Saturday, February 3, 2018

KAIMU KATIBU WA IDARA YA VYUO NA VYUO VIKUU NDUGU ZENDA AKABIDHI KADI 1500 KWA KATIBU HAMASA SENETI YA DAR

Dar es Salaam
Kaimu Katibu wa Idara ya Vyuo na Vyuo Vikuu Ndugu Daniel Zenda akikabidhi  kadi 1500 za wanachama wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) kwa Katibu wa Hamasa Seneti ya mkoa wa Dar es Salaam Ndugu Juakali Kuwanya katika hafla iliyofanyika leo Makao Makuu ya UVCCM, Upanga  jijini Dar es Salaam.

Zenda amesema, kadi hizo amezikabidhi ili zigawiwe kwa wananchama wapya ambao wamekuwa wakijiunga kwa wingi katika Chama Cha Mapinduzi na Jumuiya zake, kutokana na mwamko mkubwa wa wanafunzi wa Vyuo Vikuu kuunga mkono CCM kutokana na kuvutiwa na Utendaji kazi  wa Rais John Magufuli na Serikali yake ya awamu ya tano

Imetolewa na 
Uvccm Seneti Mkoa Dsm.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More