Thursday, February 22, 2018

LIPULI KWAANZA KUFUKA MOSHI

Timu ya Lipuli ya mkoani Iringa imepata pigo baada ya mjumbe wa Kamati ya Utendaji kutangaza kujivua uachama wa klabu hiyo na kuachia ngazi vyeo alivyokuwa navyo ndani ya klabu hiyo


Akizungumza na blog hii Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Devotha Chaula alisema kuwa ameamua kujivua uanachama na uongozi kutokana na kutoelewana na viongozi wa klabu hiyo kujali maslai yao binafsi

“kujiuzuru uongozi na kujivua uanachama ndani ya klabu ya mpira wa miguu ya lipuli kutokana na kutokukubali mambo yanayoendelea ndani ya klabu” alisema Chaula

Chaula alisema kuwa kwasasa hawezi kuongelea mambo mengi yanayoendelea ndani ya klabu ila viongozi wa lipuli wasipo sema ukweli ya nini kinaendelea ndani ya timu basi ataweka wazi kila kitu kwa umma


“Mwandishi naomba niache kidogo kwanza nipumzike maana nina hasira sana nisije ropoka mambo ambayo yataigharimu timu wewe niache hadi baadae nikwambia kila kitu” alisema Chaula



    Bi, DEVOTHA  T.  CHAULA,
                                                                                          Barua pepe; devochaullah2016@gmail.com,
                                                                                                  +255 754531183,
                                                                                                         S.  L.  P.  600,
                                                                                                                  IRINGA TZ,
                                                                                             22 - 02 – 2018.
MWENYEKITI WA KLABU YA
 MPIRA WA MIGUU YA LIPULI,
S.  L.  P.  1149/817,
IRINGA TZ.
Barua pepe; lipulifc2014@gmail.com

YAH;  KUJIUZURU UONGOZI NA KUJIVUA UANACHAMA NDANI YA KLABU  
            YA MPIRA WA MIGUU YA LIPULI.
                  Husika kichwa cha barua hapo juu, Mimi Devotha Chaula mwanachama namba LF 00000037  natangaza kujiuzuru uongozi wangu niliokuwa nao kama Mjumbe wa Kamati ya Utendaji na uanachama wangu ndani ya klabu ya Lipuli kuanzia leo tarehe 22/02/2018 kutokana na sababu zilizoko nje ya uwezo wangu kama vile matatizo na majukumu ya kifamilia.

                           WENU KATIKA KUINUA NA KUKUZA MICHEZO.
                                                        Bi, Devotha .T.  Chaula.

                                                                                        

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More