Friday, April 21, 2017

LIPULI KUFANYA UCHAGUZI TAREHE 29/05/2017

KAMATI iliyoteuliwa na shirikisho la  mpira  wa miguu Tanzania (TFF)  kwa ajili ya  kusimamia uchaguzi  wa klabu ya  Lipuli Fc  ya  mkoani Iringa  kuanza  kutoa  fomu kwa  wagombea wa nafasi mbali mbali  ndani ya Klabu  hiyo ya  Lipuli Fc  kesho  jumamosi Aprili 22  huku  ikionya mwanachama atakayekiuka  taratibu atafutwa kwa  kugombea .

Akizungumza na  wanahabari leo   katika  uwanja wa  samora ,mwenyekiti wa kamati ya  uchaguzi huo Hamimu Mahmud Omary alisema  kuwa kamati yake inaundwa  na  wajumbe watatu ambao  wameteuliwa na TFF taifa kwa  ajili ya  kumaliza  mgogoro  huo wa  Lipuli Fc pamoja na kufanya uchaguzi mkuu wa klabu hiyo .


Hivyo  alisema kwa  ajili ya  kuondoa figisu figisu katika  uchaguzi huo  wameteuliwa watu huru  ambao wataanza zoezi hilo la utoaji wa  fomu kwa wale  ambao  wanasifa ya  kugombea nafasi  zilizotanganzwa katika  klabu   hiyo ya  Lipuli Fc na kuwa  wanachama  zaidi ya 1000 ndio ambao  watashiriki kupiga  kura na kuomba uongozi .

Mwenyekiti  huyo alisema kwa  wanachama  wote wenye  sifa watatakiwa  kufika  kulipia ada ya uanachama  wao na  kuwa  mwanachama asiye hai  hataruhusiwa  kugombea au  kuchagua viongozi .

" Orodha  iliyofanyiwa  uhakiki  na kamati hii kama  maagizo ya  TFF yanavyosema  ndio  itatumika  kujua  nani ana  siafa ya kushiriki uchaguzi huo na nani harusiwi na  orodha hiyo  itatandikwa  eneo la  wazi ili  kila mwanachama aweze kuisoma na kuhakiki ....wanachama  wanapewa  siku  saba kuanzia  leo kufika kuhakiki kadi zao  "

Akisoma  kalenda  hiyo ya  uchaguzi wa  Lipuli Fc  alisema kuanzia Aprili 21-28 /2017 kwa maana ya jana ni kamati ya TFF  kutangaza uchaguzi  huo  wakati Aprili 22 pazia la  uchukuaji  fomu kwa  wanachama  wote wenye sifa  linafunguliwa wakati Aprili 29-30 kamati  yake  itabandika orodha ya awali ya wagombea  kwenye mbao za matangazo na kipindi cha  kupokea pingamizi ni  Mei 1-2 mwaka  huu .

Mwenyekiti huyo  alisema mei 6 ni siku ya kamati yake   kutangaza na kubandika  kwenye mbao za matangazo  pingamizi  na  kufanya usahili wa  wagombea baada ya hapo Mei  4-7 ni siku ya kamati yake  kuwasilisha  masuala ya kimaadili  kwenye kamati ya maadili ya TFF huku Mei 7-11 ni kipindi cha kupokea ,kusikiliza na kutolea  maamuzi masuala ya maadili kazi itakayofanywa na TFF Mei 12  kutangaza maamuzi ya kamati ya maadili .

Hata  hivyo  alitangaza kipindi  cha kukata rufaa kamati ya uchaguzi  ya TFF kwenye  kamati ya rufaa ya uchaguzi  kuwa ni mei 13-14 wakati rufaa  hizo zitasikilizwa na kamati husika Mei 15-19 mwaka  huu  na Mei  20  wagombea  wote  kujulishwa na kamati  ya rufaa ya uchaguzi ya TFF  na Mei  21 kuchapisha  orodha ya  mwisho ya  wagombea na  kutangazwa kwenye mbao za mataangazo .

Kuhusu  kipindi cha kampeni kwa  wagombea  alisema muda  ni kuanzia Mei 22-28  mwaka huu na atakayefanya  kampeni kabla ya  muda  huo au kutoa  rushwa ya aina yeyote atakuwa  amepoteza  sifa ya  kuwa  mgombea na  kuwa uchaguzi wa Klabu ya  Lipuli Fc utafanyika  siku ya Mei 29 mwaka huu wajumbea na  wagombea  wote  watapaswa  kushiriki .

Mwenyekiti  huyo  alitaja nafasi zinazogombea  na gharama ya  fomu  kwenye mabano kuwa ni mwenyekiti (200,000), makamu  mwenyekiti (200,000)  katibu na makamu  wake (200,000),mweka hazina na msaidizi wake 100,000 na wajumbe watano wa kamati ya utendaji (100,000)

Alisema  kuwa  lengo la  kutoa muda zaidi  wa uchukuaji wa fomu ni  kutaka  kutoa nafasi kwa  wanachama  waliopo nje ya nchi  nao  kushiriki  kugombea ama kuchagua  na kuwa uongozi mpya wa Lipuli Fc  utakabidhiwa pesa ya ada ya  wanachama na idadi kamili ya  wanachama  baada ya  uchaguzi huo .


Aidha  mwenyekiti huyo  alionya wagombea  ambao  wataanza kampeni za  kuchafua  watu wakiwemo viongozi wa serikali ya  mkoa wa Iringa ama viongozi wa TFF wilaya , mkoa hadi  Taifa kuwa  watakuwa  wamepoteza sifa na hatua za  kisheria  dhidi yao zitachukuliwa  .

Pia  alisema sifa  7 ambazo mgombea anapaswa  kuwa nazo  ili  kuwa  mgombea wa Lipuli  FC   kuwa ni awe  raia wa Tanzania , awe amesoma hadi kidato cha nne na  kufuaulu au elimu ya  juu ,awe na  uzoefu wa angalau wa miaka 5  katika mambo ya utawala wa  michezo ya mpira wa miguu,awe hajawahi  kukutwa na hatia ya kosa la jinai na kuhukumiwa  kufungwa bila kutolewa adhabu ya faini , awe na umri usiopungua miaka 25,awe na uwezo ,heshima, uadilifu, na haiba ya  kuweza kuiwakilisha klabu ya  Lipuli Fc  ndani  na nje ya mkoa wa Iringa na Tanzania ,asiwe na mwamuzi wa mpira wa miguu anayefanya shughuli za uamuzi kwa kipindi  hiki.

0 comments:

Post a Comment

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More