Monday, March 27, 2017

MANISPAA YA IRINGA YAAGIZWA KUSIMAMIA MIRADI KWA ZINGATIA VIWANGO VYA UBORA




Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC)imeiagiza Manispaa ya Iringa, mkoani Iringa kuboresha barabara zake za pembezoni mwa mji ili zitoe huduma kwa wananchi.

Akizungumza wakati wa majumwisho wa ziara ya siku moja ya kamati kwenye Manispaa ya Iringa jana makamu mwenyekiti wa kamati hiyo Abdallah Chikota alitoa maelekezo kuboresha miundombinu ya barabara pembezoni mwa mji.

Alisema kuwa Manispaa ya Iringa imeelekeza nguvu kubwa katikati ya mji na kusahau barabara za pembezo ambazo zitasaidai kutoa huduma kwa wananchi.

Chikota alisema kuwa wananchi walioko pembezoni mwa mji ni sawa na wananchi wa katikati ya mji.

Kuna tofauti kubwa kati ya wananchi waishio pembezoni na katikakti. Barabara za pembezoni mwa mji hazina kiwamgo vya ubora…,” alisema Chikota.

Aidha, Kamati ya Kudumu ya Bunge za Hesabu za Serikali za Mitaa ilitembelea barabara za Mkimbizi- kihesa Sokoni-Tumaini Univesrsity and Ngome na kukuta havian vivuko kwa kurahisha wananchi kufika kwa krahisa katika makazi yao.

Alisema kuwa barabara hizo pamoja na kukamilika ujenzi wake zilikuwa hazina baadhi ya alama za barabarani na vivuko vya watembelea kwa miguu. 

Hatua hiyo imetokana na ujenzi wa barabara wa hizo kutokuwa na baadhi ya miundombinu vikiwemo vivuko vya kufanya barabara hiyo kutokuwa rafiki kwa mwananchi.

Mradi wa ujenzi wa barabara unajumuisha vipande vitatu vya barabara za Mkimbizi TBA (1.10km), Kihesa Sokoni-University of Iringa (zamani Tumaini University (0.70km) na Ngome–Mwang’ingo (0.45km) uliyobuniwa ili kuinua kiwango cha barabara hizi kutoka changarawe hadi kiwango cha lami.

Halmashauri ya Manispaa ilifanya matengenezo ya barabara hizi kwa kiwango cha lami kwa kutumia fedha za mfuko wa barabara (Road Fund) kwa bajeti ya mwaka 2013/2014 ambazo zilivuka mwaka.

Akitoa taarifa kwa kamati Mhandishi wa Ujenzi wa Manispaa ya Iringa, Mashaka Luhamba alisema kuwa mradi huo ulianza kutekeleza tarehe 1/11/2013 na uilikamilika tarehe 18/09/2014.

Alisema kuwa kazi hiyo ilitekelezwa na Mkandarasi G’S Contractors kwa mkataba wa gharama ya 1,088,505,000/-.

Luhamba alisema kuwa kazi hiyo ililenga na pia kupunguza kero kwa wananchi wa eneo la mkimbizi ambalo halina barabara ya uhakika na lina wakazi wengi.

Naye, Katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu alisema amepokea maagizo hayo kutoka kamati ya kudumu ya bunge za hesabu za serikali za mitaa (LAAC)na kuahidi kuyafanya kazi mapendekezo hayo.

Wamoja alisema kuwa kupitia sekritarieti ya mkoa atahakikisha wanasimia utekelekezaji wa maagizo kwa manispaa ya iringa yanafanyika.

Kamati ya kudumu ya bunge za hesabu za serikali za mitaa (LAAC) ilitembelea miradi mbalimbali hapa manispaa ya iringa ikiwemoile ya maji, barabara na machinjio ya kisasa ambao hata hiyo mradi huo umechukua muda mrefu kukamilika (miaka kumi).

Pia kaamti hiyo imeagiza watendaji wa Manispaa ya Iringa kusimamia miradi hiyo inayotumia gharama za walipa kodi kwa kuzingatia viwango wa ubora.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More