Sunday, March 18, 2018

MKURUGENZI MNASI AFANYA ZIARA YA TATHIMINI YA ZOEZI LA UANDIKISHWAJI WAKAZI KWA NJIA YA ELETRONIKI (EPRS)

 Mkurugenzi wa halmashauri ya Ileje Haji Mnasi akiwa na viongozi wa halmashauri ya wilaya ya Ileje wakiongea na mmoja ya wananchi kujua zoezi la uandikishaji wakazi linaendeleaje na kujua changamoto kutoka kwa wananchi.
 Mkurugenzi wa halmashauri ya Ileje Haji Mnasi akiwa na viongozi wa halmashauri ya wilaya ya Ileje wakiongea na  wananchi kujua zoezi la uandikishaji wakazi linaendeleaje na kujua changamoto kutoka kwa wananchi juu ya zoezi hilo.
 Mkurugenzi wa halmashauri ya Ileje Haji Mnasi akiwa na viongozi wa halmashauri ya wilaya ya Ileje wakiwa kwenye moja ya ofisi ambayo inahusika moja kwa moja kwenye zoezi la uandikishaji wa wakazi
 Mkurugenzi wa halmashauri ya Ileje Haji Mnasi akiwa na viongozi wa halmashauri ya wilaya ya Ileje wakiongea na wananchi kujua zoezi la uandikishaji wakazi linaendeleaje na kujua changamoto kutoka kwa wananchi na kufurahia mambo kadhaa kutoka kwa wananchi.
 Mkurugenzi wa halmashauri ya Ileje Haji Mnasi akiwa na viongozi wa halmashauri ya wilaya ya Ileje wakifurahia hali ya hewa ya halmashauri hiyo
 
 Na Fredy Mgunda,Iringa.

UONGOZI wa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje Mkoani Songwe umeanza kufanya tathimini ya kujua wakazi wangapi wameandikishwa kwa njia ya eletroniki (ePRS) kwa lengo la kutaka kutambua kuwa wilaya hiyo inawakazi wangapi wanaoishi eneo hilo.

Akizungumza na blog hii mkurugenzi wa halmashauri ya Ileje Haji Mnasi alisema wameamua kufanya tathimini hiyo baada ya kubaini kuwa wafanyakazi wengi wa umma hawajaandikishwa hivyo wanatakiwa kupitiwa kwenye kaya zao na kuwaandikisha ili kupata idadi kamili ya wakazi wa wilaya ya Ileje.

“Taarifa za awali zinaonyesha kuwa watumishi wa umma hawajajiandikisha kwenye zoezi hili hivyo nawaagiza waandikishaji kuanzia sasa wahakikishe wanawapitia kwenye kaya zao na kuwaandkisha ili tujue idadi kamili ya wazi waliopo” alisema Mnasi

Mnasi alisema kuwa waandikishaji wote wanatakiwa wahakikishe wanaandaa taarifa iliyokamilika na kuiwakilisha kwa mtendaji wa kata kwa lengo la kuunganisha taarifa za kata yote na kuziwakilisha kwa mkurugenzi mtendaji wa wilaya.

“Watendaji wa vijiji (VEO’S) hakikisheni mnaanda taarifa hii na kuiwakilishakwa mtendaji wa kata (WEO’S) ili aweze kuunganisha na kuwakilisha kwa ofisi ya mkurugenzi mtendaji wa wilaya ya Ileje” alisema Mnasi

Mnasi alisema kuwa ukijua idadi ya wakazi wa eneo husika inasaidia kupanga mipangilio ya kufanya maendeleo na kuwaletea maendeleo wananchi wa maeneo husika

“Nikwambie mwandishi wa habari ukijua idadi ya wakazi inakurahisihia hata kuandaa mpango kabambe wa hlmashauri yako tofauti na kufanya kazi huku ukiwa hujui idadi ya wakazi wako itakuletea shida sana kupata maendeleo ya haraka” alisema Mnasi

Mnasi alisema kuwa ili kufanikisha zoezi hili amewaomba wadau mbalimbali,wenyeviti wa vijiji,watendaji na wananchi wanapaswa kutoa ushirikiano wa kutosha kufanikisha zoezi hili.

“Bila kupata ushirikiano kutoka kwa viongozi na wananchi wa ngazi ya kijiji hadi kata wasipotoa ushirikiano basi zoezi hili litagonga mwamba” alisema Mnasi

Mnasi alimalizia kwa kusema kuwa zoezi hilo linaendelea katika kata zote za halmashauri ya wilaya ya Ileje mkoani Songwe

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More