Monday, February 26, 2018

MBUNGE MGIMWA ATUMIA MAMILIONI KUBORESHA SEKTA YA ELIMU NA AFYA JIMBONI KWAKE

 MBUNGE wa Jimbo la Mufindi Kaskazini Mahmoud Mgimwa ametoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi vyenye thamani ya zaidi ya Sh Milioni 12 vitakavyotumika kuboresha miundombinu ya sekta ya elimu na afya jimboni humo
 MBUNGE wa Jimbo la Mufindi Kaskazini Mahmoud Mgimwa akikabidhi sim tanki ya lita 500 kwa viongozi 
  MBUNGE wa Jimbo la Mufindi Kaskazini Mahmoud Mgimwa akikabidhi msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi vyenye thamani ya zaidi ya Sh Milioni 12 vitakavyotumika kuboresha miundombinu ya sekta ya elimu na afya jimboni humo
  MBUNGE wa Jimbo la Mufindi Kaskazini Mahmoud Mgimwa bati na rangi kwa baadhi ya viongozi waliojitokeza kuja kuchukua masaada huo
  MBUNGE wa Jimbo la Mufindi Kaskazini Mahmoud Mgimwa akimkabidhi diwandi makopo ya rangi 

Na Fredy Mgunda,Mufindi.

MBUNGE wa Jimbo la Mufindi Kaskazini Mahmoud Mgimwa ametoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi vyenye thamani ya zaidi ya Sh Milioni 12 vitakavyotumika kuboresha miundombinu ya sekta ya elimu na afya jimboni humo.

Akizungumza wakati wa ugawaji wa vifaa hivyo Mgimwa alisema kuwa ametoa mabati 280, mifuko 310 ya saruji, rangi za maji na mafuta na sim tenki la lita mia tano (500) za kuhifadhia maji.

“Nilifanya ziara katika vijiji vya kata hizo nikaona wananchi wanavyojitoa kuboresha  sekta ya elimu na mimi kama mbunge wao nikaamua kuwaunga mkono kwa kuchangia vifaa hivyo” alisema Mgimwa


Mgimwa alizitaja kata zinazonufaika na msaada huo ni kata ya Mapanda, Kibengu, Ihanu na Sadani na akavitaja vijiji vinavyonufaika na msaada huo kuwa ni pamoja na Ihimbo, Ukami na Chogo katika kata ya Mapanda; na Kipanga, Igeleke, Kibengu, Usokami na Igomtwa katika kata ya Kibengu.

Vingine ni kijiji cha Lulanda katika kata ya Ihanu na katika kata ya Sadani Mgimwa sehemu ya msaada huo inakwenda kusaidia ujenzi wa bweni la wasichana katika shule ya sekondari Mgalo.

Aidha Mgimwa alisema kuwa ataendelea kusaidia maendeleo kwenye vijiji ambavyo vinafanya maendeleo katika jimbo lake

Akiongea kwa niamba ya halmashauri ya wilaya ya Mufindi na vijiji vyote vilivyonufaika na msaada huo, Makamu Mwenyekiti Asheri Mtono alisema kuwa jimbo la Mufindi Kaskazini linakabiliwa na changamoto nyingi za ujenzi wa majengo mbalimbali hivyo msaada alitoa utapunguza changamoto zilizopo kwa kiasi Fulani

“halmashauri hii ina changamoto kubwa ya uchakavu wa miundombinu ya shule na kwa msaada huu wa mbunge mazingira hayo yatakwenda kuboreshwa” alisema Mtono

 Mtono ambaye pia ni diwani wa kata ya sadani alisema pamoja na mchango wa mbunge huo na wadau wao wengine, wananchi wa vijiji hivyo na vingine vyote katika halmashauri hiyo wanahitajika kuendelea kuchangia shughuli zao za maendeleo.

 Nao baadhi ya viongozi wa vijiji wamempongeza mbunge Mgimwa  kuwa kutoa vifaa vya ujenzi kwenye vijiji vyake vyote vya jimbo la Mufindi Kaskazini ambavyo vitachochoe kuleta maendeleo kwa wananchi wa jimbo hilo.

Mmoja wa wanufaika wa msaada huo, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Isupilo, Onorata Mwanuke alisema kwa msaada waliopatapata wanakwenda kukamilisha ujenzi wa nyumba moja ya mwalimu.

“Mahitaji ya nyumba za walimu ni tisa zilizopo ni tatu na mbunge ametoa msaada wa mifuko 30 ya saruji kusaidia kukamilisha nyumba ya nne ya mwalimu. Tunategemea mbunge ataendelea kutuunga mkono”alisema Mwanuke

Kabla ya jana mbunge mgimwa alishakuwa ametoa jumla ya bati mia tano tisini (590) na saruji mifuko mia mbili ishirini (220) kwa ajili ya ujenzi  na ukarabati wa madarasa ya shule,zahanati na nyumba za wafanyakazi wa zahanati na walimu wa shule zilizopo katika kata ya Ihalimba huku lengo likiwa kuboresha sekta ya elimu na afya kwa wananchi.

Na alifanya kazi kwa kushirikiana na wananchi  wa kijiji cha Kibengu wametumia jumla ya shilingi milioni mia moja kumi na tisa na laki mbili (119,200,000) katika ujenzi wa madarasa ya shule,zahanati na nyumba za wafanyakazi wa zahanati na walimu wa shule zilizopo katika kijiji hicho lengo likiwa katika kuboresha sekta ya elimu na afya kwa wananchi.


0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More