Tuesday, March 14, 2017

Vanessa Mdee Kaachiwa Kwa Dhamana

Mwanamuziki Vanessa Mdee maarufu Vee Money ameachiwa kwa dhamana na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam baada ya kuwa ameshikiliwa kwa takribani wiki moja kufuatia tuhuma ya dawa za kulevya inayomkabili.

Mdee aliachiwa jana jioni ambapo anatuhumiwa kutumia na kusambaza dawa za kulevya. Alishikiliwa na Polisi tangu juma lililopita baada ya kwenda kuripoti kufuatia kutajwa kwenye orodha ya watuhumiwa wa dawa hizo iliyosomwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Slaam, Paul Makonda.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More