Thursday, March 29, 2018

LOWASSA NA SUMAYE WATINGA MAHAKAMANI KESI YA AKINA MBOWE

Mawaziri wakuu wastaafu Edward Lowassa na Fredrick Sumaye amehudhuria katika Mahakama ya hakimu mkazi Kisutu kufuatilia hatma ya kesi ya viongozi 6 wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo ( CHADEMA ) wakiongozwa na Mwenyekiti Freeman Mbowe kama watapata dhamana au wataendelea kusota rumande.
Viongozi waandamizi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)wamefikishwa mahakamani leo saa 2 asubuhi katika Mahakama ya Kisutu kwa ajili ya kusikiliza uamuzi wa dhamana yao huku wakisindikizwa na baadhi ya wajumbe wa Kamati kuu CHADEMA.
Kesi hiyo ya Viongozi wa CHADEMA inatarajiwa kutajwa leo chini ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri ambaye anatarajiwa kutoa uamuzi kuhusu dhamana ya washtakiwa hao.
Hata hivyo baadhi ya Viongozi wengine wa chama hicho wamefika mahakamani hapo ili kuwasindikiza viongozi wenzao wakiongozwa na Mjumbe wa Kamati Kuu CHADEMA, Edward Lowassa, Makamu Mwenyekiti wa Chadema Profesa Abdallah Safari na  baadhi ya Wabunge.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More