Tuesday, April 11, 2017

WANANCHI WA IHEFU WALALAMIKA KWA KUTOSOMEWA MAPATO NAMATUMIZI KWA MIAKA MITATU KISA WIZI WA FEDHA ZA WANANCHI.

 mwenyekiti wa kijiji cha Ihefu kilichopo kata ya Mdabulo wilayani Mufindi Bateli Basilu akizungumza wa mwandishi juu tatizo lilopelekea kutoitisha mkutano wa mapato na matumizi kwa takriba miaka mitatu kutokana na utata wa fedha za wananchi milioni irishini na tano.

Na Fredy Mgunda,Iringa

Wananchi wa kijiji cha Ihefu kilichopo kata ya Mdabulo wilayani Mufindi wameulalamikia uongozi wa kijiji kwa kutowasomea mapato na matumizi kwa takribani miaka mitatu bila kuwaambia chochote kinachoendelea ndani ya kijiji hicho.

Wakizungumza na blog hii wananchi wa kijiji hicho walisema kuwa uongozi wa kijiji umekuwa  unamatumizi yasiyo sahihi kwa rasilimali za kijiji hadi kupelekea upotevu wa zaidi ya shilingi milioni ishirini na tano ambazo hazijulikani wapi zilikopotela.

“Viongozi wetu si waadilifu wala si wawajibikaji kwa kuwa hawana uwezo wa kutuongoza haiwezekani zaidi ya miaka mitatu hatuna mkutano wa hadhara wala hatusomewi mapato na matumizi je hiki kijiji hakina mipango yoyote endelevu kwa kuwa wananchi hatujui nani anaiongoza serikali hii” walisema wananchi

Wananchi waliongoza kuwa mtendaji na mwenyekiti hawapatani hivyo hatuwezi kupata jibu wapi pesa zetu zimeenda kutoka na viongozi hawa kutokuwa waadilifu na sio wawajibikaji kwa wananchi.

“Hiki ni kijiji lazima kiwe na mipangilio ya kuleta maendeleo lakini hapa tumekuwa mabubu maana hatujui hata nini serikali yetu inamikakati gani ya kimaedeleo na saizi wananchi tumeamka hatupo tena usingizini tunaomba mkutano uitwishe na kujua kwa miaka yote mitatu kijiji kimefanya nini na vipi kuhusu upotevu wa pesa za wananchi” walisema wananchi.

Aidha wananchi hao walisema kuwa wamekuwa wakiishirikisha serikali ya kata chini mtendaji wa kata pamoja na diwani wa kata lakini kila siku wanadanganywa tu hivyo wanauomba uongozi wa wilaya au mkoa kusaidia kutatua tatizo la kuwa na viongozi ambao ni wabadhilifu wa mali za wananchi.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kijiji cha Ihefu Bateli Basilu alikili kuwepo kwa upotevu wa pesa za wananchi ambazo ni zaidi ya milioni mbili na sio milioni ishirini na tano kama wanavyosema wananchi.

“Kweli mtengaji wetu alikula fedha za wananchi na ndio kitu kilichosababisha wananchi kukataa kufanya maendeleo ya kijiji wakitaka majibu sahihi ya hizo fedha zilipo”alisema Basilu
Basili alisema kuwa anapata shida kukiongoza kijiji hicho kutokana na sitofahamu inayoendelea kijijini hapo lakini aongeza kuwa mtendaji huyo sio muadilifu kabisa saizi hakuna maendeleo yoyote yanayoendelea katika kijiji hicho.

“Ni kweli hili ni tatizo kubwa sana hapa kijijini maana hadi mimi mwenyewe najifikiria kujiudhuru kutokana sakata hili maana nimenichafua na kunialibia dira ya mipango yangu ya kukipa maendeleo kijiji na wananchi wangu naomba uongozi wa juu kulitafutia ufumbuzi hili tatizo” alisema Basilu

Mwenyekiti wa kijiji alilipongeza shirika la LEAT kwa kutoa elimu iliyowafumbua macho wananchi wa kijiji cha Ihefu na ndio kitu ambacho miaka minigi tulikuwa tunatakiwa kukifanya kwa wananchi wawe na uelewa wa maliasili zao pamoja na kujua kila mpango wa maendeleo ya kijiji.

Naye mtendaji wa kijiji Paulo Magala alikili kutoitisha mkutano wa mapato na matumizi kutokana na wananchi kutoitikia wito wa kufika kwenye mkutano ili wasomewe mapato na matumizi.

Akijibia tuhuma juu ya upotevu wa shilingi milioni ishirini na tano alisema kuwa hakuna upotevu wa pesa hizo na kuambia wananchi wawasubili wanasheria wa wilaya ndio watakuja na majibu yote kwa kuwa amejipanga na anavielezo vyote ambavyo vinaonye matumizi ya hizo fedha.

Magala aliongeza kuwa wananchi wamekuwa na uelewa kutoka na kupewa elimu na shirika la LEAT kutoa elimu ya uwazi na uwajibikaji kitu kinachotufanya wananchi wewe wanahoji kila muda na kutufanya viongozi kila muda kujibia kero za wananchi a sio kupanga mipango ya wananchi

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More