2015 hadi 2020.

“Nyie ni mashaidi kuwa zamani tulikuwa tunaishia kuwa na hospitali za mikoa tu lakini kwa sasa mambo yamebadilika kila kitu kinazidi kuwa kwenye ubora unaostahili kuwahudumia wananchi waliotuweka madarakani” alisema lulandala

Lakini sio afya tu hata ukiangalia saizi tunapata elimu bure ambayo inamwezesha kila mwanafunzi kusoma bure na kuhakikisha tunapunguza wimbi la wanafunzi kukosa elimu ambapo inasaidia kuwa nakizazi cha wasomi hapo baadae.

 Naye afisa muuguzi msaidizi wa hospital hiyo Victory Ntara aliwashukuru viongozi hao wa umoja wa wanawake wa chama cha mapinduzi (UWT) mkoa wa Iringa kwa kuwatembelea na kufanya usafi na zawadi walizozitoa kwa watumishi na wagonjwa waliokuwepo muda huo.

“Tunaomba mtufikishe salamu kwa Rais wa serikali ya awamu ya tano kwa kazi kubwa anayoifanya kwa kuboresha sekta ya afya kwa kuwa hali ya sasa kila kitu kinaenda kwa wakati” alisema Ntara


0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More