Friday, April 20, 2018

WAZIRI DKT. KALEMANI AWASHA UMEME KWA MARA YA KWANZA KATIKA KIJIJI CHA LUMWAGO



Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani,mkuu wa wilaya ya Mufindi Jamhuri Wiliam,Mbunge wa jimbo la Mafinga Mjini Cosato Chumi pamoja na mwenyekiti wa chama cha mapinduzi wilaya ya Mufindi wakiwa nafungua na kuwasha umeme kwa mara ya kwanza katika kijiji cha Lumwago kata ya Upendo Halmashauri ya Mji wa Mafinga mkoani Iringa.
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani na Mbunge wa jimbo la Mafinga Mjini Cosato Chumi wakishangilia baada ya kuona kweli umeme umewaka katika kijiji cha Lumwago
Mbunge wa jimbo la Mafinga Mjini Cosato Chumi akiwa Kwenye furaha ya ajabu baada ya kuona wananchi wake wamefanikiwa kupata umeme katika eneo hilo ambazo minasekana linakuwa kwa kasi kubwa
 Mbunge wa jimbo la Mafinga Mjini Cosato Chumi akiongea mbele ya wapiga kura wake wa jimbo hilo
 Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani akiwaonyesha wananchi wa jimbo la Mafinga Mjini kifaa cha Umeme Tayari (UMETA).


NA FREDY MGUNDA,IRINGA. 

Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani amewasha umeme kwa mara ya kwanza katika Kata ya Upendo mtaa wa Lumwago uliyopo katika Halmashauri ya Mji wa Mafinga, Mkoa wa Iringa.

Uzinduzi huo uliofanyika mbele ya mamia ya wananchi wa mtaa wa Lumwago ambao walikuwa na furaha baada ya kuona umeme huo umewaka kwa mara ya kwanza

Waziri Kalemani alifanya uzinduzi huo akiwa katika ziara ya kazi mkoani Iringa wakati wa kukagua miradi ya umeme inayotekelezwa na REA awamu ya tatu.

Awali, akiongea na wananchi Dkt. Kalemani alisema kuwa wananchi zaidi ya 200 wataanza kupata umeme kufuatia tukio la kurasimishwa kuwashwa kwa nishati hiyo Lumwago.

“Tunatoa kipaumbele chetu kwa sasa kwani ni kuhakikisha kwamba wananchi wengi wanapata umeme na huduma hiyo inakuwa ya uhakika,” alisema Dkt. Kalemani.

Akifafanua zaidi, alisema kuwa, Serikali imeanzisha harakati za kufanya ukaguzi kwenye utekelezaji wa Miradi yote ya umeme mkoani humo.

Aidha, alitumia fursa hiyo kuwataka viongozi wa Halmashauri mbalimbali za vijiji kote nchini, kuhakikisha wanajiandaa kwa ajili ya kuunganishiwa umeme katika taasisi zote za umma zikiwemo Shule, Vituo vya Afya, Miradi ya Maji, Masoko na nyinginezo.

Vilevile, alikumbushia umuhimu wa kila mmoja kuhakikisha baada ya kuunganishiwa umeme katika eneo lake anakumbuka kulipa bili za huduma hiyo muhimu.

“Usipolipa,Serikali itakukatia umeme hivyo kurudisha nyuma maendeleo yako,” alisisitiza.

Jambo jingine ambalo Waziri Kalemani alisisitiza ni kwa wakandarasi kuhakikisha wanawagawia bure wateja 200 wa kwanza watakaojitokeza kuunganishiwa umeme wa REA, kifaa cha Umeme Tayari (UMETA) kama ilivyoelekezwa na Serikali na siyo vinginevyo.

Hapo awali,mbunge wa jimbo la Mafinga Mjini Cosato Chumi pamoja na kupongeza jitihada ambazo Wizara ya nishati imekuwa ikifanya nchi nzima katika kuhakikisha huduma ya umeme inapatikana katika maeneo mbalimbali, pia alimwomba Waziri Kalemani kulipa upendeleo jimbo hilo kwa kuwa ndio kitovu cha uchimi wa viwanda mkoani Iringa.

“Mheshimiwa nikuombe utusaidia kwenye vijiji vilivyobaki katika jimbo langu kwasasababu wananchi wangu niwachapakazi na wapenda maendeleo” alisema Chumi

Chumi aliwamwambia waziri kuwa jimbo la Mafinga Mjini ni moja kati ya maeneo ambayo yanaviwanda vingi ambavyo vinasaidia kukuza uchumi wa nchi pamoja na kuongeza ajira kwa watanzania wanaoishi katika jimbo hilo.

“Hapa tunazaidi ya viwanda arobain vya mazao ya miti na tunaviwanda vingine vingi na viwanda vyote hivi vinatumia nisharti ya umeme hivyo naomba nitoe rai kuwa mji wa mafinga unahitaji sana huduma ya nishati hii kwa kiasi kikubwa” alisema Chumi

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More