Tuesday, February 20, 2018

MHE BITEKO AAGIZA NDANI YA WIKI MBILI KUFUNGULIWA MGODI WA NYAKAVANGALA MKOANI IRINGA

Naibu Waziri Wa wizara ya Madini Mhe Doto Mashaka Biteko akisisitiza jambo wakati akizungumza na wachimbaji wadogo kwenye mkutano Wa hadhara katika mgodi wa Nyakavangala uliopo Kata ya Malengamakali Wilaya na Mkoa Wa Iringa, Leo 19 Februari 2018. Picha Zote Na Mathias Canal
Naibu Waziri Wa wizara ya Madini Mhe Doto Mashaka Biteko akizungumza na wachimbaji wadogo kwenye mkutano Wa hadhara katika mgodi wa Nyakavangala uliopo Kata ya Malengamakali Wilaya na Mkoa Wa Iringa, Leo 19 Februari 2018.
Naibu Waziri Wa wizara ya Madini Mhe Doto Mashaka Biteko akisikiliza maelezo mbalimbali kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa Bi Amina Masenza ,mara baada ya kuwasili katika mgodi wa Nyakavangala uliopo Kata ya Malengamakali Wilaya na Mkoa Wa Iringa, Leo 19 Februari 2018.
Baadhi ya waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari Mkoani Iringa wakinasa kumbukumbu muhimu kwa ajili ya kuhabarisha wananchi juu ya ziara ya Naibu Waziri Wa wizara ya Madini Mhe Doto Mashaka Biteko mkoani humoLeo 19 Februari 2018.
Umati mkubwa wa wachimbaji wadogo katika mgodi wa mgodi wa Nyakavangala uliopo katika Kata ya Malengamakali Wilaya na Mkoa Wa Iringa wakisikiliza hatma ya mgodi huo kutoka kwa Naibu Waziri Wa wizara ya Madini Mhe Doto Mashaka Biteko akisisitiza jambo wakati akizungumza na wachimbaji wadogo kwenye mkutano Wa hadhara katika Leo 19 Februari 2018.

Naibu Waziri wa Madini Mhe Doto Mashaka Biteko aakikagua mashimo mbalimbali kabla ya kuzungumza na wachimbaji wadogo kwenye mkutano Wa hadhara katika mgodi wa Nyakavangala uliopo Kata ya Malengamakali Wilaya na Mkoa Wa Iringa, Leo 19 Februari 2018. 

Na Mathias Canal, Iringa

Naibu Waziri Wa wizara ya Madini Mhe Doto Mashaka Biteko ameagiza kufunguliwa ndani ya wiki mbili mgodi wa Nyakavangala uliopo katika Kata ya Malengamakali Wilaya na Mkoa Wa Iringa ili kuwarahisishia huduma wachimbaji wadogo za kujiingizia kipato chao.

Mhe Biteko ameyasema hayo Leo 19 Februari 2018 wakati akizungumza na wachimbaji wadogo kwenye mkutano Wa hadhara Mara baada ya kuwasili mgodini hapo kukagua hatua za kiusalama zilizofikiwa tangu kufungwa kwa mgodi huo 12 Februari 2018 kufuatia matukio matatu ya ajali ambayo yalipelekea vifo vya wachimbaji wanne.

Mhe Biteko akiwa ameambatana na Mkuu Wa Mkoa Wa Iringa Mhe Amina Masenza, Kamati za ulinzi na usalama Wilaya na Mkoa wa Iringa, Mkuu Wa Wilaya ya Iringa Mhe Richard Kasesela na wataalamu Wa Madini kutoka Wizara ya Madini ameagiza kuchukuliwa hatua za haraka za kujiridhisha uhakika Wa usalama Wa wachimbaji kuanzia Leo 19 Februari 2018 hadi kufikia 5 Februari 2018 mgodi uwe umeanza uchimbaji.

Alisema kuwa kufunguliwa kwa mgodi huo kutaongeza kipato cha wachimbaji hao huku akisisitiza wachimbaji hao pindi mgodi utakapofunguliwa kuzingatia taratibu za usalama mgodini na kulipa kodi stahiki za serikali.

Alisema kuwa serikali ya awamu ya Tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli imekusudia kuwanufaisha wananchi kupitia rasilimali zao ikiwemo Madini ambapo Tanzania ni nchi yenye fursa nyingi kwa uchimbaji Madini ilihali wananchi hawanufaiki ipasavyo na rasilimali hiyo.

Mhe Rais Magufuli ametuagiza kuwalea na kuwasimamia wachimbaji wadogo nchini ili kutoka kwenye uchimbaji mdogo na kuwa wachimbaji wa kati na hatimaye kuwa wachimbaji wakubwa ili uchumi wa nchi ushikwe na watanzania wenyewe.

Alisema kuwa wachimbaji hao wanapaswa kushirikiana na serikali kuwafichua waovu wanaoiibia serikali rasilimali Madini kwa kuyatorosha kwenda sehemu mbalimbali nchini na nje ya nchi pasina kulipa kodi.

"Jichungeni na kujilinda wenyewe ili kila kinachopatikana serikali ijue imepata kiasi gani na wachimbaji wameingiza kiasi gani na kisemwe hadharani, ndugu zangu Rais anahangaika kuona kila eneo ambalo lina wachimbaji wadogo wana rasimishwa na hatimaye wananufaika na madini yao, lakini bado kuna watu wanatorosha madini" Aliongea kwa msisitizo Mhe Biteko na kuongeza kuwa

"Na Mimi nataka niwaambieni wale wote wanaofikiri katika serikali hii inayoongozwa na Rais Magufuli wanaweza kupenya na dhahabu watafute jambo jingine la kufanya maana jambo hilo limepitwa na wakati"

Alisisitiza kuwa wamiliki wa leseni kote nchini wanapaswa kutunza kumbukumbu za biashara nzima ya madini ikiwemo mapato na matumizi kwa muda usiopungua miaka mitano kinyume na hapo kwa mujibu wa sheria watatozwa faini ama kifungo jela

Kwa upande wake Mhe Mkuu wa Mkoa wa Iringa Bi Amina Masenza alisema kuwa wachimbaji hao wanapaswa kutofanya kazi kwa mazoea huku akisisitiza wachimbaji hao kuwa na ushirikiano na kupendana.

Sambamba na hayo pia aliwasihi kuwa makini na kutofanya ngono zembe kwani matokeo yake ni kupata maambukizi ya virusi vya UKIMWI na UKIMWI jambo litakalopelekea kupoteza nguvu kazi katika familia na Taifa kwa ujumla.

MWISHO

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More