Tuesday, April 24, 2018

TAKUKURU MKOA WA IRINGA WAMECHUNGUZA MIRADI NANE NA MIWILI IMEKUTWA NA UBADHIRIFU


 Kamanda  wa  taasisi ya  kuzuaia  na kupambana na  rushwa  (TAKUKURU)  mkoa  wa  Iringa  Aidan  Ndomba  akizungumza na  waandishi wa habari ofisini  kwake  kuelezea juu ya kilichotokea katika kipindi cha Julai hadi Desemba 2017.


 Baadhi ya viongozi wa takukuru na waandishi wa habari wakimsikiliza Kamanda  wa  taasisi ya  kuzuaia  na kupambana na  rushwa  (TAKUKURU)  mkoa  wa  Iringa  Aidan  Ndomba 

Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Kamanda  wa  taasisi ya  kuzuaia  na kupambana na  rushwa  (TAKUKURU)  mkoa  wa  Iringa  Aidan  Ndomba 


NA FREDY MGUNDA,IRINGA.


Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoani Iringa imepokea jumla ya malalamiko 91 ya rushwa kutoka kwa wananchi katika kipindi cha Julai hadi Desemba 2017.

Hayo yamezungumzwa na Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Iringa Aidan Ndomba alipokuwa akitoa taarifa ya utendaji kazi wa TAKUKURU Mkoani hapa katika kipindi cha mwezi Julai hadi disemba 2017 na kuongeza kuwa katika sekta ya TAMISEMI kumekuwa na malalamiko 18.

Ndomba  alisema kuwa taasisi imechunguza  miradi  nane ya  sekta ya elimu ,maji na barabara  yenye  thamani  ya  takribani  bilioni 2.5 katika  wilaya ya Iringa , Mufindi na  Kilolo baada ya  kuwepo kwa dalili  ya matumizi mabaya ya  fedha  za  za  miradi hiyo .


alisema  ndani ya  kipindi  hicho  ofisi yake  ilifuatilia  na  kufanya  ukagzi  wa fedha  za  miradi  nane  ya maendeleo  katika  sekta za elimu ,maji na barabara  yenye  thamani ya  takribani shilingi bilioni  2,588,000,000 na kubaini mapungufu  katika  miradi yenye thamani ya  shilingi milioni 818 ambapo  uchunguzi  wa matumizi ya  fedha  za  miradoi umeanzishwa.

Alisema  kuwa  miradi  miwili  ilifuatiliwa  na kukaguliwa  katika  Halmashauri ya  Iringa na  ina  thamani ya   shilingi  1,164,614,899 iliyopo  katika kijiji  cha Mfyome   kata ya  Kiwere   na  Malizanga  kata ya  Mlowa   huku miradi mitatu  iliyofuatiliwa   na  kukaguliwa ipo  katika  Halmashauri ya  Kilolo ina  thamani ya shilingi 908,138,034 kuwa  miradi hii ipo  kijiji  cha Ng'uruhe , Irindi, na Ipalamwa .


 Ndomba alisema kwa upande wa barabara  miradi miwili ilifuatiliwa  na kukaguliwa  katika  wilaya ya  Mufindi  na ina thamani ya  shilingi 407,343,774 na kuwa miradi hiyo ni pamoja na barabara  za Maduma  -Tambalang'ombe  na Maguhani - Udumka .

wakati kwa  wilaya ya  Kilolo kuna  mradi  mmoja  wa barabara   wenye  thamani ya  shilingi  107,343,774 umefuatiliwa na  kukaguliwa  mradi huu ni ule wa Ilula  ujulikanao kama  KItelewasi - Ilambo .
Ndomba  alisema  kuwa  baadhi ya  sekta  zilizolalamikiwa  ni  pamoja na  TAMISEMI ( Halmashauri  na  serikali  za  mitaa,vijiji  )   kwa  kuwa na malalamiko 18  , jeshi la  polisi  malalamiko  12 na  mabaraza  ya  ardhi malalamiko 8.

Aidha  Ndomba alisema  mashauri  mawili  yalikamilika  kwa  kutolewa  hukumu  katika shauri  namba  CC 03/2017 kati ya  Jamhuri na  Upendo Mponzi  (VEO- Ilula)  na  mwenzake Tulinutwa  Alphonce  Mlangwa  ambae  ni  diwani wa  kata ya  Kipaduka wote  wakiwa ni  watumishi  wa   umma  hakimu wa  mkoa  wa Iringa John Mpitanjia  aliwatia  hatiani wote  na  kuhukumiwa  jela miezi 6 ama  kulipa faini ya  shilingi 300,000 kila  mmoja .

Pia  alisema katika  shauri  la  pili  namba CC.39/2016 mshtakiwa  Selemani Futani  ambae ni mfamasia  msaidizi  wa Halmashauri ya  Mufindi aliachiwa   huru  na mahakama  ya  wilaya ya  Mufindi  hata  hivyo upande  wa Jamhuri  (Takukuru)  wamekata  rufaa mahakama kuu .

Kamanda  Ndomba  alisema kwa  kipindi  hicho  Takukuru  mkoa  wa Iringa imefanikiwa  kuokoa  kiasi cha shilingi 100,000 baada ya  kubaini  kuwa  kiasi hicho  cha fedha  zilikuwa  zilipwe mahakamani  kama  faini zilitumiwa na mtumishi  binafsi  wa mahakama  badala ya  kuziingiza  kwenye  mfuko  wa serikali .

Hivyo  amewataka  wananchi  kuendelea  kufika  ofisini kwake ama  ofisi  za wilaya   kutoa  taarifa  mbali mbali za  rushwa ama  kutumia  simu  0784606519/0754606519 ama  kupiga  simu ya  bure 113 au  *113# kupitia  huduma ya longa  nasi kwa ujumbe  mfupi SMS 113


0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More