Monday, April 16, 2018

WAKULIMA MKOANI IRINGA WATAKIWA KUTUMIA MBOLEA YA YARA INAYOZALISHWA NA KAMPUNI YA YARA TANZANIA

Afisa Masoko wa Kampuni ya Mbolea ya Yara mkoa wa Iringa Dionis Tshonde akitoa maelezo kwa kiasi gani mbolea hiyo inawasaidia wakulima kulima kilimo chenye tija na kuvuna mavuno mengi kwenye msimu mmoja 
 Uongozi wa timu ya Singida United ya mkoani Singida na wachezaji wa timu hiyo nao walifanikiwa kutembelea shamba darasa ambalo wanatumia mbolea ya kampuni ya Yara na kuwataka wakulima wa mkoani Iringa kulima kilimo bora kwa kutumia mbolea ambazo zinazalishwa na kampuni ya Yara iliyopo kulasini jijini Dar es salaam.
Shamba darasa ambalo lipo mkoani Iringa katika kata ya Ruaha manispaa ya Iringa

NA FREDY MGUNDA,IRINGA.

WAKULIMA wametakiwa  kutumia  kulima kilimo chenye tija kwa kufuata maelekezo ya wataalamu  ili waweze kupata mazao bora.
Hayo yamesemwa na Afisa Kilimo Manispaa ya Iringa Bi.Happines Nnko wakati akizungumza na wakulima wa kata ya Ruaha Manispaa ya Iringa katika shamba darasa ambalo wakulima wamelima kwa kufuata kanuni na taratibu za kilimo bora na kufanikiwa kustawisha mazao vizuri.

Hapinpines alisema kuwa wakulima wanapoteza nguvu,muda kulima kilimo sikichokuwa na tija kwa kutofuata  kanuni za kilimo, mbegu bora na mborea za kupandia na kukuzia.

"Ninawaomba tuwatumie wataalamu wetu ili tuweze kulima kilimo chenye tija.Pia ninawaomba haya mliyoshauriwa na wataalamu kutoka kmpuni ya Mbolea Yara na Seed.co mkayafanyie kazi,lengo tunataka kuona kilimo kikimkwamua Mkulima na si kumdidimiza"

Akitoa Elimu kwa wakulima juu ya umuhimu wa kutumia Mbolea ya Yara  Vespa Kwavava,amabae ni Mkulima katika eneo la Ipogolo kata ya Ruaha alisema kuwa hapo awali  kabla hajaanza kutrumia Mbolea uzalishaji  ulikuwa mdogo ,lakini kwa hivi sasa umeongezeka.

Ninawaomba wakulima wenzangu watumie mbolea na wataalamu ili wawaeze kupiga hatua katika uzalishaji na hatimae kujikwamua kimaisha kupitia kilimo.

Kwa upande wake Afisa Masoko wa Kampuni ya Mbolea ya Yara Dionis Tshonde alisema kuwa wataendelea kutoa elimu ya kilimo bora kwa kushirikiana na wananachi ili kuhakikisha wanalima kilimo chenye faida kubwa kuliko wanavyofanya sasa wakulima wengi.

“Wananchi wengi wanapenda kulima lakini bado hawafuati taratibu na kanuni za kilimo bora hivyo atahakikisha kupitia kampuni ya Yara wanatoa elimu kwa wakulima ili kuwakomboa katika kilimo wanacholima kwa sasa hadi kufikia kulima kilimo cha kisasa na chenye faida” alisema
  
Tshonde aliwataka wakulima kutumia mbolea za kampuni ya Yara ambazo kwa sasa ndio imekuwa mkombozi wa wakulima kwa kuzalisha mazao mengi tofauti na ilivyokuwa hapo awali.

“Mbolea za kampuni ya Yara zinavirubisho ambavyo vinasaidia mazoa kukuwa na kuzalisha mazao mengi ambayo yanakuwa faida kwa wakulima”

Tshonde alisema kuwa ukitumia mbolea ya kampuni Yara utapata faida kubwa kwa kuwa ukilima hekali moja unakuwa na uhakika wa kuvuna kati ya gunia 35 hadi 40 endapo mkulima atazingatia kanuni na taratibu za kilimo che tija.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More