Thursday, February 22, 2018

KASESELA, ASIA JUMA WATINGA KARIAKOO DAR ES SALAAM, LEO, KUPATA UZOEFU WA NAMNA BORA YA KUSIMAMIA VEMA MACHINGA


 Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesera akisalimia wananchi baada ya kutambulishwa na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema (watatu kushoto) alipowapeleka Kasesera na Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Asia Juma Abdallah katika eneo la biashara za Machinga katika Mtaa wa Kongo, Kariakoo jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kupata uzoefu wa namna Wilaya ya Ilala ilivyofanikiwa katika kuboresha mazingira na kuwaweka pamoja machinga hao katika shughuli zao. Wapili kushoto ni Katibu Tawala wa Ilala Edward Mpogolo.
 Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema akimtambulisha Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Asia Juma Abdallah kwa Machinga wakati wa ziara hiyo
 Baadhi ya kinamama wakimweleza kero Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema alipokuwa na ugeni huo
 Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesera akiwa katika Mtaa wa Kongo kujionea shughuli mbalimbali zinavyoendesha na Machinga wa Kariakoo
 Msafara wa Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesera ukipita katika mitaa mbalimbali ya Kariakoo kujionea shughuli mbalimbali zinavyoendesha na Machinga
 Kasesera akiwa na Mwenyekiti wa Machinga wa kariakoo katika ziara hiyo
 Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesera akitazama bidhaa za machinga ambazo alisema hadhi ya bidhaa hizo inaonekana ni zaidi na za machinga
 Kasesera akitazama sampuli ya baadhi ya vifaa vya jikoni vinavyofanya kazi ambavyo anauza Machinga
 Mkuu wa Wilaya ya Ilala Ricard Kasesera akihoji mfumo kwenye kompyuta alipoingia katika Ofisi ya Umoja wa Machinga kujua wanavyofanya kazi.
 Machinga ambaye ni mtaalamu wa programu za kompyuta namoyo Yusuf, akimpa maelezo Kasesera ya namna ambavyo Umoja wa Machinga unavyohifadhi kumbukumbu zote za machinga katika komyupta. Kulia ni Mbunge wa Kilolo Asia Juma akifuatilia kwa karibu
 Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Asia Juma akimweleza jambo Ofisa katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya walipokuwa kwenye ofisi hiyo ya Machinga Kariakoo
 Kasesera na ujumbe wake wakitoka katika Ofisi ya Machinga
 Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesera na Mkuu wa wilaya ya Kilolo Asia Juma wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Machinga wakati wa ziara hiyo
 Kasesera akimfurahia Ustadhi ambaye ni mmoja wa machinga Kariakoo
 Kasesera akifurahia jezi la Timu ya Machinga baada ya kuzawadiwa katika ziara hiyo 
 Kasesera na Amina wakichagua nguo kwenye vitalu vya biashara za Machinga wakati wa ziara hiyo
 Kasesera akilipa fedha baada ya kuchagua nguo alizopenda
 Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesera akiagana na Mwenyekiti wa Machinga Stephen Lusinde mwishoni mwa ziara hiyo 
 Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesera akifanya majumuisho na ujumbe wake bada ya kurudi katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ilala
 Katibu Tawala wa Wilaya ya Ilala Edward Mpogolo akifanya utambulisho na kutoa maelezo machache kabla ya kuanza ziara hiyo
 Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema akizungumza ofisini kwake na ujumbe huo kabla ya ziara hiyo kuanza
 Kasesera akizungumza katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ilala kabla ya ziara kuanza
Kasesera na ujumbe wake wakijiandaa kuondoka ofisi kwa Mkuu wa wilaya kuanza ziara hiyo. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More