Thursday, March 8, 2018

BENK YA NMB IRINGA WAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNINIA NA MBUNGE RITTA KABATI

 Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakzi wanawake wa benk ya NMB tawi la Mkwawa mkoani Iringa wakishereskea maadhimisho ya siku ya wanawake dunia
 Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakzi wanaume wa benk ya NMB tawi la Mkwawa mkoani Iringa wakishereskea maadhimisho ya siku ya wanawake dunia

 Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakzi wanawake wa benk ya NMB tawi la Mkwawa mkoani Iringa wakishereskea maadhimisho ya siku ya wanawake dunia na kukata keki ya pamoja
Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati kilishwa keki na mmoja wa wafanyakzi wa benk ya NMB tawi la Mkwawa mkoani Iringa
Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakzi wa benk ya NMB tawi la Mkwawa mkoani Iringa wakishereskea maadhimisho ya siku ya wanawake dunia 

Na Fredy Mgunda,Iringa.
 
MBUNGE wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Ritta Kabati amewataka wanawake mkoani iringa kujifunza kujitegemea katika maisha kutokana na benk nyingi kutoa mikopo yenye riba ndogo ambayo inawasidia kuwainua kiuchumi.

Akizungumza na wafanyakazi wa benk ya NMB tawi la mkwawa Kabati alisema kuwa benk hiyo imesaidia kuinua maisha ya wanawake kwa kuwawezesha mitaji ya kufanyia biashara mbalimbali.

“Mimi nimeshuhudia mara kwa mara mkiviwezesha vikundi vingi vya wanawake ambavyo mmesaidia kukuza maendeleo ya wanawake wa mkoa wa Iringa na ndio maana wanawake wengi wamekuwa wakitoa ushuhuda mzuri juu ya huduma za nzuri za benk hii” alisema Kabati

Kabati alisema kuwa wanawake wanatakiwa kuwa nguzo ya uchumi kwa kuwa serikali ya awamu ya tano inataka nchi kuwa ya viwanda hivyo wanawake wasiogope kukopa kwenye benk ya NMB kwa kuwa inamashariti nafuu.

“Tunaelekea kwenye uchumi wa viwanda hivyo wanawake tunapaswa kushikamana kwenye uchumi wa viwanda kwa kuwa benk ya NMB inasaidia maendeleo ya wanawake kwa kuwawezesha mitaji ya kufania maendeleo” alisema Kabati 

Aidha Kabati amewataka wanawake kuanzisha viwanda vidogo vidogo ambavyo vitasaidia kukuza uchumi na kuleta maendeleo kwa kuwa benk ya NMB imekuwa ikitoa mikopo ya kufanikisha wajasiliamali kuanzisha viwanda.

“Hata saizi ukitaka wajasiliamali waje kwenye kazi furani utakuta wanawake wamekuja kwa wingi kwa kuwa kwasasa wanawake ndio wanafanya biashara ndogo ndogo hivyo wanawake wanaweza kufanya biashara yoyote” alisema Kabati

Kabati aliwataka wanawake kufanya kazi zaidi ya moja ili kuinua na kujiletea maendeleo na kuondokana na kuwa tegemezi kwa wanaume.

Naye meneja wa benk ya NMB tawi la mkwawa George Mwita alisema kuwa bank hiyo imekuwa ikiwawaezesha wanawake kwa kuwapatie elimu ya ujasiliamali na kuwapatia mikopo yenye riba ndogo.

“Sisi kama NMB benk tumekuwa tukifanya kazi kwa ukaribu sana na wanawake kwa kuwa tunajua wanauwezo mkubwa wakufanya biashara ndogo ndogo na zile kubwa” alisema Mwita

Mwita aliwataka wanawake kufika kwenye benk ya NMB ili kujua huduma ambazo zinatolewa na benk hiyo ambayo ipo kila mahali kwa ajili ya kukuza uchumi wa wanawake na wanaume kwa kuwa benk hiyo haichagui mtu bali inawawezesha wananchi wote.

Ukija hapa benk ya NMB utapata huduma bora ambayo itakusaidia kuinua uchumi wako na kuleta maendeleo kwa kuwa tunatoa mikopo mbalimbali yenye mashariti nafuu na riba yetu sio kubwa” alisema Mwita

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More