Sunday, April 16, 2017

MBUNGE RITTA KABATI ANASHEREKEA SIKUKU YA PASAKA NA WATOTO YATIMA

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi CCM Ritta Kabati anasherekea sikuku ya pasaka na watoto yatima wa kituo cha Huruma center kilichopo Kigamboni Donbosco

Jamii bado inauelewa mdogo katika utunzaji wa watoto wanaoishi katika mazingira magumu na kuamini kuwa suala hilo ni jukumu la wafadhili kutoka nchi nyingine.

Mchungaji Joyce Gandango msimamizi wa kituo cha Huruma Center ameeleza hayo mbele ya mbunge wa viti maalumu mkoa wa Iringa Mh Ritta Kbati alipokuwa akishiriki chakula cha mchana na watoto katika kituo hicho kwenye sikukuu ya pasaka.

Msimamizi huyo ameeleza kuwa bado jamii haina muamuko katika kujitokeza kutunza watoto wa vituoni kwa kuamini kuwa wadhamini hutoa kila kitu.

Amezitaja  changamoto nyingine zinazowakabili katika kituo hicho ni ufinyu wa bajeti kutokana na wahisani kuanza kuondoka pamoja na kituo kushindwa kujitegemea na kujiendesha chenyewe.

Kwa upande wake mbunge wa viti maalumu Mh,Ritta Kabati ameahidi kushirikiana na viongozi wa kituo hicho katika kutatua changamoto zinazowakabili kwa kuzifikisha bungeni ili serikali iweze kuona namna ya itakavyowasaidia kuzitatua.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More